Happy Birthday Rais Samia! Mwenyezi Mungu akujalie maisha marefu
Happy birthday Her Excellency Madame President. Ni siku njema kutumia siku hii kwa kuanza upya. Kusahau na kurekebisha kasoro zote. MBOWE SIYO GAIDI.
 
Mbaraka bin Shomari (1897)

9) Wakatabahu khadimu, Mimi kijitu fakiri.(9) This was written by a servant,
I’m an unimportant, poor person
Jina langu mwalimu, Mbaraka bin Shomari.My name is Mwalimu, Mbaraka bin Shomari.
Nimesifu mwazzimu, Mfalme akhiyariI’ve praised the Great, the beloved Kaiser —
Hapana tena hapana, wewe ndio
Kaizari!
There is nobody else. You are the Kaiser!
11Mbaraka bin Shomari
 
Toka maktaba :

Sisi raia inabidi tukae kutunga shairi , wimbo au tenzi kukumbuka siku hii adhimu ya kuzaliwa mtawala wetu Maulana King George V.

Heshima ya King George V ( “Respect for King George V”)16 Kaniki Nguo ya Kale, Dar es Salaam Mambo Leo (c.1923-36)

(1) Leo siku ya tatu katika mwezi wa Juni(1) Today is the third day in the month of June
Kazaliwa Bwana wetu King
George Sultani
When was born our lord and sultan King George
Jamii ya wote shime andameni
Mkongeni
Everyone hurry up and proceed to Mkongeni
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(2) King George ni mwana wa King
Edward
(2) King George is the son of King
Edward
Amezaliwa Ulaya nchi ya upande wa kaskaziHe was born in Europe in a country to the north
Kama tujuavyo yeye ni pekee asadi17As we know he is a special lion
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(3) Watakutana mabwana wakubwa na wadogo(3) The noble and the lowly will participate
Hapazuiwi kijana akuambiaye ni mrongoNo youth will not be denied; whoever tells you otherwise is a liar
Wala fujo hapatakuwa ya mafimbo na magongoNor will there be disturbances with sticks or clubs
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(4) Siku hiyo ni siku ya furija na anasa18(4) This day is a day of celebration and entertainment
Atakayejaliwa kwenda furaha hatakosaWhoever attends will certainly be happy
Kwani ni siku ya idi bashasha yatupasaFor it is a holiday and we are expected to be joyful
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(5) Atahudhuria Gavana bwana wa
Tanganyika
(5) His Lord the Governor of
Tanganyika will attend
Siku hiyo mwenye nishani itampasa kupachikaOn this day whoever has medals should wear them
Asiyekuwa na mwana hata jiwe ataeleka19The one without children should carry a stone
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(6) Akina Bwana Askari hupanda wao farasi(6) The soldiers will mount their horses
Mwendo wao taratibu kama mwendo wa papasiThey will pass slowly by, at the speed of a tick
Kuwaonyesha raia mambo yasiyo kiasiTo show the citizens extraordinary things
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(7) Tazameni ibura ya Mfalme kuwa
Ulaya
(7) Look at this extraordinary celebration for a king who is in
Europe
Huko mambo mbayana kama amehudhuria20There [at Mkongomeni] things will be celebrated as though he were attending
Jamaa ukaidi wani mbona mtaangamia21What’s the point of being stubborn lest you be destroyed?22
Tukatazame heshima ya maulana King George.So we see respect paid to His
Highness King George
(8) Kuna wingi wa Polisi wazuiao hatari(8) There are many police to prevent danger
Wapitisha kwa kiasi zote pia motakariThey only allow selected motorcars to pass
Hiyo ndiyo dunia wala nyingine haiwiThat is indeed how the world is.
It cannot be otherwise
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(9) Mfalme King George wote mnamjua(9) Sovereign King George all of you know him
Kwa alama za mataji mara utamjuaBy the symbol of his crowns you’ll immediately recognize him
Na utakapo ya zaidi soma utajuaAnd if you want to know more, read about him
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(10) King George ana sifa kupenda wake raia(10) King George is known for liking his subjects
Walio bora na hafifu wote twamfurahiaThe upper and lower classes we all are happy for him
Tumwombee Rabuka huruma amzidishieLet us pray to God will show more mercy to him
Tukatazame heshima ya maulana
King George.
So we see respect paid to His
Highness King George
(11) Sifa hapa zimekoma mwaka huu najaribu(11) The praises end here, this year I am trying
Labda nitapata yangu huwa bahati nasibuPerhaps I will have my luck
Sikukaa nasimama nangoja yangu matulubu23I am not sitting, I stand, waiting to get what I expect
Tukatazame heshima ya maulana King George.So we see respect paid to His
Highness King George
15The following example of another birthday poem for King George composed by a poet with the pen name “Komagi bin Sansa
 
