Dkt. Mwakyembe Kuongoza Uchunguzi Malalamiko ya Mtihani wa Law School

Dkt. Mwakyembe Kuongoza Uchunguzi Malalamiko ya Mtihani wa Law School

Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro amemteuwa Dk Harison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa kamati ya watu saba ili kutafuta chanzo cha kufeli kwa wingi katika mitihani ya mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST).

Kuundwa kwa tume hiyo kumekuja baada ya kelele za wananchi kufuatia hoja iliyoibuliwa na gazeti la mwananchi kuhusu kiwango cha idadi ya waliofeli mtihani wa mwisho kwa elimu ya vitendo katika taasisi hiyo.

Waziri amesema kamati hiyo itakabidhiwa hadidu rejea na Kàtibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mary Makondo kesho Oktoba 13, 2022 na itafanya kazi kwa siku 30. "Baada ya hapo, Mwenyekiti wake atakuja hadharani kutoa taarifa kwa waandishi kuhusu walichobaini lakini muamini kamati ina watu wenye weledi mkubwa sana," amesema Dk Ndumbaro.


----
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro amemteuwa Dk Harison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa kamati ya watu saba ili kutafuta chanzo cha kufeli kwa wingi katika mitihani ya mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST).

Wajumbe wengine katika kamati hiyo ni Jaji Mstaafu Cililius Matupa aliyewahi kuwa mshauri wa rais Dk Jakaya Kikwete, Rashid Asaa ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma wa Zanzibar.

Wengine ni Gloria Kalabamu, Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Alice Mtulo, Wakili mwandamizi kutoka Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Mary Mniwasa, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Dar Stock Exchange na John Kaombwe ambaye ni Mwanafunzi aliyehitimu LST.

Hayo yamebainishwa leo Jumatano Oktoba 12, 2022 na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata la kufeli katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST).

Kuundwa kwa tume hiyo kumekuja baada ya kelele za wananchi kufuatia hoja iliyoibuliwa na gazeti la mwananchi kuhusu kiwango cha idadi ya waliofeli mtihani wa mwisho kwa elimu ya vitendo katika taasisi hiyo.

Waziri amesema kamati hiyo itakabidhiwa hadidu rejea na Kàtibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mary Makondo kesho Oktoba 13, 2022 na itafanya kazi kwa siku 30.

"Baada ya hapo, Mwenyekiti wake atakuja hadharani kutoa taarifa kwa waandishi kuhusu walichobaini lakini muamini kamati ina watu wenye weledi mkubwa sana," amesema Dk Ndumbaro.

Hata hivyo amesema takwimu za miaka ya nyuma zinaonyesha shule hiyo imekuwa ikifaulisha kwa kiwango cha wastani wa asilimia 81.

Chanzo: Mwananchi
Mwakyembe ataleta ripoti ya kugushi kama ile iliyo muondoa Lowasa kwa tamaa za uwaziri mkuu
 
Tutarajie ripoti kama ya tume ya manyere ya kuwafurahisha wakubwa.
 
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro amemteuwa Dk Harison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa kamati ya watu saba ili kutafuta chanzo cha kufeli kwa wingi katika mitihani ya mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST).

Kuundwa kwa tume hiyo kumekuja baada ya kelele za wananchi kufuatia hoja iliyoibuliwa na gazeti la mwananchi kuhusu kiwango cha idadi ya waliofeli mtihani wa mwisho kwa elimu ya vitendo katika taasisi hiyo.

Waziri amesema kamati hiyo itakabidhiwa hadidu rejea na Kàtibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mary Makondo kesho Oktoba 13, 2022 na itafanya kazi kwa siku 30. "Baada ya hapo, Mwenyekiti wake atakuja hadharani kutoa taarifa kwa waandishi kuhusu walichobaini lakini muamini kamati ina watu wenye weledi mkubwa sana," amesema Dk Ndumbaro.


----
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro amemteuwa Dk Harison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa kamati ya watu saba ili kutafuta chanzo cha kufeli kwa wingi katika mitihani ya mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST).

Wajumbe wengine katika kamati hiyo ni Jaji Mstaafu Cililius Matupa aliyewahi kuwa mshauri wa rais Dk Jakaya Kikwete, Rashid Asaa ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma wa Zanzibar.

Wengine ni Gloria Kalabamu, Makamu wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Alice Mtulo, Wakili mwandamizi kutoka Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Mary Mniwasa, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Dar Stock Exchange na John Kaombwe ambaye ni Mwanafunzi aliyehitimu LST.

