Habari Njema; Nimeidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Kutoa Elimu ya Fedha

Why easy money,Ukae na hela yangu for 25 years unipe 15%. ?

Inflation ni 4.6 to 6 kwa mwaka. Mnaakili nyie?
15% ni Kila mwaka na unaweza kuuza bond yako anytime ukitaka, biashara chache sana Kwa bongo za kukupa 15% net profit, hata Kwa hiyo inflation rate & taxes bado utakuwa net on green, wala usiwe na wasiwasi tumezungukwa na nchi nyingi kuanzia Zambia,Kenya, Uganda etc kama wewe ni hustler wa bond market hizo nchi zote zina top 20% Kwa 10 years, lakini angalia sana taxes na inflation rates, wahindi na wachina ndio biashara yao kubwa sana sasa Africa, hizi serikali zetu ni ovyo lakini likija swala la kulipa hizi security wako vizuri sana
 
labda uwe na mtaji kaka but siwezi chimbia milion 10 kwa mwaka kupata 1.5 net achilia inflation kodi
 
✅👏👏👏🙏
 
Mkuu unamjua Andrew tate?

Kama unamjua, mtazamo wako ni upi kuhusu mafunzo yake ya kuupata utajiri?
Ndiyo mkuu, Tate namjua, lakini sijawahi kufuatilia mafunzo yake kwa kina juu ya utajiri.
Hivyo siwezi kucoment vizuri juu ya mafunzo yake.
Kuna watu kama Alex Hormozi ndiyo nimekuwa najifunza zaidi kwao na naona model zao zinafanya kazi vizuri hata huku kwetu.
 
Utakuwa tajiri kwa kuuza vitabu mzee ulivyoviandika...
Wengine wanasaka utajiri kwa kutafuta mali kuzigeuza pesa
Mimi binafsi hakuna mtu anaye weza kunifundisha au kunipa elimu ya kutafuta utajiri,kwa kusoma vitabu vyaje

Ova
Wazee wa kuhamisha magoli,
Mkijibiwa kitu kimoja, mnakimbilia kingine.
Kafie mbali na akili zako za kimasikini.
Utajiri sahihi unaanza na maarifa, kama unayo maarifa sahihi huwezi kucoment upupu kama huu hapa.
Na kama unaweza kucoment upupu kama huu, huwezi kuwa tajiri.
Panga na chagua.
 
tajiri anazaliwa asikudanganye mtu.

unaweza soma hicho kitabu na kuishia kama mhariri tuh
Mkuu, utaniwia radhi lakini hiki ulichoandika hapa ni ugoro mtupu.
Na kama wewe mtu mwenye access ya teknolojia kubwa kiasi cha kuweza kucoment ujinga kama huu, ni hasra sana kwa taifa, maana mkulima masikini asiyekuwa na rasilimali ulizonazo atakuwa na tumaini gani?
Jitathmini mkuu, unakuwa aibu kwa taifa.
 
Kama ningekisoma mapema kile kitabu cha THE RICHEST MAN IN BABYLON pengine ningekuwa mbali zaid ya nilipo..but sio haba...kile kimeakisi sana uhalisia wa hustling kuliko vitabu vingine
Umesema vyema mkuu,
Kile kinabu kinapaswa kuwa requred reading kwa mtu yeyote kabla hajashika pesa yoyote ile.
Lakini hakuna kuchelewa, unapojifunza ndiyo unafanyia kazi.
 
Asante sana mkuu kwa maoni haya mazuri ya kutia moyo kwenye hii harakati kubwa niliyonayo.
Hawa nawajua, hawanisumbui, miaka 10 iliyopita niliweka andiko hapa kuhusu kutajirika kwa elfu moja (Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutajirika Kwa Kuanza Na Shilingi Elfu Moja), walinikatisha tamaa sana, nilifanya, leo miaka 10 baadaye nafurahia na wao bado wanahangaika.
Kwa hiyo kuwajibu hapa ni sehemu tu ya kuchangamsha hii mada iendelee na siyo kwamba nawachukulia serious kiasi hicho.
Asante na karibu sana mkuu.
 
labda uwe na mtaji kaka but siwezi chimbia milion 10 kwa mwaka kupata 1.5 net achilia inflation kodi
Hili ni somo pana mkuu,
Hesabu siyo rahisi kihivyo, kuna vitu vingi hujazingatia hapo.
Lakini hakuna sehemu nzuri ya kukuza utajiri kama uwekezaji, hasa kwenye masoko ya mitaji.
Nitaendelea kutoa hii elimu hapa, fuatilia ili uweze kufunguka na kuchukua hatua sahihi.
 
Kuna mahali nilikusikia kuwa ulipata straight A kwenye PCB. Imekuaje hukuwa Dr?
Ndiyo mkuu,
Nilipata Division one ya point tatu form six, yaani A Physics, A biology na A Chemistry,
Kitaaluma ni daktari wa binadamu, nimehitimu chuo kikuu cha Muhimbili.
Na niko na harakati za kujenga utajiri mkubwa.
Karibu tuambatene pamoja mkuu.
 
Hongera Kaka, nakumbuka for the first time ulinitumia vitabu bure kabisa kupitia emalil yangu.. hii ilikuwa 2015 ambapo nilikuwa bado mwanafunzi wa Chuo Kikuu.

The richest man in babylon, Poor dad.. uendelee kubarikiwa Kiongozi.
Asante sana mkuu kwa mrejesho.
Naamini vitabu vilikusaidia sana.
Karibu uendelee kupata elimu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…