Hepi besdei le présidant
wasafifm~p~CZOrWONsefq~1.jpg
images%20-%202022-01-27T123229.153.jpg
 
Jinsi ya kusherehekea siku ya kuzaliwa mtawala

Sikukuu ya Kuzaliwa Mfalme ( “King’s Birthday”)25 Komagi bin Sansa, Tabora Mambo Leo (c.1923-36)

(1) Wenzangu nawahubiri, sikukuu imefika!(1) My fellows, I’m preaching to you: the birthday is here!
Sote tukae tayari, tuadhimishe ushirika!We should all be ready to celebrate together
Wala siyo kukasiri, raia tumefurahika,And we shouldn’t be angry. We citizens are happy
King George mtajika, Mfalme tunayemkiri!The renowned King George is the king we accept!
(2) Tunamtakia heri nyingi, na baraka,(2) We wish him best wishes and blessings
Mfalme mashuhuri, ambaye twamtakaThe famous king, whom we want
Atutawale dhahiri, na milele apendeke!May he rule us well and be forever loved
King George mpendeka, mwema mwenye siri!The beloved King George, good and secretive!
(3) Pasiwe na ghururi, Mungu amemsimika,(3) Let there be no deceit, God has installed him
Awali na aheri, hakika ni sikukuu,From start to finish, truly it is a holiday
Leo hakuna shauri, afisi zimefungwa,Today there’ll be no government work, the offices have closed26
King George hakika ana wengi matajiri!Truly King George has many rich people!
(4) Ni furaha ya fahari, Mfalme anatukuzika!(4) It is a great joy that the king is praiseworthy
Raia na askari, wamejishika pamoja,The citizens and armed forces are united
Tajiri na maskini, huungwa na mamlaka,The wealthy and the poor are joined by the authority
King George amefika, hali ya ujasiri.King George has reached a state of bravery…
(7) Kwa yakini nasadiki, ugonjwa ulivyoshika,(7) With certainty I believe illness attacked him
Mfalme kwa dhahiri, maradhi yalimshika,The king apparently was overtaken by disease
Katibiwa na madaktari, na ugonjwa ukatibika!He was treated by doctors and his ailment cured
King George amevuka, maradhi yaliyokuwa hatari.King George overcame the dangerous disease.
(8) Alipatwa na hatari, sasa ameokoka,(8) He faced danger but now has been saved
Nasi sote kadiri, himaya ilimofika,And we all are able to accept the extent of his rule
Siku zote twamkiri, Mfalme wa mamlaka,We always accept him as a king with authority
King George Afrika, kaitawala dhahiri.King George has transparently ruled Afrika.
(22) Salaam nyingi tayari, nafasi zinapunguka,(22) Many greetings already. Space is running out
Mambo Leo mashuhuri, pokea chakula shika,Famous Mambo Leo, take the food27
Gazeti letu zuri, busara hukutanika;Our newspaper is good, wisdom collects here
Maulana ajuika, King George dhihiri.His Highness is famous. King
George appear to us!
(23) Mtengenezaji habari, Mungu akupe baraka,(23) News editor, may God bless you
Umetutoa kiburi, gizani pia tumetoka;You removed our arrogance and we came out of the darkness
Twakusalimu dhahiri, na wengine kadhalika;We greet you openly and the others as well
Maulana hakika, King George kadiri.Truly His Highness King George is the able one.28
(24) Kaditamati shairi, kalamu ninaiweka,(24) I bring the poem to a close and set down my pen
Nawaambia kwa dhamiri,
Inshalla nikifika,
I’m telling you that my intention, God willing, is to
Hoja kuwa na umri, kutunga na kuandika,continue
To compose [poems] and to write as long as I live
Kwa heri nasimika, King George wa fahari.I bid you farewell, King George the Proud.
16These poems honoring King George V are notably different in character from those described earlier praising his first cousin Kaiser Wilhelm

MIEHE, Gudrun, Katrin BROMBER, Said KHAMIS, and Ralf GROSSERHODE. Kala Shairi: German East Africa in Swahili Poems. Archiv afrikanistischer Manuskripte, Vol. 6. Köln: Rüdiger Köppe Verlag, 2002.

MIEHE, Gudrun, and Abdilatif ABDALLA. Poems Attributed to Fumo Liyongo. Archivafrikanistischer Manuskripte, Vol. 7. Köln: Rüdiger Köppe Verlag, 2004.

Source : Mentions légales
 
Mnamo tarehe 27 Januari 1960 Rais wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Ndg. Samia Suluhu Hassan alizaliwa huko Makundichi Zanzibar.

Leo anatimiza umri wa miaka 62. Ni Rais wa kwanza mwanamke nchini kwetu na mfano wa kuigwa kwa wasichana, wanawake na watu wa rika na jinsia mbalimbali kwa namna moja ama nyingine.

Tunaamini kuwa leo asubuhi 27 Januari 2022 Saa 12:00 Asubuhi - 03:00 Asubuhi kupitia mahojiano maalum katika kipindi cha Jambo Tanzania katika Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) utakuwa na mengi ya kutueleza yakuhusuyo wewe, maendeleo endelevu ya nchi yetu na mustakabali bora wa nchi yetu pendwa ya Tanzania.

Tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu awe nawe katika uongozi wa awamu ya sita, akujalie afya njema, furaha, maisha marefu na nguvu za kuwatumikia watanzania bila kuchoka wala kukatishwa tamaa katika kuhakikisha taifa hili linapata maendeleo.

Heri ya Kumbukumbu ya Siku ya Kuzaliwa Rais wetu na daima Kazi Iendelee.

View attachment 2096714
View attachment 2096717
Heri ya kuzaliwa Mheshimiwa Rais na Mama yetu mpendwa. Tunakupenda na tunakutakia maisha marefu yenye furaha, afya tele and hofu ya Mungu ndani yako.

Binafsi nafurahi kuwa na Rais mwanamke. Ktk maandiko ya Kikristo kuna neno linalosema "wanawake ni jeshi kubwa" yaani ni nguzo muhimu kuanzia ngazi ya familia hadi taifa. Pia, ukisoma Mithali 31:10-31 inaelezea sifa ya mwanamke mwema. Wewe kama kiongozi wangu nakutakia uongozi uliotukuka na unaosimamia haki, kweli na utu wa mtu maana Mungu wetu ni Mungu wa haki na hukumu zake ni za kweli.

Hivyo, sawa na Mithali 31 hasa katika Mithali 31:12 inamtaja mume, lakini kwako iwe watanzania, naomba uwatendea na kuwawazia mema kwa nguvu zote, hata kama yuko anayekukosoa wewe mtendea mema tu maana iko siku atarudi na kuwa mtiifu kwako.

Kama isemavyo Mithali 31:20 naomba uwakunjulie maskini mikono yako kwa sababu kwa mkono utasaini na kupiga muhuri sera na sheria zinazopinga uonevu na udidimizwaji wa wananchi maskini, na hata ikikupendeza kuwapa katiba inayowaheshimisha na kuwa na mamlaka.

