Dodoma: RC Antony Mtaka amchana Waziri wa Elimu kuhusu mwisho wa Watoto kusoma kuwa ni saa tisa
Kuwaweka wanafunzi makambi na kurudi hiyo saa 12 ni kupoteza muda.....

Tufanye wanafunzi wakeshe kwa ajira gani?

Sisi tulikesha sana, mwisho wa siku tupo wapi?......

Kunamaisha nje ya elimu, mtoto arudi hiyo saa 9, ajifunze vitu vya ziada kama kupaka rangi, kutengeneza bustani, kujifunza ufundi wa baiskeli na magari, kujifunza ufundi uwashi.....

utamtoa saa 12 baada ya miaka 8 (form 1 - chuo) anakuwa anasjinda chumbani na laptop kusubiria ajira, hajui hata kutengeneza tuta.....

Tutengeneze mazingira mazuri ya mtoto kuwa serious na elimu kwa muda stahili na pia kupata muda wa kujifunza stadi za maisha...

Kuna mafundi wazuri wa tv, kuna graphic designers, kuna wakulima wazuri walijifunza mda wa ziada.....
 
Mkuu wa mkoa yuko sahihi, Ndalicho, Dr Dorothy Gwajima,Dr mollel, RAS shinyanya, RAS mwanza,RAS Geita, RC manyara,DED same, Kaimu DED Moshi manispaa, Hawa ni viongozi mzigo awamu ya SITA.
Mkuu umetumia vigezo vipi kuwaona hao ni mizigo? TUELIMISHE.
 
..Elimu yetu ina MATATIZO makubwa.

..Na SERIKALI ipo njia panda ktk suala hili.

..Je, waziri akiruhusu utaratibu huo ina maana watoto watakuwa hawaendi likizo na hawana ratiba za kujifunza kulingana na muongozo wa kitaalamu?

..Utaratibu wa makambi na jinsi ulivyo maarufu unaonyesha kwamba kuna tatizo ktk UFUNDISHAJI.

..Wanafunzi wangekuwa wanafundishwa inavyopaswa kusingekuwa na ulazima wa kuwa na makambi mengi kiasi hiki nchi nzima.

..Kwenye mataifa ambayo wanatoa elimu ya uhakika wanafunzi wachache ndio huhitaji msaada wa ziada. Lakini kwa hapa kwetu ni kinyume na hivyo.

..Makambi ya kujiaandaa na mitihani ni hatua ya kizimamoto. Tunatakiwa tuka-solve mzizi wa tatizo hili ili wanafunzi wote wapate ELIMU YENYE VIWANGO.
Jitahidi kutofautisha mambo
Nani kakataa watoto wasiende likizo?.

elimu hata ya chuo kikuu baada ya lecture lazima ujisomee binafsi ama kama kikundi

kuna shida gani mwanafunzi wa Sekondari kujisomea binafsi au kama vikundi mara baada ya masomo ya kawaida?

past paper mtasolve muda wa vipindi vya kawaida?homework huwa inafanywa sa ngapi?

sioni kama Elimu ina shida kiasi hicho ila wasilazimishwe kutoka sa 9 kama watu wanaridhia kuweka kambi muda wa ziada wasome
 
Kwa hiyo watoto wa Mtaka wenyewe wako shule za kata na Wana mazingira sawa na wa anaowahutubia 😁!

Ni heri hao wananchi wakawapuuza wote,Waziri pamoja na Mtaka then wawasikilize viongozi wao wa mitaa na vijiji ambao wanaishi miongoni mwao.

Uwasilishaji mbovu sana,sitoshangaa Bimkubwa akimpiga chini.

BTW:Waziri kawaambia nini wanaDodoma kuhusu saa Tisa?
 
[emoji106][emoji106]. Mkoa wa Njombe wana mkakati huo wa kambi toka miaka mingi unaitwa "UWANJO". Msingi wa kambi hizi ni kuwa Wanafunzi ambao ni senior pamoja na walimu wa shule husika husaidiana kuwaanda wanafunzi wanaojiandaa kufanya mitihani ya Form IV.
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na walimu wa shule husika husaidiana kuwaanda wanafunzi wanaojiandaa kufanya mitihani ya Form VI.
Hivyo RC Mtaka yuko sahihi kabisa. Anaanzisha kitu ambacho mikoa mingine kilishaanza miaka mingi iliyopita.
Tatizo mawaziri wanapenda kuingiza siasa kwenye kila kitu
 
..Nakubaliana na wewe.

..Naamini na wewe utakubaliana na mimi kwamba " makambi ya kukariri mitihani " ni matokeo ya elimu hafifu / duni inayotolewa ktk shule nyingi hapa nchini.

..Kwenye nchi za wenzetu wanafunzi hawapigi kambi kukariri mitihani, bali hupiga kambi kwa ajili ya klabu za debate, sayansi, mashindano ya hesabu, michezo, etc etc.

Cc Chige, Augustine Moshi , Nguruvi3
Hivi debate ama clubs za masomo nk ni kitu cha kila siku?

mbona tulijisomea extra hours na michezo tulicheza siku za michezo na usafi tulifanya kila siku na debate na clubs pia zilifanyika kwa siku husika
Ratiba za watoto zipangwe kuaccomodate na kujua activities zote
Inawezekana...ila kikubwa zaidi wapate maarifa ya shule
 
Sio privatezote ni shule za bweni, au unamaanisha hadi shule za kutwa(day) nazo wanasoma hadi usiku?
Sasa hawa wa day hawasomi shule usiku bado unataka watoke sa 9 ili?.

ndo mana on average shule za boarding wanafaulu kuliko day
Muda mwingi ni kusoma.,ratiba binafsi kidogo na michezo
 
Kunywa soda popote ulipo
Makambi ni ujinga uliopitiliza, Kama tatizo ni watoto hawafundishwi vizuri basi waangalie namna nzuri ya kuwafanyia wafundishwe vizuri kuanzia wanapoingia form 1 hadi wanapomaliza form 4. Na sio haya makambi ambayo yanalenga tu mwanafunzi kufaulu, anafaulu alafu baada ya mwezi kasahau kila kitu.
Tatizo ni ufundishaji hafifu, hapo ndio inabidi waangalie wanafanyaje. Huu ujinga nchi zilizoendelea hakuna.
Hat shule wanazofundisha vizuri watoto wanasoma mchana na usiku juu

ama mnadhani wanafaulu kimiujiza?
Hakuna miujiza kazi yao ni kufundishwa na kujisomea over
 
Wote wangekuwa na akili kama yako ingekua raha Sana, hata huyo mkuu wa mkoa hii akili hana
Hii kitu inaitwa makambi ni ujinga uliopitiliza. Watoto wanapaswa kufundishwa vizuri kuanzia siku ya kwanza anaingia form 1 hadi siku ya mwisho anamaliza form 4
Haya makambi ni kuzima moto tu, na ndio tunarudi palepale kuwa wanafunzi hawasomi kuelewa bali wanasoma kujibu mitihani
Na huo ndo ukweli huyu kazoea makambi ya KISABATO ndo anataka wanafuzi wakae makambini yani nchi nzima kila mkoa makambi? Nini maana ya madarasa. Hapa cha msingi serkali iboreshe mazingira ya kujifunzia ikiwa ni pamoja na kuboesha masrahi ya walimu.

Haya mambo ya kuhangaisha watoto kwenye makambi bado ni temporary solution, Watu wenye akili kubwa hiyo haiwezi kuwa mwafaka wa elimu yetu kwangu mimi binafsi naamini mtotot akifundisha vizuri masaa 9 yanatosha, pia wakumbuke shule sio kusoma tu pia kuna suala la vipaji vya watoto kuendelezwa kama mpira,uigizaji na talent zingine pia.

Inamaana mkuu wa mkoa anataka watu wote wawe na division one na two ili kufurahisha wazazi wakati product yake bado ni sifuri kutokana na ukosefu wa ajira.

Tatizo la elimu yetu ni kukariri ndo maana tunalazimisha watoto wasome mpaka usiku wa manne kukariri makaratasi.
 
..Elimu yetu ina MATATIZO makubwa.

..Na SERIKALI ipo njia panda ktk suala hili.

..Je, waziri akiruhusu utaratibu huo ina maana watoto watakuwa hawaendi likizo na hawana ratiba za kujifunza kulingana na muongozo wa kitaalamu?

..Utaratibu wa makambi na jinsi ulivyo maarufu unaonyesha kwamba kuna tatizo ktk UFUNDISHAJI.

..Wanafunzi wangekuwa wanafundishwa inavyopaswa kusingekuwa na ulazima wa kuwa na makambi mengi kiasi hiki nchi nzima.

..Kwenye mataifa ambayo wanatoa elimu ya uhakika wanafunzi wachache ndio huhitaji msaada wa ziada. Lakini kwa hapa kwetu ni kinyume na hivyo.

..Makambi ya kujiaandaa na mitihani ni hatua ya kizimamoto. Tunatakiwa tuka-solve mzizi wa tatizo hili ili wanafunzi wote wapate ELIMU YENYE VIWANGO.
Umeandika vizuri.
Elimu yetu ina matatizo makubwa.
Nakubali.
Mwenye jukumu la kuyatatua haya matatizo makubwa ni Waziri wa Elimu.
Asaidiwe namna ya kuyatatua.
Mahali pazuri pa kuanzia, ni kuwasikiliza Viongozi wenzake wenye uchungu na Elimu, wakiongozwa na Anthony Mtaka.
Badala ya Waziri kutoa matamko hadharani ambayo nayo pia yanajibiwa hadharani, alitakiwa akutane na Wadau, wazungumze, asikilize kwa nini zinawekwa Kambi za kujisomea, kisha akirudi Ofisini kwa PhD wenzake, wachakate walichokipata ili kutatua matatizo.
Matatizo ya Elimu hayawezi kutatuliwa kwa amri za Kipolisi za kufuata sheria pasipo shurti.
 
Naona staili ile ile ya Dialo ya kutema nyongo. Nahisi kuna kitu hakipo sawa baina ya viongozi hawa na kauli hizi. Kuna haja ya kutoa miongozo juu ya nani wa kusemea mambo yanayogusa maslahi makubwa ya wananchi kama hili la elimu na si kupingana hadharani hivi.
 
Kama nimeelewa vizuri ELIMU ya Tanzania inamatatizo haiko sawa kwamba tayari kuna tofauti ya elimu anayopata mtoto maisha bora na mtoto maisha duni/kawaida. Kikawaida mfumo wa elimu unategemea muda, mazingira, rasilimali na nyenzo zingine. Je hivyo vyote vipo au vinatosheleza kwenye utoaji wa elimu Tanzania?, Hao watoto wa mawaziri, maRC sijui wakurugenzi au hata watu wenye uwezo wananafasi kubwa kupewa elimu nzuri kutokana na uwekezaji kwenye vitu hivyo muhimu. Serikali ya Tanzania ingekua kweli ina uchungu na kizazi cha watoto wa Tanzania wangewekeza zaidi kwenye elimu kuliko mambo kama sijui mwenge, maslahi makubwa kwa viongonzi wa kisiasa, uchaguzi usio huru na haki yaani ikiwezekana waacha kununua magari ya kifahari pesa wapeleke kwenye ELIMU ELIMU ELIMU
 
Mimi napenda sana viongozi wanaothubutu ku challenge status quo. napenda sana.
 
Amesema ukweli bila kupepesa macho. Bravo Honourable Mtaka. The best RC in Tanzania
 
Waziri yupo sahihi,

Muda wa kazi wa Serikali ni saa tisa na nusu.

Waziri kafuata sheria ya kazi ilivyo.

Kinyume na hapo ni fujo.

RC amemkosea heshima Waziri.

Hakupaswa ajibu.Angepiga kimya na akaendelea na mipango yake kimya kimya tu.
Wewe umesoma shule za kina Junior ndio maana tuulize sisi tuliosoma Kayumba tukusimulie ugumu wa hii elimu ya huku kwetu.
 
..Nakubaliana na wewe kwamba RC Mtaka hakutakiwa kumshambulia Waziri Ndalichako waziwazi kana kwamba hawatumikii serikali moja.

..Mtaka angeweza kuwaambia waalimu na wanafunzi waendelee na kambi zao za mafunzo ya ziada, na yeye kama RC wao atakwenda kuzungumza na Waziri wa Elimu ili kuweka mambo sawa.

..Mambo ya international school, sijui gari yenye kiyoyozi, etc etc hayakupaswa kuzungumzwa na RC mwenye heshima zake kama Mh.Mtaka.
Hapa nimekukubali mkongwe. BTW ameomba radhi kiungwana. Tusahau tusonge mbele. Ni mtu mwema na mchapakazi.
 
Back
Top Bottom