English Medium ziko Ovarated sana. Hakuna elimu pale zaidi ya utapeli. Shida ni tumekuwa Brainwashed sana

English Medium ziko Ovarated sana. Hakuna elimu pale zaidi ya utapeli. Shida ni tumekuwa Brainwashed sana

Wazazi, mnashirikiana na shule kuwatesa watoto.

Vitoto vyenyewe bado vidogo, miaka 11-13, vinaamshwa saa 10 au 11 alfajiri kuwahi shule. Wanawahi nini exactly?

Na bado watakaa shule mpaka saa 12 kisa remedials, kurudi nyumbani saa 1 jioni.. mtoto anafika hoi, hajiwezi, hajacheza, hajafanya hobby zake. Kateseka tu.

Yote kwa faida gani?

- Mitihani ya darasa la saba haina umuhimu tena kama ilivyokuwa.
Wenye shule wanawatumia watoto wetu ku-market shule zao ili waonekane wana average ya A, ilhali hata kwa C mtoto anaenda zake secondary school. Au mnataka wakasome St. Francis na Marian? Shule zipo tu. Waliosoma huko si tumewaona chuo na mitaani tunao.

- Masomo ya ziada si kwa kila mwanafunzi kama ambavyo hizi shule zimewaaminisha. Mwanao kipanga, remedials za nini?
Acha wanaostruggle ndo wapambane.
Obviously, wanaunda tu room ya kupiga hela ya michango ya hapa na pale.

Mwisho, tuache watoto wakue kwa amani. Hizo efforts tuzitie form 4 na kuendelea, watakuwa wamekuwa wakubwa na matokeo ya form 4 yana impact mpaka kwenye admission ya chuo, so ni muhimu. Siyo darasa la saba.
Well said mkuu ndio maana watoto wangu niliwarudisha Kayumba. Wa kwanza ndio alinipuna Ems kuanzia chekechea hadi la saba
 
Utofautii ni mkubwaa mnooo, commitment kwenye public schools ni zeroo kabisaa ni huu umaskini wetu tu lkn hapafai, imagine darasa linawanafunzi 300 nini kinafanyika hapoo. Tusidanganyaneee public wanaambiwa waandike notes tu.
mbona tumesoma kwenye shule za kayumba na tukatoboa mpk University na kupata hadi Phd.?

Pesa ya kulipia mtoto ada milioni 4 ni bora uwe unamnunulia viwanja kila mwaka ili akikua akute baba yake kashamuandalia assets za kutosha.
 
lakini ni ukweli usiopingika kujua kiingereza kunampa fursa zaidi kuliko yule ambaye anajua kiswahili pekee.

Wenye biashara Kariakoo karibu robo Tatu hawajui Kingereza.
Alafu waliowaajiri wanajua.

Kuchangamkia Fursa ni akili ya mtu haihusiani na kujua Lugha Fulani

Mbona Tanzania tunajua Kiswahili kuliko Kenya lakini Wakenya wanatupiga bao Kupata Fursa kimataifa

Usijesema Watanzania hawajui Kingereza
 
Nasomesha Englisha Medoum ila ukweli ni kwamba sijawaji zikubali hizi shule, Shule zimejaa janja janja nyingi sana kuliko kutoa elimu ni full hadaa na wanajua fika kucheza na akili za wazazi wajinga

Sijawaji amini kwamba kuna elimu bora kwenye shule za English medoum, kuna elimu ya kawaida sana na tofauti yake na shiule za Serikali mimi sioni kabisa ukitoa sisi kuwa Barainwashed.

Niliwahi sema humu Baadhi ya hizi shule huwa hazina mtoto wa mwisho yaani kama Darasa lina wanafunzi 40 huwezi ona mtoto wa 40, wanaishia namba 10 na na wanadaia wamefungana. Namba 1 unaweza kuta watoto 10 huu mchezo wazazi hawajaushitukia.

Ukiondoa kupanda Mabasi asubuhi hakuna kingine ambacho nakiona kwa hizi shule. Wengi wanapondea shule za Serikali kwenda na Mifahia na vidumu vya maji ila ni sehemu ya kufundisha watoto na sio adhabu. Ni wazazi wajinga ndio wanao na mtoto kubeba fahioa kwrnda nao shule ni adhabu au ushamba.

Watoro wanakuwa legelege sana, mtoto wa shule ya Serikali anaweza panda Daladala na akenda shule mwenyewe umbali wa km 15 hapa ni mtoto mdogo darasa la 3, hii mtoto wa English medium hawezi, ni sawa na kuku wa Broiler tu. Matoto yanakuwa legelege tu.Basi la shule likiharibika hakuna kwenda shule.

English medium zimejaa janja janja sana, kuanzia kutoa elimu na hadi michango yao ya kihuni. Hakuna Englisha ya maana inafundishwa pale,watoto wanatoka pale wako kawaida sana hakuna maajabu pale.

Kucheza na akili za Wazazi na ziara zao za kwenda vijwana vya ndege kupigisha watoto picha kule ni full ujinga.Wanakuambia ziara za mafunzo, mtoto yuko Baby class anatakiwa atoe sh 50,000 ya ziara ya mafunzo.

Unatoa 50,000/ wanawanunulia watoto chips kavu, biskut na juice za azam, hapo 50,000/ imakata na ni ziara ya ndani ya mkoa. Mtoto anarudi nyumbani full njaaa ukiuliza mtoto anakuambia walitupatia juice, chips na biscut tu.
Wewe wacha kulialia humu na umasikini wako

Huna ada na shule ndiyo zinaelekea kufunguliwa, hukujipanga

Hukujipanga, hujalazimishwa shule za bure zipo
 
Katika vitu ambavyo siwezi fanya kosa nikumpeleka mwanangu shule ambayo hahawezi kumfundisha english language akaelewa vizuri pindi akiwa mdogo kwa hiyo hizi st kayumba ni big no.

Kwa ulimwengu wa sasa especially hapa tz mtoto anatakiwa aelewe lugha ya kimataifa kwa ufasaha, hisabati, na computer.
Fursa nyingi hapa nchini zinawataka wanaujua lugha yaani lugha ndio kila kitu hata uwe kilaza namna gani ukijua tu kutema yai fursa za pesa zitakutafuta na st kayumba swala la mtoto kujua lugha halipo hata walimu wenyewe hawajui.
 
Mkuu ungana nami kwenye kampeni ya Back to Kayumba Schools

Andika Uzi tuwafungue watu wengi hawajitambui

Hamna Mkuu.
Waache wafanye wapendavyo.
Ila mtu kama Kazi yake ya jasho, kipato hakifiki Milioni Moja kwa mwezi alafu anapoteza pesa English Medium hizi za mtaani atakuwa hajafikiri sawasawa.

Bora waende zile English Medium zenye waalimu WA Kenya, lakini hawa wabongo wengi wao nakuambia hawana C za kingereza sasa watakuwa wanafundisha vitu gani.

Wengine C Zao ni zile zinachechemea
 
Katika vitu ambavyo siwezi fanya kosa nikumpeleka mwanangu shule ambayo hahawezi kumfundisha english language akaelewa vizuri pindi akiwa mdogo kwa hiyo hizi st kayumba ni big no.

Kwa ulimwengu wa sasa especially hapa tz mtoto anatakiwa aelewe lugha ya kimataifa kwa ufasaha, hisabati, na computer.
Fursa nyingi hapa nchini zinawataka wanaujua lugha yaani lugha ndio kila kitu hata uwe kilaza namna gani ukijua tu kutema yai fursa za pesa zitakutafuta na st kayumba swala la mtoto kujua lugha halipo hata walimu wenyewe hawajui.
EMS hazifundisha kingereza bora ni ujinga unaendelea kule.

Bora English course za ras simba
 
Vingereza vyao vyenyewe vya ajabu ajabu the the nyingi hamna kitu

Zipo shule chache Sana wanajitahidi.

Moja ya dalili kuwa mAxi anapoteza pesa kusomesha English Medium ni kuangalia Mishahara ya hao waalimu WA English.

Hivi mtu Anayelipwa Laki mbili u tatu anajua nini kuhusu kingereza?

Wengine wanalipwa mpaka elfu 80 hata wafanyakazi WA ndani ambao ni darasa la Saba hawalipwi hiyo.

Kama Mwalimu anayemtundisha mtoto wako mshahara wake unaanzia Walau Laki tano tunaweza kusema huyo Mwalimu anauwezekano wa kumfundisha mtoto wako kingereza.
 
Mtoto wako kusoma English Medium anajiweka karibu na Connections hata ma classmates wake Wanakuwa na asilimia kubwa kufika sehemu flan tofauti na kayumba Mnaanza 100 Watafukuzwa 20 Wataacha 10 zero 50 div 3 zipo 10 div 2 zipo 6 div 1 4 kuna nini hapo? Acha ubahili
 
Mwaka huu kwenye interview nimeingia kwenye panel nakutana na wafaransa watatu wote wanakupiga maswali ndani ya lisaa lizima nguvu na mateso mtu unayopitia hata kujiandaa na kujiumama ni makubwa sitaki fedhea kama hizo ziwakute wanangu.

Tunafanya kazi na waganda watanzania wengi wanajua mambo sana lakini tunadharaulika kisa kujua lugha ambayo imetokana na mifumo mibovu ya st kayumba
Niliwahi kutana na kajamaa goba kwenye bajaji anavitoto vyake vidogo vinatema yai yaani nibalaa
 
Zipo shule chache Sana wanajitahidi.

Moja ya dalili kuwa mAxi anapoteza pesa kusomesha English Medium ni kuangalia Mishahara ya hao waalimu WA English.

Hivi mtu Anayelipwa Laki mbili u tatu anajua nini kuhusu kingereza?

Wengine wanalipwa mpaka elfu 80 hata wafanyakazi WA ndani ambao ni darasa la Saba hawalipwi hiyo.

Kama Mwalimu anayemtundisha mtoto wako mshahara wake unaanzia Walau Laki tano tunaweza kusema huyo Mwalimu anauwezekano wa kumfundisha mtoto wako kingereza.
Mishahara ya wengi inasikitisha
 
Back
Top Bottom