Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

Bilashaka wewe utakuwa ni wakala wa Shetani..

Kwaiyo katika kufikilia kwako kote, ndiyo ukaona dini ndiyo tatizo kubwa katika maendeleo ya afrika.

Nchi nyingi duniani zimepokea dini hizo kama zilivyopokelewa afrika lakini zina maendeleo makubwa sana. Mfano, Brazil, Turkey, n.k

Tatizo haliwezi kuwa dini, kuna mambo makubwa muhimu mawili ya kuangalia hapa kama;
- Mfumo wa elimu ( Quality people )
- Mfumo wa Utawala ( Quality leadership )

Uwezi kuwa na taifa bora kama hauna watu bora na viongozi bora !!
Mawazo ya mkoloni bado yanaishi kwenye kichwa chako
 
Mawazo ya mkoloni bado yanaishi kichwani kwako. Jielimishe kuhusu dini za waafrika. Utapata mengi mazuri positive kuliko negativity uliofundishwa na dini za wakoloni. Wakoloni wangekua wana nia nzuri na dini. Wasingeweka rangi kwenye dini. Maana kuanzia malaika.....etc wote ni wazungu. Amka my african brother. Waafrika tulikua tunamjua mungu wa kweli na kuabudu hata kabla ya wazungu. Usidharau kila kitu cha muafrika. Unadharau kwa sababu historia nzuri ya muafrika umefichiwa toka utotoni.
duuu! Aisee kumbe dini ni mawazo ya mkoloni pole Sana kwakua bado hujui hata dini ni Nini?. Nakusema tumefichwa toka utotoni. Si dhani Kama kunamazuri makubwa ambayo yalikuwepo kwenye dini ya sisi waafrika ambayo tumefichwa. Wakati masalia ya hii dini bado yapo na tunayaona na kuyasikia pia. Hivi labda nikuulize unavyoona albino wanauwawa watoto wanatolewa Sehemu za Siri, watu wanarogana, watu wanalala makaburini, watu wanakosana, magonjwa yanapuziwa kwa imani potofu,. Mimi ni kwambie tu huna mawazo yoyote kwenye hili swala zaidi ya kupotosha jamii.


Wewe na mtoa maada hamjui dini ya mwafrika wala dini inayomuhusu mungu Kama mnajua moja wapo Basi ni lazima iwe dini ya waafrika ambayo ilikua ni chukizo mbeleni mwa macho ya mbwana na Kama upo huko kweli Basi toka haraka kabla gazabu ahijakuwakia
 
1. Ni vizuri tukajenga hoja kwa ushahidi (with cogent justification). Kwa vile umesema hapa Afrika kuna dini kubwa mbili - Uislamu na Ukristo - na kwa vile mimi ni Mkatoliki (Mkiristo), nimeamua nitoea mifano ya baadhi ya waumini wa Kikristo (bofya hapa List of Christians in science and technology - Wikipedia) waliaomini uwepo wa Mungu kupitia imani yao ya kuwa Wakristo, waliweza kugundua mambo mbalimbali ambayo sayansi na teknolojia tunazotumia zimetokana nayo au baadhi ya hayo mambo.
2. Kwa msingi huu siwezi kuamini kwamba kama hawa watu waliweza kuamini na kugundua mambo waliyogundua, kwa nini sisi katika kuamini katika hiyo dini yao kutufanye kudumaze ufahamu wetu kama kichwa chako cha habari kinavyoeleza?
3. Kutokana na hili, siwezi kuamini kwamba kuamini katika dini ndiko kunakodumaza ufahamu wa Mwafrika na hujatoa ushahidi wowote wa kimaandishi jinsi dini inavyodumaza ufahamu wa Mwafrika isipokuwa umetumia hoja 'zoazoa' (blanket/wholesale conclusion) bila kuangalia mtiririko wa 'premises' zako.
nadhani hujanielewa hapa naongelea dini ilivyochangia kudumaza ufahamu wa mwafrika.

kwani kwenye hiyo list kuna mwafrika hata mmoja?

au kuna mwafrika yoyote mkristo aliyeugundua chochote chenye faida afrika?
kama wapo wataje hapa.
 
Blah blah hizi,ujinga na umasikini wenu unautupia kwenye dini. Kuna watu wanaamini ushirikina kama waafrika? afrika kuna watu badala ya kwenda hospitali wanaenda kwa waganga na kuzidisha maradhi yao na hadi kufa halafu ujinga kama huo wa waafrika unaenda kutupia lawama dini? Waarabu wameshika dini kweli kweli kuliko sie hata hatuwafikii ila bado wanatuzidi uwezo.
 
Blah blah hizi,ujinga na umasikini wenu unautupia kwenye dini.
Soma kwa makini hakuna sehemu nimeandika ujinga na umasikini nimeutupia kwenye dini bali nimeandika dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika.