Hayo yamebainishwa leo Jumatano Oktoba 12, 2022 na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata la kufeli katika Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST).

Kuundwa kwa tume hiyo kumekuja baada ya kelele za wananchi kufuatia hoja iliyoibuliwa na gazeti la mwananchi kuhusu kiwango cha idadi ya waliofeli mtihani wa mwisho kwa elimu ya vitendo katika taasisi hiyo.

Waziri amesema kamati hiyo itakabidhiwa hadidu rejea na Kàtibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mary Makondo kesho Oktoba 13, 2022 na itafanya kazi kwa siku 30.

"Baada ya hapo, Mwenyekiti wake atakuja hadharani kutoa taarifa kwa waandishi kuhusu walichobaini lakini muamini kamati ina watu wenye weledi mkubwa sana," amesema Dk Ndumbaro.

Hata hivyo amesema takwimu za miaka ya nyuma zinaonyesha shule hiyo imekuwa ikifaulisha kwa kiwango cha wastani wa asilimia 81.

Chanzo: Mwananchi
Binafsi naomba nisema yafuatayo kuhusu shule ya sheria Tanzania:

Mosi, kutokana na uhitaji wa elimu ya kusoma kwa vitendo (Post-Graduate Diploma in Legal Practice) haikutakiwa kuwe na shule moja nchi nzima tena ambayo iko kwenye mji kama Dar es salaam. Walau hizi shule zingekuwepo kikanda ili kuwaepusha na kadhia wale wanafunzi wanaotoka mikoa ya mbali kuja kurudia mitihani Dar es Salaam. Mtoto anasafiri kutoka Tarime, hana hata mkopo halafu anakuja Dar es salaam kufanya mtihani akiwa na 50/50 kwamba hilo somo analorirudia atafuaulu au lah.

Pili, mbinu ya kumpima mwanafunzi (Mode of Assessment) siyo rafiki kabisa na haizingatia utaalamu wa kisaikolojia kwamba wanafunzi wana uelewa tofauti. Mtoto anasoma mwaka mzima halafu anapewa mitihani 24 ndani ya mwaka ambayo kama akifeli hata mmoja basi anaweza kupoteza zaidi hata ya miaka 2 anarudia tu kozi hiyo hiyo. Kikawaida tulitegemea kwenye elimu ya vitendo wanafunzi wapimwe kupitia kazi nyingine muhimu ambazo lazima ziwe na alama, kama PRESENTATIONS, GROUP ASSIGNMENTS, CLINICS + WORKSHOPS and INTERNSHIP WITH MARKS.

Sasa wanaitwa DIPLOMA IN LEGAL PRACTICE huku wakichukua ada ya zaidi ya milioni moja, ilhali vipimo vyote vinatolewa kupitia mitihani. Hii siyo sahihi, kwasababu hata mahakamani kwenyewe wanasheria huwa hatuviziani ila tunapewa muda wa kujiandaa. Sasa mtoto anakaa INTERNSHIP miezi zaidi ya sita huku akija kukaguliwa kihunihuni tu mara moja, bila kupewa alama yoyote ile ya muhimu. Kwanini hawa wanafunzi wasipangiwe hata miezi miwili-miwili kufanya kazi la lazima zenye alamu mahakama za mwanza, mabaraza ya ardhi, mabalaza ya usuluhishi, dawati la jinsia ???

Jingine, ambalo nimeliona ni jambo la ajabu kufanywa na watu wanaojiita wasomi ni kitendo cha kutoa matokeo ya mitihani yote ya mwaka mzima ndani ya siku moja, baada ya mwaka mzima na miezi mitatu kupita. Kwanini matokeo ya ICA (Individual Continous Assessment), WPE (WRITTEN PRACTICAL EXAMINATION) na FINALS NON-CORE hayatolewi mapema, ili mwanafunzi ajue mbivu na mbichi na aweze kujipanga vizuri kwenye mitihani ya mwisho ??? Pia wawekewe utaratibu maalamu kabisa wa kuyarudia haya masomo wakati hata wako shule, hasa wiki moja baada ya kumaliza WPE ???

