Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

yani umekiri kabisa kua ni vitabu viwili tu ambavyo umeviona machoni. halafu hapo hapo tena unarukia hitimisho kua hakijawahi tokea kitabu cha mfanano wa model ya uandishi kama huo

tukueleweje?
usikaze fuvu
 
Kusema umezusha unanuna,sasa kama kweli lazima utaambiwa ili kesho uwe makini.

Unazusha mambo bila ushahidi,ushahidi unaokimbilia ati nimefuta 😃😃😃😃.

Unahamisha magoli kijana.
Ongea ongea toa dukuduku utoe nyongo za roho mkuu.

Angalia sasa.

Sasa nimeongopa nini mbona wanchekesha mkuu ?
mkuu nilidhani utaweka hoja badala yake umeweka hisia mbele kuliko upeo wako wa kufikili.
 
Ujumbe sio lazima uandikwe.
Kusoma na kuyaelewa maneno basi ndo ujumbe umeshafika.
hayo maneno ya kusomwa yataonekana vipi bila kuandikwa?

au unatumia telepathic communication?
 
watu wenyewe walioleta hz dini waliwatesa na kuwapiga mijeredi mababu zetu ili kuwalazmisha wazikubali hzo dini. sasa unajiuliza hv kama kweli znahubiri upendo wa kweli je kwa nn wawapige mijered wenzety? yaan mambo ya dini yana story nyng sana ambazo huwa sizielewi!
 
Wewe ni nani jf wa kuniambia mimi nirekebishe mada yangu?

Una mamlaka yoyote kuniambia hivyo?
Unadhani kwanini mods wameipitisha?
Anamamlaka ya kukuambia urekebishe kama upeo wako wa uelewa ni mdogo kuliko yeye.
 
Duuu! Kweli kwa mawazo haya shida za duniani Zitatuwasha na mbinguni hatutafika. Hivi mnavyo sema dini imemdumaza mwafrika. Je mmesha jiuliza mchango wa dini hizikatika jamii ?. Je dini ya asili ya mwafrika Inamchango gani kwenye jamii. Binafsi siungi mkono hata kidogo kwa sababu dini za nje zinamchango mkw bwa mf.zimeleta elimu, na inavunja ukabila hata utaifa, inashirikiana na serikali kupunguza uharibifu. Leo hii nikikutana na mukristo au muislam mwenye Iman kiasi najua kiwango flani naweza kuwa salaam kwakuwa ana mafundisho sahihi yenye kumpendaza mungu. Sasa hii African culture ni dhaana ambayo kiukweli tulichochola zaana mpaka leo umeonyesha mapungufu makubwa mauwaji ya albino, ndugu kukosana, kwanza ni dini sizo taka maarifa utaskia flani kamloga mtoto wa flani. Kutokuwa na umoja utaskia wayakyusa wa Mila zao, wahehe zao, wachaga zao Sasa hapa kweli kunamaendeleo kweli. Isikitisha Sana kuona hata hao wapiga lamli wanamtambua mungu ndio maana ni waoga Sana hata katika swala kifo kwa kuwa wanakujua waendako




Hitimisho mtoa maada ni Bora kuwa wajinga wakosefu wa maarifa kuliko kuwa na wenye maarifa na wasio na iman sahihi Kama wewe maana kwa huu uzi wako ni Bora tu ungekuwa ni mjinga usiyejua lolote hata kuposti huumu jamii forum. Ila siku laumu sana sana humu duniani ni uwanja wa kampeni mgombea ni mungu na shetani. kwahiyo hata hi post yako inawakilisha mgombea wako
 
