Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

Hili tunalijua miaka mingi sana imepita ndiyo maana wa TZ a tunajichanganya tu, x mass, IDD EL FITR zwooote tuna sherehekea tunaishi kiujirani zaidi na kuoleana hatubagui. kwa sababu zilisha kuja zitaondoka tuuu
 
Waafrika bwana,tukizidiwa kete na mzungu tunaanza kusingizia dini.Kwani hizi dini zina muda gani hapa nchini?

Mbona kabla ya ujio wa hizi dini hatukuwa hata na maendeleo yoyote yale?
Tuache kusingizia dini Bwana!
 
Waafrika tungekuwa wavivu kama unavosema tusingeijenga marekani na ulaya. Acha kuchukia waafrika wenzako.

Self hate ndo inatusumbua. Yani unadiriki kuandika gazeti kwa ajili ya kupinga positivity. Stop that brother.
Naona huelewi maana ya neno "uvivu" pia uache kukariri kuwa mtu akikukosoa au akikuambia ukweli usioupenda kuusikia maana yake anakuchukia. Kwa taarifa yako Marekani haikujengwa na Waafrica lakini pia wale weusi unaowaona kule siyo Waafrica bali ni Wamarekani weusi, japo kuwa weusi wana asili ya Africa lakini siyo Waafrica usikariri.

Ukiwa Kiongozi muungwana jitahidi kupata kupokea mawazo tofauti hata kama mawazo hayo huyapendi, sasa kwa baadhi ya Waafrica na Viongozi wa Afrika huu ni mtihani na tabia ya kutopenda kuambiwa ukweli haianzii kwa Viongozi bali inaanzia ngazi ya familia, angalia hata kwenye mitandao ya kijamii hususan Facebook, ikitokea mtu akaweka picha yake ukamsifia atafurahi lakini ukimkosoa anaweza hata kukufungia (block) hiki ni kiashiria cha kutopenda mawazo mbadala.
 
Waafrika bwana,tukizidiwa kete na mzungu tunaanza kusingizia dini.Kwani hizi dini zina muda gani hapa nchini?
Sijasingizia dini bali ni uhalisia au wewe unaweza kuniambia kwanini wazungu wametuzidi hizo kete?
Mbona kabla ya ujio wa hizi dini hatukuwa hata na maendeleo yoyote yale?
Tuache kusingizia dini Bwana!
Ndio maana nikasema dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika sababu mwafrika alikuwa na ufahamu uliodumaa hapo kabla.
 
Siyo kweli kuwa kabla ya kuja kwa dini hakukuwa na maendeleo yoyote Africa, yalikuwepo na watu walikuwa wameishajikusanya na kuwa na utawala (hayo siyo maendeleo!!) Kule Bukoba watu walikuwa wanafua vyuma na kutengeneza majembe ya kulimia, visu na mapanga ya kukatia. pia wazungu walikuta tumeshagundua moto hivyo tunakula vyakula vilivyopikwa. kulikuwepo na shughuli za kilimo na ufugaji ndiyo maana watu walipata chakula cha kutosha.

Kilichotokea ni kuwa Wazungu na Waarabu walikuwa na akili kubwa kuliko sisi, hivyo waliweza kudidimiza maendeleo yale kwa njia mbalimbali ikiwemo dini kwa kutuaminisha kuwa MUNGU hapendi mambo yaliyokuwa yakifanywa na Babu zetu na pia walitoa misaada iliyosaidia kuzuia kuambukiza elimu ya uhunzi, utabibu na mambo mbalimbali kutoka kizazi kimoja hadi kingine. UKWELI NI KWAMBA HAYO YOTE YALITOKANA NA KUZIDIWA AKILI (japo roho inaniuma lakini ndiyo ukweli)
 
UKWELI NI KWAMBA HAYO YOTE YALITOKANA NA KUZIDIWA AKILI
Mkuu tumia facts na sio hisia.

Kabla ya kusema wazungu wametuzidi akili itabidi utuelezee kwako akili ni nini.
Na jinsi gani wazungu wametuzidi akili?
Sababu haiwezekani ukageneralize kitu ambacho hakijafafanuliwa.

Kwako akili ni nini?
Na jinsi gani wazungu wametuzidi akili?

Tumia facts mkuu.
 
Mkuu tumia facts na sio hisia.

Kabla ya kusema wazungu wametuzidi akili itabidi utuelezee kwako akili ni nini.
Na jinsi gani wazungu wametuzidi akili?
Sababu haiwezekani ukageneralize kitu ambacho hakijafafanuliwa.

Kwako akili ni nini?
Na jinsi gani wazungu wametuzidi akili?

Tumia facts mkuu.
Mwambi kama yeye ni mwafrika na anahisi hana akili ni yeye sio wote. Hana akili as individual sio wote.
 
