Dkt. Mwakyembe Kuongoza Uchunguzi Malalamiko ya Mtihani wa Law School

Dkt. Mwakyembe Kuongoza Uchunguzi Malalamiko ya Mtihani wa Law School

Issue hapa siyo kufundisha shule ya msingi bali ni ile hali ya kustruggle kwa miaka 7 anatafuta digrii ya sheria halafu eti aje kuwa na ufaulu LST itakuwa ni kichekesho
Ndg MTU akiweka malengo anatusua tu bila shida, wapo maprofesa Leo WaLianza Kazi na cheti Cha darasa la saba B, leo hii ndo walimu wenu Huko varsity
 
Msingi mkubwa wa tatizo ni siasa kuwa ndio kuwa kipaumbele katika nchi hii kwa kwa ccm kuwekeza kwenye ujinga.

Sio huko tu kwenye matatizo, fani zoooote hali ni mbaya. MD anasoma miaka mitano na mmoja wa intership jumla miaka 6, akienda kazini hata kupasua jipu hawezi. Nenda kwa mainjinia hali ni hiyo, nenda ualimu hali ni hiyo.
Hilo ni tatizo la kitaifa kwa fani zote.
Matokeo yake hata profesa anaenda kugombea u diwani, u wenyekiti wa ccm wa wilaya, ubunge, n.k

Hakuna msingi mzuri kwenye shule za msingi kama neno lenyewe linavyomaanisha. Mtoto anachaguliwa kujiunga kidato cha kwanza hata jina lake kuandika ni mtihani, huko mbele ataweza nini?

Bado tuna safari ndefu hadi tutakapojitambua.
Umesema jambo la maana sana ambalo wengine labda hawalijui au hawataki kulisema. Bila kutenganisha siasa na taaluma, itakuwa ngumu sana nchi hii kuondoa ujinga.

Tunachofanya sasa hivi si kuondoa ujinga bali kuufunika kwa vyeti na ufaulu usio na msingi wa maarifa ya kweli.
 
Ndg MTU akiweka malengo anatusua tu bila shida, wapo maprofesa Leo WaLianza Kazi na cheti Cha darasa la saba B, leo hii ndo walimu wenu Huko varsity
Elewa ndugu issue siyo kuanza na cheti cha LY bali umeipataje digrii? kwa sababu kuna watu ni LY lakini uwezo wao ni mkubwa sana ila tu hawakupata nafasi ya kuendelea kimasomo. Sasa huyo ticha digrii ya kuipata kwa miaka 3 anakuja kuipata kwa miaka 7, kuna mtu hapo kweli au ndo wale wa TRAB na TRAT?
 
Uvccm wanaotegemea teuzi[emoji1787][emoji1787]
Apo eka siasa pemben mkuu.. jamaa kaongea ukwel watz tunapenda kubenwa bebwa sn mpk kwmy ishu nyeti kama elimu... kama watu wamefeli means wameshindwa kufkia passmark tusilazimishe kila mtu awe na elimu ilihali hastahili kuwa nayo
 
Nyie ni wasomi wa ajabu sana, sijui unashangilia nini, ushamba tu.

Navyojua, mwalimu hutakiwa kuweka kitu kwenye ubongo wa mwanafunzi, nyie mmeshindwa kufanya hivyo halafu mnapeleka lawama pengine, tena za kijinga, kuwa wanafunzi hawasomi, mko selfish sana.

Unataka kutuambia "wanaosoma" ni hao 26 pekee waliofaulu kati ya 600 waliofanya mitihani? kwako wanafunzi 574 wote walikuwa wanapenda starehe!. stop this nonsense.

Zaidi, hao wafanyakazi wa umma 22 uliowasifia kwa kufaulu ndio umeniacha na maswali mengi zaidi, hicho chuo kina tatizo, wafanyakazi wa umma wanafaulu kwa wingi kwenye taasisi ya umma, hapa hakuna connection?

Ajabu sana, wale wanafunzi walio busy na kazi ndio wanafaulu, halafu wale fresh from school ndio wanafeli wote kasoro wanne!
Mkuu wasomi wa nchi hii niwa hafidhina wa ajabu Sana ambao hawa paswi kuwepo katika taasisi za umma Kuna Padre mmoja anafundisha chuo fulani aliwahi niambia kwamba shinda kubwa ya wahadhiri wengi wa chuo kikuu ni kujiona wenye akili kuzidi wengine hili naliona hapa kwetu Tanzania

Ndio maana unakutana na wakili anasema vyuo vya Sasa vinatoa product mbovu ndio maana wanafeli Sana ukimuuliza Wewe ulisoma chuo gani? Jibu linakuja ni vyuo vyetu hivi hivi Sasa una mshangaa yeye kujiona product bora na kudharau product nyingine kutoka vyuo hivyo hivyo kaitoa wapi?