Lingine muhimu ni kwamba LST, kuna mitihani ya WPE (Written Practical Examination) ambayo kwingineko duniani mwanafunzi huifanya kwa kufanya tafiti pamoja na majadiliano na wanafunzi wenzake, kisha baadae huenda kufanya huo mtihani. Ilhali sasa pale LST, wanafunzi wanafungiwa masaa manne (4) wakisoma mavitabu, bila kuruhusiwa kuzungumza halafu wanapewa saa moja kupumzika, ili warudi kufanya mtihani huohuo kwa masaa matatu. (It's just emotional debilitating)

Tatu, hili la kulazimisha kila anayesoma sheria awe wakili nadhani ni jambo la kishenzi ambalo lilifanywa kwa mihemko bila kufikiriwa. Miaka yote huko nyuma watu tuliajiriwa kama STATE ATTORNEYS bila hata kuwa wanasheria. Tulitakiwa tu tufanye INTERNSHIP miezi tisa kwa ATTORNEY GENERAL halafu tunaenda kufanya BAR-EXAMINATION kule Arusha. Kinachoshangaza ni kwamba wengi ambao hawakupita Law School wako vizuri kuliko hata hawa watoto wenu wa Mawasiliano nyuma kule.

Kubwa zaidi, wanasheria tuko kwenye nyanja kuu mbili ambazo ni LEGAL PRACTITIONER (ADVOCATES) na JURIST (LEGAL SCHOLARS/LEGAL RESEARCHERS). Hawa ni watu wawili tofauti na wanafanya kazi tofauti kabisa, sasa ukitaka kuwalazimisha wawe kitu kimoja utakuwa unapuyanga mno. Leo hii ushauri wa sheria wa JURIST unaweza kuwa una uzito kuliko hata ORDINARY LEGAL PRACTITIONER, kutokana na tafiti na ufahamu. Sasa kwenye nchi fulani ya kusadikika, wenyewe kwasababu hawana SPECIALIZATION basi wanalazimisha kila mtu awe wakili, kwamba hata JURIST haweza kutoa ushauri kama hana muhuri. Just Lackadaissical and Nonsensical....

Nne, mtaala wa shule ya sheria ni wa kizamani sana na hauwezi kumfanya mwanafunzi awe vizuri kwenye soko la kimataifa. Kuna baadhi ya masomo tulitegemea yafundishwe pale LST, lakini hayapo kwenye mtaala. Mfano, INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, INVESTMENT LAW, BASICS OF INTERNATIONAL ECONOMICS LAW/ INTERNATIONAL TRADE AND FINANCE LAW. Nchi haina wataalamu wa haya masomo, sisi tunakomaa kufundisha PROPABATE & ADMINISTRATION OF ESTATES, COMMERCIAL LAW, LEGAL ETHICS, HUMAN RIGHTS and ACCOUNTS FOR LAWYERS masomo ambayo vyuo vingi vinayafundisha na vinaweza kuyafundisha vizuri.

Kesi kubwa kama zila za makinikia, DOWANS, ESCROW n.k zinahitaji mwanasheria walau awe anajua masomo ya INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, ambapo anatakiwa aifahamu mikataba mikubwa BIT (Bilateral Investment Treaties), pamoja na taasisi muhumu kama ICSID, PIC, ICC. Lakini sisi tunakomaa kuwafelisha watoto masomo kama ACCOUNTS. Sijui hii nchi haina watu wenye akili kabisa. Mambo ya ajabu yanafanyika na hakuna hata anayestuka.

Tano, mradi wa LST tangu mwaka 2006 marehemu Prof. Mukoyogo aliupinga kweli kwasababu aliona hauna maana zaidi ya kuwatengenezea ulaji baadhi ya wataalamu wa pale University of Dar es Salaam. Hivi kweli, tuna uhakika kwamba haya masomo ya LST hayawezi kufundishwa vizuri kwenye vyuo ambavyo wanafunzi wanasoma wakiwa wanatafuta Shahada ya kwanza kweli ???

Jambo jingine ni kwamba wataalamu wengi wa pale LST wameamua kufanya biashara ya vitabu. Wanatunga mitihani ambayo majibu yake utayapata kama tu umenunua vitabu vyao. Hili nilishawahi kuambiwa nikathibitisha mwenyewe kwenye baadhi ya vitabu. Hii ni tabia ya kishezi ambayo inaumiza na kukwamisha wengine huku wengine wakipata ukwasi mkubwa. Mwanafunzi anataoa pesa nyingi za Ada lakini hivyo vitabu havipo maktaba, utavipata mpaka umfuate mwandishi mwenyewe na umlipe 50,000. Kwanini msiweke vitabu vingi kule maktaba wanafunzi wakavisoma ???

