Beijing: Maonesho ya mafanikio ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) yafanyika siku chache kabla ya mkutano mkuu

Beijing: Maonesho ya mafanikio ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) yafanyika siku chache kabla ya mkutano mkuu

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
1665643662893.png


Zikiwa zimebakia siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano mkuu wa Chama cha Kikomnisti cha China (CPC) maonyesho mbalimbali yameandaliwa jiji Beijing ambayo kwa sehemu kubwa yanaonyesha mafanikio ya utawala wa chama hicho ndani ya muongo mmoja uliopita.

Maonyesho hayo yenye kauli mbiu isemayo 'Forging Ahead in the New Era' yanaonyesha mafanikio ya CPC katika kipindi cha miaka 10, yanagusa sekta zote muhimu kwa nchi, maelfu ya watu wanatembelea kujionea mambo mbalimbali.

1665643688732.png


Katika ukumbi wa taifa wa maonyesho wa Beijing yanakofanyika maonyesho hayo, kumewekwa picha za mambo mbalimbali ambayo yanatajwa kuwa ni mafanikio yaliyofikiwa katika kipindi hicho, watembeleaji hupata maelezo na kujibiwa maswali yao.

Miongoni mwa vitu vilivyovutia wengi ni maendeleo ya teknolojia katika zana za ulinzi, na ubunifu unaotoa masuluhisho kwa changamoto mbalimbali ambazo awali zilikuwa zikiikabili jamii.
 
VCG111405603783.png
Mkutano Mkuu wa 20 wa Wajumbe Wote wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) ambacho ni chama tawala cha China umefunguliwa leo saa nne asubuhi mjini Beijing, na kuhudhuriwa na wajumbe zaidi ya 2,300 wa wanachama wa CPC. Mkutano huo utafanyika kuanzia leo hadi tarehe 22, Oktoba.

Mkutano huo utasikiliza na kuchunguza ripoti ya Kamati Kuu ya 19 ya CPC, na ripoti ya Kamati ya Ukaguzi wa Nidhamu ya Kamati Kuu hiyo, kuchunguza na kupitisha Marekebisho ya Katiba ya Chama, na kuchagua na kuunda awamu mpya ya Kamati Kuu ya Chama na Kamati ya Ukaguzi wa Nidhamu ya Kamati Kuu hiyo.

Tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China, Chama cha Kikomunisti cha China chenye historia ya miaka 101 kimeendelea kutawala nchi hiyo kwa miaka 73, kikiwa na wanachama zaidi ya milioni 96. Mkutano Mkuu wa Wajumbe Wote na Kamati Kuu inayochaguliwa kwenye mkutano huo, ni mamlaka za juu zaidi za uongozi za CPC, na Mkutano Mkuu wa wajumbe wote wa CPC unafanyika kila baada ya miaka mitano.
 
1211693069_16658901689231n.jpg
Rais Xi Jinping wa China ametoa hotuba muhimu kwenye Mkutano Mkuu wa 20 wa Wajumbe Wote wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) uliofunguliwa leo hapa Beijing.

Kwenye hotuba yake, rais Xi amesema, kuanzia sasa jukumu kuu la CPC ni kuongoza wananchi wa makabila mbalimbali nchini China kujenga nchi ya kisasa ya kijamaa katika pande zote, na kutimiza lengo la pili la miaka mia moja, ili kusukuma mbele ustawi wa taifa la China kwa njia ya kichina.

Rais Xi amesema, China inafuata sera za kidiplomasia ambazo ni huria, za kujiamulia na za amani. Amesema siku zote China inaamua msimamo na sera zake kufuatia hali halisi, kulinda kanuni za kimsingi za uhusiano wa kimataifa na haki duniani, na inapinga kithabiti aina yoyote ya umwamba na siasa ya kinguvu, pia inapinga wazo la Vita Baridi, vitendo vya kuingilia kati mambo ya ndani ya nchi nyingine, na kupinga vigezo viwili. Amesisitiza kuwa, China haitafanya umwamba, wala haitavamia nchi nyingine daima.

Amesema, China imekuwa mshirika mkubwa wa kibiashara wa nchi na sehemu zaidi ya 140, na inashika nafasi ya kwanza duniani kwa thamani ya biashara ya bidhaa. Pia rais Xi amesema, China inashika nafasi ya kwanza katika kuvutia uwekezaji wa nje na kutoa uwekezaji kwa nchi za nje, na imeendeleza sera ya kufungua mlango kwa nje kwa upana na kina zaidi.