Kuna mhadhiri yupo SAUT anafundisha philosophy anaitwa Komu alisha sema kwamba mhadhiri ukiona unafundisha na mwisho wanafunzi wengi wanafeli basi jifanyie tathimini au jitafakari binafsi Kuna shida.
 
-Vijana wanataka first sitting ziwe 100
-Dr zakayo lukumay alisema tatizo vyuo vile vya degree pia ni tatizo.
Shida sio chuo mkuu Kuna wahadhiri wanafundisha chuo na hao hao ni wahadhiri hapo law school Sasa mhadhiri anakutana na product yake mwenyewe aliyo izalisha toka chuo kitendo Cha kusema shida iko chuo basi nae ni sehemu ya tatizo lenyewe.
 
Na bado watakuja kutana na pepa za utumoshi na watagonga 3/100, sasa ndiyo watamlilia mwalimu ummy...
 
Mwakyembe haaminiki , hata matokeo ya uchunguzi wa kamati yake hayataaminika na jamii .

Kwa mfano , alipokuwa Mbunge wa Kyela aliwahi kuwaaminisha wananchi wa Jimbo hilo kwamba ATAWATAFUTIA SOKO LA MCHELE WAO NCHINI MAREKANI , lakini hadi anapigwa chini hakuwahi kutimiza ahadi hiyo
Kuna uwezekano tume yake ikaja,ba,majibu yalkyopangwa tayari. .mtu aliikana thesis yake mwenyewe ambayo ilikuwa inatetea serikali tatu ili tu kulinda maslahi ya kisiasa ambapo mfumo ulikuwa unatetea serikali mbili.
 
Kulingana na maelezo hapo juu yupo mwanafunzi wa LST aitwaye John Kaombwe
 
Mkuu wasomi wa nchi hii niwa hafidhina wa ajabu Sana ambao hawa paswi kuwepo katika taasisi za umma Kuna Padre mmoja anafundisha chuo fulani aliwahi niambia kwamba shinda kubwa ya wahadhiri wengi wa chuo kikuu ni kujiona wenye akili kuzidi wengine hili naliona hapa kwetu Tanzania

Ndio maana unakutana na wakili anasema vyuo vya Sasa vinatoa product mbovu ndio maana wanafeli Sana ukimuuliza Wewe ulisoma chuo gani? Jibu linakuja ni vyuo vyetu hivi hivi Sasa una mshangaa yeye kujiona product bora na kudharau product nyingine kutoka vyuo hivyo hivyo kaitoa wapi?

Kuna mhadhiri yupo SAUT anafundisha philosophy anaitwa Komu alisha sema kwamba mhadhiri ukiona unafundisha na mwisho wanafunzi wengi wanafeli basi jifanyie tathimini au jitafakari binafsi Kuna shida.
Ajabu huu ujinga hao walimu hapo LST wameshaurithisha kwa wanafunzi wao, wote wanaopita hapo nao wakiulizwa kwanini wengi wanafeli, watakujibu hawakuandaliwa vizuri kule walipotoka.

Unabaki kujiuliza, huyu ndie msomi aliyefaulu hapo alipo ikiwa analaumu kule alipotoka, hajui elimu ni muendelezo wa ngazi moja kwenda nyingine, sasa ukianza kuiponda ngazi uliyotoka maana yake wanataka isiwepo au ifanyweje?

Nagundua mwisho wa siku haya yote yanasababishwa na ubinafsi, aliyenacho hamkumbuki yule asiyenacho, anajiona yeye ndie bora zaidi yake, na hii tabia ndio inazidi kuliharibu hili taifa.

Hii precedence ya kuwaponda wahadhiri wa sheria wa vyuo vikuu ikiendelea itaharibu morali ya walimu, na hilo jibu kwangu najua ni ujanja wa walimu wa hapo LST kujikwepesha lawama, wao kazi yao ni kufelisha tu, sio kuingiza kitu kwenye ubongo wa mwanafunzi.
 
Binafsi naomba nisema yafuatayo kuhusu shule ya sheria Tanzania:

Mosi, kutokana na uhitaji wa elimu ya kusoma kwa vitendo (Post-Graduate Diploma in Legal Practice) haikutakiwa kuwe na shule moja nchi nzima tena ambayo iko kwenye mji kama Dar es salaam. Walau hizi shule zingekuwepo kikanda ili kuwaepusha na kadhia wale wanafunzi wanaotoka mikoa ya mbali kuja kurudia mitihani Dar es Salaam. Mtoto anasafiri kutoka Tarime, hana hata mkopo halafu anakuja Dar es salaam kufanya mtihani akiwa na 50/50 kwamba hilo somo analorirudia atafuaulu au lah.

Pili, mbinu ya kumpima mwanafunzi (Mode of Assessment) siyo rafiki kabisa na haizingatia utaalamu wa kisaikolojia kwamba wanafunzi wana uelewa tofauti. Mtoto anasoma mwaka mzima halafu anapewa mitihani 24 ndani ya mwaka ambayo kama akifeli hata mmoja basi anaweza kupoteza zaidi hata ya miaka 2 anarudia tu kozi hiyo hiyo. Kikawaida tulitegemea kwenye elimu ya vitendo wanafunzi wapimwe kupitia kazi nyingine muhimu ambazo lazima ziwe na alama, kama PRESENTATIONS, GROUP ASSIGNMENTS, CLINICS + WORKSHOPS and INTERNSHIP WITH MARKS.

Sasa wanaitwa DIPLOMA IN LEGAL PRACTICE huku wakichukua ada ya zaidi ya milioni moja, ilhali vipimo vyote vinatolewa kupitia mitihani. Hii siyo sahihi, kwasababu hata mahakamani kwenyewe wanasheria huwa hatuviziani ila tunapewa muda wa kujiandaa. Sasa mtoto anakaa INTERNSHIP miezi zaidi ya sita huku akija kukaguliwa kihunihuni tu mara moja, bila kupewa alama yoyote ile ya muhimu. Kwanini hawa wanafunzi wasipangiwe hata miezi miwili-miwili kufanya kazi la lazima zenye alamu mahakama za mwanza, mabaraza ya ardhi, mabalaza ya usuluhishi, dawati la jinsia ???

Jingine, ambalo nimeliona ni jambo la ajabu kufanywa na watu wanaojiita wasomi ni kitendo cha kutoa matokeo ya mitihani yote ya mwaka mzima ndani ya siku moja, baada ya mwaka mzima na miezi mitatu kupita. Kwanini matokeo ya ICA (Individual Continous Assessment), WPE (WRITTEN PRACTICAL EXAMINATION) na FINALS NON-CORE hayatolewi mapema, ili mwanafunzi ajue mbivu na mbichi na aweze kujipanga vizuri kwenye mitihani ya mwisho ??? Pia wawekewe utaratibu maalamu kabisa wa kuyarudia haya masomo wakati hata wako shule, hasa wiki moja baada ya kumaliza WPE ???

Lingine muhimu ni kwamba LST, kuna mitihani ya WPE (Written Practical Examination) ambayo kwingineko duniani mwanafunzi huifanya kwa kufanya tafiti pamoja na majadiliano na wanafunzi wenzake, kisha baadae huenda kufanya huo mtihani. Ilhali sasa pale LST, wanafunzi wanafungiwa masaa manne (4) wakisoma mavitabu, bila kuruhusiwa kuzungumza halafu wanapewa saa moja kupumzika, ili warudi kufanya mtihani huohuo kwa masaa matatu. (It's just emotional debilitating)

Tatu, hili la kulazimisha kila anayesoma sheria awe wakili nadhani ni jambo la kishenzi ambalo lilifanywa kwa mihemko bila kufikiriwa. Miaka yote huko nyuma watu tuliajiriwa kama STATE ATTORNEYS bila hata kuwa wanasheria. Tulitakiwa tu tufanye INTERNSHIP miezi tisa kwa ATTORNEY GENERAL halafu tunaenda kufanya BAR-EXAMINATION kule Arusha. Kinachoshangaza ni kwamba wengi ambao hawakupita Law School wako vizuri kuliko hata hawa watoto wenu wa Mawasiliano nyuma kule.

Kubwa zaidi, wanasheria tuko kwenye nyanja kuu mbili ambazo ni LEGAL PRACTITIONER (ADVOCATES) na JURIST (LEGAL SCHOLARS/LEGAL RESEARCHERS). Hawa ni watu wawili tofauti na wanafanya kazi tofauti kabisa, sasa ukitaka kuwalazimisha wawe kitu kimoja utakuwa unapuyanga mno. Leo hii ushauri wa sheria wa JURIST unaweza kuwa una uzito kuliko hata ORDINARY LEGAL PRACTITIONER, kutokana na tafiti na ufahamu. Sasa kwenye nchi fulani ya kusadikika, wenyewe kwasababu hawana SPECIALIZATION basi wanalazimisha kila mtu awe wakili, kwamba hata JURIST haweza kutoa ushauri kama hana muhuri. Just Lackadaissical and Nonsensical....

Nne, mtaala wa shule ya sheria ni wa kizamani sana na hauwezi kumfanya mwanafunzi awe vizuri kwenye soko la kimataifa. Kuna baadhi ya masomo tulitegemea yafundishwe pale LST, lakini hayapo kwenye mtaala. Mfano, INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, INVESTMENT LAW, BASICS OF INTERNATIONAL ECONOMICS LAW/ INTERNATIONAL TRADE AND FINANCE LAW. Nchi haina wataalamu wa haya masomo, sisi tunakomaa kufundisha PROPABATE & ADMINISTRATION OF ESTATES, COMMERCIAL LAW, LEGAL ETHICS, HUMAN RIGHTS and ACCOUNTS FOR LAWYERS masomo ambayo vyuo vingi vinayafundisha na vinaweza kuyafundisha vizuri.

Kesi kubwa kama zila za makinikia, DOWANS, ESCROW n.k zinahitaji mwanasheria walau awe anajua masomo ya INTERNATIONAL COMMERCIAL ARBITRATION, ambapo anatakiwa aifahamu mikataba mikubwa BIT (Bilateral Investment Treaties), pamoja na taasisi muhumu kama ICSID, PIC, ICC. Lakini sisi tunakomaa kuwafelisha watoto masomo kama ACCOUNTS. Sijui hii nchi haina watu wenye akili kabisa. Mambo ya ajabu yanafanyika na hakuna hata anayestuka.

Tano, mradi wa LST tangu mwaka 2006 marehemu Prof. Mukoyogo aliupinga kweli kwasababu aliona hauna maana zaidi ya kuwatengenezea ulaji baadhi ya wataalamu wa pale University of Dar es Salaam. Hivi kweli, tuna uhakika kwamba haya masomo ya LST hayawezi kufundishwa vizuri kwenye vyuo ambavyo wanafunzi wanasoma wakiwa wanatafuta Shahada ya kwanza kweli ???

Jambo jingine ni kwamba wataalamu wengi wa pale LST wameamua kufanya biashara ya vitabu. Wanatunga mitihani ambayo majibu yake utayapata kama tu umenunua vitabu vyao. Hili nilishawahi kuambiwa nikathibitisha mwenyewe kwenye baadhi ya vitabu. Hii ni tabia ya kishezi ambayo inaumiza na kukwamisha wengine huku wengine wakipata ukwasi mkubwa. Mwanafunzi anataoa pesa nyingi za Ada lakini hivyo vitabu havipo maktaba, utavipata mpaka umfuate mwandishi mwenyewe na umlipe 50,000. Kwanini msiweke vitabu vingi kule maktaba wanafunzi wakavisoma ???

Sita, hivi inawezekanaje mwanafunzi ambaye amefauli vizuri shahada yake afeli vibaya kwa kiwango cha DISCONTINUE pale LST ??? Ina maana huyu mwanafunzi hafahamu kitu chochote kabisa ??? Lakini, kubwa zaidi ni hili la wanafunzi 600 kuanza pamoja, lakini wanaofaulu ni watu 30, huku nusu ingine ikiwa inafanya SUPPLEMENTARY au DISCONTINUED. Sijui kwanini hili haliwastui Majaji na Wizara. Watu hufeli, lakini siyo kwa kiwango hicho ambacho kinafanyika pale Law School.



Credit: Malcom Lumumba
Sasa hapa tume ya mwakyembe ya kazi gani tena??! Maana hii ni ripoti tosha na imesheeni sababu zote msingi za mapungufu ya hiyo law school!
 
Kuna Mwanachuo alimaliza Kidato cha 4 Mwaka 1990 akaenda Chuo cha Ualimu akafundisha Shule ya Msingi Mwaka 2000 akaanza kusoma Sheria Tumaini Dar amehangaika Mwaka 2016 akapata degree ya Sheria akaendele kufundisha Shule ya Msingi Mwaka jana 2021 akajiunga na LAW SCHOOL amekuwa ni Miongoni mwa wale 200 WALIODISCO na Yeye analalamika
je kwa Elimu hiyo na Degree hiyo ulitarajia AFAULI LAW SCHOOL?
VYUO VYETU viache kujali ADA tu kuliko UWEZO wa WANAFUNZI
Unataka kumaanisha nini hapa?!
 
Issue hapa siyo kufundisha shule ya msingi bali ni ile hali ya kustruggle kwa miaka 7 anatafuta digrii ya sheria halafu eti aje kuwa na ufaulu LST itakuwa ni kichekesho
Kama wewe ni mfuatiliaji wa learning protocols utabaini kuwa huyu anashindwa mtihani ila sio uelewa! Time exposure yake kwenye kitu kilekile kwa muda huo inampa avenues nyingi za ubobezi na ukizingatia kuwa kufaulu mtihani hasa kwa Tanzania yetu ni matakwa ya msahisha mtihani mostly.
 
Ana maana kwamba shule ya huyo mtu ni ya kuungaunga mno, hivyo siyo rahisi kufanya vizuri hapo Law school ambapo vipimo vyake vimekaza sana.

Sir robby
Sio kweli, kama umekuwepo tangia Tanganyika kupata uhuru utakumbuka kwamba watendaji wengi wa Serikali ya Mwl. JKN walikuwa wa elimu ya kujiendeleza hiki unachoita kuungaunga, lakini ndio watendaji walioweka misingi mizuri ya taifa hili ambayo inabomolewa na wasomi wa sasa wa kukariri (kumeza) kwa ajili ya paper na kisha kufaulu mtihani bila kufaulu maharifa!
 
Elewa ndugu issue siyo kuanza na cheti cha LY bali umeipataje digrii? kwa sababu kuna watu ni LY lakini uwezo wao ni mkubwa sana ila tu hawakupata nafasi ya kuendelea kimasomo. Sasa huyo ticha digrii ya kuipata kwa miaka 3 anakuja kuipata kwa miaka 7, kuna mtu hapo kweli au ndo wale wa TRAB na TRAT?
Mkaruka you're becoming too judgemental! Jitahidi kuacha kuongelea nadhalia juu ya mtu huyo mpaka umfanyie mahojiano utapata hoja nzuri za kuwasilisha jukwaani hapa.
 
Mkuu wasomi wa nchi hii niwa hafidhina wa ajabu Sana ambao hawa paswi kuwepo katika taasisi za umma Kuna Padre mmoja anafundisha chuo fulani aliwahi niambia kwamba shinda kubwa ya wahadhiri wengi wa chuo kikuu ni kujiona wenye akili kuzidi wengine hili naliona hapa kwetu Tanzania

Ndio maana unakutana na wakili anasema vyuo vya Sasa vinatoa product mbovu ndio maana wanafeli Sana ukimuuliza Wewe ulisoma chuo gani? Jibu linakuja ni vyuo vyetu hivi hivi Sasa una mshangaa yeye kujiona product bora na kudharau product nyingine kutoka vyuo hivyo hivyo kaitoa wapi?

Kuna mhadhiri yupo SAUT anafundisha philosophy anaitwa Komu alisha sema kwamba mhadhiri ukiona unafundisha na mwisho wanafunzi wengi wanafeli basi jifanyie tathimini au jitafakari binafsi Kuna shida.
Moja la vyuo na shule za siku hizi kutoa products mbaya ni sawa kwa sababu tushaona chanzo ni lugha ya kufundishia inavyotenganishwa na lugha ya taaluma fundishwa na nyongeza ni mtu aliyefeli wakati wa masomo yake kuja kuwa mwalimu wa kufundisha wengine baada ya kufaulu kwa njia zingine ambazo mmejizuia sana kuzitaja kwenye uzi huu!

Lakini pia ni kweli kuwa kufeli kwa mwanafunzi ni msiba kwa mwalimu wake, ukiona mwalimu anashangilia mwanafunzi wake kufeli ni wazi kwamba mwalimu huyo hakuwahi kufaulu kihalali wakati anasoma angetamani kuona mwanafunzi wake anajiongeza kufuata mbinu alizotumia kufaulu mwalimu huyo.
 
Mwakyembe amekaza, hataki kuachia nafasi kwenye Kamati. Sasa kamati ya Mwakyembe inapokea ushauri wa wadau, mwisho wa kutoa ushauri ni Oktoba 24,2022.
 

Attachments

Back
Top Bottom