Sita, hivi inawezekanaje mwanafunzi ambaye amefauli vizuri shahada yake afeli vibaya kwa kiwango cha DISCONTINUE pale LST ??? Ina maana huyu mwanafunzi hafahamu kitu chochote kabisa ??? Lakini, kubwa zaidi ni hili la wanafunzi 600 kuanza pamoja, lakini wanaofaulu ni watu 30, huku nusu ingine ikiwa inafanya SUPPLEMENTARY au DISCONTINUED. Sijui kwanini hili haliwastui Majaji na Wizara. Watu hufeli, lakini siyo kwa kiwango hicho ambacho kinafanyika pale Law School.



Credit: Malcom Lumumba
 
Mnapolalamika kukazwa kwa mitihani na usahishaji kwenye level ya juu ya elimi msisahau na kulalamikia kubebwa bebwa kwa watoto wa sekondari na primary...

Elimu haipaswi kupelekwa kilele mama ili tuu wengi wawe na elimu umakini wa katka usahishaji ni muhimu na sio kubeba beaba watu ovyo

Leo hii unakutana na dogo kamaliza darasa la saba na wastan wa B unamuuliza tuu tebo ya tatu, 3 mara 9 hajuii

Same mtoto aliemaliza form 4 na ufaulu wa div 1 maswali ya kawaida tuu unamuulza amna kitu

Kizazi kijacho tutakua na wataalam wa ovyo kuwah kutokea katka sekta muhim
 
Wewe kama mwalimu wa LST ulichukua hatua gani kuwaboreshea ubongo hao ambao ulikuwa unajiuliza chuo wamefauluje! Acha egoism we mama
Mimi siyo mwalimu wa IST wala sijawahi chukua degree ya sheria, ila ninazo degree nyingine. Hapo nilikuwa natoa mfano tu.
 
Binafsi naomba nisema yafuatayo kuhusu shule ya sheria Tanzania:

Mosi, kutokana na uhitaji wa elimu ya kusoma kwa vitendo (Post-Graduate Diploma in Legal Practice) haikutakiwa kuwe na shule moja nchi nzima tena ambayo iko kwenye mji kama Dar es salaam. Walau hizi shule zingekuwepo kikanda ili kuwaepusha na kadhia wale wanafunzi wanaotoka mikoa ya mbali kuja kurudia mitihani Dar es Salaam. Mtoto anasafiri kutoka Tarime, hana hata mkopo halafu anakuja Dar es salaam kufanya mtihani akiwa na 50/50 kwamba hilo somo analorirudia atafuaulu au lah.

Pili, mbinu ya kumpima mwanafunzi (Mode of Assessment) siyo rafiki kabisa na haizingatia utaalamu wa kisaikolojia kwamba wanafunzi wana uelewa tofauti. Mtoto anasoma mwaka mzima halafu anapewa mitihani 24 ndani ya mwaka ambayo kama akifeli hata mmoja basi anaweza kupoteza zaidi hata ya miaka 2 anarudia tu kozi hiyo hiyo. Kikawaida tulitegemea kwenye elimu ya vitendo wanafunzi wapimwe kupitia kazi nyingine muhimu ambazo lazima ziwe na alama, kama PRESENTATIONS, GROUP ASSIGNMENTS, CLINICS + WORKSHOPS and INTERNSHIP WITH MARKS.

Sasa wanaitwa DIPLOMA IN LEGAL PRACTICE huku wakichukua ada ya zaidi ya milioni moja, ilhali vipimo vyote vinatolewa kupitia mitihani. Hii siyo sahihi, kwasababu hata mahakamani kwenyewe wanasheria huwa hatuviziani ila tunapewa muda wa kujiandaa. Sasa mtoto anakaa INTERNSHIP miezi zaidi ya sita huku akija kukaguliwa kihunihuni tu mara moja, bila kupewa alama yoyote ile ya muhimu. Kwanini hawa wanafunzi wasipangiwe hata miezi miwili-miwili kufanya kazi la lazima zenye alamu mahakama za mwanza, mabaraza ya ardhi, mabalaza ya usuluhishi, dawati la jinsia ???

Jingine, ambalo nimeliona ni jambo la ajabu kufanywa na watu wanaojiita wasomi ni kitendo cha kutoa matokeo ya mitihani yote ya mwaka mzima ndani ya siku moja, baada ya mwaka mzima na miezi mitatu kupita. Kwanini matokeo ya ICA (Individual Continous Assessment), WPE (WRITTEN PRACTICAL EXAMINATION) na FINALS NON-CORE hayatolewi mapema, ili mwanafunzi ajue mbivu na mbichi na aweze kujipanga vizuri kwenye mitihani ya mwisho ??? Pia wawekewe utaratibu maalamu kabisa wa kuyarudia haya masomo wakati hata wako shule, hasa wiki moja baada ya kumaliza WPE ???