Maana yake mwafrika alikuwa na ufahamu duni kabla ya dini.
Kuna watu wanaamini ushirikina kama waafrika?
Ndio maana nimesema dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika.
afrika kuna watu badala ya kwenda hospitali wanaenda kwa waganga na kuzidisha maradhi yao na hadi kufa halafu ujinga kama huo wa waafrika unaenda kutupia lawama dini?
Kwa hiyo unataka kuniambia hakuna waafrika wanaokwenda kwa mashekhe na wachungaji ili waombewe ila hawaponi na mwisho wake wanakufa?
halafu ujinga kama huo wa waafrika unaenda kutupia lawama dini?
Kwenda msikitini au kanisani kuombewa ili uwe tajiri na upone HIV huo sio ujinga?
Waarabu wameshika dini kweli kweli kuliko sie hata hatuwafikii ila bado wanatuzidi uwezo.
Hapa kwa asilimia 90% naongelea waafrika weusi Sasa wale sio waafrika weusi.
 
nadhani hujanielewa hapa naongelea dini ilivyochangia kudumaza ufahamu wa mwafrika.

kwani kwenye hiyo list kuna mwafrika hata mmoja?

au kuna mwafrika yoyote mkristo aliyeugundua chochote chenye faida afrika?
kama wapo wataje hapa.
Na ukikuta yupo utafanya nini?
 
nadhani hujanielewa hapa naongelea dini ilivyochangia kudumaza ufahamu wa mwafrika.

kwani kwenye hiyo list kuna mwafrika hata mmoja?

au kuna mwafrika yoyote mkristo aliyeugundua chochote chenye faida afrika?
kama wapo wataje hapa.
Kuna hii list ya wanasayansi na educationists Waafrika (bofya hapa List of African educators, scientists and scholars - Wikipedia). Ina mchanganyiko ya wanasayansi na educationists wenye imani ya dini na wengine hapana. Sijui utasemaje kwa hawa!
 
Wee jamaa unjikutaga great thinker kumbe huna lolote. Nilikuwaga nakudhania hivyo zamani lkn nilipokugundua nikakudharau mazima
Ukunidharau haipunguzi chochote kwangu ujue, sana utapata vidonda tumbo tu. If yako ndio naion hapa leo
 
Ninukuu maneno ya rais Xi Jin Ping

1. The only thing black man has inherited from Arab and European colonization is the religion that he practices and that’s exactly what the colonizers wanted.2. Notice that in black countries, the education is a disaster, the administration is corrupt, health is deplorable, but relagion is doing wonderfully well.

3. Black people rebels against everything Except religion. They even think they are more religious than those who brought them this concepts and that the colonizers are not good Christians.

4. Black people even claimed themselves to be original race of which JESUS Christ has descended. This is how black people stupidity can go.

5. Notice that any society that is full with superstitions. Religious indoctrination, lack of education and nationalism, is always ridden with violence.

Tafsiri isiyo rasmi

1. Kitu pekee ambacho mtu mweusi amerithi kutoka kwa ukoloni wa Kiarabu na Ulaya ni dini ambayo anafanya na ndivyo haswa wakoloni walivyotaka. Ona kwamba katika nchi nyeusi, elimu ni janga, utawala ni rushwa, afya ni mbaya, lakini dini linafanya vizuri sana.

3. Watu weusi wanaasi kila kitu Isipokuwa dini. Wanafikiri hata wao ni waumini kuliko wale waliowaletea dhana hizi na kwamba wakoloni sio Wakristo wazuri.

4. Watu weusi hata walidai wenyewe kuwa ni jamii asili ambayo YESU Kristo ameshuka. Hivi ndivyo upumbavu wa watu weusi wanaweza kwenda.

5. Ona kuwa jamii yoyote ambayo imejaa ushirikina. Ufundishaji wa kidini, ukosefu wa elimu na utaifa, daima hujaa vurugu.

Haya maneno yanafikirisha sana
Daahhh kwanini nilichelewa kuyaona maneno haya matukufu .... Binafsi mimi nilishajitoa kabisa katika ujinga wakuamini katika dini yoyote ile siingii kanisani wala msikitini nasitakagi kuusikia huo ujinga
 
Unachekewa kazini eti alikuwa anapiga maombi!! Kila kitu unamuachia Mungu! Ukipigwa shavu la kulia mgeuzie na shavu la kulia! Ndio mzungu!!! maisha ni haya : ukipigwa shavu la kulia rudisha katika shavu hilohilo mpaka meno yote yadondoke. Atashika adabu na maisha yanaendelea. Usiwe mtumwa wa dini!
 
Daahhh kwanini nilichelewa kuyaona maneno haya matukufu .... Binafsi mimi nilishajitoa kabisa katika ujinga wakuamini katika dini yoyote ile siingii kanisani wala msikitini nasitakagi kuusikia huo ujinga
Umenifurahisha sana ulivyosema matukufu.

Ila yana ukweli mwingi sana ndani yake ingawa wafia dini watabisha kama alivyosema Xi
 
Umenifurahisha sana ulivyosema matukufu.

Ila yana ukweli mwingi sana ndani yake ingawa wafia dini watabisha kama alivyosema Xi
Walk brainwashed wanapaswa kuhurumiwa .... Ila dini ni ulevi 1 mbaya sana 😂
 
Du lakini inafikirisha. Kwanini rangi nyeusi iwakilishe jambo baya, msiba, uzamani, uovu, hata orodha ya wabaya wanaita black list. Je giza au weusi ni kiwakilishi cha ubaya? Rangi yetu sie weusi kweli ina maanisha laana au ubaya? Inafikirisha ujue!
 
