Boeing wamefeli tena. Safari ya siku 8 imekuwa ya miezi 8

Boeing wamefeli tena. Safari ya siku 8 imekuwa ya miezi 8

Ni habari yenye kuhuzunisha masaa kadhaa yaliyopita Boeing Starliner imeshindwa kuwarudisha duniani wanaanga wawili waliopelekwa kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu, International Space Station (ISS)

Ikumbukwe kuwa wanaanga hawa Barry Wilmore (M) na Sunita Williams (F) walienda na Boeing Starliner June 6, 2024 na ilikuwa ni safari ya siku 8 tu.

Lakini mpaka kufikia sasa Boeing na NASA wameshindwa kuwarudisha kwa sababu ya hitilifu (technical issues) kwenye chombo hicho.


View attachment 3089234
Boeing Starliner Space Capsule jana imerudi duniani bila wanaanga iliowapeleka

Kwa sasa Boeing na NASA zinashirikiana na SpaceX ya Elon Musk kuona jinsi ya kuwanasua wanaanga hao wawili. Ambapo inasemekana huenda kufikia February 2025 wataweza kuwarudisha. Safari ya wiki moja yawa ya miezi 8.

Boeing imekuwa na technical issues kwenye ndege zake na sasa hata kwenye spacecraft.

Mwaka 2011 Marekani iliizuia China isijiunge kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu cha ISS na China ikaamua kuanzisha rasmi kituo chake cha anga za juu kinachoitwa Tiangong Space Station.

Kwa sasa kuna vituo viwili tu vya anga za juu cha Kimataifa na cha China.


View attachment 3089246
Wanaanga wa China wakifurahia kwenye Tiangong Space Station hawana wasiwasi wa kutorudi duniani

Je, ifike wakati NASA na Boeing waombe kushirikiana na China kuwanasua wanaanga hao?
Nionavyo mimi Wamarekani wapo radhi hao wenzao wafie huko. MAGA itawazuia kuomba msaada kwa Wachina.
 
Humu bwana ubako kucheka yani mchini amzid uwezo marekani mtu ambae kaaanza kwenda space tpka 1998 huko come one bhana
 
Tazama pace ya projects. Hii hapa ya Boeing iliyofeli ni capsule yao ya kwanza wanafanya majaribio na hao astronauts wawili ni test pilots.

Sasa Urusi anayo wapi service kama ya Starlink au reusable rocket kama ilivyo Falcon 9 ambayo ni reusable. Angara ndio rocket yao mpya ya kuistaafisha Soyuz-2 ila bado sio reusable.

Soyuz-7 ndio itakuwa reusable na iko kwenye development ila hata prototype hawana. Kama kawaida ya miradi yao watachelewa vibaya hawa. Soyuz-7 itakuwa na Angara wawe nazo mbili. Of course Marekani itaistaafisha ISS na ushirikiano wa Urusi na Marekani unaisha hapo, probably 2031. Kila mtu ataanza kushinda mechi zake sasa, Mrusi atakuwa amezidiwa na Mchina parefu.
Mfano kwa sasa Urusi haijafanikiwa kurudi mwezini, wamekaa miaka 47 baada ya kutua mwezini vizuri ila mwaka jana wameshindwa. India mwaka jana imetua mwezini. Urusi pale legacy ya USSR kwenye anga imeisha.
Dah!... Africa lini tutapata mwakilishi huko anga za juu ?
 
Humu bwana ubako kucheka yani mchini amzid uwezo marekani mtu ambae kaaanza kwenda space tpka 1998 huko come one bhana
Acha kukariri, Soviet Union ndio walikuwa wa kwanza kutuma chombo anga za juu lakini wakaja kuachwa na Marekani kwenye space tech

Soviet Union walikuwa wa kwanza kutuma chombo mwezini, Marekani akadai amepeleka mwanadamu wa kwanza mwezini

Wakati huohuo China limekuwa taifa la kwanza duniani kufika moon's far side ambako hakuna taifa lolote limewahi kufika

Hiyo ni mifano michache inapohusu space tech au tech yoyote muda wowote unaweza kupitwa kiteknolojia watu wanafanya R&D na innovation usikariri
 
Hapo watengeneza movie tayari ni idea hiyo,itakuja movi inaitwa Trapped in the Outaa
Ni habari yenye kuhuzunisha masaa kadhaa yaliyopita Boeing Starliner imeshindwa kuwarudisha duniani wanaanga wawili waliopelekwa kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu, International Space Station (ISS)

Ikumbukwe kuwa wanaanga hawa Barry Wilmore (M) na Sunita Williams (F) walienda na Boeing Starliner June 6, 2024 na ilikuwa ni safari ya siku 8 tu.