Siyo kweli kuwa kabla ya kuja kwa dini hakukuwa na maendeleo yoyote Africa, yalikuwepo na watu walikuwa wameishajikusanya na kuwa na utawala (hayo siyo maendeleo!!) Kule Bukoba watu walikuwa wanafua vyuma na kutengeneza majembe ya kulimia, visu na mapanga ya kukatia. pia wazungu walikuta tumeshagundua moto hivyo tunakula vyakula vilivyopikwa. kulikuwepo na shughuli za kilimo na ufugaji ndiyo maana watu walipata chakula cha kutosha.

Kilichotokea ni kuwa Wazungu na Waarabu walikuwa na akili kubwa kuliko sisi, hivyo waliweza kudidimiza maendeleo yale kwa njia mbalimbali ikiwemo dini kwa kutuaminisha kuwa MUNGU hapendi mambo yaliyokuwa yakifanywa na Babu zetu na pia walitoa misaada iliyosaidia kuzuia kuambukiza elimu ya uhunzi, utabibu na mambo mbalimbali kutoka kizazi kimoja hadi kingine. UKWELI NI KWAMBA HAYO YOTE YALITOKANA NA KUZIDIWA AKILI (japo roho inaniuma lakini ndiyo ukweli)
Huna akili wewe as an individual. Kutokua na akili wewe usijumuishe na waafrika wenzako
 
Wewe ni nani jf wa kuniambia mimi nirekebishe mada yangu?

Una mamlaka yoyote kuniambia hivyo?
Unadhani kwanini mods wameipitisha?
Aisee ukristo sio dini acha kubishana ukirekebishwa
 
Straight to the topic.

Africans wengi wanaamini kwenye dini kuliko chochote kile hapa duniani.

Na watu wanaomini kwenye dini wanaamini wapo hapa duniani ili kumuabudu mungu tu na si kingine.

Well hapa kwetu africa kuna dini kubwa mbili yaani uislamu na ukristo.

Na kwenye hizo dini kubwa mbili kila mtu anajiona yuko sahihi na kitabu chake ni sahii na dini ndio sahihi.
Na dini nyingine zaidi ya kwake ni ya uongo wala si ya kweli.

Cha ajabu hizi dini sio za africa bali zinatoka nje ya africa. Unaona akili ya mwafrika ilivyo hapo?

Na cha kushangaza zaidi hizi dini kwa karibu asilimia 90% zinatoka kwa wakoloni walioivamia africa.

Na sio wakoloni tu waliotukandamiza watu weusi, hapana hata hizo dini zimekandamiza watu weusi.

Na bila shaka hizo dini zilikuwa na mipango ya muda mrefu kuanzia miaka 100 mbele ili zifanikiwe na kweli zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Kumbuka ukitaka kumteka mtu kwenye kila kitu basi anza kumteka ufahamu wake.

Dini za wakoloni ndio chanzo mojawapo leo tuko hapa.

**********

Binadamu unatakiwa uwe na uwezo wa kujitambua na kujielewa ili kuepuka kuendeshwa na hisia ila ukishindwa kujitambua na kujielewa basi tegemea uwe controlled na hisia na hiyo ni sign ya ukosefu wa hivyo vitu hapo juu na vingine vya ziada yaani

=Kujitambua
=Kujielewa


Unajua kuna vitu vya kuchagua na kuvifanya au kuvitenda na kuna vitu vya kuacha. Hayo yote yanategemea na ufahamu wako.

Sasa huyu muafrika kwa yote yale aliyofanyiwa kuteswa, kudhihakiwa, kudharirishwa na mengine mengi mabaya.
Still mwafrika huyu alikubali kupokea dini hizi za mkoloni na kukubali kuwa ndio ufahamu wake na kila kitu kwenye hiyo dini kipo sahihi na hatoruhusiwa kupinga au kuhoji chochote juu ya hiyo dini au atalaaniwa.

Mwafrika huyu mweusi amekubali kupokea dini ambayo.
=Amepewa na watu weupe waliomfanyia kila aina ya ubaya na ukatili.
=Kila mtume kwenye hizo dini ni mweupe
=Hata mungu wa kwenye hizo dini katuma watu weupe waje kutangaza hizo dini weusi sijui kwanini kawaacha
=Alikubali kupokea dini ambazo mtu mweusi ni nembo ya shetani na nyeupe ni nuru ya malaika.
(Huo ni ubaguzi pure)
=Dini ambazo inasema mweusi amelaaniwa nk

Hapohapo Yaani mwafrika yupo tayari
=Akuue
=Akutukane
=Akudharirishe
=Akudharau
=Akupige
=Akudhihaki au chochote kile kibaya mwafrika atamfanyia mwafrika mwenzake sababu ya dini aliyopewa na mtu aliyemtesa, kumtukana, kumdhihaki na kumdharirisha.

