DART Special Thread: Tunaomba Maoni Ushauri, Malalamiko, Pongezi na Mapendekezo kuhusu Mabasi ya Mwendokasi

DART Special Thread: Tunaomba Maoni Ushauri, Malalamiko, Pongezi na Mapendekezo kuhusu Mabasi ya Mwendokasi

Niliuliza mustakbali wa malipo ya fidia kupisha ujenzi wa BRT phase 5.
Kila awamu ambayo mradi unapita na wananchi kutoa maeneo yao kupisha maendeleo watalipwa fidia kwa mujibu wa kanuni na taratibu za serikali. Ulishawahi kuona serikali imechukua eneo la mtu akadhulumiwa?
 
Kila awamu ambayo mradi unapita na wananchi kutoa maeneo yao kupisha maendeleo watalipwa fidia kwa mujibu wa kanuni na taratibu za serikali. Ulishawahi kuona serikali imechukua eneo la mtu akadhulumiwa?
Sijazungumzia kudhulumiwa. Uthamini umefanyika siku nyingi. Nataka kujuwa tu malipo yatafanyika lini au zoezi halipo tena ili tupange mambo ya maboresho ya nyumba zetu.
 
Kila awamu ambayo mradi unapita na wananchi kutoa maeneo yao kupisha maendeleo watalipwa fidia kwa mujibu wa kanuni na taratibu za serikali. Ulishawahi kuona serikali imechukua eneo la mtu akadhulumiwa?

Swali:

Kwanini magari huwa yamepaki na Madereva wakiwa wanapiga story while Abiria wamepanga folen zaidi ya 45 minutes?

2. Why magari yasiwe yanapaki then Abiria wanaingia na wakiwa level siti basi linaondoka linakuja kupaki lingine?

3. Kwanini Gari linatoka posta likiwa tupu na
kwenda kupaki ubungo ? Why lisibebe Abiria ambao wanaishia ubungo?
 
Sijazungumzia kudhulumiwa. Uthamini umefanyika siku nyingi. Nataka kujuwa tu malipo yatafanyika lini au zoezi halipo tena ili tupange mambo ya maboresho ya nyumba zetu.
Fika Ofisini Ubungo Maji kwa maelezo zaidi mana kwenye threads kama hizi hatutaelewana, ofisi zipo wazi na majibu yote yanapatikana.
 
Tunaendelea kuwasisitiza abiria wetu kuachana na mazoea ya kutumia tiketi za karatasi kwani zinachafua mazingira na kupoteza muda kwa sasa tumezindua huduma ya Kadi janja ambazo zinapatikana katika vituo vikuu vya Kimara, Morocco,Gerezani, Kivukoni na Ubungo terminal, matumizi ya Kadi yanasaidia pia tatizo la upatikanaji wa chenchi, okoa muda wa kupanga foleni kununua tiketi kuwa mjanja nunua kadi janja kwa Tsh 5,000/= tu ,ujanja ni kuchanja tuache mazoea. Ikumbukwe awali malalamiko ya kurudishwa kwa huduma ya Kadi yalikua makubwa mno sasa zimekuja zitumike, na itafika wakati tiketi za karatasi haziatumika tena hivyo wakati ni sasa hujachelewa.
 
Kwanini mnanunuwa mabasi ya gas ya gharama kubwa kuliko kununuwa nabasi ya umeme ya kichina na sasa tuna umeme wa kutosha?
 
Tunaendelea kuwasisitiza abiria wetu kuachana na mazoea ya kutumia tiketi za karatasi kwani zinachafua mazingira na kupoteza muda kwa sasa tumezindua huduma ya Kadi janja ambazo zinapatikana katika vituo vikuu vya Kimara, Morocco,Gerezani, Kivukoni na Ubungo terminal, matumizi ya Kadi yanasaidia pia tatizo la upatikanaji wa chenchi, okoa muda wa kupanga foleni kununua tiketi kuwa mjanja nunua kadi janja kwa Tsh 5,000/= tu ,ujanja ni kuchanja tuache mazoea. Ikumbukwe awali malalamiko ya kurudishwa kwa huduma ya Kadi yalikua makubwa mno sasa zimekuja zitumike, na itafika wakati tiketi za karatasi haziatumika tena hivyo wakati ni sasa hujachelewa.
Makaratasi ni biodegradable hayachafui mazingira, labda ulete sababu nyingine.
 
Tunaendelea kuwasisitiza abiria wetu kuachana na mazoea ya kutumia tiketi za karatasi kwani zinachafua mazingira na kupoteza muda kwa sasa tumezindua huduma ya Kadi janja ambazo zinapatikana katika vituo vikuu vya Kimara, Morocco,Gerezani, Kivukoni na Ubungo terminal, matumizi ya Kadi yanasaidia pia tatizo la upatikanaji wa chenchi, okoa muda wa kupanga foleni kununua tiketi kuwa mjanja nunua kadi janja kwa Tsh 5,000/= tu ,ujanja ni kuchanja tuache mazoea. Ikumbukwe awali malalamiko ya kurudishwa kwa huduma ya Kadi yalikua makubwa mno sasa zimekuja zitumike, na itafika wakati tiketi za karatasi haziatumika tena hivyo wakati ni sasa hujachelewa.

Kama sina haraka huwa natumia basi la mwendokasi.Unakuta abiria wamerundikana lakini mabasi yapo ila hayapakii ama yanaondoka kituoni matupu na kuwaacha abiria.

Mwendo Kasi yalianza vizuri ila hivi Sasa ni aibu sana. Haya wangepewa wakenya ama wanyarwanda wayasimamie tusingeona huu ujinga
 
Kwanini mnanunuwa mabasi ya gas ya gharama kubwa kuliko kununuwa nabasi ya umeme ya kichina na sasa tuna umeme wa kutosha?
Mabasi yanayotarajia kuja kwa Awamu ya Pili kuelekea Mbagala ni ya kutumia gesi asilia ambayo inapatikana hapa nchini kwa gharama nafuu sana ndiomaana unaona hata watu binafsi wanachangamkia fursa kwa kubadilisha mifumo yao ya awali ya mafuta na kutumia gesi asilia CNG, aidha kwenye awamu nyingine tutakuwa na options zote yaani gesi asilia pamoja na umeme na tutakwenda mbali zaidi hata kutumia umeme wa jua, kimsingi suala la nishati ondoa shaka kwani Tanzania sio kijiji inakwenda na wakati kama dunia inavyotaka sambamba na kuhakikisha utunzaji wa mazingira ndio kipaumbele.
 
Kama sina haraka huwa natumia basi la mwendokasi.Unakuta abiria wamerundikana lakini mabasi yapo ila hayapakii ama yanaondoka kituoni matupu na kuwaacha abiria.

Mwendo Kasi yalianza vizuri ila hivi Sasa ni aibu sana. Haya wangepewa wakenya ama wanyarwanda wayasimamie tusingeona huu ujinga
Matatizo ya mrundikano wa abiria yanatokana na uchache wa Mabasi tuliyonayo kwa sasa hata hivyo kama ni mfuatiliaji mzuri wa mradi huu kuna jitihada kubwa zinafanyika kuhakikisha wanapatikana watoa huduma ya mabasi zaidi ya mmoja jambo ambalo litaleta ushindani na kuboresha huduma. Pia kwakuwa tumeanza kutumia mfumo wa kadi janja suala hili litafuatiwa na matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa kuongozea magari Inteligency Transport Systerm (ITS) huu ndio utakuwa mwarobaini wa upangaji wa mabasi kulingana na mahitaji, mfumo huo utakuwa na uwezo wa kuangalia ni vituo vipi vina abiria wengi na uhitaji wa namba ya mabasi kwa wakati husika. Hatujafikia hatua ya kudharau Tanzania yetu na kujilinganisha na wageni na nchi jirani jitihada kubwa sana zinafanyika kuhakikisha usafiri huu unakuwa wa kisasa na kimbilio kwa wote kwa kutatua changamoto zote zilizopo, ni suala la muda tu tuvute subra.
 
Makaratasi ni biodegradable hayachafui mazingira, labda ulete sababu nyingine.
Inategemea aina ya karatasi zinazotumika sio kila karatasi ni bio-degredable, pia kama wewe ni mtumiaji wa huduma zetu utaona uchafuzi ninaouzungumzia hapa hasa nyakati za jioni kwenye vituo vikuu kama vile Gerezani na Kimara, hakuna nchi iliyoendelea duniani ambayo bado inatumia makaratasi hata risiti za ununuzi wa bidhaa zikuhizi nyingi ni za kidijitali na lengo kuu hasa ni kuhifadhi mazingiza.
 
Tunaendelea na zoezi letu la uhamasishaji pamoja na kuuza kadi janja za Mwendokasi, leo tupo Kivukoni karibuni sana tuwahudumie, ujanja ni kuchanja karatasi zimepitwa na wakati.
 
Tunaendelea na zoezi letu la uhamasishaji pamoja na kuuza kadi janja za Mwendokasi, leo tupo Kivukoni karibuni sana tuwahudumie, ujanja

Tunaendelea na zoezi letu la uhamasishaji pamoja na kuuza kadi janja za Mwendokasi, leo tupo Kivukoni karibuni sana tuwahudumie, ujanja ni kuchanja karatasi zimepitwa na wakati.
Kadi yangu ya zamani inasalio la kutosha, Na haitumiki tena. Pia zile kadi zipo nyingi mtaani. Je hamuoni umuhimu wa kutafuta namna bora ya matumiz ya kadi zile? Au kwann mfumo wenu msiufunganishe na N card inayotumika maeneo mengi??
 
Kadi yangu ya zamani inasalio la kutosha, Na haitumiki tena. Pia zile kadi zipo nyingi mtaani. Je hamuoni umuhimu wa kutafuta namna bora ya matumiz ya kadi zile? Au kwann mfumo wenu msiufunganishe na N card inayotumika maeneo mengi??
Kadi ya zamani haiwezi kutumika kwa sasa kwani mfumo unaotumika kwa sasa hauendani na ule wa awali, aidha kadi janja hii ina teknolojia mpya ya kisasa kabisa tofauti na ile ya zamani, ndani yake tunaweza kuunganisha na mifumo mingine hata minne (4) ya usafiri wa umma, inachotakiwa ni sera tu ya kuunganisha na mifumo mingine ili iweze kutumika kadi hii hii. Tunawashauri mnunue kadi hii na kuanza kuzoea kuitumia kwani hivi karibuni tunatarajia kusitisha huduma ya tiketi za karatasi.
 
sababu kubwa ya kutumia card ni kuepuka serikali kupoteza mapato kwa watu kuiba hela wanazokusanya cash huyu aliepewa kuongoza na kujibu comment za DART jamiiforum naona hana huelewa vizuri.kuchafua manzingira kwa karatasi ni sababu ndogo sana .
Makaratasi ni biodegradable hayachafui mazingira, labda ulete sababu nyingine.
 
sababu kubwa ya kutumia card ni kuepuka serikali kupoteza mapato kwa watu kuiba hela wanazokusanya cash huyu aliepewa kuongoza na kujibu comment za DART jamiiforum naona hana huelewa vizuri.kuchafua manzingira kwa karatasi ni sababu ndogo sana .
Ni mjinga mmoja. Inaonesha hiyo kampuni wamejazana wajinga na wezi.

Ndiyo maana wameiuwa mapema, kampuni inayoingiza pesa kila siku ya Mungu.
 
Tunawashukuru abiria wetu wanaoendelea kununua na kutumia kadi janja za Mwendokasi, tumeendelea kufunga vifaa (validators) kwenye Mabasi yetu ya Mbezi na Mloganzila hivyo tunatarajia baada ya muda mfupi ujao nao wataanza kutumia kadi badala ya tiketi za karatasi. Kwa maoni ama ushauri usisite kuwasiliana nasi Bure kwa namba 0800110147. Ama kwenye mitandao yakijamii ya Twitter,Facebook,Instagram, Thread na Linkedlin kwa anuani ya @ DART Mwendokasi.
 
Back
Top Bottom