Straight to the topic.

Africans wengi wanaamini kwenye dini kuliko chochote kile hapa duniani.

Na watu wanaomini kwenye dini wanaamini wapo hapa duniani ili kumuabudu mungu tu na si kingine.

Well hapa kwetu africa kuna dini kubwa mbili yaani uislamu na ukristo.

Na kwenye hizo dini kubwa mbili kila mtu anajiona yuko sahihi na kitabu chake ni sahii na dini ndio sahihi.
Na dini nyingine zaidi ya kwake ni ya uongo wala si ya kweli.

Cha ajabu hizi dini sio za africa bali zinatoka nje ya africa. Unaona akili ya mwafrika ilivyo hapo?

Na cha kushangaza zaidi hizi dini kwa karibu asilimia 90% zinatoka kwa wakoloni walioivamia africa.

Na sio wakoloni tu waliotukandamiza watu weusi, hapana hata hizo dini zimekandamiza watu weusi.

Na bila shaka hizo dini zilikuwa na mipango ya muda mrefu kuanzia miaka 100 mbele ili zifanikiwe na kweli zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Kumbuka ukitaka kumteka mtu kwenye kila kitu basi anza kumteka ufahamu wake.

Dini za wakoloni ndio chanzo mojawapo leo tuko hapa.

**********

Binadamu unatakiwa uwe na uwezo wa kujitambua na kujielewa ili kuepuka kuendeshwa na hisia ila ukishindwa kujitambua na kujielewa basi tegemea uwe controlled na hisia na hiyo ni sign ya ukosefu wa hivyo vitu hapo juu na vingine vya ziada yaani

=Kujitambua
=Kujielewa


Unajua kuna vitu vya kuchagua na kuvifanya au kuvitenda na kuna vitu vya kuacha. Hayo yote yanategemea na ufahamu wako.

Sasa huyu muafrika kwa yote yale aliyofanyiwa kuteswa, kudhihakiwa, kudharirishwa na mengine mengi mabaya.
Still mwafrika huyu alikubali kupokea dini hizi za mkoloni na kukubali kuwa ndio ufahamu wake na kila kitu kwenye hiyo dini kipo sahihi na hatoruhusiwa kupinga au kuhoji chochote juu ya hiyo dini au atalaaniwa.

Mwafrika huyu mweusi amekubali kupokea dini ambayo.
=Amepewa na watu weupe waliomfanyia kila aina ya ubaya na ukatili.
=Kila mtume kwenye hizo dini ni mweupe
=Hata mungu wa kwenye hizo dini katuma watu weupe waje kutangaza hizo dini weusi sijui kwanini kawaacha
=Alikubali kupokea dini ambazo mtu mweusi ni nembo ya shetani na nyeupe ni nuru ya malaika.
(Huo ni ubaguzi pure)
=Dini ambazo inasema mweusi amelaaniwa nk

Hapohapo Yaani mwafrika yupo tayari
=Akuue
=Akutukane
=Akudharirishe
=Akudharau
=Akupige
=Akudhihaki au chochote kile kibaya mwafrika atamfanyia mwafrika mwenzake sababu ya dini aliyopewa na mtu aliyemtesa, kumtukana, kumdhihaki na kumdharirisha.

Still mwafrika mweusi huyohuyo anaamini yeye amelaaniwa kwa rangi yake na yeye si chochote mbele ya mweupe kwani mweupe amebarikiwa.
Hapo hakumbuki kama hiyo dini kampa huyohuyo mweupe aliyemtesa na kumpiga mijeredi ya mgongo ili asiangushe pembe za tembo.

Yes huyo ndio mwafrika wa africa usijali hata humu watajitokeza watu kama hao. Asilimia kadhaa za hao watu wapo humu jf.

Na hapo mwafrika huyo bado ataendelea kumchukia mwafrika wa dini nyingine kivyovyote vile.

*******

Labda mababu zetu walikosa hivyo vitu yaani kujielewa na kujitambua hivyo wakawa wanaendeshwa na hisia bila wao kujua hivyo ikawafanya wasie na akili wala maarifa ya kueleweka.
Lakini binadamu anabadirika kadri muda unavyozidi kwenda
Hivyo hata sisi tunaweza kubadirika na kuanza kujitambua na kujielewa na sio kuendeshwa na hisia tena au Africans itakuwa ngumu kubadirika.

kila kitu kimerahisishwa na hao wazungu ambavyo si vya kupotosha na kukandamiza kama dini hivyo tunaweza kutumia hivyo vitu vizuri kuweza kubadirika na kujiongeza na sio kuendelea kubomoka.

Kumbuka nilikwambia binadamu anatakiwa awe na sifa ya kujitambua na kujielewa ili aisendeshwa na hisia au imani hivyo ni lazima kujua kipi cha kuchukua na kuacha na sio kupelekeshwa kama fuso bovu na hizo hisia kama mababu zetu waliokubali hizi imani.

*******

SASA HII IMEATHIRI VIPI UFAHAMU AU UBONGO WA MWAFRIKA.