Still mwafrika mweusi huyohuyo anaamini yeye amelaaniwa kwa rangi yake na yeye si chochote mbele ya mweupe kwani mweupe amebarikiwa.
Hapo hakumbuki kama hiyo dini kampa huyohuyo mweupe aliyemtesa na kumpiga mijeredi ya mgongo ili asiangushe pembe za tembo.

Yes huyo ndio mwafrika wa africa usijali hata humu watajitokeza watu kama hao. Asilimia kadhaa za hao watu wapo humu jf.

Na hapo mwafrika huyo bado ataendelea kumchukia mwafrika wa dini nyingine kivyovyote vile.

*******

Labda mababu zetu walikosa hivyo vitu yaani kujielewa na kujitambua hivyo wakawa wanaendeshwa na hisia bila wao kujua hivyo ikawafanya wasie na akili wala maarifa ya kueleweka.
Lakini binadamu anabadirika kadri muda unavyozidi kwenda
Hivyo hata sisi tunaweza kubadirika na kuanza kujitambua na kujielewa na sio kuendeshwa na hisia tena au Africans itakuwa ngumu kubadirika.

kila kitu kimerahisishwa na hao wazungu ambavyo si vya kupotosha na kukandamiza kama dini hivyo tunaweza kutumia hivyo vitu vizuri kuweza kubadirika na kujiongeza na sio kuendelea kubomoka.

Kumbuka nilikwambia binadamu anatakiwa awe na sifa ya kujitambua na kujielewa ili aisendeshwa na hisia au imani hivyo ni lazima kujua kipi cha kuchukua na kuacha na sio kupelekeshwa kama fuso bovu na hizo hisia kama mababu zetu waliokubali hizi imani.

*******

SASA HII IMEATHIRI VIPI UFAHAMU AU UBONGO WA MWAFRIKA.

=Well baada ya hapo mwafrika akawa muoga wa kuhoji "kwanini. sababu ya kuogopa kukufuru na kulaaniwa alafu alishaalaniwa mara kwanza.
=Mwafrika akawa mvivu wa kufikiri kwa kusema kila kitu anapanga mungu hivyo huyo mwafrika kubweteka chini akitegemea mungu atamfanya apate anachokitaka huku amekaa tu chini ya mwembe. Hadi leo hawa watu wapo na ndio masikini wa kwanza yaani mafukara.
=mwafrika huyu anaamini wazungu ndio wamebarikiwa na ndio maana wameendelea.
=mwafrika ubongo wake wote umelala sababu ameaminishwa yeye si chochote kwani amelaaniwa na ndo maana rangi yake nyeusi.
=mwafrika anaamini duniani anapita tu na yupo hapa kumuabudu mungu tu.
Hivyo huyo mwafrika kuendelea kufa masikini na kuendelea kuishi na changamoto sababu yeye kaja kumuabudu mungu tu na kuijaza dunia na si kingine wakati huo weupe wakiendelea kukua kila siku.
=Mwafrika anaogopa kutumia na kutegemea ufahamu wake sababu dini imemwambia asitumie ufahamu wake sababu mungu yupo.
Na anashindwa kujiuliza vitu vyote anavyotumia vimetokana na ufahamu.
=Na watu kugombana sababu ya dini iliyoletwa na weupe hata huyo mweupe akiona anaweza shangaa akili zao zilivyo za ajabu hao Africans wakimpigania mtume mweupe wa kwenye kitabu.

Na mpaka leo africa hatuna kitu ambacho kimetokana na sisi wenyewe, labda kama wangetuacha kipindi kike labda tungechelewa lakini tungepata ufahamu taratibu kuliko kutuharibu kabisa na hizi dini.

Mbona china wana dini zao lakini wana maendeleo makubwa sana na ni wamoja tena wana ufahamu mkubwa ukilinganisha na sisi.

Africans hatuna umoja wala ushirikiano sababu tunachukiana na kubaguana kidini kwa dini ambazo zililetwa na watu kutoka nje kitu ambacho ni ujinga.

Najua wengi mmerukia mwisho sababu ndio tabia zenu za kutokupenda kushughulisha vichwa vyenu.
Sasa nakuambia popote utakapomtukana mtu yoyote sababu ya tofauti za kidini basi tambua hiyo dini si asili yako bali ulipewa na mweupe ili apate kukuendesha na kukucontroll so think again.

Nadhani baada ya hapo tutaacha kutukanana, kudhihakiana, kudharauriana, kubaguana sababu ya dini na hapo ndio mwanzo wa kujitambua.

na wote kuwa kitu kimoja kitu ambacho hakiwezekani.

Ila natumaini unajua tofauti kati ya :

Dini na Imani?
 
Back
Top Bottom