Gari Brevis tamu sana kwa safari ndefu!

Gari Brevis tamu sana kwa safari ndefu!

Nina gari Brevis Cc 3000 hii chuma nikitangulia usinifuate aisee, gari inakimbia sana na imetulia kabisa safari ndefu huwa nakimbiza huku nacheka tu jana nimetoka Dar asubuhi mpaka Mwanza gari imetulia kabisa ukiwa speed 150 unaona kama iko speed 50.

Nina prado ila prado huwa naliacha nasafiri na brevis inakimbia sana na inachanganya haraka.
Una prado gani? Prado zipo zinazokimbia na brevis ya 2Jz pekee ndio yenye cc3000 ntingin ni 2.5
 
Mkuu, jaribu na Toyota Mark X (DBA-Grx 120), ni chuma kwelikweli. Kina comfortability ya maana, acceleration ya kufa mtu na stability ya kutisha barabarani. Tofauti na Brevis, Mark X haili mafuta kijini jini na pia ina umbo au sura yenye mvuto.

NB: Maneno yote yenye utata ni kwa lengo la kusifia na sio vinginevyo.
Iko vizuri pia
 
Hana akili huyu,anadhani mbio ndio kujua kuendesha gari!
Wanaume tuna tabia ya kutaka kusifiwa usafiri tunaotumia.

Mwenye ist atataka asifiwe gari haili mafuta, mwenye brevis/Cresta atataka asifiwe mbio n.k Ni kawaida kwetu wanaume kutaka kusifiwa gari zetu.

Ni tatizo la saikolojia tulilo nalo wanaume kama ambavyo wanawake wanavyotaka kusifiwa mawigi sijui nywele.

Tatizo huwa kubwa zaidi pale mtu anapolazimika kumiliki gari inayopatikana badala ya gari anayoitaka.

Hapa sasa ndo utakuta mtu mpo carwash anasifia gari lake kuukuu kuwa lina mbio wakati hata kuwaka limegoma baada ya kuingia maji.
 
Mimi sikuongelea mbio watu ndiyo wanakurupuka walio wajinga humu sijui wametoka fb nimesema nimetoka nayo dar mpaka mwanza na hii gari nilinunua mpya kabisa kwahiyo nimetumia muda mrefu lazima niwe nimewahi kukimbiza speed zote maana wakati mwingine unakuwa na haraka ila majinga mengi mengi humu yanapenda kudakia tu na kurefusha mambo
Ok boss. Nimekuelewa. Huenda ni namna ulivyowasilisha hoja ndo wadau wakaelewa vinginevyo.
 
Sijui ndiyo ujana maji ya moto, ila ni hatari sana🙄
Watu wamepoteza viungo, wengine wamekufa na kuacha watoto wanateseka,Kisa mbio barabarani.Kuna kampuni Moja hapa nchini, nikiwa salesman hapo speed kubwa mwisho 80,na walifunga car track system na kila anayeendesha gari, alikuwa na funguo yake ya gari kumsoma Yeye anayeendesha.Gari zenyewe ni brand new kutoka kiwandani!Zingine zinasoma hadi kms240,ole wako mara 3ikusome umeover speed!Maelezo yake uwe nayo ya kutosha.Kwa mfumo huo ajali hazikuwepo kabisa kwenye kampuni hiyo hadi nimeondoka 2013,Narudia mbio kama Ngiri sio udereva Bali ni kukuita Kifo Cha mapema na Uzembe.Mwenye masikio na Asikie maneno haya.Tahadhali Muhimu.
 
Watu wamepoteza viungo, wengine wamekufa na kuacha watoto wanateseka,Kisa mbio barabarani.Kuna kampuni Moja hapa nchini, nikiwa salesman hapo speed kubwa mwisho 80,na walifunga car track system na kila anayeendesha gari, alikuwa na funguo yake ya gari kumsoma Yeye anayeendesha.Gari zenyewe ni brand new kutoka kiwandani!Zingine zinasoma hadi kms240,ole wako mara 3ikusome umeover speed!Maelezo yake uwe nayo ya kutosha.Kwa mfumo huo ajali hazikuwepo kabisa kwenye kampuni hiyo hadi nimeondoka 2013,Narudia mbio kama Ngiri sio udereva Bali ni kukuita Kifo Cha mapema na Uzembe.Mwenye masikio na Asikie maneno haya.Tahadhali Muhimu.
Kupoteza viungo sio mbio kama umepangiwa utagongwa hata kama unatembea
 
Wanaume tuna tabia ya kutaka kusifiwa usafiri tunaotumia.

Mwenye ist atataka asifiwe gari haili mafuta, mwenye brevis/Cresta atataka asifiwe mbio n.k Ni kawaida kwetu wanaume kutaka kusifiwa gari zetu.

Ni tatizo la saikolojia tulilo nalo wanaume kama ambavyo wanawake wanavyotaka kusifiwa mawigi sijui nywele.
Mbio mkuu barabarani sio sifa NJEMA,yakikukuta ya ajali mbaya ndio tutajua!Bora ufe peke Yako kuliko upone utangulize wenzako,kichwa hakitokaa sawa Maishani.
 
Back
Top Bottom