Bunge liitishe kikao cha dharura kujadili kufungwa kwa ubalozi wa Denmark 2024

Mkuu ishu ya mbowe ina utata mwingi sana, unaonaje tusubiri tuone ushahidi utaoletwa mahakami upoje, sidhani kama mpenda demokrasia yeyote anapenda Mbowe kuwa ndani muda huu, ila ngoja tuone nini wanasema hawa wanasheria!! Kwa upande wangu natamani Mbowe aachiwe huru, Mwamba ana mchango mkubwa kwa taifa hili, hamna mtu hajawahi kukosea, serikali ijifikirie kwa hilo
 
Hamza is the hero. Not the one who was killed by covid-19


Hawamuelewi Mulamula Liberata...hata mimi simuelewi! Wameona isiwe taabu!
Mkitaka waghairi nendeni mezani mkaruhusu.....!
 
Mkuu uko sawa hii nchi haitakuja kuendelea sie tuishi wewe watu tumewafundisha kulima nazi, chikichi na mpunga leo wanavuna mwingi na kutuuzia sisi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ sie tuishi
 
He he heeeeee haloooo hii kiboko.....
Mkuu ungetumia japo tafsida kidogo kwamba wabunge wetu wanakusanyikaga dodoma kupigana miti tu badala ya kushughulika na kujadili mambo muhimu kabisa ya nchi yetu...
Wewe unaona wanajadili mambo serious ya nchi ?
 
Waziri wa mambo ya nje anapaswa kutoa taarifa rasmi ya serikali bungeni kuelezea uamuzi huo wa Denmark.
Ninakubaliana nawe juu ya hili pekee katika mengine yote uliyoandika kwenye mada yako.

Hii tabia ya utegemezi imekuwa kilema kikbwa sana kwenye nchi yetu.

Yaani wewe unaona kabisa maana ya kuwa na ubalozi hapa nchini ni kupata misaada?

Miaka 60 tokea tupate uhuru wetu na kuwa wategemezi wa misaada, bado tunalialia tuonewe huruma ya misaada?

Hao waliosomeshwa na digrii zao za "uvamizi" hadi leo hii wamefanya nini, au ni pamoja na wewe mleta mada hii?

Umesomea "uvamizi" ili uwe mzuri sana kuililia misaada hiyo?

Tunachohitaji sana ndani ya nchi hii sasa ni kumpata kiongozi atakayeamsha ari ya wananchi kujiona kuwa uwezo wa kujitafutia maendeleo yetu tayari runao mkubwa sana, tunachokosa tu ni uongozi wa kutuwezesha kuyaleta maendeleo hayo sisi wenyewe.

Halafu unataka bunge lifanye nini? Bunge lipi, hili la 'comedy' ya Ndugai?

Denmark wanafanya jambo jema sana, ningewasihi na nchi nyingine na wao wafuate mfano wao.
 
Pesa wanawapa mnaenda kufadhili wasiojulikana na Magaidi
 
Denmark tulikuwa nao sawa uchumi lakini leo wanatupa misaada kanchi SAwa na mkoa.
Tatizo la ukosefu wa uongozi bora.
Wao wanapata viongozi sisi tunapata watawala.
Kwani hao watawala wenyewe wapo?
 
Ni matokeo ya Tundu Lissu kuichafua nchi nje ya nchi, Bunge msipoteze muda kwa ujinga kama huu, waTZ tutaprevail tu, hawa wapinzani uchwara wanaoomba nchi yao ikose hela kwa manufaa yao ya kisiasa watashindwa tu, TZ will stand always
Hata hizo pesa ccm huzitumia kwa manufaa ya kisiasa. Mtalia mwaka huu.
 
Kwani sisi situnawaitaga Mabeberu,na pia wao wanaamini katika democrasia ya kweli,sisi tunaamini katika democrasia janja janja,Pia Susi situlishaingia uchumi wa Kati? Wameona wapo wahitaji kuliko sisi, ukanda wa sahel na pembe ya Afrika na maeneo yaliyoathiriwa na migogoro. Baada tu yakuona tuna uwezo wa kuibua miradi mikubwa mikubwa kwa mafweza ya ndani tena bila mikopo wameona, pia makusanyo mapya yamewapa moyo, kuwa tutatoboa, Bila misaada.
 
Ni matokeo ya Tundu Lissu kuichafua nchi nje ya nchi, Bunge msipoteze muda kwa ujinga kama huu, waTZ tutaprevail tu, hawa wapinzani uchwara wanaoomba nchi yao ikose hela kwa manufaa yao ya kisiasa watashindwa tu, TZ will stand always
Nchi ikose hela za mabeberu wakati ni tajiri aka donakantle?😝😝😝😝
 
Hata hizo pesa ccm huzitumia kwa manufaa ya kisiasa. Mtalia mwaka huu.
Siku tukipata upinzani wa kweli nitafurahi sana, siyo hawa wahuni wanaotaka ubunge na ujinga mwingine! Kifupi mzee wapinzani wetu njaa kali, wanajali matumbo yao tu, kwa sasa wanachoangalia ni jinsi gani Samia anaweza kuwatua, in the process nao wapate hela
 

Bunge la majizi ya kura ndio la kuishawishi Denmark kusitisha mpango wa kuondoka kwenye nchi yenye siasa za kishenzi? Kwa jinsi nchi hii ilivyoingiza siasa za kipuuzi ndani ya miaka 6, nashangaa hata balozi nyingine zinangoja nini.
 
kuna nchi nyingi tu tunaweza kushirikiana nazo zenye GDP kubwa kuliko Danmark..mathalan Iran, Malaysia to mention a few.. kwann tuendelee kuhemea since 1960s?? ndio uezo wetu ulipoishia?

Mbona hamshirikiani nazo sasa?
 

Hizi ni balozi za Danmark Africa
Ni Tanzania tu wanafunga. Ni nini kimetokea?
Je na wenzao katika Nordic group (Norway, Sweden na Finland) wana mipango hiyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…