Chongolo: Mbowe ana wajomba zake Nyeri na Zitto baadhi ya baba zake wanakaa Bukavu

Chongolo: Mbowe ana wajomba zake Nyeri na Zitto baadhi ya baba zake wanakaa Bukavu

Namsikiliza hapa Katibu wangu redioni anasema suala la Mama Samia kuwa na wajomba sehemu nyingine ya dunia sio kubwa Kama linavyotaka kuaminishwa.

Ameenda mbali na kusema mababu zake Zitto wakati wanahamia Kigoma wakitokea Bukavu DRC baadhi ya ndugu zao walibaki huko na wanatembeleana mara kadhaa.

Kwa Upande wa Mbowe amedai pia ujombani kwake Wana asili ya Nyeri nchini Kenya na hata akiwa Kenya huwa hakai hotelini, huwa anakaa nyumba za familia lakini bado alipata nafasi ya kuombea urais.

Amedai wapinzani wafanye kazi waache kutweet vitu vidogo vidogo.
Hamkutenda Haki kabisa kutokwenda Kumzika Mwendakuzimu kwao Burundi
 
Kama kweli katibu kasema hivyo , ni aibu sana na amepwaya sana kwenye hiyo nafasi ,
Bora wangesema woropokaji Kama yule wa dodoma na yule Geita
Aonywe mapema aachane na siasa za kijinga
Katibu wa chama anatakiwa aongelee Mambo makubwa na ya maana yenye maslahi ya kitaifa
 
Yaani Tanzania wahamiaji kuanzia wamakua wa Msumbiji akina Membe na Nape Nnauye na Wabembe wa kongo akina Zitto Kabwe nk ndio wanajifanya wazalendo sana kuliko wazawa
 
Halafu bado mnawalipa TISS WA kazi gani sijui? Nawaambia siku zote taasisi yenye shida kubwa nchi hii si Polisi ni TISS. Kuwa kiongozi wa nchi si Jambo dogo, Leo tunafikia kuwa na Kiongozi wa nchi mwenye ukoo mkubwa nje ya nchi kuliko nchini. Tusisingizie Obama na Marekani, hao vetting yao Inajulikana ilivyofanyika na kabla hata Obama hajaja Kenya dunia yote ilijua kuna Bibi na shangazi yake. Leo Sisi tunashitukizwa Kwa ziara ya Kwa Mjomba?
Umeshtukizwa nini acha uongo bibie, itakuwa umepitwa sehemu. Hii habari inafahamika kwenye public tangu wakati wa Jiwe. Alipokutana na viongozi fulani wa Oman pale Ikulu, aliwachomekea. Aliwaambia kwamba Makamo wa Rais amemtuma Oman kumuwakilisha na anajua kwamba kule kuna wajomba zake.
View attachment 2265433
View attachment 2265440
 
Namsikiliza hapa Katibu wangu redioni anasema suala la Mama Samia kuwa na wajomba sehemu nyingine ya dunia sio kubwa Kama linavyotaka kuaminishwa.

Ameenda mbali na kusema mababu zake Zitto wakati wanahamia Kigoma wakitokea Bukavu DRC baadhi ya ndugu zao walibaki huko na wanatembeleana mara kadhaa.

Kwa Upande wa Mbowe amedai pia ujombani kwake Wana asili ya Nyeri nchini Kenya na hata akiwa Kenya huwa hakai hotelini, huwa anakaa nyumba za familia lakini bado alipata nafasi ya kuombea urais.

