Freeman Mbowe: CCM ijenge mifumo ya kudhibiti viongozi wake ndani ya Chama ili wasiumize Watanzania

Freeman Mbowe: CCM ijenge mifumo ya kudhibiti viongozi wake ndani ya Chama ili wasiumize Watanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki Kongamano la Siku ya Wanawake Duniani lilioandaliwa na Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) katika Ukumbi wa Kuringe - Mkoa wa Kilimanjaro leo tarehe 08 Machi, 2023.




View attachment 2541597

Rais Samia akipokelewa na Viongozi wa Chadema kwenye uwanja ndege wa KIA baada ya kuwasili.
Rais Samia amewasili ukumbini na kupokelewa na Viongozi mbalimbali wa chadema akiwemo Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe. Mkutano huu umehudhuriwa pia na Viongozi wa kamati kuu ya Chadema, viongozi wa kanda na mabaraza, Mawaziri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, viongozi wa dini, wageni wengine waalikwa pamoja na wanachama na wapenzi wa Chadema.

View attachment 2541670
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiwasili ukumbini

CATHERINE RUGE, KATIBU WA BAWACHA
Amemshukuru Rais Samia kwa kukubali kuwa mgeni rasmi kwenye Mkutano huo na amesema kuwa hawakumualika Rais kimakosa kwani ni mwanamke mwenzao.

Amejivunia kujenga baraza imara lenye ushawishi mkubwa nchini, amemkumbusha Rais kuwa wanawake ni jeshi kubwa na wapo Milioni 31 kwa mujibu wa Sensa iliyopita. Pamoja na wingi huu, hadhi ya wanawake nchini ni ndogo, wanaishi maisha duni. Kwenye mkutano huu pekee, wanawake 3234 wamehudhuria.


View attachment 2541631
Catherine Ruge, Katibu wa BAWACHA
Amemshauri Rais Samia kutokuogopa kukatishwa tamaa na wale wasio itakia mema nchi hii ambao kwa kiasi kikubwa ni wanaume kwani mwanamke akiamua jambo lake hulifanya pasipo kurudi nyuma.

BAWACHA imetambua juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Samia akishirikiana na Mhe. Freeman Mbowe katika maridhiano na kutafuta katiba mpya kabla ya mwaka 2025. Ameomba jambo hili liendelee kufanyika kwa kasi kubwa ili matamanio ya watu yaweze kutimia.

Kuhusu Kuuliwa kwa watu na polisi, Mhe. Ruge amesema BAWACHA inalaaani vikali mauaji yanayofanywa na Polisi kwa raia wakiwa Mtaani na vituoni.

"Hatufurahishwi na mauaji yanayotokea katika maeneo mbalimbali yanayofanywa na jeshi la polisi hasa katika vituo vya polisi na maeneo mengine ya ukamataji. BAWACHA tutaendelea kutetea haki ya kuishi, haki ya uchaguzi, haki ya kupata ajira, haki ya kupata huduma bora za afya hasa za wanawake na watoto, haki hizi zote zimekuwa zinavunjwa kinyume cha Katiba" amesema Ruge


SHARIFFA SULEIMAN, MWENYEKITI BAWACHA
Ametaja mafaniko kadhaa yaliyochangiwa na BAWACHA kichama na katika ngazi ya Taifa, pia ameelezea mambo waliyofanyiwa wanawake kwenye chaguzi za mwaka 2019 na 2020 ambao amesema ulikuwa ni unyanyasi mkubwa uliofanywa kidikteta.

View attachment 2541680
Shariffa Suleiman, Mwenyekiti BAWACHA
Kwa niaba ya BAWACHA, Mhe. Sharifa akimuona ametoa mambo manne kwa Rais akimuomba-
  • Kupunguza bei za vyakula na kudhibiti mfumuko wa bei
  • Kuongeza kima cha chini cha mshahara
  • Kuboresha sekta ya afya
  • Kurejesha mchakato wa Katiba na tume huru ya uchaguzi, katiba itakayorudisha heshima ya nchi
Kuhusu suala la Wabunge 19 linaloendelea Mahakamani, Mhe. Shariffa amemuomba Rais alitazame kwa undani na kulipatia majibu. Amewakaribisha wanachama waliokimbia nchi wajisikie nyumbani nankuwahakikishia kuwa zama za kutekana na kupotezana hazina nafasi kwa sasa.

