DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

DOKEZO Habari hii ikufikie Waziri wa Afya, ubabe wa Hospitali ya Muhimbili utaniua

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mkuu,
Kwanza pole sana kwa changamoto unazozipitia. Nakuelewa mimi. Kikawaida,japo maelezo hapa ni kama hayajitoshelezi,ila kuna haya:
1. Kiukweli mpaka CT-Scan, ni kwamba kuna tatizo.
2. Ili ifanyike hiyo CT-Scan au vipimo vya mashine hizo, lazima kuna daktari aliyekuandikia kufanya hivyo vipimo.
Mara zote iwe hiyo X-ray, Iwe CT-Scan, iwe MRI, Cd zinazotolewa huambatana na karatasi inayoripoti waliokupima wameona nini.
Hawa watu wanaokupima,ni watumiaji tu wa mashine hizo,hawawezi kamwe kuintapreti walichokiona na kumwambia mgonjwa. Wanaheshimu sana maagizo. Hivyo,unapopewa majibu,yanakuwa yamefungwa na hurudishwa kwa daktari alieomba vipimo hivyo tu.
Ikitokea hayupo karibu,huomba anaemfahamu mwenye uwezo wa kusoma na kuelewa.
Nadhani kutoka huko ulikozipata,iwe praiveti au hospitali ya serikali kwenda Muhimbili,ulipewa referal na ulitakiwa umuone either doctor fulani au uende kitengo furani na majibu yako,wakutengee doctor wa kuyasoma na kukusaidia.
Kama uliondoka na CD tu,bado unakosa ripoti inayoelezea ugonjwa wako,kwa sababu wengine akishasoma ile ripoti ataelewa tatizo lako hata asipocheza hiyo CD.
Kingine nachokiona hapa,hutaki kukili lakini ulikosea. Na kamwe usirudie au na mwingine asijaribu.
Wewe umesema kwamba hiyo CD kwenye computer inacheza. Ni kweli.
Ulijuaje inacheza?
Kwa sababu inapotoka sehemu kwenda sehemu nyingine,licha ya kuwa labda aliyekuandikia mara ya kwanza aliitazama,hawezi kukupa wazi wazi kuipeleka bila kufungwa,hiyo ni siri ya mgonjwa na ajuae ni daktari tu. Labda yeye akwambie mwenyewe. Sasa,kuna uwezekano pia wa wao kuisusia baada ya kuona imeletwa katika mazingira yasiyo salama. Kama ulifungua,ulitakiwa uombe radhi na uahidi kutorudia.
Maana akisema ulipewa uwaletee,ukapeleka kwingine,ana point.

Harafu,kwa jazba ulonayo hapa,inaoekana huenda ulifika ukawagombeza. Na wale jamaa wana akili mbovu asikwambie mtu. Japo hupaswi kubembeleza tiba,inapobidi huna namna.
Mi nahisi haya makosa mawili ulifanya.
Japo sikumbuki vizuri,si lazima watu wa ICT waupload ndo aicheze,kama ana computer inayoisoma ni rahisi.
Changamoto ipo tu kwenye hizo gharama.
Nadhani ungeweka wazi kitengo,na waliotakiwa wafanye hivyo.
JF ina kila aina ya watu na si kwamba hili hawalioni. We elezea shida bila kupindisha maneno,nakuhakikishia utapata msaada tena haraka sana. Na kama ni kosa ulifanya,we jishushe uwe mkweli,wengine ni watu wazima wanaelewa ujana na maumivu,utasaidiwa
Aiseee.

[emoji1666][emoji1666][emoji1666]
 
Waziri wa Afya ninaandika hili kwa uchungu mkubwa na majuto ya kujitawala, mimi ninaumwa nilikwenda hosipitali ya mkoa nikafanya X-Ray na Ct-Scan, kisha nikapewa rufaa kwenda Muhimbili.

Nimeenda Muhimbili tarehe 9/11/2023 nikiwa na CD ya Ct-Scan ili daktari aicheze kuona tatizo langu, daktari hawezi kuicheza mpaka niipeleke ICT eti waikopi waiweke kwenye mfumo wa Muhimbili!