Aidha, Rais Xi amesema, China itasukuma mbele kwa hatua madhubuti na tulivu kufika kilele cha utoaji wa hewa chafu na kutimiza usawa wa utoaji na ufyonzaji wa hewa hiyo. Pia amesema, China itashiriki kwenye usimamizi wa kimataifa wa juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
 
Kwenye hotuba yake, rais Xi amesema, kuanzia sasa jukumu kuu la CPC ni kuongoza wananchi wa makabila mbalimbali nchini China kujenga nchi ya kisasa ya kijamaa katika pande zote,
Hili ni Jambo zuri kwa kuwa sasa pia tuna ishi ulimwengu wa kisasa hivyo ni njema pia falsafa zikienda kisasa zaidi.
 
na kutimiza lengo la pili la miaka mia moja, ili kusukuma mbele ustawi wa taifa la China kwa njia ya kichina.
Daaah! miaka mia moja [ 100] Afrika [ especially Tanzania ] tuna kila sababu ya kujifunza namna ya mipango endelevu na iliyo bora ya miaka mingi kutoka China.
 
Kumbe kamwenendo ka CPC kanafanana sana na ka CCM ndo maana wana share hata zile herufi mbili za cc......!!
 
Chama cha CPC cha China kipo kwenye msimu wa mkutano mkuu wa 20, mkutano unaokaliwa kila baada ya miaka 5, ikumbukwe kuwa CPC ndio chama kikubwa duniani kilichopo madarakani kwa sasa, kina jumla ya wanachama milioni 96.

CPC ndio chama cha kwanza chenye ushawishi mkubwa ulimwenguni kutokana na nafasi ya Taifa la China duniani.

Katika mkutano huu uchaguzi wa Viongozi wa juu wa Chama cha CPC (China Communist party) utafanyika, jumla ya Wajumbe (delegates) 2300 wanategemewa kuchagua halmashauri kuu ya chama yenye Wajumbe 200.

Baada ya hawa wajumbe 200 kupatikana, nao watachagua Wajumbe wa juu kabisa wa chama, wajumbe hao idadi yao ni 25 tu, ambao huitwa “politburo”.

Hao 25 (politburo) nao huchagua wakuu wa chama ambao ni 7, hawa wakuu chama ndio viongozi wa juu wa serikali, mfano ni katibu mkuu wa chama cha CPC ambae automatic ndie huwa Raisi wa China.

Moja ya sifa kuu ya kuchaguliwa kuwa wajumbe wa politburo na viongozi 7 wa juu wa chama lazima wawe wamehudumu kwenye ngazi mbalimbali za uongozi ndani ya chama na serikali kwa muda mrefu.

Mfano Xi Jinping kabla ya kuwa Rais 2013 alihudumu kwenye ngazi mbalimbali ndani ya chama na serikali kwa takribani miaka 40.

Ndimi Comred Mbwana Allyamtu CMCA
 
Jimping ni Rais wa maisha wa China na kwenye chama chake, Sasa takataka kama unatuletea hapa ili tujadilini nini?

Hii peleka Lumumba huko ndio wanapenda mifumo ya kijinga kama hii.
 
Nasikia amezungumzia issue za reunification na Taiwan kitu kilichoikera sana Taiwan
 
Vipi ule ujio wa Polos kuitembelea Taiwan ? Na Yale mazoezi ya China yaliishia wapi ? Chezea uchumi wa china wewe . Mchina mjanja sana . Kuliko uchumi wake uharibiwe na vita Bora aiachie TAIWAN sio Sawa na huyu asshole Putin.
 
Vipi ule ujio wa Polos kuitembelea Taiwan ? Na Yale mazoezi ya China yaliishia wapi ? Chezea uchumi wa china wewe . Mchina mjanja sana . Kuliko uchumi wake uharibiwe na vita Bora aiachie TAIWAN sio Sawa na huyu asshole Putin.
Duuuh bora aiachie taiwan? Una akili kweli?
 
Viva china hakika dunia lina la kujifunza toka kwenu kwa maendeleo yenu na ustawi wa dunia kwa ujumla
 
Back
Top Bottom