Mawazo ya mkoloni bado yanaishi kichwani kwako. Jielimishe kuhusu dini za waafrika. Utapata mengi mazuri positive kuliko negativity uliofundishwa na dini za wakoloni. Wakoloni wangekua wana nia nzuri na dini. Wasingeweka rangi kwenye dini. Maana kuanzia malaika.....etc wote ni wazungu. Amka my african brother. Waafrika tulikua tunamjua mungu wa kweli na kuabudu hata kabla ya wazungu. Usidharau kila kitu cha muafrika. Unadharau kwa sababu historia nzuri ya muafrika umefichiwa toka utotoni.
Duuu! Kweli kwa mawazo haya shida za duniani Zitatuwasha na mbinguni hatutafika. Hivi mnavyo sema dini imemdumaza mwafrika. Je mmesha jiuliza mchango wa dini hizikatika jamii ?. Je dini ya asili ya mwafrika Inamchango gani kwenye jamii. Binafsi siungi mkono hata kidogo kwa sababu dini za nje zinamchango mkw bwa mf.zimeleta elimu, na inavunja ukabila hata utaifa, inashirikiana na serikali kupunguza uharibifu. Leo hii nikikutana na mukristo au muislam mwenye Iman kiasi najua kiwango flani naweza kuwa salaam kwakuwa ana mafundisho sahihi yenye kumpendaza mungu. Sasa hii African culture ni dhaana ambayo kiukweli tulichochola zaana mpaka leo umeonyesha mapungufu makubwa mauwaji ya albino, ndugu kukosana, kwanza ni dini sizo taka maarifa utaskia flani kamloga mtoto wa flani. Kutokuwa na umoja utaskia wayakyusa wa Mila zao, wahehe zao, wachaga zao Sasa hapa kweli kunamaendeleo kweli. Isikitisha Sana kuona hata hao wapiga lamli wanamtambua mungu ndio maana ni waoga Sana hata katika swala kifo kwa kuwa wanakujua waendako




Hitimisho mtoa maada ni Bora kuwa wajinga wakosefu wa maarifa kuliko kuwa na wenye maarifa na wasio na iman sahihi Kama wewe maana kwa huu uzi wako ni Bora tu ungekuwa ni mjinga usiyejua lolote hata kuposti huumu jamii forum. Ila siku laumu maana Sana maana humu duniani ni uwanja wa kampeni mgombea ni mungu na shetani. kwahiyo hata hi post yako inawakilisha mgombea wako
 
Bilashaka wewe utakuwa ni wakala wa Shetani..

Kwaiyo katika kufikilia kwako kote, ndiyo ukaona dini ndiyo tatizo kubwa katika maendeleo ya afrika.

Nchi nyingi duniani zimepokea dini hizo kama zilivyopokelewa afrika lakini zina maendeleo makubwa sana. Mfano, Brazil, Turkey, n.k

Tatizo haliwezi kuwa dini, kuna mambo makubwa muhimu mawili ya kuangalia hapa kama;
- Mfumo wa elimu ( Quality people )
- Mfumo wa Utawala ( Quality leadership )

Uwezi kuwa na taifa bora kama hauna watu bora na viongozi bora !!
 
Straight to the topic.

Africans wengi wanaamini kwenye dini kuliko chochote kile hapa duniani.

Na watu wanaomini kwenye dini wanaamini wapo hapa duniani ili kumuabudu mungu tu na si kingine.

Well hapa kwetu africa kuna dini kubwa mbili yaani uislamu na ukristo.

Na kwenye hizo dini kubwa mbili kila mtu anajiona yuko sahihi na kitabu chake ni sahii na dini ndio sahihi.
Na dini nyingine zaidi ya kwake ni ya uongo wala si ya kweli.

Cha ajabu hizi dini sio za africa bali zinatoka nje ya africa. Unaona akili ya mwafrika ilivyo hapo?

Na cha kushangaza zaidi hizi dini kwa karibu asilimia 90% zinatoka kwa wakoloni walioivamia africa.

Na sio wakoloni tu waliotukandamiza watu weusi, hapana hata hizo dini zimekandamiza watu weusi.

Na bila shaka hizo dini zilikuwa na mipango ya muda mrefu kuanzia miaka 100 mbele ili zifanikiwe na kweli zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Kumbuka ukitaka kumteka mtu kwenye kila kitu basi anza kumteka ufahamu wake.

Dini za wakoloni ndio chanzo mojawapo leo tuko hapa.

**********

Binadamu unatakiwa uwe na uwezo wa kujitambua na kujielewa ili kuepuka kuendeshwa na hisia ila ukishindwa kujitambua na kujielewa basi tegemea uwe controlled na hisia na hiyo ni sign ya ukosefu wa hivyo vitu hapo juu na vingine vya ziada yaani

=Kujitambua
=Kujielewa


Unajua kuna vitu vya kuchagua na kuvifanya au kuvitenda na kuna vitu vya kuacha. Hayo yote yanategemea na ufahamu wako.

Sasa huyu muafrika kwa yote yale aliyofanyiwa kuteswa, kudhihakiwa, kudharirishwa na mengine mengi mabaya.
Still mwafrika huyu alikubali kupokea dini hizi za mkoloni na kukubali kuwa ndio ufahamu wake na kila kitu kwenye hiyo dini kipo sahihi na hatoruhusiwa kupinga au kuhoji chochote juu ya hiyo dini au atalaaniwa.

Mwafrika huyu mweusi amekubali kupokea dini ambayo.
=Amepewa na watu weupe waliomfanyia kila aina ya ubaya na ukatili.
=Kila mtume kwenye hizo dini ni mweupe
=Hata mungu wa kwenye hizo dini katuma watu weupe waje kutangaza hizo dini weusi sijui kwanini kawaacha
=Alikubali kupokea dini ambazo mtu mweusi ni nembo ya shetani na nyeupe ni nuru ya malaika.
(Huo ni ubaguzi pure)
=Dini ambazo inasema mweusi amelaaniwa nk

Hapohapo Yaani mwafrika yupo tayari
=Akuue
=Akutukane
=Akudharirishe
=Akudharau
=Akupige
=Akudhihaki au chochote kile kibaya mwafrika atamfanyia mwafrika mwenzake sababu ya dini aliyopewa na mtu aliyemtesa, kumtukana, kumdhihaki na kumdharirisha.

Still mwafrika mweusi huyohuyo anaamini yeye amelaaniwa kwa rangi yake na yeye si chochote mbele ya mweupe kwani mweupe amebarikiwa.
Hapo hakumbuki kama hiyo dini kampa huyohuyo mweupe aliyemtesa na kumpiga mijeredi ya mgongo ili asiangushe pembe za tembo.

Yes huyo ndio mwafrika wa africa usijali hata humu watajitokeza watu kama hao. Asilimia kadhaa za hao watu wapo humu jf.

Na hapo mwafrika huyo bado ataendelea kumchukia mwafrika wa dini nyingine kivyovyote vile.

*******

Labda mababu zetu walikosa hivyo vitu yaani kujielewa na kujitambua hivyo wakawa wanaendeshwa na hisia bila wao kujua hivyo ikawafanya wasie na akili wala maarifa ya kueleweka.
Lakini binadamu anabadirika kadri muda unavyozidi kwenda
Hivyo hata sisi tunaweza kubadirika na kuanza kujitambua na kujielewa na sio kuendeshwa na hisia tena au Africans itakuwa ngumu kubadirika.

kila kitu kimerahisishwa na hao wazungu ambavyo si vya kupotosha na kukandamiza kama dini hivyo tunaweza kutumia hivyo vitu vizuri kuweza kubadirika na kujiongeza na sio kuendelea kubomoka.

Kumbuka nilikwambia binadamu anatakiwa awe na sifa ya kujitambua na kujielewa ili aisendeshwa na hisia au imani hivyo ni lazima kujua kipi cha kuchukua na kuacha na sio kupelekeshwa kama fuso bovu na hizo hisia kama mababu zetu waliokubali hizi imani.

*******

SASA HII IMEATHIRI VIPI UFAHAMU AU UBONGO WA MWAFRIKA.