Lakini mpaka kufikia sasa Boeing na NASA wameshindwa kuwarudisha kwa sababu ya hitilifu (technical issues) kwenye chombo hicho.


View attachment 3089234
Boeing Starliner Space Capsule jana imerudi duniani bila wanaanga iliowapeleka

Kwa sasa Boeing na NASA zinashirikiana na SpaceX ya Elon Musk kuona jinsi ya kuwanasua wanaanga hao wawili. Ambapo inasemekana huenda kufikia February 2025 wataweza kuwarudisha. Safari ya wiki moja yawa ya miezi 8.

Boeing imekuwa na technical issues kwenye ndege zake na sasa hata kwenye spacecraft.

Mwaka 2011 Marekani iliizuia China isijiunge kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu cha ISS na China ikaamua kuanzisha rasmi kituo chake cha anga za juu kinachoitwa Tiangong Space Station.

Kwa sasa kuna vituo viwili tu vya anga za juu cha Kimataifa na cha China.


View attachment 3089246
Wanaanga wa China wakifurahia kwenye Tiangong Space Station hawana wasiwasi wa kutorudi duniani

Je, ifike wakati NASA na Boeing waombe kushirikiana na China kuwanasua wanaanga wao?
[/QUOT
 
Hapo wazee wa Hollywood wameshapata idea ya movie
"Trapped in the Outer space"
 
Hapo watengeneza movie tayari ni idea hiyo,itakuja movi inaitwa Trapped in the Outaa
Directors wa Hollywood wa movies za sci-fi wanalifuatilia tukio hili kwa ukaribu kupata idea sio?
 
Nionavyo mimi Wamarekani wapo radhi hao wenzao wafie huko. MAGA itawazuia kuomba msaada kwa Wachina.
Marekani ni watu makini kwenye safety ya watu wake. Ndio maana OSHA ndio wao waliianzisha na ilikuwa chini ya mamlaka yao ya ajira, kabla hawajaifundisha na kuisambaza duniani. Vitu vingi sana unavyotumia kwenye usalama ni vya Wamarekani.

Huwezi walinganisha Wamarekani na Wachina ambao waliwahi kuuana mamilioni kwa mamilioni kila baada ya miaka kadhaa. Mara ya mwisho hapo Mao Zedong alisababisha njaa kuanzia 1959, njaa kubwa zaidi ya mwisho kutokea duniani wakafa Wachina zaidi ya milioni 30 kwa sera mbovu za kiongozi wao.

Kwanza kwa taarifa yenu Boeing Starliner imetua duniani salama kabisa kwa autopilot, na haikuwa na tatizo lolote hivyo hata wangekuja nayo hawa astronauts wawili isingekuwa shida. Boeing walihakikisha iko sawa, NASA hawakubisha ila walitaka kuwa na uhakika kabisa. Wamefanya hivi tabia za Kimarekani kuzingatia usalama.

Wachina waombwe msaada kwa lipi? Tueleze ni capsule gani ya Kichina inaweza dock pale ISS.
 
Huwezi walinganisha Wamarekani na Wachina ambao waliwahi kuuana mamilioni kwa mamilioni kila baada ya miaka kadhaa. Mara ya mwisho hapo Mao Zedong alisababisha njaa kuanzia 1959, njaa kubwa zaidi ya mwisho kutokea duniani wakafa Wachina zaidi ya milioni 30 kwa sera mbovu za kiongozi wao
Mbona Marekani wameshawahi kuuana sana kwenye American Civil War
 
Ni habari yenye kuhuzunisha masaa kadhaa yaliyopita Boeing Starliner imeshindwa kuwarudisha duniani wanaanga wawili waliopelekwa kwenye Kituo cha Kimataifa cha Anga za Juu, International Space Station (ISS)

Ikumbukwe kuwa wanaanga hawa Barry Wilmore (M) na Sunita Williams (F) walienda na Boeing Starliner June 6, 2024 na ilikuwa ni safari ya siku 8 tu.

Lakini mpaka kufikia sasa Boeing na NASA wameshindwa kuwarudisha kwa sababu ya hitilifu (technical issues) kwenye chombo hicho.
Bora hata ya hao Boeing sisi tunaowasema tumeweza nini hata kwa 2% sanasana kutekana na kupotezana Tumeshindwa hata kulindda rasilimali zetu
 
Kwanza kwa taarifa yenu Boeing Starliner imetua duniani salama kabisa kwa autopilot, na haikuwa na tatizo lolote hivyo hata wangekuja nayo hawa astronauts wawili isingekuwa shida. Boeing walihakikisha iko sawa, NASA hawakubisha ila walitaka kuwa na uhakika kabisa. Wamefanya hivi tabia za Kimarekani kuzingatia usalama
Kwa hiyo kusema watawarudisha February 2025 ni kwa sababu za kiusalama?

Kutua duniani salama kwa autopilot bila astronauts ndio kufeli kwenyewe

Boeing wamekiri wenyewe kuwa Starliner ina hitilafu wewe ni nani uwabishie?
 
Marekani ni watu makini kwenye safety ya watu wake. Ndio maana OSHA ndio wao waliianzisha na ilikuwa chini ya mamlaka yao ya ajira, kabla hawajaifundisha na kuisambaza duniani. Vitu vingi sana unavyotumia kwenye usalama ni vya Wamarekani.

Huwezi walinganisha Wamarekani na Wachina ambao waliwahi kuuana mamilioni kwa mamilioni kila baada ya miaka kadhaa. Mara ya mwisho hapo Mao Zedong alisababisha njaa kuanzia 1959, njaa kubwa zaidi ya mwisho kutokea duniani wakafa Wachina zaidi ya milioni 30 kwa sera mbovu za kiongozi wao.

Kwanza kwa taarifa yenu Boeing Starliner imetua duniani salama kabisa kwa autopilot, na haikuwa na tatizo lolote hivyo hata wangekuja nayo hawa astronauts wawili isingekuwa shida. Boeing walihakikisha iko sawa, NASA hawakubisha ila walitaka kuwa na uhakika kabisa. Wamefanya hivi tabia za Kimarekani kuzingatia usalama.

Wachina waombwe msaada kwa lipi? Tueleze ni capsule gani ya Kichina inaweza dock pale ISS.
Sure wamarwkani usalama kwanza hao wachina usalama kwao 0 hata wakifa hawana shida.
 
China wana Spacesail kucompete na Starlink, upande wa reusable spacecraft wana Mengzhou
Mengzhou itawapeleka astronauts wa China watue kwenye mwezi. Project ni waweze kutua mwezini miaka ya 2030s, jambo ambalo Marekani walifanya 1969. Hiyo ni gap ya miaka 60!

Alafu anatokea muuza nyanya mmoja anakwambia eti Marekani iwaombe msaada China kurudisha astronauts😂

Alafu China wanacompete na SpaceX kwa product iliyopo, bado hujui ni kampuni gani nyingine ya Marekani inakuja na lipi. Wakati SpaceX ina maelfu ya satellites angani inatoa internet hadi Kenya, hadi Ghana. Ndio kwanza Wachina wanataka kuwa na uwezo kuanzia mwakani. Elon Musk amerusha rockets zake za Falcon 9 mara 381 tangu 2010. Wana satellites zaidi ya 6,000 za internet.

Wachina tulieni kwanza haya sio mayeboyebo kwamba unafyatua tu.
 
Mengzhou itawapeleka astronauts wa China watue kwenye mwezi. Project ni waweze kutua mwezini miaka ya 2030s, jambo ambalo Marekani walifanya 1969. Hiyo ni gap ya miaka 60!
Soma meseji #45
 
Wakati SpaceX ina maelfu ya satellites angani inatoa internet hadi Kenya, hadi Ghana. Ndio kwanza Wachina wanataka kuwa na uwezo kuanzia mwakani
Mbona wameshatuma satellite mkuu? Au hauna hizo taarifa?
 
Back
Top Bottom