=Well baada ya hapo mwafrika akawa muoga wa kuhoji "kwanini. sababu ya kuogopa kukufuru na kulaaniwa alafu alishaalaniwa mara kwanza.
=Mwafrika akawa mvivu wa kufikiri kwa kusema kila kitu anapanga mungu hivyo huyo mwafrika kubweteka chini akitegemea mungu atamfanya apate anachokitaka huku amekaa tu chini ya mwembe. Hadi leo hawa watu wapo na ndio masikini wa kwanza yaani mafukara.
=mwafrika huyu anaamini wazungu ndio wamebarikiwa na ndio maana wameendelea.
=mwafrika ubongo wake wote umelala sababu ameaminishwa yeye si chochote kwani amelaaniwa na ndo maana rangi yake nyeusi.
=mwafrika anaamini duniani anapita tu na yupo hapa kumuabudu mungu tu.
Hivyo huyo mwafrika kuendelea kufa masikini na kuendelea kuishi na changamoto sababu yeye kaja kumuabudu mungu tu na kuijaza dunia na si kingine wakati huo weupe wakiendelea kukua kila siku.
=Mwafrika anaogopa kutumia na kutegemea ufahamu wake sababu dini imemwambia asitumie ufahamu wake sababu mungu yupo.
Na anashindwa kujiuliza vitu vyote anavyotumia vimetokana na ufahamu.
=Na watu kugombana sababu ya dini iliyoletwa na weupe hata huyo mweupe akiona anaweza shangaa akili zao zilivyo za ajabu hao Africans wakimpigania mtume mweupe wa kwenye kitabu.

Na mpaka leo africa hatuna kitu ambacho kimetokana na sisi wenyewe, labda kama wangetuacha kipindi kike labda tungechelewa lakini tungepata ufahamu taratibu kuliko kutuharibu kabisa na hizi dini.

Mbona china wana dini zao lakini wana maendeleo makubwa sana na ni wamoja tena wana ufahamu mkubwa ukilinganisha na sisi.

Africans hatuna umoja wala ushirikiano sababu tunachukiana na kubaguana kidini kwa dini ambazo zililetwa na watu kutoka nje kitu ambacho ni ujinga.

Najua wengi mmerukia mwisho sababu ndio tabia zenu za kutokupenda kushughulisha vichwa vyenu.
Sasa nakuambia popote utakapomtukana mtu yoyote sababu ya tofauti za kidini basi tambua hiyo dini si asili yako bali ulipewa na mweupe ili apate kukuendesha na kukucontroll so think again.

Nadhani baada ya hapo tutaacha kutukanana, kudhihakiana, kudharauriana, kubaguana sababu ya dini na hapo ndio mwanzo wa kujitambua.

na wote kuwa kitu kimoja kitu ambacho hakiwezekani.
NAITOSHE KUSEMA MTOA MADA UPO SAHIHI NA ASANTE SANA KWA KULETA HII TOPIC,

According to history hizi dini kubwa mbili hapa Africa zimeletwa na watu kutoka western/ European countries(ukristo) na Middle East countries (uislamu). Hawa watu kwa nyakati tofauti walitutawala na kuchukua rasilimali zetu kwa faida zao binafsi wali watesa sana Babu zetu walifanya kila wawezalo kutu kandamiza na kutu nyanyasa tukiwa katika ardhi yetu na machoni kwao mtu mweusi hakua mtu alikua ni kiumbe kisicho na samani kabisa na hii mpaka leo tunaiona.

Swali la kujiuliza kwa mapenzi gani walio nayo kwetu sisi weusi na huruma ipi walio nayo kwetu mpaka watufundishe mambo mazuri kumuhusu mungu ambae hatumuoni???? Hivi kweli Quran na Bible vingekua na thamani kiasi hicho kwa walivyo kua na roho mbaya ya kumtesa na kumuu mtu mweusi akiwa katika ardhi yao wenge tukabidhi kweli??? Hivi kweli mambo ya Heaven na aljana kama yange kua ya ukwel wangetufundisha kweli jinsi ya kwenda uko??? Kama kweli wana moyo mzuri kiasi hicho kwanini hawakuifanya hii dunia kuwa pepo kwa kuishi kwa misingi ya haki.

Ukwel mchungu lakini haina budi kuusema kwa yeyeto mtu mweusi anae usoma ujumbe huu naomba utambue yakua White people and Arabians wengi wao hawatupendi sisi weusi hakuna ethnicity yeyeto ambayo ina mapenzi ya kweli ma mtu mweusi hata wachina au wahindi na kama hawatupendi na mifano iko wazi leo inakuaje watueleze na kutufundisha mambo mazuri ya mungu kiukwe hii haingii akilini hata kidogo yani kwa mfano unaishi na mtu ambae humpedi na unatafuta kila njia ya kumuibia na kumkandimza kiuchumi alafu una mwambia usiangalie sana ya dunia duniani tunpita fanya mema uende kweny uzima wa milele [emoji15][emoji15][emoji15] shame on us black people.