Lingine muhimu ni kwamba LST, kuna mitihani ya WPE (Written Practical Examination) ambayo kwingineko duniani mwanafunzi huifanya kwa kufanya tafiti pamoja na majadiliano na wanafunzi wenzake, kisha baadae huenda kufanya huo mtihani. Ilhali sasa pale LST, wanafunzi wanafungiwa masaa manne (4) wakisoma mavitabu, bila kuruhusiwa kuzungumza halafu wanapewa saa moja kupumzika, ili warudi kufanya mtihani huohuo kwa masaa matatu. (It's just emotional debilitating)

Tatu, hili la kulazimisha kila anayesoma sheria awe wakili nadhani ni jambo la kishenzi ambalo lilifanywa kwa mihemko bila kufikiriwa. Miaka yote huko nyuma watu tuliajiriwa kama STATE ATTORNEYS bila hata kuwa wanasheria. Tulitakiwa tu tufanye INTERNSHIP miezi tisa kwa ATTORNEY GENERAL halafu tunaenda kufanya BAR-EXAMINATION kule Arusha. Kinachoshangaza ni kwamba wengi ambao hawakupita Law School wako vizuri kuliko hata hawa watoto wenu wa Mawasiliano nyuma kule.

Kubwa zaidi, wanasheria tuko kwenye nyanja kuu mbili ambazo ni LEGAL PRACTITIONER (ADVOCATES) na JURIST (LEGAL SCHOLARS/LEGAL RESEARCHERS). Hawa ni watu wawili tofauti na wanafanya kazi tofauti kabisa, sasa ukitaka kuwalazimisha wawe kitu kimoja utakuwa unapuyanga mno. Leo hii ushauri wa sheria wa JURIST unaweza kuwa una uzito kuliko hata ORDINARY LEGAL PRACTITIONER, kutokana na tafiti na ufahamu. Sasa kwenye nchi fulani ya kusadikika, wenyewe kwasababu hawana SPECIALIZATION basi wanalazimisha kila mtu awe wakili, kwamba hata JURIST haweza kutoa ushauri kama hana muhuri. Just Lackadaissical and Nonsensical....

Nne, mtaala wa shule ya sheria ni wa kizamani sana na hauwezi kumfanya mwanafunzi awe vizuri kwenye soko la kimataifa. Kuna baadhi ya masomo tulitegemea yafundishwe pale LST, lakini hayapo kwenye mtaala. Mfano, INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, INVESTMENT LAW, BASICS OF INTERNATIONAL ECONOMICS LAW/ INTERNATIONAL TRADE AND FINANCE LAW. Nchi haina wataalamu wa haya masomo, sisi tunakomaa kufundisha PROPABATE & ADMINISTRATION OF ESTATES, COMMERCIAL LAW, LEGAL ETHICS, HUMAN RIGHTS and ACCOUNTS FOR LAWYERS masomo ambayo vyuo vingi vinayafundisha na vinaweza kuyafundisha vizuri.

Kesi kubwa kama zila za makinikia, DOWANS, ESCROW n.k zinahitaji mwanasheria walau awe anajua masomo ya INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, ambapo anatakiwa aifahamu mikataba mikubwa BIT (Bilateral Investment Treaties), pamoja na taasisi muhumu kama ICSID, PIC, ICC. Lakini sisi tunakomaa kuwafelisha watoto masomo kama ACCOUNTS. Sijui hii nchi haina watu wenye akili kabisa. Mambo ya ajabu yanafanyika na hakuna hata anayestuka.

Tano, mradi wa LST tangu mwaka 2006 marehemu Prof. Mukoyogo aliupinga kweli kwasababu aliona hauna maana zaidi ya kuwatengenezea ulaji baadhi ya wataalamu wa pale University of Dar es Salaam. Hivi kweli, tuna uhakika kwamba haya masomo ya LST hayawezi kufundishwa vizuri kwenye vyuo ambavyo wanafunzi wanasoma wakiwa wanatafuta Shahada ya kwanza kweli ???

Jambo jingine ni kwamba wataalamu wengi wa pale LST wameamua kufanya biashara ya vitabu. Wanatunga mitihani ambayo majibu yake utayapata kama tu umenunua vitabu vyao. Hili nilishawahi kuambiwa nikathibitisha mwenyewe kwenye baadhi ya vitabu. Hii ni tabia ya kishezi ambayo inaumiza na kukwamisha wengine huku wengine wakipata ukwasi mkubwa. Mwanafunzi anataoa pesa nyingi za Ada lakini hivyo vitabu havipo maktaba, utavipata mpaka umfuate mwandishi mwenyewe na umlipe 50,000. Kwanini msiweke vitabu vingi kule maktaba wanafunzi wakavisoma ???

Sita, hivi inawezekanaje mwanafunzi ambaye amefauli vizuri shahada yake afeli vibaya kwa kiwango cha DISCONTINUE pale LST ??? Ina maana huyu mwanafunzi hafahamu kitu chochote kabisa ??? Lakini, kubwa zaidi ni hili la wanafunzi 600 kuanza pamoja, lakini wanaofaulu ni watu 30, huku nusu ingine ikiwa inafanya SUPPLEMENTARY au DISCONTINUED. Sijui kwanini hili haliwastui Majaji na Wizara. Watu hufeli, lakini siyo kwa kiwango hicho ambacho kinafanyika pale Law School.



Credit: Malcom Lumumba
Huyu mwamb wakili Malcom ndie aliye andiak hbr hi kwenye gazeti la mwananchi mnk mjadala ulianza kuutani utani tu Kisha mwana body mwandamiz pascal akawa anatoa majibu ya ovyo ovyo ,
 

Kitaifa




Mapya ‘msoto’ kupata uwakili, LST wafunguka​

Jumatano, Oktoba 12, 2022
mapyaaapiic.jpg

By James Magai & Juma Issihaka

Muktasari:​

  • Baadhi ya wanafunzi wa Shule Kuu ya Sheria Tanzania (LST) waliolazimika kurudia baadhi ya masomo kwa muda mrefu bila mafanikio, wametoa shuhuda zao huku wakiibua mambo mazito kuhusiana na matokeo chuoni hapo.

Dar es Salaam. Baadhi ya wanafunzi wa Shule Kuu ya Sheria Tanzania (LST) waliolazimika kurudia baadhi ya masomo kwa muda mrefu bila mafanikio, wametoa shuhuda zao huku wakiibua mambo mazito kuhusiana na matokeo chuoni hapo.

Wametoa shuhuda hizo kutokana na matokeo ya mitihani yao iliyotoka mwishoni mwa wiki ililopita yanayoonyesha mamia ya wanafunzi washindwa kuendelea huku wengine wakitakiwa kurudia baadhi ya masomo.
Katika mtihani wa uwakili wa shule hiyo uliofanywa na wanafunzi 633 mwaka huu, kati yao ni 26 pekee ndiyo waliofaulu, 342 walitakiwa kurudia (suplimentary) huku 265 walifeli na kukatishwa masomo (discontinued).

RELATED​

  • Wahitimu UDSM wahimizwa kujitolea, kujiajiri​

    Kitaifa 9 hours ago
Si jambo jipya katika shule hiyo, kwani katika mwaka wa masomo 2018/2019 kati ya wanafunzi 1,735 ni 347 walifaulu kuendelea, 484 walirudia mitihani na 468 walifeli.
Mwaka 2016/17-2017/18 kati ya wanafunzi 2,662 waliofanya mtihani 445 (sawa na asilimia 16.72) walifaulu, 1,611 (sawa na asilimia 60.53) walirudia na 606 (sawa na asilimia 22.76) walifeli.
Matokeo hayo yameibua mjadala maeneo mbalimbali huku Jaji wa Mahakama Kuu, Gabriel Malata akisema jawabu la changamoto zote zinazoikabili hatua hiyo ya taaluma ya sheria litapatikana iwapo utafanyika utafiti.
Hata hivyo, naibu mkuu wa Taasisi anayeshughulikia mafunzo kwa vitendo, machapisho, utafiti na utaalamu elekezi wa LST, Profesa Zakayo Lukumay akizungumzia madai ya rushwa ya ngono, alisema ni vigumu hilo kutokea kwa kuwa mtihani wa mwanafunzi wa taasisi hiyo hausahihishwi na mtu mmoja.
“Kila swali linasahihishwa na mhadhiri wake, unakuta yapo maswali matatu yanasahihishwa na wahadhiri watatu sasa rushwa utawapa wote?” alihoji.
Kuhusu madai ya wanafunzi kufeli, Profesa Lukumay alisema, “tuzungumze kwa lugha nyepesi, tatizo tunacholetewa hakijaiva (hawajaiva kutokea vyuo vikuu).”

Kwa upande wake, Mwandishi mkongwe nchini, Deogratius Mushi alisema “kuna hoja mawakili wamekuwa wengi Tanzania kwa sasa, lakini si kweli. Kuna mawakili vijana wengi wapo nyumbani kwa wazazi wao hapa Dar, lakini huko mikoani na wilayani hakuna mawakili.”
Katibu mtendaji mMwanzilishi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Anthony Ngaiza alisema, “tatizo halitokani na wahitimu wa vyuo vikuu kutokaa kwenye ‘law firms’ kwa muda mrefu.”
Ngaiza alisema tatizo ni ubora wa wahitimu, “hawana uelewa unaotakiwa kwa wanasheria. Hawana viwango stahiki vya lugha ya Kiingereza kuweza kumudu. Hata walimu wao wakiwa wazuri namna gani (ingawa naamini asilimia zaidi ya 50 ya walimu wao nao hawana ubora unaotakiwa.”
…arudia mara 13
Lusajo Mwakasege, mmoja wa wanafunzi waliofeli ambaye yuko chuoni hapo kwa mwaka wa tano sasa kwa ajili ya somo moja ambalo hata katika matokeo ya mwaka huu hajafaulu, alisema sasa anakusudia kuandika barua apewe nyaraka zinazomwezesha kuhakiki alama zake kisha akate rufaa na kama atanyimwa atakwenda mahakamani kuiomba mahakama iulazimishe uongozi wa chuo kumwezesha kuhakiki matokeo yake.
Akizungumza na Mwananchi, Mwakasege alisema alijiunga na chuo hicho Machi, 2016 akamaliza 2017, lakini matokeo yalipotoka akatakiwa kurudia masomo manane.
“Kila mwaka nimekuwa nafanya mitihani na nimekuwa napunguza kidogokidogo, lakini nyingine zimekuwa hazipunguziki. Kwa mwaka tunafanya mitihani mara mbili, hivyo mpaka sasa nina miaka mitano na nimeshafanya supp (nimesharudia) mara 13, lakini sijafaulu, kipengele kimoja cha somo moja.

Hata hivyo, alisema alipoona mambo yamezidi kuwa magumu mwaka 2019 alikata rufaa na akafanikiwa kufaulu somo moja, lakini akasema kuwa rufaa pale chuoni ni jambo linaloogopesha sana.
“Inasemekana ukikata rufaa wanakukariri ndo hutakuja kufaulu tena,” alisema Mwakasege.
Mwakasege alisema kuna kila dalili za kuamini wanafunzi wengi wanashindwa kwa mipango na kwamba lengo ni kuwafanya waendelee kuwepo na hivyo kuwa kama sehemu ya kitega uchumi cha chuo. Kurudia kipengele kimoja cha somo ni Sh30,000.
Aliongeza sababu nyingine inayoashiria wanafunzi wafanywa kurudia mitihani kwa makusudi ni kitendo cha kunyimwa alama wanazopata, ili wajumlishe na kujiridhisha kuwa wamepata daraja stahili.
Mwanafunzi mwingine ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema amesharudia mitihani hiyo kwa miaka saba sasa na amesharudia kipengele kimoja kwa zaidi ya mara 10, lakini bado hajafaulu.
“Mpaka juzi nilikuwa napiga mahesabu kwamba nikate rufaa au nifanyeje, lakini sasa ukishakata rufaa unaingia kwenye fitina na watu. Kwanza wananakiri namba yako. Nina ushuhuda na watu kama watano hivi.
“Kuna mtu toka court (intake) ya sita alishakata rufaa, lakini mpaka leo ni court ya 35 bado yupo na anachoshukuru tu ni kwamba amepewa uongozi kwenye sehemu tofauti,” alisema.
Alisema alijiunga na chuo hicho mwaka 2015 baada ya kuuza ng’ombe kijijini kwao, lakini katika mtihani wa kwanza alishindwa masomo yote na akalazimika kuanza upya mwaka uliofuata.
Mwanafunzi huyo alisema chuoni hapo kuna mambo mengi yanaendelea ikiwamo ya rushwa na rushwa ya ngono na kwamba kuna mtu mmoja anamjua alitoa hela na akapita.