Amedai wapinzani wafanye kazi waache kutweet vitu vidogo vidogo.
Lakini mbowe na zitto hawajawahi kutumia rasilimali za nchi kwa ajili ya kwenda kusalimia wajomba zao na ikulu kupiga piga na kututangazia, pia hawajawahi kuwafurusha watanzania kwenye maeneo yao kwa ajili ya kuwagawia wajomba zao sehemu ya tanzania
 
mtu wa Kigoma muulize kabila akikwambia ni mmanyema huyo ukoo wake nusu uko Congo DR au Burundi!! Zitto hawezi kuwa exceptional! ukitaka kuamini chukueni simu yake muone wajomba zake wako wapi!!Mbona pale Kigoma sio stori watu wanaenda kwao DR Congo na Burundi na wa huko wanakuja Kigoma na maboti tu tena bila passport na wanakaa muda wanaotaka na kurudi kwao!

Ila turudi nyuma wa Kilimanjaro kwao Kenya, Mbeya sijui Mbamba Bay kwao nje, wa Ruvuma kwao nje, Tanga kwao nje, Rukwa kwao nje, Kibondo kwao nje, Bukoba kwao nje, Wajaluo?Wanyasa? Wamakonde? Wadigo?Wangoni?Barbaig? Wamasai kwao wapi? nusu ya ukoo zao ziko nchi jirani! Tanga watu wengi nusu ya ndugu zao wako Mombasa na ni raia wa Kenya!na sio stori Tanga mabasi kila siku yanajaza kwenda na kurudi Mombasa!!

Hivi nani ni mtanzania halisi? tuanzie hapo! labda mi naona Ndugai peke yake kutoka kwa wagogo walio katikati ya nchi ndio raia OG na ndo maana Ndugai ana uchungu wa kweli kweli na akakataa "nchi yake" isiuzwe kwa mikopo isiyo na mwelekeo!
"Dhambi ya ubaguzi ni sawa na Kula nyama ya mtu" mkianza izo tabia hamtabaki salama na wanaoharibu hii nchi ni hawa chawa na viongozi wao
 
Halafu bado mnawalipa TISS WA kazi gani sijui? Nawaambia siku zote taasisi yenye shida kubwa nchi hii si Polisi ni TISS. Kuwa kiongozi wa nchi si Jambo dogo, Leo tunafikia kuwa na Kiongozi wa nchi mwenye ukoo mkubwa nje ya nchi kuliko nchini. Tusisingizie Obama na Marekani, hao vetting yao Inajulikana ilivyofanyika na kabla hata Obama hajaja Kenya dunia yote ilijua kuna Bibi na shangazi yake. Leo Sisi tunashitukizwa Kwa ziara ya Kwa Mjomba?
Ni uvivu wa kusoma history au ni hasadi na udwanzi? Hebu tumieni vyema neema ya akili Mliyopewa na Mola
 
Katibu Mkuu wa hovyo sana kuwahi kutokea pale Lumumba.
 
Mtu kuwa na ndugu nje ya nchi imekua kosa?

Dunia ya leo inabidi kila mtu awe na uraia pacha sio ndugu tu. Kwa akili hizi TZ bado sanaaaaa, hili li nchi bado watu wake wapo zama za ujima kabisa
 
Siasa hizi
2010 kuna Vibabu vya Mchongo viliigiza vinatoka Malawi Lilongwe eti vimeenda Kilosa kumtafuta Mjukuu wao anaitwa Mustafa Mkulo …wakati huo Mkulo ni Waziri wa Fedha

eti aliingia Tanzania na Marehemu Mtoto wao akiwa na Mjukuu wao ambae ndio Mustafa

alipopoteza uwaziri na vile vizee vikayayuka
Duh!
 
Labda Ndugai na Palamagamba kwa kuwa wanatokea katikati ya Nchi

Hayati Iddy Simba aliwahi kuzushiwa Mrundi na mashhidi wa Uongo wakataja hadi nyumba aliyozaliwa Bujumbura wakati ni mzaliwa wa Kigamboni
Wengi ni wahamiaji haramu..VP Mpango alipopata Umakamu Rais alipongezwa na Warundi Tena na Serikali yao kabisaa..

Tukitafutana hapa ,wenye Nchi tuko wachache sana.
 
Back
Top Bottom