Harusi ya Majizzo, Millard Ayo: Vijana matajiri hawapendi kuchezea pesa zao wala kusumbua watu na michango

Harusi ya Majizzo, Millard Ayo: Vijana matajiri hawapendi kuchezea pesa zao wala kusumbua watu na michango

Tatizo lenu mnaishi kwa kuwaza au kuogopa eti "Watu watanionaje"

Mtu anaingia gharama kisa kuogopa kusemwa na watu! Huwezi kuwaridhisha binadamu,vijana mna kazi sana,

Live the life u love,love the life u live.
Mstari wa mwisho uwekewe lamination.
 
Nilishaliongelea hili swala. Mambo ya kuchangishana yanakera mno! Tena unakuta lijitu hata hamna mazoea, kama mpo ofisi moja linajinunisha ovyo sometimes linakwamisha mishe za kazi.

Then ghafla likitaka kuoa au kuolewa linajifanya liko poa linajichekesha chekesha ovyo na kuanzisha shobo, linakuvutia timing likupe kadi ya mchango ulichangie. Sifanyi upumbavu huo!!!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nimecheka had machozi, khaaah
 
Wengi mnaongea tu hapa kufurahisha genGe ila mkiwa wenyewe huko hela zinawatoka mnachanga sana tu mnakuja kutolea machungu huku
Kabisaaa yaan [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Harusi zina kamati...ndo zinachangisha...wanaoana unaweza kuta hawana hata mbwembwe
Nipo added kwenye group la mchango wa harusi na aliyeniadd ni bwana harusi. Na huyo huyo ndio mshereheshaji na mshawishi mkuu kwenye hilo group watu watoe michango.

Nilichofanya kwavile namuheshimu jamaa nikaamua ku-mute group waendelee na harambee zao wenyewe.
 
Hivi Millard ni kweli alioa, mbna ilisemekana ni tangazo lile? Duuh bas hongera zake.

Kuoa ni swala binafsi na watu wake wa karibu,, familia yake na familia ya bibi harusi.

Kwa record za msajili wa ndoa Tanzania rita Millard ayo ana mke halali kabisa aliyefunga nae ndoa ya kikatoliki kanisani

Mambo ya tangazo ama sio Tangazo hayo siyajui
 
Saa nyingine utakuta hutaki kabisa hayo mambo ila familia zinalazimisha hasa mama. Sisi mama zetu na dada huwa wana mitazamo tofauti sana. Siku ya graduation yangu nilimpa dada Tsh laki 3 aniandalie tu msosi kidogo na vinywaji kwa ajili ya familia na watu wengine wachache. Mama sikumshirikisha kwasababu najua tusingeelewana. Siku ya Graduation baada ya pilika za pale chuo ndo ninatoka niende home nashangaa kuona kundi kubwa la ndugu, marafiki na jamaa wamejitokeza. Nashangaa zaidi naambiwa panda gari hili limeandaliwa kwa ajili yako. Badala ya kuelekea nyumbani tukaelekea kwenye ukumbi fulani kuna hadi Muziki umeandaliwa. Yaani ni sherehe kubwa ya zaidi ya milioni kwa wakati ule. Kumbe mama na dada waliamua kutonishirikisha kabisa kwenye mipango yao na kuamua kufanya kila kitu wenyewe kwa gharama zao.
Mimi nilitaka kufanyiwa tena na mama zangu wadogo baki ,ila niligoma zote form four ambayo niikuwa na ndugu yangu nasoma nae darasa moja siku ya graduation sisi tulikuwa kweny tuition tunafanya practical.

Zote form six mpaka chuo niligomea na niliwachenga mpaka trh ya graduation ..
 
Kuoa ni swala binafsi na watu wake wa karibu,, familia yake na familia ya bibi harusi.

Kwa record za msajili wa ndoa Tanzania rita Millard ayo ana mke halali kabisa aliyefunga nae ndoa ya kikatoliki kanisani

Mambo ya tangazo ama sio Tangazo hayo siyajui
Bas sawaa.
 
Nikiona mwanaume anashoboka na mambo ya sherehe sijui naonaje ..
Mambo mengine kuleta wasiwasi mtu mpaka sherehe ipite kakonda kwa kuwazia shughuli itaendaje?

Kistaarabu kanisani au msikitini pale tena fasta na wala viongozi wa dini hawachukui pesa nyingi kama mna pesa andaeni hata karamu kwa watoto yatima au kutoa msaada ...Sasa mnaanza kupiga kelele kwa miziki baadae kuna vitu vinapotea mnalipa , mara walevi wamepigana ..Mambo kibao ya hovyo.

Millardayo ,Majizzo hata Mengi sio kwamba ni matajiri hawa watu ni wastaarabu ndio maan hawapendi vurugu..
 
Ni vijana matajiri na maarufu nchi nzima wanajulikana. Ndio maana wametolewa mfano.

Unaweza ukawa wewe ni kijana tajiri ila sio maarufu. Hivyo jina lako likitumika kwwnye mfano watu wanashindwa kuelewa...maana hawakujui kwa chochote
Kama utajiri ni kumiliki radiostation and online tv; basi mimi ni bilionea
 
Pole mkuu. Mi waliniunga group la harusi simjui ata member mmoja wala bwana harusi.