=Well baada ya hapo mwafrika akawa muoga wa kuhoji "kwanini. sababu ya kuogopa kukufuru na kulaaniwa alafu alishaalaniwa mara kwanza.
=Mwafrika akawa mvivu wa kufikiri kwa kusema kila kitu anapanga mungu hivyo huyo mwafrika kubweteka chini akitegemea mungu atamfanya apate anachokitaka huku amekaa tu chini ya mwembe. Hadi leo hawa watu wapo na ndio masikini wa kwanza yaani mafukara.
=mwafrika huyu anaamini wazungu ndio wamebarikiwa na ndio maana wameendelea.
=mwafrika ubongo wake wote umelala sababu ameaminishwa yeye si chochote kwani amelaaniwa na ndo maana rangi yake nyeusi.
=mwafrika anaamini duniani anapita tu na yupo hapa kumuabudu mungu tu.
Hivyo huyo mwafrika kuendelea kufa masikini na kuendelea kuishi na changamoto sababu yeye kaja kumuabudu mungu tu na kuijaza dunia na si kingine wakati huo weupe wakiendelea kukua kila siku.
=Mwafrika anaogopa kutumia na kutegemea ufahamu wake sababu dini imemwambia asitumie ufahamu wake sababu mungu yupo.
Na anashindwa kujiuliza vitu vyote anavyotumia vimetokana na ufahamu.
=Na watu kugombana sababu ya dini iliyoletwa na weupe hata huyo mweupe akiona anaweza shangaa akili zao zilivyo za ajabu hao Africans wakimpigania mtume mweupe wa kwenye kitabu.

Na mpaka leo africa hatuna kitu ambacho kimetokana na sisi wenyewe, labda kama wangetuacha kipindi kike labda tungechelewa lakini tungepata ufahamu taratibu kuliko kutuharibu kabisa na hizi dini.

Mbona china wana dini zao lakini wana maendeleo makubwa sana na ni wamoja tena wana ufahamu mkubwa ukilinganisha na sisi.

Africans hatuna umoja wala ushirikiano sababu tunachukiana na kubaguana kidini kwa dini ambazo zililetwa na watu kutoka nje kitu ambacho ni ujinga.

Najua wengi mmerukia mwisho sababu ndio tabia zenu za kutokupenda kushughulisha vichwa vyenu.
Sasa nakuambia popote utakapomtukana mtu yoyote sababu ya tofauti za kidini basi tambua hiyo dini si asili yako bali ulipewa na mweupe ili apate kukuendesha na kukucontroll so think again.

Nadhani baada ya hapo tutaacha kutukanana, kudhihakiana, kudharauriana, kubaguana sababu ya dini na hapo ndio mwanzo wa kujitambua.

na wote kuwa kitu kimoja kitu ambacho hakiwezekani.
Wanakosea kuamini katika Dini badala yake wanapaswa kuamini katika Mungu
 
Hawa wazungu sijui walifanikiwaje kwenye hili mbona kule China & India walitawaliwa na wazungu lakini bado walibaki na dini zao
Ishu sio kubaki na cha kwako au kuiga cha mwingine.Ishu ni hicho kitu kina manufaa gani yanayojipambanua wazi wazi!
 
Straight to the topic.

Africans wengi wanaamini kwenye dini kuliko chochote kile hapa duniani.

Na watu wanaomini kwenye dini wanaamini wapo hapa duniani ili kumuabudu mungu tu na si kingine.

Well hapa kwetu africa kuna dini kubwa mbili yaani uislamu na ukristo.

Na kwenye hizo dini kubwa mbili kila mtu anajiona yuko sahihi na kitabu chake ni sahii na dini ndio sahihi.
Na dini nyingine zaidi ya kwake ni ya uongo wala si ya kweli.

Cha ajabu hizi dini sio za africa bali zinatoka nje ya africa. Unaona akili ya mwafrika ilivyo hapo?

Na cha kushangaza zaidi hizi dini kwa karibu asilimia 90% zinatoka kwa wakoloni walioivamia africa.

Na sio wakoloni tu waliotukandamiza watu weusi, hapana hata hizo dini zimekandamiza watu weusi.

Na bila shaka hizo dini zilikuwa na mipango ya muda mrefu kuanzia miaka 100 mbele ili zifanikiwe na kweli zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Kumbuka ukitaka kumteka mtu kwenye kila kitu basi anza kumteka ufahamu wake.

Dini za wakoloni ndio chanzo mojawapo leo tuko hapa.

**********

Binadamu unatakiwa uwe na uwezo wa kujitambua na kujielewa ili kuepuka kuendeshwa na hisia ila ukishindwa kujitambua na kujielewa basi tegemea uwe controlled na hisia na hiyo ni sign ya ukosefu wa hivyo vitu hapo juu na vingine vya ziada yaani

=Kujitambua
=Kujielewa


Unajua kuna vitu vya kuchagua na kuvifanya au kuvitenda na kuna vitu vya kuacha. Hayo yote yanategemea na ufahamu wako.

Sasa huyu muafrika kwa yote yale aliyofanyiwa kuteswa, kudhihakiwa, kudharirishwa na mengine mengi mabaya.
Still mwafrika huyu alikubali kupokea dini hizi za mkoloni na kukubali kuwa ndio ufahamu wake na kila kitu kwenye hiyo dini kipo sahihi na hatoruhusiwa kupinga au kuhoji chochote juu ya hiyo dini au atalaaniwa.

Mwafrika huyu mweusi amekubali kupokea dini ambayo.
=Amepewa na watu weupe waliomfanyia kila aina ya ubaya na ukatili.
=Kila mtume kwenye hizo dini ni mweupe
=Hata mungu wa kwenye hizo dini katuma watu weupe waje kutangaza hizo dini weusi sijui kwanini kawaacha
=Alikubali kupokea dini ambazo mtu mweusi ni nembo ya shetani na nyeupe ni nuru ya malaika.
(Huo ni ubaguzi pure)
=Dini ambazo inasema mweusi amelaaniwa nk

Hapohapo Yaani mwafrika yupo tayari
=Akuue
=Akutukane
=Akudharirishe
=Akudharau
=Akupige
=Akudhihaki au chochote kile kibaya mwafrika atamfanyia mwafrika mwenzake sababu ya dini aliyopewa na mtu aliyemtesa, kumtukana, kumdhihaki na kumdharirisha.

Still mwafrika mweusi huyohuyo anaamini yeye amelaaniwa kwa rangi yake na yeye si chochote mbele ya mweupe kwani mweupe amebarikiwa.
Hapo hakumbuki kama hiyo dini kampa huyohuyo mweupe aliyemtesa na kumpiga mijeredi ya mgongo ili asiangushe pembe za tembo.

Yes huyo ndio mwafrika wa africa usijali hata humu watajitokeza watu kama hao. Asilimia kadhaa za hao watu wapo humu jf.

Na hapo mwafrika huyo bado ataendelea kumchukia mwafrika wa dini nyingine kivyovyote vile.

*******

Labda mababu zetu walikosa hivyo vitu yaani kujielewa na kujitambua hivyo wakawa wanaendeshwa na hisia bila wao kujua hivyo ikawafanya wasie na akili wala maarifa ya kueleweka.
Lakini binadamu anabadirika kadri muda unavyozidi kwenda
Hivyo hata sisi tunaweza kubadirika na kuanza kujitambua na kujielewa na sio kuendeshwa na hisia tena au Africans itakuwa ngumu kubadirika.

kila kitu kimerahisishwa na hao wazungu ambavyo si vya kupotosha na kukandamiza kama dini hivyo tunaweza kutumia hivyo vitu vizuri kuweza kubadirika na kujiongeza na sio kuendelea kubomoka.

Kumbuka nilikwambia binadamu anatakiwa awe na sifa ya kujitambua na kujielewa ili aisendeshwa na hisia au imani hivyo ni lazima kujua kipi cha kuchukua na kuacha na sio kupelekeshwa kama fuso bovu na hizo hisia kama mababu zetu waliokubali hizi imani.

*******

SASA HII IMEATHIRI VIPI UFAHAMU AU UBONGO WA MWAFRIKA.