Na ili waikopi ninatakiwa nilipe sh 86,000/=? Bila hivyo nikae na CD yangu nikafilie mbali, sina hela hiyo na pia sioni uhalali wa malipo hayo kwani hiyo CD ukiweka kwenye kompyuta inafunguka haihitaji uchawi wowote ule.

Mhe. Waziri walionipa CD hiyo ni hospitali ya Serikali na niligharamia hiyo Ct- Scan kwa ajili ya madaktari wajue tatizo langu na si kwa ajili yangu binafsi ya kutengeneza Bongo muvi, hiyo CD kwangu mimi ni nyangarakasha kwani sina utaalamu wa kuisoma na nimeingia hasara ya kufanya Ct- Scan.

Kwaheri kuonana ni majaliwa.
Dah nchi ngumu sana hii, kuja kuendelea si leo wala kesho, pole sana mkuu
 
Mkuu mimi nimekuelewa Vizuri sana na nafikir nakuelewa pia...
Ila nina Maswali kadhaa kwako!
Ulijisajili Kam mgonjwa?
Ulipeleka rufaa ili usajiliwe kwenye mfumo?
Ulilipa Pesa ya Consultation?
Ulitoa tena maelezo juu ya ugonjwa wako?

Ukinijibu maswali haya Nitaweza kukuuliza follow up Qns na baasae nitakupa mrejesho wapi ulikuwa sawa na wapi ulikosea
Hatua zote muhimu nimezipitia ndiyo sababu niliweza kuonana na dakitari na kupata huduma za awali. Naomba unieleze umuhimu wa hiyo CD kuingizwa kwenye mfumo wa Muhimbili badala ya kuwa ni kati ya mimi na dakitari wangu, mimi si mtu maarufu kiasi hicho cha kuingizwa kwenye kumbukumbu za hosipitali.
 
Wewe ni mgonjwa ujiwezi wala hujui kama kuna vifungashio vingine vinatakiwa viambatanishwe unapofanyiwa transfer...au umesahau wengine wanafanyiwa transfer wakiwa hawajiwezi na wanaoshughulikia wanakuwa hawana uelewa wowote wa hizo nyaraka, je huko Mhimbili hawana uwezo wa kuwasiliana na Hospitali iliyotoa transfer ili missing documents zitumwe? Mbona taasisi zingine wanafanya mawasiliano?
Yaani kwa akili yako timamu unadiriki kumlaumu mgonjwa kuwa amesahau nyaraka ya hospitali kwenda hospitali nyingine!!! Badala ya kutoa lawama kuwa amesahau kutumia dawa kwa wakati.

Acha kutetea upumbavu
Komaa.:
1. Hospitali haina jukumu la kufatilia majibu ulopewa ulete. Ni wajibu wako.
2. Huruhusiwi kutoa taarifa kwa wasiohusika. Na inaonekana alifanya hilo. Bora angekiri kwamba kiutunduutundu alitaka kuona kilichomo.
Niliposema kasahau ni wapi? Na kama kasahau,kasahau kwake haijabaki sospitali.
Wauguzi hawana uelewa. Hospitali nzima walikosa mtu wa kuwaelekeza?
Jeuri zenu ndo zinazopelekea matatizo kama hayo. Kikubwa narudia,humu kuna watu wenye uwezo mkubwa wa kumsaidia akapata tiba,ila kama kibri bado kipo pale pale,nenda kamsaidie
 
Mkuu Kufanya Upload ya Data ni muhimu sana Vinginevyo kama asipokubali itabidi wamcharge Pesa nyingine ya kufanya Kipimo kingine cha CT-scan...
Kwanini kwa sababu kapewa Rufaa Kwenda muhimbili na bahati nzuri kaenda akiwa na CD (Hajaiacha Nyumbani)..

Ili Daktari aweze kufanya Uchunguzi na kufanya Maamuzi kwenye mfumo wa Tiba ni lazma Data ziingie kwenye mfumo endapo Tatzo litakuwa kubwa au linahusu kitengo kingine aweze Kupass Kwenda kitengo husika ndani ya mfumo wa matibabu ..Hivyo kufanya Registration ya Matibabu ikiwemo kuandika historia yake,Vipimo na uchunguzi uliofnywa kwa Taarifa za kidaktari ni muhimu kuliko chochote kile..
Cha msingi kama ataweza aongee na ICT hapo waiupload chap au afanye njia yoyote...

Mifumo kwa sasa ya utibuji Afya haisomani....
Hilo swala lipo kwenye mchakato Though Kuna pilot kama Tatu zilishafeli kutokana na ufinyu wa mtandao na vitendea kazi
Ishu ni kwamba kwanini DAKTARI asiweze ku_upload yeye mpk Mgonjwa aende kwa mtu wa ICT?

Kingine.. unavyosema ufinyu wa Mtandao unamaanisha nini exactly..?
 
X-ray na CT scan vyote vinaonesha kinachoendelea ndani ya mwili wako na vinawekwa kwenye mfumo wa picha ili dakitari aone, sasa kwanini nilipie kiasi hicho cha fedha huku lengo la kulipia kufanya ct-scan ni kumuwezesha dakitari aone kinachoendelea ndani ya mwili wangu, hiyo sh 86,000/= ninalipia nini tena?
 
Ishu ni kwamba kwanini DAKTARI asiweze ku_upload yeye mpk Mgonjwa aende kwa mtu wa ICT?

Kingine.. unavyosema ufinyu wa Mtandao unamaanisha nini exactly..?
Mkuu,ni kweli hapa tunaongelea sensitive case na issue,lakini. CD haiwezi kuwa tatizo. Ripoti inayoambatana na CD na yenyewe inatosha. Nadhani wenye uelewa wajitokeze au kama kuna mtu wa Mhimbili kitengo husika,aje hapa atueleze utaratibu huo unatoka wapi
 
Ndo nimeuliza maswali mkuu..
Ulijisajili ulipofika Hospitali nyingine?
Ulilipia pesa ya Consultation?
Kila kitu nimelipia pasi na shaka, ila hilo la kulipia ili iwekwe kwenye mfumo wao kwangu mimi ni nje ya kuhudumiwa.
 
Toka ameondoka mwamba mtetezi wa wanyonge Hali hii ipo karibu Kila sekta serikalini.
 
Kumbee! Hongera! Au unadhani una kinga ya matatizo wewe! Leo kwake kesho kwako.
tatizo letu wabongo hatupendi kuambiwa ukweli.! afuate utaratibu uliowekwa na mamlaka husika apate matibabu.

Leo unakuta mtu analalamika system mbovu wakati uchaguzi ukifika unamkuta polling station na kikofia chake na litisheti likubwa la kile chama cha matapeli, useless 🛃
 
Ndugu zangu hili tunaloongelea hapa linawapata wengi, wapo wanaishia kimya kimya na wengine tumo humu ili tujaribu kujitetea na kuwatetea wasio na sauti kama yule mama mzazi aliyefariki Handeni.
 
Waziri wa Afya ninaandika hili kwa uchungu mkubwa na majuto ya kujitawala, mimi ninaumwa nilikwenda hosipitali ya mkoa nikafanya X-Ray na Ct-Scan, kisha nikapewa rufaa kwenda Muhimbili.

Nimeenda Muhimbili tarehe 9/11/2023 nikiwa na CD ya Ct-Scan ili daktari aicheze kuona tatizo langu, daktari hawezi kuicheza mpaka niipeleke ICT eti waikopi waiweke kwenye mfumo wa Muhimbili!

Na ili waikopi ninatakiwa nilipe sh 86,000/=? Bila hivyo nikae na CD yangu nikafilie mbali, sina hela hiyo na pia sioni uhalali wa malipo hayo kwani hiyo CD ukiweka kwenye kompyuta inafunguka haihitaji uchawi wowote ule.

Mhe. Waziri walionipa CD hiyo ni hospitali ya Serikali na niligharamia hiyo Ct- Scan kwa ajili ya madaktari wajue tatizo langu na si kwa ajili yangu binafsi ya kutengeneza Bongo muvi, hiyo CD kwangu mimi ni nyangarakasha kwani sina utaalamu wa kuisoma na nimeingia hasara ya kufanya Ct- Scan.

Kwaheri kuonana ni majaliwa.
Mkuu,mtafute Komredi BASHITE ndio asaidie hilo suala lako,huoni KENGE zinavyomsifia humu kwamba anatatua matatizo ya Wananchi papo kwa papo?au kuna zile KENGE LUCAS MWASHAMBWA, JIDULABAMBASI nk ziambie zikusaidie shida yako?zaidi ya hapo hiyo CD wamelekee Bongo Movie tu
 
Hatua zote muhimu nimezipitia ndiyo sababu niliweza kuonana na dakitari na kupata huduma za awali. Naomba unieleze umuhimu wa hiyo CD kuingizwa kwenye mfumo wa Muhimbili badala ya kuwa ni kati ya mimi na dakitari wangu, mimi si mtu maarufu kiasi hicho cha kuingizwa kwenye kumbukumbu za hosipitali.
Mkuu kuna kitu kimoja unakisahau sana (Samahani kusema hivyo)
Kumbuka Taarifa zako zote za ugonjwa pamoja Na CT-Scan ulopiga zipo Huko Hospitali ya mkoa ulikotoka..

Muhimbili ni hospitali Ya Rufaa Haiwezi kurelly Kwenye Report uliyokuja nayo kutoka Hopitali nyingine hii hairuhusiwi katika Refferal system guildlines..

Kusoma report uliyokuja nayo atasoma Ili kujua Anaanzia wapi kuangalia na nini hasa afanye zaidi ili.kugundua tatizo lako..
Hawezi kuchukua Moja kwa moja Report iliyoandikwa na hospitali Nyingine na yeye akaifanyia kazi bila kufanya na yeye uchunguzi wa vipimo vilivyofanywa ikiwa atarely only kwwnye report ya uchunguzi uliyokuja nayo bila kuangalia CD uliyoleta...

Unfikiri kama Yule Daktari wa Ulikotoka alikosea Kuku-Diagnose na yeye akachkua report yko kama ilivyo Ingekuwepo maana ya Wewe kupewa Rufaa

Umuhimu wa kuingizwa Taarifa zako Kwenye Mfumo wa kimatibabu (HMIS)
Kuingiza Taarifa zako katika mfumo wa kimatibabu ni muhimu sio lazima uwe maarufu kwa sababu kwanza...

  • Inafanya Taarifa zako ziwe more accesible na jopo jingine la madaktari kama Taarifa zako zitabidi zitatuliwe na Wataalamu wa juu zaid kama mabingwa zaidi...hakutakuwa na haja tena ya kwenda kitengo kingine wakuulize maswali ambayo tayari wanayoma kwenye mfumo au kufanya vipimo ambavyo tayari vimeshafnywa
  • kutafanya iwe vyepesi kurejea Taarifa zako za kimatibabu pale ambapo Utapata tatizo jingine na ili wajue jinsi ya kukusaidia ensapo tatizo jipya linaweza kuwa ni chanzo kutoka tatizo la zamani
  • mambo ya legas cases pia
  • ziko nyingi sana ila ni muhimu taarufa kutunzwa kwa ajili ya marejeo ya baadae
NB: kumbukumbu za Hospitali hawaingizwi maarufu tu ni kwa sababu ya Taarifa za kimatibabu kwa ajili na kwa ajili ya ofisi...

Nakupa scenario chukulia Umetibiwa Muhimbiri miaka Mitatu ilopita lets say Kisukari na ukawa unatumia Dawa aina fulani ambazo ulipewa umetumia dawa kwa muda mrefu na una Mzio (Allgy ) na dawa fulani ukitumia unazidiwa..
BAada ya miak miwili umepelekwa ukiwa umepata ajali n hujitambui unafikiri zile Taarifa zilizowekwa hazitakufaa kuchagua aina ya matibabu Utakayopewa?
 
Pole sana mkuu, hii ndio ccm, iyena iyena nyigiiiiiii wizi kila kona
 
tatizo letu wabongo hatupendi kuambiwa ukweli.! afuate utaratibu uliowekwa na mamlaka husika apate matibabu.

Leo unakuta mtu analalamika system mbovu wakati uchaguzi ukifika unamkuta na kikofia chake na litisheti likubwa la kile chama cha matapeli, useless 🛃
Ulichokiandika hapa umesoma vizuri maelezo yangu yote? Kama umesoma sema nilipokosea ni wapi.
Kwa kifupi CD na tipoti ya maandishi kuhusu kinachoonekana kwenye picha nimewasilisha na malipo muhimu nimelipa.
 
Mkuu kuna kitu kimoja unakisahau sana (Samahani kusema hivyo)
Kumbuka Taarifa zako zote za ugonjwa pamoja Na CT-Scan ulopiga zipo Huko Hospitali ya mkoa ulikotoka..

Muhimbili ni hospitali Ya Rufaa Haiwezi kurelly Kwenye Report uliyokuja nayo kutoka Hopitali nyingine hii hairuhusiwi katika Refferal system guildlines..

Kusoma report uliyokuja nayo atasoma Ili kujua Anaanzia wapi kuangalia na nini hasa afanye zaidi ili.kugundua tatizo lako..
Hawezi kuchukua Moja kwa moja Report iliyoandikwa na hospitali Nyingine na yeye akaifanyia kazi bila kufanya na yeye uchunguzi wa vipimo vilivyofanywa ikiwa atarely only kwwnye report ya uchunguzi uliyokuja nayo bila kuangalia CD uliyoleta...

Unfikiri kama Yule Daktari wa Ulikotoka alikosea Kuku-Diagnose na yeye akachkua report yko kama ilivyo Ingekuwepo maana ya Wewe kupewa Rufaa

Umuhimu wa kuingizwa Taarifa zako Kwenye Mfumo wa kimatibabu (HMIS)
Kuingiza Taarifa zako katika mfumo wa kimatibabu ni muhimu sio lazima uwe maarufu kwa sababu kwanza...

  • Inafanya Taarifa zako ziwe more accesible na jopo jingine la madaktari kama Taarifa zako zitabidi zitatuliwe na Wataalamu wa juu zaid kama mabingwa zaidi...hakutakuwa na haja tena ya kwenda kitengo kingine wakuulize maswali ambayo tayari wanayoma kwenye mfumo au kufanya vipimo ambavyo tayari vimeshafnywa
  • kutafanya iwe vyepesi kurejea Taarifa zako za kimatibabu pale ambapo Utapata tatizo jingine na ili wajue jinsi ya kukusaidia ensapo tatizo jipya linaweza kuwa ni chanzo kutoka tatizo la zamani
  • mambo ya legas cases pia
  • ziko nyingi sana ila ni muhimu taarufa kutunzwa kwa ajili ya marejeo ya baadae
NB: kumbukumbu za Hospitali hawaingizwi maarufu tu ni kwa sababu ya Taarifa za kimatibabu kwa ajili na kwa ajili ya ofisi...

Nakupa scenario chukulia Umetibiwa Muhimbiri miaka Mitatu ilopita lets say Kisukari na ukawa unatumia Dawa aina fulani ambazo ulipewa umetumia dawa kwa muda mrefu na una Mzio (Allgy ) na dawa fulani ukitumia unazidiwa..
BAada ya miak miwili umepelekwa ukiwa umepata ajali n hujitambui unafikiri zile Taarifa zilizowekwa hazitakufaa kuchagua aina ya matibabu Utakayopewa?
Mbona CD dakitari ameweza kuifungua, kwahiyo unanishauri nipige picha hapo nyingine ya x-ray na ct-scan!
 
Daktari aliyeitisha vipimo huko ulikotoka ndo alitakiwa aandike ripoti ya kilichoonekana ili uende nayo huko muhimbili, daktari wa muhimbili anaweza kuamua kutoa matibabu kwa kuzingatia ripoti uliyokuja nayo au akaamua kufanya vipimo upya.......hilo la kusoma CD au vipimo ambavyo hajaagiza yeye vifanyike sidhani kama huwa wanakuwa radhi kwa hilo.​
 
Back
Top Bottom