Nikaahidi nitatoa laki 5 hafu nikaleft. Nilitafutwa aisee ova sio SMS sio kupigiwa. Akijitambulisha tu anakula block.
Haha safi . Hii ilinitokea wakati ndo nimemliza shule za juu juu , jamaa etu anajua kabisa sisi bado apeche alolo katuweka kwenye kamati eti tuanze kuahidi nyie mnaita kupledge sijui mi nikawambia Mr Emmanuel andikeni laki nne .. yule jamaa angu akanifata inbox et kua serious mwanangu. Nikamwambia serious uanze kuwa wewe , Katibu wa ile kamati alikua ni mdada mmama majibu niliyokuwa nampa aliona bora aachane na mimi tu na kejeli nyingi kwamba unaahidi halafu kumbe masikini tu. Nikamjibu masikini baba ako
 
Nashkuru Mungu
Huu ujinga wa michango ya hovyo ilishakataliwa kwny ukoo wetu tangu nakua Hadi hivi sasa

Harusi ya mwanafamilia yeyote itagharamiwa full na Wana ukoo wote kwa kushangishana sisi kwa sisi, sio Watu wa nje.

Labda wale wa hiari yao
 
Haha safi . Hii ilinitokea wakati ndo nimemliza shule za juu juu , jamaa etu anajua kabisa sisi bado apeche alolo katuweka kwenye kamati eti tuanze kuahidi nyie mnaita kupledge sijui mi nikawambia Mr Emmanuel andikeni laki nne .. yule jamaa angu akanifata inbox et kua serious mwanangu. Nikamwambia serious uanze kuwa wewe , Katibu wa ile kamati alikua ni mdada mmama majibu niliyokuwa nampa aliona bora aachane na mimi tu na kejeli nyingi kwamba unaahidi halafu kumbe masikini tu. Nikamjibu masikini baba ako
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mtoa post upo sahihi sanaaaa.kuna jamaa yangu alifungaaa ndoa ya milion 35+ chaa ajabu week mojaa anasema oyaaa nikopeshe ten thousand...hivi hizi n akil au ufalaaa ..hapaaa nina kadi 3 za 30k single nachanga mojaa tuu...
 
Hakuna dhambi ukiamua kuoa, huko huko mlipokubaliana muishi mume na mke hata kama mlikutana vichakani mkaanza kunyanduana shahidi ni Mungu ndiye aliyeshuhudia mkianzisha mahusiano ya kuunda familia. Hizi zingine ni mambo ya ziada tu, kupeana mi certificate ni utaratibu tu usio na lazima. Mara vifijo na nderemo kwenye nyumba za ibada na ukumbini, hizo ni show tu zisizo na maana, ni fasheni tu. Ndoa ni muunganiko wa nafsi kati ya mwanaume na mwanamke walioungana kuishi pamoja katika hali zao za maisha. Maisha ni yao yawe ya shida au raha wamekubaliana wakabiliane na hali hizo. Hayo mambo ya shamrashamra za gharama ni anasa na starehe tu. Sasa starehe zako uwasumbue wengine wakuchangie? Jamii ya kipuuzi ndiyo hukubaliana na mambo ya kupuuzi yafanyike
safi sana , ndoa ni muunganiko wa kiroho baina ya nafsi mbili. Haya mengine kanisani , Msikitini ni mbwembwe tu, hakuna kwenye bible kasisi kafungisha ndoa

Watu walikuwa wanapatana tu na mzazi au wenyewe , tayari ndoa

Ila kufanya sherehe sio mbaya ,lakini usikele watu kwa michango
 
Habari wadau,

Nimeungwa group la harusi ghafla la kijana mfanyakazi mwenzangu anadai michango ya harusi yake.

Nimesoma Bajeti ya harusi yake ni milioni 25.

Nikawaza huyu jamaa ni maskini mwenzangu. Anategema ajira na mshahara ni wa kawaida tu.

Why ana akili ndogo namna hii ya kuchezea pesa.

Mbona vijana waliofanikiwa na wenye utajiri wa mali na utajiri wa watu na connections kali hawapendi mbwembwe wameoa kwa harusi za kimya kimya.

Millard Ayo ni kijana aliyefanikiwa mwenye utajiri wa kutosha tu. Marafiki anao kibao wa kuwachangisha, ila hakufanya hivyo wakati anaoa alioa kimya kimya harusi simple ya kwenda kanisani tu na mkewe kisha kila mtu kwake. Hakuna cha ukumbi wala cha Mc garab wala nani.

Majizo nae mmiliki wa efm hivyo hivyo alioa kimya kimya, yeye na lulu kanisani tu then kila mtu kwake.

Why na kina sisi vijana maskini hatujifunzi. Yaani mtu anachukua mkopo ofisini kwa ajili ya kufanikisha harusi.

Mtu anasumbua watu michango kisa harusi.

MASKINI TUNA UJINGA MWINGI SANA
Akili za KIMASIKINI huwa ni KUKARIRI yasiyo ya maana ,kubweteka na kufurahisha jamii.....

#Jiamini Mwenyewe

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom