Nashangaa serikali kuunda kamati ya watu saba kuchunguza matokeo ya Law school of Tanzania.
Hichi kizazi cha malaptop huku kichwani hamna kitu?
Angalia hata wakihitimu wanavyokuwa weupe vichwani. Sasa wanafeli kihalali wanabaki kulalama.
Huu ni upuuzi
SABABU KUU ZA TATIZO:
1. Vyakula hovyo/vya kisasa, Watoto hawanyonyeshwi zaidi ya miaka miwili ili kukomaza afya ya ubongo na kinga + makuku mataira + miyai yao + mipiza, mibaga, michipsi mfano ubongo wa samaki + viini vya mahindi yasiyokobolewa + ufuta + parachichi + ndizi hupelekea kujenga akili nzuri sana kwa kumbukumbu na uelewa mpana.
2. Maadili mabovu tokana na malezi hovyo ya house maids sababu wazazi wako bize kutafuta pesa 24 hrs kwa wiki tokana na motives ya "HAKI SAWA" hivyo hupelekea wazazi kutojua Watoto wameshindaje kiafya, kimichezo na huenda hata wamenyanyaswa kijinsi (kubakwa + kulawitiwa + vitisho vya uhai).
3. Utandawazi, nyimbo hazina maadili kusikiliza hata kuzitazama videos zake + simu janja kuachiwa watoto + makundi mabaya ya urafiki + mazingira ya malezi mabovu.
4. Malezi ya mzazi upande mmoja (single mothers & fathers) mtoto hukosa kujiamini kisaikolojia kwa kutopata upendo wa wazazi wote wawili akijilinganisha na Watoto wenzake wa malezi ya pande 2 + sumu toka kwa single mothers.
5. Uzungu mwingi, watoto waliozaliwa miaka ya 60 - 89 wamestaarabika sana sababu ya "sticks and carrots caring systems" yani Mtoto akikosea anadhibiwa papo hapo na akifanya vizuri anatunukiwa zawadi/pongezi, siku hizi huu mfumo tumebakiwa nao wahenga pekee.
6. Kukosa uchaji wa Mungu(nguvu za kiroho) Bila maombi ya kiroho na nguvu za Mungu malezi ya watoto ni changamoto kubwa sana kwa wazazi, ijulikane shetani yupo kazini 24 hrs akitumia mawakala wake(Watu wasiomcha Mungu) kurushia Watoto mapepo wachafu.
Ndiyomaana unawezakuta Mtoto yuko vizuri sana shuleni kiakili ghafla akakataa shule hataki kabisa kusoma, au akapofuka macho kimiujiza.
7. Kukosekana kwa Mazoezi mashuleni, mazoezi huchangamsha ubongo kuwa hai kiutendaji wa akili wakati wowote, mfano enzi zetu tulikuwa tunakimbia mchaka mchaka shuleni na tukirudi home tukishamaliza kazi ni michezo lakini muda wa twisheni uko pale pale.
MAISHA NI WEWE NA KUPANGA NI KUCHAGUA.