Pia, kama isemavyo Mithali 31:26 Mola akusaidie kuwa na kawaida ya kufumbua kinywa kwa hekima na sheria ya wema ikawe katika ulimi wako daima.

Zaidi ya yote, kama isemavyo Mithali 31:30 Mwenyenzi Mungu akusaidie upate kumcha na kumuabudu yeye kwa sababu "mwanamke amchaye BWANA, ndiye atakayesifiwa".

Nikutakie utendaji mwema, Mwenyenzi Mungu akupe afya njema.

Happy Birthday - HE. President SSH!!!
 
Fisadi Bwana Chato kupewa salamu za happy birthday haihalalishi fisadi Hangaya kupewa salamu za happy birthday.Two wrongs don't make a right.
Mkuu unaishi na maumivu ya nafsi, pole sana. Kumbuka ukikubalika na wengi umekubalika kwa Mungu pia.
 
Na yeye alipe kodi kutoka kwenye mshahara wake, posho zake zipunguzwe pamoja na watawala wenzake, na mishahara yao minono ipunguzwe.
Fanya kazi toka jasho kuwa mbunifu ili pato lako liongezeke. Mabilionea wasingekuwa na ukwasi walionao kama wangekuwa na mawazo kama haya ya aliye juu mgojee chini, utagonja mpaka siku ya kwenda kaburini.
 
Na yeye alipe kodi kutoka kwenye mshahara wake, posho zake zipunguzwe pamoja na watawala wenzake, na mishahara yao minono ipunguzwe.
Fanya kazi toka jasho kuwa mbunifu ili pato lako liongezeke. Mabilionea wasingekuwa na ukwasi walionao kama wangekuwa na mawazo kama haya ya aliye juu mgonje chini, utagonja mpaka siku ya kwenda kaburini.
Huyu ndiye amekubalika na wengi?!🐒🐒🐒View attachment 2097420View attachment 2097421
JPM na Samia wanaunganishwa na CCM tu lakini ni watu wawili tofauti kabisa. Naona unajaribu kujenga hoja lakini inaishia juu juu haina mashiko mazito.
 
Acha kumpa ujinga Wewe mwanaume na watoto unakubali kuongozwa na mwanamke?
Kuongozwa na mwanamke muda ulikuwa haujafika miaka yote ya nyuma na sasa umefika. US wana running mate mwanamke hivyo lolote likimpata Biden mwenye miaka 80 Kamala anakabidhiwa nchi. Kuwa mpole tu.
 
Mmh yale ya kuteua mkurugenzi mpya wa tpdc na kumtumbua usiku wake, sio kukurupukaa huko?
Au Yale ya wenzake na mbowe wameshtakiwa
Kukurupuka kubaya ni kumtumbua mtu 2015 halafu akaendelea kulipwa mshahara wa serikali akiwa hafanyi kazi mpaka 2020 mwishoni.
 
Bado hawajakamatwa . Upinzani kuteseka imekua ni kitu cha kawaida kwasasa. Lakini nafurahi zaidi samia anavowanyoosha mbogamboga hasa kundi lile[emoji847][emoji847][emoji847]
 
Bado hawajakamatwa . Upinzani kuteseka imekua ni kitu cha kawaida kwasasa. Lakini nafurahi zaidi samia anavowanyoosha mbogamboga hasa kundi lile[emoji847][emoji847][emoji847]
Sio mbogamboga tu, hata mwenyekiti mbowe ananyooshwa ni miezi mitano sasa yupo jela kwa kesi ya kubumba.
 
Sio mbogamboga tu, hata mwenyekiti mbowe ananyooshwa ni miezi mitano sasa yupo jela kwa kesi ya kubumba.
Mbowe hajaanza kukaa jela utawala huu au unajifanya hukumbuki? Hukuona kesi zilikua za kubumba? Pelekeni unafki huko
 
Back
Top Bottom