Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Siwezi kuumizwa na kitu ambacho hakina tija kwangu ndio maana nimesema aitwe vyovyote siwezi kuzuia chochote iwe nataka au sitaki, Nafikiri umekasirishwa na maoni yangu lakini hilo lipo juu ya uwezo wako kwani haiwezekani kila mtu atoe maoni yatakayokufurahisha wewe.
Nikasurishwe kwa huu upuuzi wako mkuu?
 
Wewe nawe usituvuruge na dini dini kila uchwao sijui Nyerere Bibi Titi bla bla nyingiiii
Nchi yetu haina dini watu ndio wenye dini na tupo murua kabisa
Wewe kila siku kulia lia uislamu hivi uislamu vile wametengwa wamenyanyaswa hebu punguza kidogo unachosha
Historia kama historia so what get over it
Watu wamezaa bila kujali dini mkristo kazaa na muislamu muislamu kazaa na mkristo mkristo kazaa na mpagani muislamu kazaa na mpagani mpunjabi budhaa etc. sasa unataka watu waanze kuchukiana majumbani mwao sababu ya dini?

Old man get over it!

Mwl. Nyerere ni Baba wa Taifa utake Usitake period hupendi kusikia hili hama
Bibi Titi naye alifanya yake naye Historia yake iliandikwa tukasoma mashuleni shida iko wapi?

Chuo au vyuo ni taasisi zinazojitegemea - kubwa ni kusoma masomo sio Kusali na Kuabudu
Jenga Msikiti kufuata muongozo wa serikali period.

Udini unakupunguzia furaha na faraja

Nchi yetu haina udini acha kutufikirisha kama tupo Taliban
 
May Day,
Hivi unajua Nyerere kaja Dar es Salaam hana ndugu wala jamaa?

Unawajua waliompokea?

Unadhani endapo wazee wetu wamgekuwa wabaguzi wa dini au kabila Nyerere angefika hapo alipofika?

Wewe unaridhishwa na hii hali ya leo katika mgawanyo wa fursa 20:80?
Nilidhani Tanganyika yote ni ndugu na jamaa au Dar ilukuwa ni part ya Mombasa ? Sasa kama watangayika baadhi wasingempokea Mtanganyika mwenzao nadhani wala uhuru usingepatikana (tungekuwa hatuna umoja)

Katika Mafanikio kuna wanaosikika na wasiosikika, wengi Tanganyika walitoa michango yao, na huenda asingepokelewa Dar basi angepokelewa Ujiji (hizo zote ni happenstances) waliompokea walimsaidia ila sio kwamba ndio walimjenga (he has something extra kuliko waliomzunguka) na bila nguvu ya kila mwananchi aliyekuwepo ni kweli asingefika alipo...

Ni sawa sawa kwenye nyumba tuanze kuulizana hivi bila mlango bati au tofali la kwenye kona kona nyumba ingekuwa nyumba ?, basi tuache kuisifu nyumba na tulisifu tofali la kona....
 
Sasa unaangaika nini,nimetoa maoni yangu tu uoni kama wewe ndio mpuuzi mwenyewe!
Wewe ndiye mpuuzi unayehangaika na Nyerere kuitwa baba wa taifa.

Na mtaendelea kulialia,madrasa hazijengwi UDOM.

Labda mjenge UDOM yenu NYINGINE ambayo mtaenda kujenga misikiti na madrasa.
 
Wewe ndiye mpuuzi unayehangaika na Nyerere kuitwa baba wa taifa.

Na mtaendelea kulialia,madrasa hazijengwi UDOM.

Labda mjenge UDOM yenu NYINGINE ambayo mtaenda kujenga misikiti na madrasa.
Sawa,maliza hedhi kwanza halafu tutaendelea siku nyingine.
 
Tk...
Hakika soma mchango wa masheikh waliokuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika utajifuunza mengi.

Sina sababu ya kujificha.
Jina langu liko hapa.

Uliyejificha ni wewe.
Nini kinakutisha?
Mzee Mohamed endelea kufundisha historia..basi!

Wewe jua linazama, Hizi chuki za kidini unazopandikiza utawaachia madhila makubwa sana wajukuu zako.
 
Ndugu zanguni mjadala umepandisha watu ghadhabu nyingi na tumeingia katika kutukanana.

Mimi kama nisingezaliwa kipindi kile na watu hawa labda nisingeijua historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Labda nisingeandika kitabu kusahihisha historia ya uhuru iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni.

Labda pia nisingeguswa na dhulma nilizoona zinafanywa dhidi ya jamii iliyopigania uhuru lakini ikajikuta inakandamizwa kiasi kuwa daraja la tatu.

Nikijiuliza kwa nini hawa ndugu zetu wamefuta historia ya uncle Abdul?

Mengi maswali nikijiuliza.

Nikanyanyua kalamu kuandika "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (1998).

Yaliyotokea hata mimi yamenishangaza.

Jonathan Glassman wa Northwestern University, Chicago baada ya mimi kuzungumza chuoni kwake katika kunishukuru anaieleza hadhira kuwa hakujua kabisa historia hii niliyoandika hadi aliposoma kitabu changu.

Na hii ndiyo sababu ya wao kunialika chuoni kwao kuzungumza.

Northwestern University wanaongoza dunia nzima katika utafiti wa African History.

Kitabu changu kinasomeshwa hapo.

Vyuo vingi nimepita na kuzungumza Marekani, Ulaya na Afrika.

Nashukuru nimeibadili historia ya Tanganyika na leo historia ya kweli ndiyo hii tunayo sasa si ile ya Kivukoni.

Leo naalikwa hadi TBC chombo cha serikali kuzungumza historia ya mashujaa wa uhuru wa Tanganyika.

Tuendelee kujadiliana kwa ustaarabu.

Lipi tatizo nchini petu na waliosababisha wanafahamika.

Tuwasamehe na tujitahidi tuliondoe.
 
Wewe kila sehemu junayoenda ni kupandikiza udini na kupindisha historia. Kila ukienda mahali unafukuzwa na kukosa marafiki.

Wakati huo wewe ulikuwa professor UDSM mbona hukusema lolote, leo mhii unakuja kuwadanganya vijana wadogo humu JF kuhusu hilo wakati ulishindwa kule TANZANET ya miaka ya nyuma. Huoni aibu kupandikiza chuki kwa wajukuu zako!

Oh mara Nyerere hakuleta uhuru uhuru uliletwa na Faki, oh Nyerere hakuwa mpigania uhuru halali, wapigania uhuru walikuwa Dossi na wenzake. Oh mara huyu hapewi hiki, lakini yule kapata bila stahili. Mwishowe uttuam,bia baba yako alinyang'anywa urasi kinywani na Nyerere. Pumzika mzee mwenzangu achana na chuki usijepata vidonda vya tumbo au hypertension bure!
 
Mzee Leo Ameteleza Asamehewe Bure
Ameleta Mada Ambayo Mods Walitakiwa Waifute Haraka Kulinda Heshma Ya Mzee



Vinginevyo Nao Ziro Tolerance Haipo Kwa Wachangiaji
Mzee Ameleta Uzi Ulio Na Ukakasi Hasa Dini
 
Wewe unaridhishwa na hii hali ya leo katika mgawanyo wa fursa 20:80?

Hizi takwimu Mohamed za 20:80 ni za lini ? Yaani utawala wote wa Mwinyi, Kikwete na sasa Samia tumeona mabadiliko makubwa juu ya fursa walizozipata hao unaowatetea; lakini wewe bado unang'ang'ania hiyo ratio yako isiyo na uhalisia!! Ni vizuri ukawa objective sometimes.
 
Nashangaa sijui kwanini baadhi ya watu wanakuwa wakali kama pilipili kila Mohamed Said anapoleta story za wanaharakati wa uhuru wa Tanganyika,sijui walidhani uongo wa kumtukuza mtu mmoja tu ungedumu milele na milele!
 
Wewe kila sehemu junayoenda ni kupandikiza udini na kupindisha historia. Kila ukienda mahali unafukuzwa na kukosa marafiki. Wakati huo wewe ulikuwa professor UDSM mbona hukusema lolote, leo mhii unakuja kuwadanganya vijana wadogo humu JF kuhusu hilo wakati ulishindwa kule TANZANET ya miaka ya nyuma. Huoni aibu kupandikiza chuki kwa wajukuu zako! Oh mara Nyerere hakuleta uhuru uhuru uliletwa na Faki, oh Nyerere hakuwa mpigania uhuru halali, wapigania uhuru walikuwa Dossi na wenzake. Oh mara huyu hapewi hiki, lakini yule kapata bila stahili. Mwishowe uttuam,bia baba yako alinyang'anywa urasi kinywani na Nyerere. Pumzika mzee mwenzangu achana na chuki usijepata vidonda vya tumbo au hypertension bure!

Mohamed Said hajawahi kufundisha UDSM!!! Umemkweza sana.
 
May Day,
Hivi unajua Nyerere kaja Dar es Salaam hana ndugu wala jamaa?

Unawajua waliompokea?

Unadhani endapo wazee wetu wamgekuwa wabaguzi wa dini au kabila Nyerere angefika hapo alipofika?

Wewe unaridhishwa na hii hali ya leo katika mgawanyo wa fursa 20:80?
Kuna sababu hii 20 mkuu haikuja bure. Kuna kitu tulikisahau mpka sas kinatupiga penati watu wa pwani
 
Kuna sababu hii 20 mkuu haikuja bure. Kuna kitu tulikisahau mpka sas kinatupiga penati watu wa pwani
Sir...
Hakikusahaulika kitu.
Mwaka wa 1962 baada ya uhuru tu palifanyika First Muslim Congress chini ya EAMWS agenda ikiwa ELIMU.

Ikaamuliwa zijengwa shue za msingi, sekondari majimbo yote kwa ili sasa Waislam wajinyanyue katika elimu ambayo ilikuwa ikitolewa kwa ubaguzi baina ya wakoloni na wamishionari.

Mwaka wa 1963 pakafanyika Second Muslim Congress na ikaamuliwa kuwa ijengwe Chuo Kikuu.

Jiwe la msingi la Chuo Kikuu likawekwa na Mwalimu Nyerere mwaka wa 1968.

Hapa ndipo matatizo yakaanza.

Waislam wakajikuta wapo katika mgogoro.

Hiki kisa ni kirefu sana na nimekieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

EAMWS ikavunjwa na serikali na kuunda BAKWATA na Chuo Kikuu na miradi yote ya elimu ikafa.

Pakawa pia na njama ndani ya Wizara ya Elimu ya kuhujumu nafasi za elimu ya juu kwa Waislam.

Hili ni jambo nyeti sana kwa serikali na haipo tayari kulizungumza.

Matokeo yake ndiyo haya.

Nadhani umepata kusikia matatizo ya NECTA jinsi wanavyohujumu shule zetu Waislam tunazojenga kwa jasho, vumbi na damu zetu.

Waislam waliandamana mwaka wa 2012 kueleza vipi Ndalichako ndani ya NECTA inavyohujumu mitihani ya shule za Kiislam.

Serikali ilionya Waislam kutoshiriki katika maandamano haya lakini Waislam walikaidi na Sheikh Ponda aliongoza maadamano haya kutokea Msikiti wa Kichangani hadi Kidongo Chekundu.

Ni kisa kirefu siwezi nikaeleza kila kiu hapa.

Askari hawakuwashambulia wanaandamanaji.

Akili zilirejea na serikali ilijua kuwa Waislam wanaandamana kwa jambo la haki na laiti wakiwashambulia na labda kuwaua au kuwaumiza kwa kukataa dhulma balaa laki litakuwa kubwa.

Picha hiyo hapo chini ni kabla ya maandamano baada ya kuwahutubia Waislam Sheikh Ponda aliweka ushahidi wa hujuma mbele ya Waislam na akasema lazima tuandamane.

Hotuba ilikuwa ya kusisimua sana.

Alipomaliza ndipo akageuka akaangaia kibla akamkabili Allah kuomba dua.

Umma wote msikitini walitoka kuandamana.


1635094515792.png
 
Back
Top Bottom