Geita: Baraza la Madiwani laukataa Mkoa mpya wa Chato

Geita: Baraza la Madiwani laukataa Mkoa mpya wa Chato

Mkuu wa wilaya ya Geita Fadhili Juma amaesema amepeleka mapendekezo Serikalini ya kukataa mpango huo wa kuchukua maeneo ya wilaya hiyo kwenda Chato kwakuwa yatasababisha athari kwa wananchi.

Safi sana madiwani kuongea kama watu-huru . Pia sijaona mmevaa yale majoho ya ki-diwani na kofia zake ambazo kwa kweli ziliongeza mzigo wa gharama kwa wananchi wa Geita.

Kwa mapendekezo haya 'mkoa' wa Chato umekosa sifa na vigezo, hivyo usiundwe.
Tujikumbushe tarehe 26 Machi 2021 Mh. Samia Suluhu Hassan rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisisitiza vigezo
Majibu ya Rais Samia kwa mzee wa Chato aliyelilia mkoa wa Chato uundwe
 
Baraza la Madiwani Geita limeukataa Mkoa wa Chato. Je, Hayati Magufuli angekuepo wangeweza kukataa hiki kitu. CCM wakikusifia au wakikubaliana na wewe ujue wana maslahi au ni Unafiki tu.

Wanajitahidi kufuta Legacy ya Shujaa wetu. Sio sahihi Hata kidogo.

=======

Baraza Maalum la Madiwani Halmashauri ya Wilani Geita Mkoa wa Geita wamepinga wilaya mpya ya Busanda pamoja na hifadi ya Taidfa ya Kisiwa cha Rubondo kuchukuliwa na mkoa mpya wa Chato unaotarajiwa kuanzishwa hivi karibuni wakidai kuwa itasababisha wananchi kusafiri umbali wa kilomita 200 kwenda kutafuta huduma na na kusababisha mkoa wa Geita kukosa sifa kiutawala.

"Tunaenda kupata huduma hii Chato -- kilomita zaidi ya 200. Sasa, ni namna gani tunazidi kuwaongezea wananchi wetu mzigo wakati wakihitaji huduma. Mimi naona mapendekezo haya yaheshimiwe..." Bw. Salehe Juma, Diwani wa Kata ya Nyarugusu

Kisiwa cha Rubondo wakiache katika mkoa wa Geita kwasababu mkoa mpya ambao unaenda kuundwa, mkoa wa Chato, ukiangalia Ngara kuna misitu

Mkuu wa wilaya ya Geita Fadhili Juma amaesema amepeleka mapendekezo Serikalini ya kukataa mpango huo wa kuchukua maeneo ya wilaya hiyo kwenda Chato kwakuwa yatasababisha athari kwa wananchi.

"Maazimio ambayo natoka nayo hapa na muhtasari, topo ridhaa kuacha kisiwa cha Rubondo lakini hatutakubali. Bora mkoa usipatikane kuliko wilaya ya Busanda kuingia kwenye mkoa mpya. Tuliwapa sababu zote kwamba ukitoa wilaya ya Busanda kwenye mkoa wa Geita maana yake mkoa wa Geita unakosa sifa za kuwa mkoa."

hakuna logic mkoa mdogo kama geita kumegwa na kuunda mkoa mpya wa Chato ni bora wangeigawanya Tabora au Morogoro kwanza maana angalau ina ukubwa fulani unadunisha huduma kwa jamii.
 
Kuna mambo ata Magufuli angekuwa hai iwapo asingekamilisha ndani ya muda wake; raisi ajae angeyafuta.

Bado hospitali ya kanda, kuwekeza kitega uchumi kama hiko Chato ni kwenda kuwapelekea stress wataalamu utakaowalazimisha kwenda kuishi huko.
 
Baraza la Madiwani Geita limeukataa Mkoa wa Chato. Je, Hayati Magufuli angekuepo wangeweza kukataa hiki kitu. CCM wakikusifia au wakikubaliana na wewe ujue wana maslahi au ni Unafiki tu.

Wanajitahidi kufuta Legacy ya Shujaa wetu. Sio sahihi Hata kidogo.

=======

Baraza Maalum la Madiwani Halmashauri ya Wilani Geita Mkoa wa Geita wamepinga wilaya mpya ya Busanda pamoja na hifadi ya Taidfa ya Kisiwa cha Rubondo kuchukuliwa na mkoa mpya wa Chato unaotarajiwa kuanzishwa hivi karibuni wakidai kuwa itasababisha wananchi kusafiri umbali wa kilomita 200 kwenda kutafuta huduma na na kusababisha mkoa wa Geita kukosa sifa kiutawala.

"Tunaenda kupata huduma hii Chato -- kilomita zaidi ya 200. Sasa, ni namna gani tunazidi kuwaongezea wananchi wetu mzigo wakati wakihitaji huduma. Mimi naona mapendekezo haya yaheshimiwe..." Bw. Salehe Juma, Diwani wa Kata ya Nyarugusu

Kisiwa cha Rubondo wakiache katika mkoa wa Geita kwasababu mkoa mpya ambao unaenda kuundwa, mkoa wa Chato, ukiangalia Ngara kuna misitu

Mkuu wa wilaya ya Geita Fadhili Juma amaesema amepeleka mapendekezo Serikalini ya kukataa mpango huo wa kuchukua maeneo ya wilaya hiyo kwenda Chato kwakuwa yatasababisha athari kwa wananchi.

"Maazimio ambayo natoka nayo hapa na muhtasari, topo ridhaa kuacha kisiwa cha Rubondo lakini hatutakubali. Bora mkoa usipatikane kuliko wilaya ya Busanda kuingia kwenye mkoa mpya. Tuliwapa sababu zote kwamba ukitoa wilaya ya Busanda kwenye mkoa wa Geita maana yake mkoa wa Geita unakosa sifa za kuwa mkoa."

Kuunda mkoa mpya wa Chato ilikuwa hatua ya kumfurahisha mwendazake na siyo kusogeza huduma kwa wananchi. Haina uhalali kisiasa wala kiuchumi.
 
JPM mwenyewe alisema kwa hatakubali kuanzishwa kwa mikoa mipya kwenye kipindi chake, ameenda zake sasa wanatafuta namna ya kumuenzi ambayo hakuitaka.

Vv
 
Ningeehangaa sana endapo wangekubali kwa sasa ambapo Jiwe ni kiongozi wa Malaika huko upande wa pili.

Mama Samia aliposema wataangalia kama vigezo vitakidhi, hilo lilikuwa ni jibu la kukataa kiaina.
Wewe unaongea kinyume, mama alisema wale wanaosimamia hilo zoezi la kuifanya chato mkoa waharakishe kumpelekea vigezo na kama havijakamilika basi waseme ili vitafutwe vigezo na kuifanya kuwa mkoa! Kwa maana nyingine mama ashabariki Chato lazima iwe mkoa!
 
Wewe unaongea kinyume, mama alisema wale wanaosimamia hilo zoezi la kuifanya chato mkoa waharakishe kumpelekea vigezo na kama havijakamilika basi waseme ili vitafutwe vigezo na kuifanya kuwa mkoa! Kwa maana nyingine mama ashabariki Chato lazima iwe mkoa!
Kama aliowatuma ndio wametoa majibu haya, hapo basi hawezi kushurutisha lifanyike
 
Hawa hawa wengi wao walisaidiwa kupita udiwani wao bila kupingwa ndiyo hao hao wanamkaanga....kama leo mwendazake angeibuka wangesema wamenukuliwa vibaya!! Walimaanisha isiwe mkoa bali liwe jiji.
Ha ha ha!
 
Kuweka kila kitu Chato, si jambo lililomfurahisha kila mwenye akili, wakiwemo hao madiwani.

Kuna wakati unajiuliza juu ya uwezo wa marehemu katika kufikiri na kufanya maamuzi, unashindwa kuelewa kama alikuwa sawa wakati wote maana kuna mambo ambayo hata average brain, hawezi kufanya.
He was "kilaza" .
 
Ndio maana tunahitaji inclusive leadership - uongozi shirikisha sio utawala. Sasa mtawala kaondoka, hata hao wa Geita hawataki kujiunga na huo mkoa wa Mwendazake.
 
Kwa nini makao makuu yasiwe biharamulo na mkoa usiitwe biharamulo wachukue sehemu ya muleba, biharamulo,ngara,kakonko,bukombe na chato yenyew?
 
Back
Top Bottom