Dar: Mvua kubwa sana imenyesha usiku wa kuamkia leo 21/01/2024

Dar: Mvua kubwa sana imenyesha usiku wa kuamkia leo 21/01/2024

kijiografia na kitaalamu kwa kina cha bahari ya hindi na kwa jiografia ya jiji la dar es salaam hakuna siku ambayo tsunami itaikumbuka. rejea kwa huyo nabii wako na ukamwambie kuwa he's a damn fool sawa?
Kwa sababu ya kina naweza kubaliana na wewe japo sijui usahihi wa vipimo vya kina kwa upande wetu! Kijiografia hapo sijakupata vzr
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja. Mvua kubwa sana inanyesha mahali hapa sijapata kuona. Haki tangu nizaliwe sijawahi kushuhudia mvua kubwa kiasi hiki.

Serikali ijiandae kukabiliana na adhari za mafuriko zitakazsababishwa na mvua hii kwani kadri muda unavyoenda mvua inazidi kuongezeka

Mara ya mwisho mvua iliponyesha ilingo'a madaraja na kuua watu watatu. Safari hii tujiandae kwa maafa zaidi.

Tuambie mahali ulipo hali ikoje na nini tutarajie baada ya mvua hii.

Nawasilisha.

UPDATES
Mawasiliano kati ya Tegeta na Kunduchi yamekatika baada ya daraja la Kunduchi-Mtongani kukatika. Magari, nyumba na mali za raia zimesombwa na maji. Nguzo za umeme zimeanguka na baadhi ya raia wamefariki. Tatizo watu wamejenga karibu na mto kwa kupewa vibali na maofisa ardhi wa serikal.

Hadi sasa mvua inaendelea kunyesha baadhi ya maeneo hapa Dar. Serikali itoe tahadhari kwa wananchi na ichukue hatua kukabiliana na mafuriko.

Nitaendelea kuwapa updates na picha kadri nitakavyozipata.........
Heng Over
 
1h non stop
 

Attachments

  • 20240121_083322.jpg
    20240121_083322.jpg
    930.3 KB · Views: 4
  • 20240121_083308.jpg
    20240121_083308.jpg
    713.8 KB · Views: 3
Back
Top Bottom