=Well baada ya hapo mwafrika akawa muoga wa kuhoji "kwanini. sababu ya kuogopa kukufuru na kulaaniwa alafu alishaalaniwa mara kwanza.
=Mwafrika akawa mvivu wa kufikiri kwa kusema kila kitu anapanga mungu hivyo huyo mwafrika kubweteka chini akitegemea mungu atamfanya apate anachokitaka huku amekaa tu chini ya mwembe. Hadi leo hawa watu wapo na ndio masikini wa kwanza yaani mafukara.
=mwafrika huyu anaamini wazungu ndio wamebarikiwa na ndio maana wameendelea.
=mwafrika ubongo wake wote umelala sababu ameaminishwa yeye si chochote kwani amelaaniwa na ndo maana rangi yake nyeusi.
=mwafrika anaamini duniani anapita tu na yupo hapa kumuabudu mungu tu.
Hivyo huyo mwafrika kuendelea kufa masikini na kuendelea kuishi na changamoto sababu yeye kaja kumuabudu mungu tu na kuijaza dunia na si kingine wakati huo weupe wakiendelea kukua kila siku.
=Mwafrika anaogopa kutumia na kutegemea ufahamu wake sababu dini imemwambia asitumie ufahamu wake sababu mungu yupo.
Na anashindwa kujiuliza vitu vyote anavyotumia vimetokana na ufahamu.
=Na watu kugombana sababu ya dini iliyoletwa na weupe hata huyo mweupe akiona anaweza shangaa akili zao zilivyo za ajabu hao Africans wakimpigania mtume mweupe wa kwenye kitabu.

Na mpaka leo africa hatuna kitu ambacho kimetokana na sisi wenyewe, labda kama wangetuacha kipindi kike labda tungechelewa lakini tungepata ufahamu taratibu kuliko kutuharibu kabisa na hizi dini.

Mbona china wana dini zao lakini wana maendeleo makubwa sana na ni wamoja tena wana ufahamu mkubwa ukilinganisha na sisi.

Africans hatuna umoja wala ushirikiano sababu tunachukiana na kubaguana kidini kwa dini ambazo zililetwa na watu kutoka nje kitu ambacho ni ujinga.

Najua wengi mmerukia mwisho sababu ndio tabia zenu za kutokupenda kushughulisha vichwa vyenu.
Sasa nakuambia popote utakapomtukana mtu yoyote sababu ya tofauti za kidini basi tambua hiyo dini si asili yako bali ulipewa na mweupe ili apate kukuendesha na kukucontroll so think again.

Nadhani baada ya hapo tutaacha kutukanana, kudhihakiana, kudharauriana, kubaguana sababu ya dini na hapo ndio mwanzo wa kujitambua.

na wote kuwa kitu kimoja kitu ambacho hakiwezekani.
1. Ni vizuri tukajenga hoja kwa ushahidi (with cogent justification). Kwa vile umesema hapa Afrika kuna dini kubwa mbili - Uislamu na Ukristo - na kwa vile mimi ni Mkatoliki (Mkiristo), nimeamua nitoea mifano ya baadhi ya waumini wa Kikristo (bofya hapa List of Christians in science and technology - Wikipedia) waliaomini uwepo wa Mungu kupitia imani yao ya kuwa Wakristo, waliweza kugundua mambo mbalimbali ambayo sayansi na teknolojia tunazotumia zimetokana nayo au baadhi ya hayo mambo.
2. Kwa msingi huu siwezi kuamini kwamba kama hawa watu waliweza kuamini na kugundua mambo waliyogundua, kwa nini sisi katika kuamini katika hiyo dini yao kutufanye kudumaze ufahamu wetu kama kichwa chako cha habari kinavyoeleza?
3. Kutokana na hili, siwezi kuamini kwamba kuamini katika dini ndiko kunakodumaza ufahamu wa Mwafrika na hujatoa ushahidi wowote wa kimaandishi jinsi dini inavyodumaza ufahamu wa Mwafrika isipokuwa umetumia hoja 'zoazoa' (blanket/wholesale conclusion) bila kuangalia mtiririko wa 'premises' zako.
 
Tukaambiwa Mungu amejigawa sehemu tatu, tukaitikia "ndio mzungu " Mungu ameandaa moto wa kuchoma watu wake! Ndio mzungu! Hakuna aliyehoji .
 
Back
Top Bottom