Hali ilivyo Stendi Kuu ya mabasi Chato

Hali ilivyo Stendi Kuu ya mabasi Chato

Umefika Chato lakini mkuu? Unajua magari mangapi yanaanzia safari zake Chato? Unajua magari mangapi yanapita Chato kuelekea Mwanza kutokea Bukoba na kutokea Bukoba kwenda Mwanza?

Hiyo video ni ya stendi ndogo ambayo ukifika saa 11 jioni hakuna mtu wala gari kabisa.
Stendi ya mabasi ndo ilikua inakamilishwa lakini ndo itakuwa hahari kuliko hiyo ya magari madogo. Kumbuka hakuna Basi inayoanza safari yake Chato hivyo stendi ya Mabasi kuna Mabasi yataanza kupita hapo saa tano asubuhi kutokea Mwanza kwenda Bukoba na pia zitapita hapo saa tatu/nne kutokea Bukoba kwenda Mwanza.
Stendi kubwa utashangaa haina watu kabisa.

Wito: Serikali ichukue hatua madhubuti namna ya kutumia hayo majengo ili kuyaokoa na uchakavu kwasababu yatakaa muda mrefu bila kutumika tofauti na hapo SIJUI.
Umenena vema. Ni kweli stendi ya mabasi makubwa haijaanza operation. Ila hii ya kwenye video ni stendi ndogo na inafanya kazi mpaka saa 12 jioni. Magari yanayotoka chato kwenda Mwanza kweli ni machache e.g Mkwema, & stendi ndogo inafanya kazi kila siku (Mabasi ya kwenda katoro, Muganza, Mwanza, Bukoba, Mutukura e.t.c yanapakia na kushusha abiria hapo daily!)., Wamachinga wapo, wamama wanaouza maziwa wapo, wapiga debe wapo, mama ntilie wapo, bodaboda na bajaji wapo daily kujipatia riziki kdg. Let's avoid pessimism wakuu! . Nakataa mtoa mada kupost video indicating stendi iko completely dormant. Let's be optimistic bhana..
 
Mheshimiwa alikua na msimamo sana. Alichokipanga kichwani kwake ilikua lazima akitimize. Najua alitamani sana kuwainua watu wa Chato maana ni kwao. Ni kitu kizuri, ila angewasaidia kwa kufuata utaratibu unaotumika kuinua wilaya zingine hapa nchini na sio kufanya ki upendeleo kama alivyofanya yeye.

Kilichomuharibia, hakua smart kwenye ulimwengu wa siasa na uchumi. Fedha za umma huwezi kuzitumia hivyo. Alishindwa kuset vizuri na kuzisimamia priorities za nchi.

Achana na Chato, ulishawahi kwenda ile Stand kubwa ya Dodoma? Jengo kubwa, vyumba vingi ambavyo havijapangishwa, eneo kuuuubwaaa for what? Kwanza Bus nyingi hazipiti pale. Siku za katikati ya wiki ukiwa unahitaji kusafiri haraka ukaenda kule nanenane ndio umebugi kabisa, hamna kitu. Pamepoa vibaya mno mpaka unajiuliza nini ilikua Motives ya Serikali kuweka nguvu kubwa hivi? Bora hata wangefanya Chuo pangekua utilized vizuri kuliko walivyofanya Stand lile eneo!

Anyway, kila mtu na kichwa chake!
Ni suala la watendaji kutengeneza na kusimamia by-laws, ili miradi hiyo iwe na tija.
 
Ni makusudi tu inafanyika, maana sijaona sababu yakuwa hivyo maana kama mabus chato pale yanapita na yanakwenda na kutoka pia.. Nafikiri kuna mtu anataka kujustify anachowaza na kuamini.
 
Maghufuli bhana badala ya kureinforce Mwanza sehemu ambayo chochote ukiendeleza lazima kilipe anaenda kule chato , moja ya akili mbovu Sana hyo

Mwendazake amekwenda na stendi yake!!! R.I.P kwa Mwendazake. . .!!! R.I.P Kwa Stendi. . .!!!

Hizo fremu wakipangisha hata kwa Tsh 10,000/= kwa mwezi, hawapati mpangaji ng'o.
Kwani kuna Wilaya ambayo haikupata Stendi? Tena si bora Chato palichelewa sana hiyo stendi imemalizika mwaka jana?

Juzi nilifika Iringa huko Stand mpya Igumilo sijui wanapaita pamepoa vibaya mno! Nenda Kibaha stand ilipo! Nafikiri walikuwa na malengo ya kutanua miji kwaiyo sion kama ni issue
 
Chato international airport! Runway kilometer 3
Screenshot_2023-03-15-17-24-22-05_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg
 
Hii ndiyo hali ilivyo katika stendi ya mabasi chato, Je tatizo ni nini? au watu wapo busy na kilimo hawasafiri tena? Je Nini kifanyike kwenye huu mradi ili fedha (kodi za wanyonge) zilizotumika ziweze kuwanufaisha wananchi?
Mwenye stendi yake alishakufanayo
 
Kuna mwingine anaitwa Kisamv anataka nchi igawanywe kwa sababu kuna watu wanamsema vibaya jiwe huku serikali na chama vikiwa kimya tu!
Mods tunaomba hio video iondolewe mara Moja
Na huu Uzi ufutwe mara Moja

Kila comment humu Ina m portray JPM aonekane ni mtu mbaya


SIO MANENO YANGU...ALISIKIKA MCHANGIAJI MMOJA
Cc
 
Hii ndiyo hali ilivyo katika stendi ya mabasi chato, Je tatizo ni nini? au watu wapo busy na kilimo hawasafiri tena? Je Nini kifanyike kwenye huu mradi ili fedha (kodi za wanyonge) zilizotumika ziweze kuwanufaisha wananchi?
Tuletee kwanza hali ya Airport
 
Back
Top Bottom