Harusi ya Majizzo, Millard Ayo: Vijana matajiri hawapendi kuchezea pesa zao wala kusumbua watu na michango

Harusi ya Majizzo, Millard Ayo: Vijana matajiri hawapendi kuchezea pesa zao wala kusumbua watu na michango

Haha safi . Hii ilinitokea wakati ndo nimemliza shule za juu juu , jamaa etu anajua kabisa sisi bado apeche alolo katuweka kwenye kamati eti tuanze kuahidi nyie mnaita kupledge sijui mi nikawambia Mr Emmanuel andikeni laki nne .. yule jamaa angu akanifata inbox et kua serious mwanangu. Nikamwambia serious uanze kuwa wewe , Katibu wa ile kamati alikua ni mdada mmama majibu niliyokuwa nampa aliona bora aachane na mimi tu na kejeli nyingi kwamba unaahidi halafu kumbe masikini tu. Nikamjibu masikini baba ako
[emoji2956]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Nikiona mwanaume anashoboka na mambo ya sherehe sijui naonaje ..
Mambo mengine kuleta wasiwasi mtu mpaka sherehe ipite kakonda kwa kuwazia shughuli itaendaje?

Kistaarabu kanisani au msikitini pale tena fasta na wala viongozi wa dini hawachukui pesa nyingi kama mna pesa andaeni hata karamu kwa watoto yatima au kutoa msaada ...Sasa mnaanza kupiga kelele kwa miziki baadae kuna vitu vinapotea mnalipa , mara walevi wamepigana ..Mambo kibao ya hovyo.

Millardayo ,Majizzo hata Mengi sio kwamba ni matajiri hawa watu ni wastaarabu ndio maan hawapendi vurugu..
[emoji2956]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Habari wadau,

Nimeungwa group la harusi ghafla la kijana mfanyakazi mwenzangu anadai michango ya harusi yake.

Nimesoma Bajeti ya harusi yake ni milioni 25.

Nikawaza huyu jamaa ni maskini mwenzangu. Anategema ajira na mshahara ni wa kawaida tu.

Why ana akili ndogo namna hii ya kuchezea pesa.

Mbona vijana waliofanikiwa na wenye utajiri wa mali na utajiri wa watu na connections kali hawapendi mbwembwe wameoa kwa harusi za kimya kimya.

Millard Ayo ni kijana aliyefanikiwa mwenye utajiri wa kutosha tu. Marafiki anao kibao wa kuwachangisha, ila hakufanya hivyo wakati anaoa alioa kimya kimya harusi simple ya kwenda kanisani tu na mkewe kisha kila mtu kwake. Hakuna cha ukumbi wala cha Mc garab wala nani.

Majizo nae mmiliki wa efm hivyo hivyo alioa kimya kimya, yeye na lulu kanisani tu then kila mtu kwake.

Why na kina sisi vijana maskini hatujifunzi. Yaani mtu anachukua mkopo ofisini kwa ajili ya kufanikisha harusi.

Mtu anasumbua watu michango kisa harusi.

MASKINI TUNA UJINGA MWINGI SANA
Hiii imeenda
 
Pole mkuu. Mi waliniunga group la harusi simjui ata member mmoja wala bwana harusi.

Nikaahidi nitatoa laki 5 hafu nikaleft. Nilitafutwa aisee ova sio SMS sio kupigiwa. Akijitambulisha tu anakula block.
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂 wewe kiboko😃😃😃😃
 
Hili suala ni mapenzi ya mtu. Kama ameamua kufanya harusi kubwa ama la....
Kuhusu michango ni hiari yako kutoa ama la....
Kama hutaki kutoa ww sema live kuwa hutoi au huna hela sio unapigiwa simu ooh nitatoa mwisho wa mwezi ukitafutwa mwisho wa mwezi unaona usumbufu. We sema tu jamani Mimi nimebanwa Sina hela uone Kama utasumbuliwa.
Sasa kwann mnatuunga kwenye magroup kwa lazima....bila ridhaa yetu
 
Masuala ya michango naona yafanyike kwa ndugu tuh masuala ya kuunga magroup ya marafiki mtu umejuana nae mwezi tuh [emoji23]
Tayar kakueka kwenye group la michango
 
Back
Top Bottom