Nimalizie kwa kusema hizi DINI zimeletwa na walio zileta walizieleta kwa sabau zao na faida zao wao wenyewe, kama wewe ni muislamu unamuita mkristo kafiri my brother/ sister wewe ni mpuuzi namba moja au kama wewe ni mkristo unamuita muislmu mtu wa dunia na wewe pia ni mpuuzi kwa sababu kabla ya wageni kuja na kuzileta hizi dini mlikua mnaishi vzr kwa amani na upendo bila kuitana hayo majina. WAKE UP AFRICANS
 
NAITOSHE KUSEMA MTOA MADA UPO SAHIHI NA ASANTE SANA KWA KULETA HII TOPIC,

According to history hizi dini kubwa mbili hapa Africa zimeletwa na watu kutoka western/ European countries(ukristo) na Middle East countries (uislamu). Hawa watu kwa nyakati tofauti walitutawala na kuchukua rasilimali zetu kwa faida zao binafsi wali watesa sana Babu zetu walifanya kila wawezalo kutu kandamiza na kutu nyanyasa tukiwa katika ardhi yetu na machoni kwao mtu mweusi hakua mtu alikua ni kiumbe kisicho na samani kabisa na hii mpaka leo tunaiona.

Swali la kujiuliza kwa mapenzi gani walio nayo kwetu sisi weusi na huruma ipi walio nayo kwetu mpaka watufundishe mambo mazuri kumuhusu mungu ambae hatumuoni???? Hivi kweli Quran na Bible vingekua na thamani kiasi hicho kwa walivyo kua na roho mbaya ya kumtesa na kumuu mtu mweusi akiwa katika ardhi yao wenge tukabidhi kweli??? Hivi kweli mambo ya Heaven na aljana kama yange kua ya ukwel wangetufundisha kweli jinsi ya kwenda uko??? Kama kweli wana moyo mzuri kiasi hicho kwanini hawakuifanya hii dunia kuwa pepo kwa kuishi kwa misingi ya haki.

Ukwel mchungu lakini haina budi kuusema kwa yeyeto mtu mweusi anae usoma ujumbe huu naomba utambue yakua White people and Arabians wengi wao hawatupendi sisi weusi hakuna ethnicity yeyeto ambayo ina mapenzi ya kweli ma mtu mweusi hata wachina au wahindi na kama hawatupendi na mifano iko wazi leo inakuaje watueleze na kutufundisha mambo mazuri ya mungu kiukwe hii haingii akilini hata kidogo yani kwa mfano unaishi na mtu ambae humpedi na unatafuta kila njia ya kumuibia na kumkandimza kiuchumi alafu una mwambia usiangalie sana ya dunia duniani tunpita fanya mema uende kweny uzima wa milele [emoji15][emoji15][emoji15] shame on us black people.

Nimalizie kwa kusema hizi DINI zimeletwa na walio zileta walizieleta kwa sabau zao na faida zao wao wenyewe, kama wewe ni muislamu unamuita mkristo kafiri my brother/ sister wewe ni mpuuzi namba moja au kama wewe ni mkristo unamuita muislmu mtu wa dunia na wewe pia ni mpuuzi kwa sababu kabla ya wageni kuja na kuzileta hizi dini mlikua mnaishi vzr kwa amani na upendo bila kuitana hayo majina. WAKE UP AFRICANS
Maneno kuntu hayo
 
Straight to the topic.

Africans wengi wanaamini kwenye dini kuliko chochote kile hapa duniani.

Na watu wanaomini kwenye dini wanaamini wapo hapa duniani ili kumuabudu mungu tu na si kingine.

Well hapa kwetu africa kuna dini kubwa mbili yaani uislamu na ukristo.

Na kwenye hizo dini kubwa mbili kila mtu anajiona yuko sahihi na kitabu chake ni sahii na dini ndio sahihi.
Na dini nyingine zaidi ya kwake ni ya uongo wala si ya kweli.

Cha ajabu hizi dini sio za africa bali zinatoka nje ya africa. Unaona akili ya mwafrika ilivyo hapo?

Na cha kushangaza zaidi hizi dini kwa karibu asilimia 90% zinatoka kwa wakoloni walioivamia africa.

Na sio wakoloni tu waliotukandamiza watu weusi, hapana hata hizo dini zimekandamiza watu weusi.

Na bila shaka hizo dini zilikuwa na mipango ya muda mrefu kuanzia miaka 100 mbele ili zifanikiwe na kweli zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Kumbuka ukitaka kumteka mtu kwenye kila kitu basi anza kumteka ufahamu wake.

Dini za wakoloni ndio chanzo mojawapo leo tuko hapa.

**********

Binadamu unatakiwa uwe na uwezo wa kujitambua na kujielewa ili kuepuka kuendeshwa na hisia ila ukishindwa kujitambua na kujielewa basi tegemea uwe controlled na hisia na hiyo ni sign ya ukosefu wa hivyo vitu hapo juu na vingine vya ziada yaani

=Kujitambua
=Kujielewa


Unajua kuna vitu vya kuchagua na kuvifanya au kuvitenda na kuna vitu vya kuacha. Hayo yote yanategemea na ufahamu wako.

Sasa huyu muafrika kwa yote yale aliyofanyiwa kuteswa, kudhihakiwa, kudharirishwa na mengine mengi mabaya.
Still mwafrika huyu alikubali kupokea dini hizi za mkoloni na kukubali kuwa ndio ufahamu wake na kila kitu kwenye hiyo dini kipo sahihi na hatoruhusiwa kupinga au kuhoji chochote juu ya hiyo dini au atalaaniwa.

Mwafrika huyu mweusi amekubali kupokea dini ambayo.
=Amepewa na watu weupe waliomfanyia kila aina ya ubaya na ukatili.
=Kila mtume kwenye hizo dini ni mweupe
=Hata mungu wa kwenye hizo dini katuma watu weupe waje kutangaza hizo dini weusi sijui kwanini kawaacha
=Alikubali kupokea dini ambazo mtu mweusi ni nembo ya shetani na nyeupe ni nuru ya malaika.
(Huo ni ubaguzi pure)
=Dini ambazo inasema mweusi amelaaniwa nk

Hapohapo Yaani mwafrika yupo tayari
=Akuue
=Akutukane
=Akudharirishe
=Akudharau
=Akupige
=Akudhihaki au chochote kile kibaya mwafrika atamfanyia mwafrika mwenzake sababu ya dini aliyopewa na mtu aliyemtesa, kumtukana, kumdhihaki na kumdharirisha.

Still mwafrika mweusi huyohuyo anaamini yeye amelaaniwa kwa rangi yake na yeye si chochote mbele ya mweupe kwani mweupe amebarikiwa.
Hapo hakumbuki kama hiyo dini kampa huyohuyo mweupe aliyemtesa na kumpiga mijeredi ya mgongo ili asiangushe pembe za tembo.

Yes huyo ndio mwafrika wa africa usijali hata humu watajitokeza watu kama hao. Asilimia kadhaa za hao watu wapo humu jf.

Na hapo mwafrika huyo bado ataendelea kumchukia mwafrika wa dini nyingine kivyovyote vile.

*******

Labda mababu zetu walikosa hivyo vitu yaani kujielewa na kujitambua hivyo wakawa wanaendeshwa na hisia bila wao kujua hivyo ikawafanya wasie na akili wala maarifa ya kueleweka.
Lakini binadamu anabadirika kadri muda unavyozidi kwenda
Hivyo hata sisi tunaweza kubadirika na kuanza kujitambua na kujielewa na sio kuendeshwa na hisia tena au Africans itakuwa ngumu kubadirika.

kila kitu kimerahisishwa na hao wazungu ambavyo si vya kupotosha na kukandamiza kama dini hivyo tunaweza kutumia hivyo vitu vizuri kuweza kubadirika na kujiongeza na sio kuendelea kubomoka.

Kumbuka nilikwambia binadamu anatakiwa awe na sifa ya kujitambua na kujielewa ili aisendeshwa na hisia au imani hivyo ni lazima kujua kipi cha kuchukua na kuacha na sio kupelekeshwa kama fuso bovu na hizo hisia kama mababu zetu waliokubali hizi imani.

*******

SASA HII IMEATHIRI VIPI UFAHAMU AU UBONGO WA MWAFRIKA.

=Well baada ya hapo mwafrika akawa muoga wa kuhoji "kwanini. sababu ya kuogopa kukufuru na kulaaniwa alafu alishaalaniwa mara kwanza.
=Mwafrika akawa mvivu wa kufikiri kwa kusema kila kitu anapanga mungu hivyo huyo mwafrika kubweteka chini akitegemea mungu atamfanya apate anachokitaka huku amekaa tu chini ya mwembe. Hadi leo hawa watu wapo na ndio masikini wa kwanza yaani mafukara.
=mwafrika huyu anaamini wazungu ndio wamebarikiwa na ndio maana wameendelea.
=mwafrika ubongo wake wote umelala sababu ameaminishwa yeye si chochote kwani amelaaniwa na ndo maana rangi yake nyeusi.
=mwafrika anaamini duniani anapita tu na yupo hapa kumuabudu mungu tu.
Hivyo huyo mwafrika kuendelea kufa masikini na kuendelea kuishi na changamoto sababu yeye kaja kumuabudu mungu tu na kuijaza dunia na si kingine wakati huo weupe wakiendelea kukua kila siku.
=Mwafrika anaogopa kutumia na kutegemea ufahamu wake sababu dini imemwambia asitumie ufahamu wake sababu mungu yupo.
Na anashindwa kujiuliza vitu vyote anavyotumia vimetokana na ufahamu.
=Na watu kugombana sababu ya dini iliyoletwa na weupe hata huyo mweupe akiona anaweza shangaa akili zao zilivyo za ajabu hao Africans wakimpigania mtume mweupe wa kwenye kitabu.

Na mpaka leo africa hatuna kitu ambacho kimetokana na sisi wenyewe, labda kama wangetuacha kipindi kike labda tungechelewa lakini tungepata ufahamu taratibu kuliko kutuharibu kabisa na hizi dini.

Mbona china wana dini zao lakini wana maendeleo makubwa sana na ni wamoja tena wana ufahamu mkubwa ukilinganisha na sisi.

Africans hatuna umoja wala ushirikiano sababu tunachukiana na kubaguana kidini kwa dini ambazo zililetwa na watu kutoka nje kitu ambacho ni ujinga.

Najua wengi mmerukia mwisho sababu ndio tabia zenu za kutokupenda kushughulisha vichwa vyenu.
Sasa nakuambia popote utakapomtukana mtu yoyote sababu ya tofauti za kidini basi tambua hiyo dini si asili yako bali ulipewa na mweupe ili apate kukuendesha na kukucontroll so think again.

Nadhani baada ya hapo tutaacha kutukanana, kudhihakiana, kudharauriana, kubaguana sababu ya dini na hapo ndio mwanzo wa kujitambua.

na wote kuwa kitu kimoja kitu ambacho hakiwezekani.
Habari,

Binafsi nakushukuru kwa kuleta mada fikirishi kama hii, umeandika mambo mengi kwa kadiri ya uwezo wako wa kuchambua ulipofikia na kwangu mimi naona siyo jambo baya. Watu wengi hawajui hasa nini maana ya dini na nini lengo la dini miongoni mwetu sisi wanadamu ndiyo maana wengine wanapinga, wanalaumu na wengine wanaunga mkono lakini bado hawajatoa suluhu hasa ya nini matatizo yetu au dini imetusaidia nini. Binafsi nitajitahidi kadiri ya nilivyojaliwa kuelezea mawazo yangu machache.

Kwa kadri ninavyofahamu ni kuwa Dini ni njia ya Mwanadamu kumtafuta na kumuabudu MUNGU (Tafsiri yangu), hivyo basi dini ni ya Mwanadamu maana MUNGU hana dini kwa kuwa yeye anaabudiwa na haabudu kiumbe chochote. Mambo mengine mengi yaliyomo ndani ya vitabu vya dini (Biblia na Quran) ni sheria, mila na tamaduni zao (hao waleta dini) kwa jinsi walivyoishi zama zao hivyo kwetu sisi hazina uzito maana hata sisi tunazo. Kama Babu zetu wangekuwa na akili kubwa wangeweza kuhoji mathalani kuhusu majina maana tumeaminishwa kuwa majina ya kizungu ndiyo ya kikristo na majina ya kiarabu ni ya kiislamu wakati kiuhalisia siyo kweli maana majina yalikuwapo kabla ya dini hizo kuja na hakuna mtume yoyote aliyekuja na majina. Pia sisi Africa tuna majina yetu hivyo kama tukifikiri kwa kina tutagundua kuwa hatukua na haja ya kutumia majina yao.

Hao wazungu na waarabu tunaoshindana kuwalaumu kuwa walituletea dini hizi hata wao hawakuwa nazo hapo awali hivyo na wao waliletewa na wakati wakiletewa dini hizo za Ukristo na Uislamu siyo kwamba wao hawakuwa na dini, zilikuwepo ila hazikuwa za kumuabudu MUNGU wa kweli bali masanamu, jua, mwezi na wengine waliabudu nyota. (Hii ikiwa na maana kuwa walikuwa na MIUNGU ila hawakuwa na MUNGU wa kweli)

Kuhusu maendeleo na ustaarabu siyo kwamba vililetwa na dini bali dini hizi mbili zilikuta jamii za wakati huo zikiwa zimestaarabika maana tayari walikuwa na mavazi, walijenga majengo na walijua kuchimba visima vya maji pia walimiliki mali na walikuwa na mifumo ya utawala yenye kueleweka, hivyo ilichofanya dini ni kunogesha ustaarabu huo kwa kuwafanya watu kumjua MUNGU wa kweli, kupendana, kuheshimiana na pia kuelimika kwa kujifunza zaidi. Hivyo ukisema dini imeleta maangamizi Afrika utakuwa unakosea.

Kwangu mimi binafsi naona ni ujinga kumlaumu mzungu au muarabu kwa umaskini wetu, inafaa tukubali kuwa sisi tuna akili ndogo na wenzetu wana akili kubwa, bila hivyo hatuwezi kupiga hatua, tutaendelea kuwalaumu viongozi wetu huku tukijua wametokana na sisi hivyo na wao wana akili ndogo kama sisi. Kama ambavyo mgonjwa akienda kwa Daktari akaambiwa kuwa homa inayomsumbua ni malaria, inatakiwa mgonjwa huyo akubali kuwa ana malaria ndipo apewe doze lakini akikataa kuwa hana malaria hata akipewa dawa hawezi kuzimeza. Sasa kama sisi hatutakubaliana kuwa tuna akili ndogo basi kujifunza na kukosoana itakuwa vigumu hivyo tutaendelea kupiga marktime.

Matatizo tuliyonayo Waafrica yametokana na tabia ya uvivu, kutopenda elimu na kujidharau/kudharauliana sisi wenyewe kwa wenyewe (KUJIENDEKEZA) na kisha kumtukuza Mzungu na Muarabu, yaani imefikia hatua kuwa Muafrika mbele ya mzungu au muarabu ni kama mmbwa mbele ya chatu.

Suluhisho ni kuwa, tukiacha kujiendekeza na kudharauliana na kisha tukachapa kazi kwa bidii na kuwa waaminifu miongoni mwetu, tutapiga hatua ya kimaendeleo na tutafika mbali, hata tusipowafikia wazungu au waarabu lakini angalau tutaweza kutatua matatizo yetu ya msingi kama vile ukosefu wa chakula bora (ardhi tunayo), elimu bora na uchumi endelevu. (Nina mengi ila nimechoka kuandika)
 
Habari,

Binafsi nakushukuru kwa kuleta mada fikirishi kama hii, umeandika mambo mengi kwa kadiri ya uwezo wako wa kuchambua ulipofikia na kwangu mimi naona siyo jambo baya. Watu wengi hawajui hasa nini maana ya dini na nini lengo la dini miongoni mwetu sisi wanadamu ndiyo maana wengine wanapinga, wanalaumu na wengine wanaunga mkono lakini bado hawajatoa suluhu hasa ya nini matatizo yetu au dini imetusaidia nini. Binafsi nitajitahidi kadiri ya nilivyojaliwa kuelezea mawazo yangu machache.

Kwa kadri ninavyofahamu ni kuwa Dini ni njia ya Mwanadamu kumtafuta na kumuabudu MUNGU (Tafsiri yangu), hivyo basi dini ni ya Mwanadamu maana MUNGU hana dini kwa kuwa yeye anaabudiwa na haabudu kiumbe chochote. Mambo mengine mengi yaliyomo ndani ya vitabu vya dini (Biblia na Quran) ni sheria, mila na tamaduni zao (hao waleta dini) kwa jinsi walivyoishi zama zao hivyo kwetu sisi hazina uzito maana hata sisi tunazo. Kama Babu zetu wangekuwa na akili kubwa wangeweza kuhoji mathalani kuhusu majina maana tumeaminishwa kuwa majina ya kizungu ndiyo ya kikristo na majina ya kiarabu ni ya kiislamu wakati kiuhalisia siyo kweli maana majina yalikuwapo kabla ya dini hizo kuja na hakuna mtume yoyote aliyekuja na majina. Pia sisi Africa tuna majina yetu hivyo kama tukifikiri kwa kina tutagundua kuwa hatukua na haja ya kutumia majina yao.

Hao wazungu na waarabu tunaoshindana kuwalaumu kuwa walituletea dini hizi hata wao hawakuwa nazo hapo awali hivyo na wao waliletewa na wakati wakiletewa dini hizo za Ukristo na Uislamu siyo kwamba wao hawakuwa na dini, zilikuwepo ila hazikuwa za kumuabudu MUNGU wa kweli bali masanamu, jua, mwezi na wengine waliabudu nyota. (Hii ikiwa na maana kuwa walikuwa na MIUNGU ila hawakuwa na MUNGU wa kweli)

Kuhusu maendeleo na ustaarabu siyo kwamba vililetwa na dini bali dini hizi mbili zilikuta jamii za wakati huo zikiwa zimestaarabika maana tayari walikuwa na mavazi, walijenga majengo na walijua kuchimba visima vya maji pia walimiliki mali na walikuwa na mifumo ya utawala yenye kueleweka, hivyo ilichofanya dini ni kunogesha ustaarabu huo kwa kuwafanya watu kumjua MUNGU wa kweli, kupendana, kuheshimiana na pia kuelimika kwa kujifunza zaidi. Hivyo ukisema dini imeleta maangamizi Afrika utakuwa unakosea.

Kwangu mimi binafsi naona ni ujinga kumlaumu mzungu au muarabu kwa umaskini wetu, inafaa tukubali kuwa sisi tuna akili ndogo na wenzetu wana akili kubwa, bila hivyo hatuwezi kupiga hatua, tutaendelea kuwalaumu viongozi wetu huku tukijua wametokana na sisi hivyo na wao wana akili ndogo kama sisi. Kama ambavyo mgonjwa akienda kwa Daktari akaambiwa kuwa homa inayomsumbua ni malaria, inatakiwa mgonjwa huyo akubali kuwa ana malaria ndipo apewe doze lakini akikataa kuwa hana malaria hata akipewa dawa hawezi kuzimeza. Sasa kama sisi hatutakubaliana kuwa tuna akili ndogo basi kujifunza na kukosoana itakuwa vigumu hivyo tutaendelea kupiga marktime.

Matatizo tuliyonayo Waafrica yametokana na tabia ya uvivu, kutopenda elimu na kujidharau/kudharauliana sisi wenyewe kwa wenyewe (KUJIENDEKEZA) na kisha kumtukuza Mzungu na Muarabu, yaani imefikia hatua kuwa Muafrika mbele ya mzungu au muarabu ni kama mmbwa mbele ya chatu.

Suluhisho ni kuwa, tukiacha kujiendekeza na kudharauliana na kisha tukachapa kazi kwa bidii na kuwa waaminifu miongoni mwetu, tutapiga hatua ya kimaendeleo na tutafika mbali, hata tusipowafikia wazungu au waarabu lakini angalau tutaweza kutatua matatizo yetu ya msingi kama vile ukosefu wa chakula bora (ardhi tunayo), elimu bora na uchumi endelevu. (Nina mengi ila nimechoka kuandika)
Waafrika tungekuwa wavivu kama unavosema tusingeijenga marekani na ulaya. Acha kuchukia waafrika wenzako.

Self hate ndo inatusumbua. Yani unadiriki kuandika gazeti kwa ajili ya kupinga positivity. Stop that brother.
 
Back
Top Bottom