China yaongoza duniani katika utengenezaji na uuzaji wa mabasi ya abiria

China yaongoza duniani katika utengenezaji na uuzaji wa mabasi ya abiria

Kampuni kubwa za kichina, mfano Wachina wa Huawei, huwekeza walau 50% au zaidi ya faida yao kwa mwaka kwenye R&D. Jamaa wana R&D centres katika nchi tofauti tofauti kwenye kila bara...

Ona sasa wanavyokimbiza hadi mmarekani kawawekea zengwe baada ya kuwaona walivyo tishio...
Ukiona kampuni inaanza kufungua R&D centers nje ya mipaka ya nchi yake ujue tayari wana uwanda mkubwa wa soko na ina billions of dollars in market value
 
hapa nakupinga kaka , boeing na airbus kuja kupata mpinzani mkali kutoka china kuna safari ndefu kidogo. Labda hiyo kampuni ifanye competition na akina ambraer, gulfstream,dasault ,bomberdier n.K japo napo kuna kakipengele
Kwa sasa C919 wana order ya ndege 1061 imagine hawajamaliza hata mwaka tangu izinduliwe rasmi
 
Xi Jinping amekazania sana hili suala la R&D kwa makampuni ya ndani naona wameanza kujionea matunda yake. Good news ni kwamba serikali pia inatoa financial support kwa makampuni na hata watu binafsi sasa hivi kila province ya China haukosi kuona centers zinazojihusisha na R&D na FTZs na SEZs
Msaada kwenye tuta,tufungulieni hizo code wakuu R&D,FTZs na SEZs,hapo nimetoka kapa
 
Kwa miaka 9 mfululizo kampuni ya Yutong ya China imekuwa kinara kwa kuuza mabasi mengi zaidi duniani.

Utengenezaji na uuzaji wa mabasi ya abiria imekuwa biashara kubwa yenye ushindani hasa mabasi ya umeme. Mabasi yamekuwa yakitengenezwa kwa kazi na makusudi tofauti tofauti.

Kinachoangaliwa katika ushindani wa biashara hii ni idadi (units) za mabasi ambazo makampuni katika nchi husika yameuza.

Ifuatayo ni 10 bora ya majina ya makampuni yaliyouza mabasi mengi zaidi duniani mwaka 2022 na idadi ya mabasi yaliyouzwa;

(1)YUTONG (China) – 58,688
View attachment 2679250


(2)DIAMLER (Ujerumani) – 32,612

View attachment 2679307

(3)KING LONG (China) – 26,450
View attachment 2679303

(4)GOLDEN DRAGON (China) – 19,392
View attachment 2679306

(5)MARCOPOLO S.A (Brazil) – 15,831
View attachment 2679298

(6)ZHONGTONG (China) – 15,054
View attachment 2679295

(7)MAN (Ujerumani) – 13,972
View attachment 2679308

(8)HIGER (China) – 11,412
View attachment 2679302

(9)VOLVO (Sweden) – 9,731
View attachment 2679309

(10)SCANIA (Sweden) – 7,777
View attachment 2679310

Katika tatu (3) bora duniani, makampuni matano ya China yameongoza kwa pamoja yaliuza mabasi 130,996, ikifuatiwa na makampuni mawili ya Ujerumani yaliuza jumla ya mabasi 46,584 na Sweden mabasi 17,148

REKODI YA CHINA KATIKA BIASHARA YA MABASI
●Kwa miaka 9 mfululizo kampuni ya Yutong ya China imekuwa kinara kwa kuuza mabasi mengi zaidi duniani.

●China ndilo taifa linalouza karibu asilimia 50 ya mabasi katika soko la dunia.

●China inaongoza kwa kutengeneza mabasi yasiyotumia mafuta (new energy vehicle) Asilimia 90 ya mabasi ya umeme duniani ni yaliyotengenezwa na makampuni ya China.

●Youngman ndilo basi kubwa zaidi lililovunja rekodi duniani lenye urefu wa mita 25 lenye uwezo wa kupakia abiria 300. Lilipewa jina la utani triple bus. Lilitengenezwa na kampuni ya China Youngman Automobile Group Co., Ltd.

View attachment 2679287

●China ndilo taifa pekee duniani lenye viwanda 16 vikubwa vya kutengeneza mabasi; Yutong, Higer, Zhongtong, Kinglong, JMC, Foton, BYD, Golden Dragon, Asia Star, Ankai, Changan, Dongfeng, Nanjing Iveco, Briliance Renault, Sunwin na Sunlong.
Nimeona katarama polo g7 aiseee hio gari ni balaaa kwa michina inayokuja Africa sijaona wa kukaa mbele

Mchina lazima akimbize sababu kuu ni magari yake yanakaa mda kidogo yanachoka

Sema kuvuta IRIZAR I8 route za dar mwanza ni matumizi mabaya ya akili
 
ila hizo Scania nazikubali sana jamani
Mabasi ya kichina ni kwa kuwa wafanyabiashara wanayaleta maana bei chee na hivyo wanapata faida mapema but quality wise hayawezi shindana na western hata kidogo. Kwa kifupi mchina kuuza sana wala si ajabu maana bei za bidhaa zake zipo chini sababu ya cheap labour na kutumia raw material za ubora wa kawaida au chini. Ndiyo maana hata company nyingi za europe na US wanaviwanda china sababu ya cheap labour. Iko wazi kabisa hata kariakoo tecno na nduguze utakuta wanauzika sana kuliko I phone au samsung sasa check ubora wa tecno na samsung au i phone ardhi na mbingu🤣😂 simu ya kichina warranty miezi 12+1 wakati brand zinazoeleweka warranty 2 years! Kwa kifupi kinachombeba mchina ni bei chee.
 
Sidhani kama mchina ana innovation yake, karibu 90% ya product zake copy from western.
hilo lipo wazi sana mkuu western ni wavumbuzi then mchina kwa kuwa ana cheap labour plus kutumia raw material za ubora wa chini au kawaida automatically anaonekana ameuza sana sokoni! Au makampuni ya western yanapotaka kupunguza gharama za uzalishaji ndipo yanaenda china. Ndiyo maana kila kinachogunduliwa na western baadae unakuta mchina huyu hapa anauza kwa wingi. Hayo mabasi, malori, na vingine vingine ni copy paste ya western tech, ndiyo maana unakuta imeanza insta china kakopy ana tiktok🤣 sijui western wapo na watsapp china ana wechat🤣, western ana ebay na amazon china ana alibaba🤣 . R&D za universities za western au makampuni ya US ni balaaaaa. R&D za kampuni za kichina mainly hulenga kupunguza gharama, na kuangalia alternative raw materials ili gharama ishuke then wapate kushindana na bidhaa za western🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom