Hiyo sh 800 mbona haifiki hata robo ya tip tunayoacha bar? Mwulize hata Evelyn Salt anajua. Tena tuaachaga bila hata shuruti wala kulipiwa kodi yoyote. Si bora vituo vya mafuta watoaga risiti?Kazi ipo.
Yaani ndani ya mwezi mmoja bei imeongezeka kwa zaidi ya shilingi 800.
Huyu mama hana mbinu yoyote ya kukabiliana na mfumo wa bei, bando bei ghali, mafuta bei ghali, mshahara haiongezeki miaka 7.
Hii nchi sijui nani alituroga.
Safi sanaKesho mapema sana naenda kununua baiskeli gari napaki nyumbani kwanza baiskeli nitakuwa nafanya na mazoezi
Mwachen aupige wakutosha. HahahaMafuta yamepanda tena Bei, Dar Lita ya petrol kuanzia kesho ni 3148, dizeli 3258
View attachment 2210381
Bei za mafuta kuanzia April 4, 2022
Bei ya petrol kwa Dar itakuwa ni Tsh 3,148 kwa lita. Kwa watu wa Tanga watanunua kwa Tsh 3,161 na kwa watu wa Mtwara kwa 3,177 kwa lita.
Dizeli itauzwa Tsh. 3,258 kwa lita kwa Dar, na kwa Tanga watanunua kwa Tsh. 3,264. Mtwara watauziwa kwa Tsh. 3,309 kwa lita.
Mafuta ya taa hayako nyuma ambapo bei ya lita kwa Dar itakuwa Tsh 3,112. Mikoa mingine itakuwa na bei kutokana na hesabu zitakvyofanyika.
EWURA wamesema mabadiliko ya bei katika soko la dunia yamesababisha 93% ya mabadiliko ya bei
Bei za Jumla
Port Petrol
(TZS/Litre)Diesel
(TZS/Litre)Kerosene
(TZS/Litre)DAR ES SALAAM 3,015.88 3,125.18 2,980.56 TANGA 3,028.72 3,131.39 -- MTWARA 3,044.88 3,176.87 --
View attachment 2210436
View attachment 2210437
View attachment 2210438
View attachment 2210439
View attachment 2210440
Mama yupo kazini anaendelea kuupiga mwingi.Tunalamba asali
exactlyTehteh muhogo je ,tutauitaje
Au muhoho
Ova
Wakikujibu nitag!Kuna kipindi mafuta yaliuzwa lita 1500 jee hao bodaboda na daladala walishusha nauli?
Sent using Jamii Forums mobile app
mafuta yalikuwa 2,200 petrol na 2100 diesel kama sikoseiSIKU ZINAENDA KASI SANA. MWAKA MMOJA ULIOPITA UKIWA NA BUKU UNA UHAKIKA WA KUWEKA WESE LA KUFANYA MISELE YA HAPA NA PALE. KWA SASA ELFU 5 SI KITU TENA.