“Kwa hiyo vitu vingine hivi ndio maana nimekwambia siwezi kuviongelea sana kwa sababu mwisho wa siku utajikuta unaumia.”
Hoja hiyo imeungwa mkono na Alexander Barunguza ambaye tayari amefungua kesi ya kupinga matokeo yake katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki na nyingine ya kikatiba Mahakama Kuu, Masjala Kuu akipinga kanuni za ukataji rufaa kupinga matokeo, huku akidai haki yake kuelekea kukiukwa kwa kutishiwa maisha na mmoja wa walimu kutokana na hatua yake ya kukata rufaa.


Mwananchi. Fikiri Tofauti.​

Tumekufikia. Mara kwa mara tunaangalia namna ya kuboresha habari zetu. Tufahamishe nini ulichopenda na nini tuboreshe.
Sema nasi!

HABARI KUU


  • Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini​

    Licha ya wingi wa rasilimali maji zilizopo nchini, upatikanaji wa maji safi na salama, bado ni changamoto kwa wananchi ambao baadhi hupata maji kwa mgawo, huku wengine hasa vijijini wakitegemea...
    Kitaifa Okt 05

  • Bei ya mafuta yazidi kushuka​

    Bei ya mafuta imeendelea kushuka, baada ya Ewura kutangaza bei mpya kuanzia kesho, ambapo lita moja ya petroli itauzwa Sh2, 886, dizeli Sh3083 na mafuta ya taa Sh3, 275 kwa lita.
    Kitaifa Okt 04

  • Rais Samia aomba mjadala changamoto bunifu sekta ya afya​

    Rais Samia Suluhu Hassan ameziomba Jumuiya ya Kimataifa kujadili changamoto tatu zinazorudisha nyuma juhudi za kufanya bunifu kwenye sekta ya afya
    Kitaifa Okt 04
ALL

Mwananchi © 2022
 
Huyu mwamb wakili Malcom ndie aliye andiak hbr hi kwenye gazeti la mwananchi mnk mjadala ulianza kuutani utani tu Kisha mwana body mwandamiz pascal akawa anatoa majibu ya ovyo ovyo ,
Ahaa! Ashukuriwe na apewe ulinzi maana kuna mawakili hawapendi mawakili wapya mtaani
 
Nashangaa serikali kuunda kamati ya watu saba kuchunguza matokeo ya Law school of Tanzania.

Hichi kizazi cha malaptop huku kichwani hamna kitu?

Angalia hata wakihitimu wanavyokuwa weupe vichwani. Sasa wanafeli kihalali wanabaki kulalama.

Huu ni upuuzi
 
Screenshot_20221012-203043_Gallery.jpg

MIKE MUGALA, KAPALA CHISUNKA, Lusaka

THE list of candidates who passed the final examination at Zambia Institute of Advanced Legal Education (ZIALE) only has one name – Hlezipe Alexis Halwiindi. The rest of the 394 students will have to re-sit the examination. Halwiindi also emerged as the best student in the legal practitioners qualifying examination held between September 20 and October 4, 2021. As one would expect, Ms Halwiindi was over the moon. “I am overwhelmed with excitement and I am not yet in a position to give a comprehensive interview of how I am feeling until I settle down and absorb this exciting news,” she said. Of course she was the only one of the 395 students smiling. One student who failed the examination expressed disappointment over the results but said she is not discouraged. The student, who spoke on condition of anonymity, said she would attempt the repeaters examinations next year
 
Nashangaa serikali kuunda kamati ya watu saba kuchunguza matokeo ya Law school of Tanzania.

Hichi kizazi cha malaptop huku kichwani hamna kitu?

Angalia hata wakihitimu wanavyokuwa weupe vichwani. Sasa wanafeli kihalali wanabaki kulalama.

Huu ni upuuzi
Kuandika dodoso za sheria wanatumia quillbot.com we unategemea nini...wanategemea grammarly nk...madogo wanashinda kidimbwi, wanakula kubeli hata kuandika hati ya mashtaka hawawezi, kutofautisha 'l' na 'r' peke yake ni mtihani....

Miaka kama mitatu iliyopita wakati wa mahafali pale Law School Jaji Mkuu akiwa Mgeni Rasmi wa Sherehe ya Mahafali aliwachana live wahitimu akisema "na huu ndio ukweli lazima tuuseme, wengi wenu bado lugha hasa Kiingereza kinawasumbua..."

Sasa wewe unatarajia nini kama Advocate tarajali hajui Kiingereza atawezaje kupambana na Mitihani na Msamati wa Sheria....Kamati naamini itabaini uzembe upo kwa wanafunzi wenyewe wasome waache vizingizio
 
Back
Top Bottom