JOHN MNYIKA, KATIBU MKUU CHADEMA
Akimkaribisha Mwenyekiti wa Chama chake, Mhe. Mnyika ametoa mapendekezo ya kuikumbusha serikali pamoja na vyama vyote vya kisiasa kuwa kila jambo wanalofanya liwe linazingatia maslahi na makatwa ya wananchi kwa kuwa hii ni nchi yao. Pia, amesema watanzania wanalia ugumu wa maisha na katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.

View attachment 2541685
John Mnyika, Katibu Mkuu Chadema
Amemuomba Rais pamoja na Mhe. Mbowe katika safari ya maridhiano wanayoenda nayo kutokusahau mambo hayo mawilli.

Naomba nioneshwe sehemu Freeman Mbowe amesema "Rais Samia, CCM ilipora uchaguzi na kuumiza watu" kama heading ilivyo hapo juu!!
 
Mh. Rais Samia "Hiki KINACHOFANYIKA sasa cha mimi kushirikiana na nyie sio kirahisi, sio kirahisi kwa upande wangu na sio rahisi kwa upande wenu pia. Mimi huwa napitia comment za jamii forums na ninaona ni namna gani wanavyituandika"

Mama ni member mwenzetu ila hatujui ni ID ipi anatumia
 
Naomba nioneshwe sehemu Freeman Mbowe amesema "Rais Samia, CCM ilipora uchaguzi na kuumiza watu" kama heading ilivyo hapo juu!!

Acha kujificha , fuatilia live hapa TBC. Mbona mambo yapo wazi, shida mnajificha halafu mnaleta ubishi.
 
Upo sahihi, hiyo itategemea na utayari au ukomavu wa ansyeambiwa. Kibongobongo ni lazima rais akitetee chama chake na hapo ndiyo patawaka.
Ila kama atakuwa na maturity ya kuweza kukiri basi litakuwa jambo jema ila halutamuacha salama ndani ya Chama chake
Fundi Mchundo naona mama hajajali wahafidhina, ameonyesha maturity ya hali ya juu sana
 
Covid19 wamepewa za uso🤣
Wamepewa za uso na Nani kama sio wanachama wenu wanaopigania hizo nafasi,Sema nnachotaka kukwambia wewe jamaa na wanachadema wenu mjifunze kuwa Rais ni Taasisi na yeye sio msemaji wa mwisho, wale 19 bungeni wapo kimkakati wa kukivunja chama chenu ndo mana Rais hajalizungumzia kabsaaa.
 
Leo tarehe 8/03/2023 kunafanyika kongamano kubwa la Siku ya wanawake Duniani lililoandaliwa na ile ile Taasisi bora ya Akina Mama Barani Africa (BAWACHA)...
Hutopata bali watakuja na agenda nyingine tofaut na ile walisema wale vovido 19 watakua kweny kongamano!! Na wengine tayar humu washabadili gia wameendelea na mamb ya asali na CCM A,B...
 
Zii kivipi? Mwendazake alikuwa na akili ndogo ndio maana alishindwa kuishi na Wapinzani

Wapinzani wap? hawa wachumia tumbo?

Mpaka sasa Watanzania wanaendelea kujifunza kujua usanii wa kisiasa kwemye majukwaa ya vyama ila nyuma ya pazia ni tofauti.
 
Enzi ya Magufuli mlisema ni laana kuunga juhudi zake lakini leo kumwimbia na kumsifu Mama Rais Samia na kumuunga mkono ni baraka.

Kweli siasa ni mchezo, Hongera Rais Samia, hongera CCM, karata mmeicheza vizuri.

Kaka unataka ugomvi kila siku?

Sometimes Acha mambo mengine mazuri yaendelee,

Uwez kushindana na serikali uwez kushindana na rais

Sasa hata ukikaza inakusaidia nn?
 
Back
Top Bottom