Hii ndio safari yangu ya Kigoma na niliyoyashuhudia

Hii ndio safari yangu ya Kigoma na niliyoyashuhudia

Forodhani ujiji
FB_IMG_1695613839253.jpg
 
Safari yangu ilianzia Mwanza to Kigoma, then Kigoma to Dar...

Saa 12 asubuhi nilifika stand ya Nyegezi nikapanda gari moja maarufu linaitwa adventure, Mwanza kwenda Kigoma yapo magari maarufu kama Saratoga, adventure, yehova yille kati ya hayo hakuna gari lolote lile lenye unafuu magari ni 3 by 2, yaani upande mmoja watu watatu upande Mwingine wanakaa wawili, gari chache sana ni 2 by 2 na tajiri ndio anapanga lini likae barabarani...

Kwenye Ili gari picha inaanza hakuna customer care yoyote ile nilikata ticket ya mbele Kufika asubuhi nikaambiwa nikakae nyuma huko vurugu ikaanzia hapa ikabidi huyo mtu wampeleke huko nyuma.

Watu wachache walikosa seat wakasimama kuanzia Stand ya Nyegezi nakumbuka stand yoote tulipopita kuanzia Sengerema, Geita, Katoro nk watu walikua wanaingia na kusimama.

Humo ndani ya gari yalikua yanauzwa mahindi, mihogo, karanga vitumbua, mayai yaani tulikua tunapakia Muda wote non stop, story zinapigwa sana mtu wa seat ya mbele anapiga story na rafiki yake aliye seat ya nyuma, kweli waha ni kiboko.

Kufika Nyakanazi kundi kubwa la watu liingia yaani waliosimama ni wengi saana kuliko tuliokaa, nafasi hata ya kugeuka pembeni hupati mabegi yetu wengine tukawa tumebeba kichwani imagine hupo ndani ya gari Lakini begi lako umebeba kichwani..

Barabara ya lami inaishia Kakonko kwa mbele tukaanza kula vumbi mpaka Kibondo, wazee nimefika Kibondo pale mwili wote unauma Mwili mzima shingo haifanyi kazi tena, nikawauliza wenyeji wakanambia safari ya Mwanza to Kibondo ni karibu kuliko Jibondo tu Kigoma mjini, yaani Kibondo ni wilaya ambayo ni kubwa kuitembea ni mwendo wa masaa 4/5 Kufika Kasulu....

Raha ya kusema unasafiri usiitegemee kama unakuja Kigoma panda gari Ili ufike na sio u-enjoy nature, safari iliendelea tukafika mjini Kigoma saa 3 usiku.

NB: KIGOMA ni mji ambao una manispaa moja na town council inayoitwa Kasulu... Kigoma wanaishi watu kama watu wa mikoa mingine, Lakini Kigoma watu wa huku Kigoma Wana amini mno mambo ya kishirikina sio mdogo au mkubwa...

Kigoma Ujiji inapatikana Kigoma mjini. Huko ndio kwao Hashim Rungwe, Baruani Muhuza, Juma Kaseja huko ndio mji ulipoanzia, ni ngome ya kiislamu Watu wa huko ni masikini mno pia Kuna waganga wengi sana na mambo ya kichawi ni mengi mno, kukuta vyungu vimepasuliwa njia panda ni jambo la kawaida HAKUNA MTUMISHI YOYOTE WA SERIKALI ANAEKAA KIGOMA UJIJI, huko Hadi watoto wanajua uchawi ni nini kwenda kwa mganga ni jambo la kawaida.....huku Kigoma Ujiji harusi ni Kila siku huwezi pitisha siku hakuna harusi maisha magumu nyumba za udongo Lakini ni waswahili balaa, huko Ujiji maduka yanayokodisha mziki yanafika 40.

PALE KIGOMA MJINI.....ni center ndogo ya Kibiashara Lakini hakuna mzunguko wowote wa Hela Hapo wenyeji ni wengi na wengi wanauza kwa madawa usitegemee wa kuja ukafungua duka huku utapigwa zengwe mpaka uone moto.

Huu ni mji wa kinafiki, watu wanaishi kinafiki kinafiki saana, mvua zikinyesha unaomba Mungu radi zinapiga vibaya mno tena Kwa sauti kubwa sana.
Vipi ile biashara yetu pendwa ya mbususu ipo na huko?
Bei zao ni elekezi?
 
Mwendelezo!?
Jambo la Mwisho saaana huku mashamba Bado ni mengi mno, kama Maeneo ya uvinza -nguruka unaweza uziwa ekari moja kwa 50,000/= nikifanikiwa kwenda kibondo huko mashambani sikuona tractor Bali nguvu kazi ni watu nilivyouliza wenyeji wakanambia wanaolima wengi ni wakimbizi kutoka Burundi wanalimishwa hekari moja Kwa SHILINGI 30,000/_40,000/= warundi ni watu wenye roho mbaya sana na makatili story niliyoipata huko ni kwamba hawapendi dhuruma ukimlimisha Shamba alafu umcheleweshee malipo yake basi jiandae kukutana na kitu kizito sana Huwa hawapendi masikhara kwenye haki Yao, story iliyopo huku ni kwamba Zamani kulikua Kuna watekaji wengi walitokea Burundi, serikali ilijitahidi sana kupambana nao hao maharamia kwa Sasa hizo story za utekaji ni kama hazipo...

Kutoka kigoma kwenda dar, ni safari ya masaa 24 non stop Lakini ukitoka daresalam kuja kigoma lazima mtalala pale kaliua -tabora kwa sababu ya usalama, pale mbele kidogo ya kaliua Kuna mbuga na misitu Pamoja na vichaka kwahiyo watu wenye Nia ovu ni rahisi kutimiza adhima yao.

Wafanyabiashara wengi wakubwa huku lazima awe anapeleka mzigo congo na kwenda congo njia nyepesi lazima uvuke maji so kama sio katili au mtu wa fitina basi omba Mungu tu maana mnavuka kwenye mitumbwi na usalama wa huko sio guarantee sana.

Kigoma fursa zipo Lakini usiwe na jicho tu la Kuona fursa lazima Uwe na jicho la kujikinga na mazindiko ya kutosha, huko mtu kuongea swala la ndagu ni kugusa tu wala sio jambo la ajabu.


Anyway karibuni sana kigoma
 
Safari yangu ilianzia Mwanza to Kigoma, then Kigoma to Dar...

Saa 12 asubuhi nilifika stand ya Nyegezi nikapanda gari moja maarufu linaitwa adventure, Mwanza kwenda Kigoma yapo magari maarufu kama Saratoga, adventure, yehova yille kati ya hayo hakuna gari lolote lile lenye unafuu magari ni 3 by 2, yaani upande mmoja watu watatu upande Mwingine wanakaa wawili, gari chache sana ni 2 by 2 na tajiri ndio anapanga lini likae barabarani...

Kwenye Ili gari picha inaanza hakuna customer care yoyote ile nilikata ticket ya mbele Kufika asubuhi nikaambiwa nikakae nyuma huko vurugu ikaanzia hapa ikabidi huyo mtu wampeleke huko nyuma.

Watu wachache walikosa seat wakasimama kuanzia Stand ya Nyegezi nakumbuka stand yoote tulipopita kuanzia Sengerema, Geita, Katoro nk watu walikua wanaingia na kusimama.

Humo ndani ya gari yalikua yanauzwa mahindi, mihogo, karanga vitumbua, mayai yaani tulikua tunapakia Muda wote non stop, story zinapigwa sana mtu wa seat ya mbele anapiga story na rafiki yake aliye seat ya nyuma, kweli waha ni kiboko.

Kufika Nyakanazi kundi kubwa la watu liingia yaani waliosimama ni wengi saana kuliko tuliokaa, nafasi hata ya kugeuka pembeni hupati mabegi yetu wengine tukawa tumebeba kichwani imagine hupo ndani ya gari Lakini begi lako umebeba kichwani..

Barabara ya lami inaishia Kakonko kwa mbele tukaanza kula vumbi mpaka Kibondo, wazee nimefika Kibondo pale mwili wote unauma Mwili mzima shingo haifanyi kazi tena, nikawauliza wenyeji wakanambia safari ya Mwanza to Kibondo ni karibu kuliko Jibondo tu Kigoma mjini, yaani Kibondo ni wilaya ambayo ni kubwa kuitembea ni mwendo wa masaa 4/5 Kufika Kasulu....

Raha ya kusema unasafiri usiitegemee kama unakuja Kigoma panda gari Ili ufike na sio u-enjoy nature, safari iliendelea tukafika mjini Kigoma saa 3 usiku.

NB: KIGOMA ni mji ambao una manispaa moja na town council inayoitwa Kasulu... Kigoma wanaishi watu kama watu wa mikoa mingine, Lakini Kigoma watu wa huku Kigoma Wana amini mno mambo ya kishirikina sio mdogo au mkubwa...

Kigoma Ujiji inapatikana Kigoma mjini. Huko ndio kwao Hashim Rungwe, Baruani Muhuza, Juma Kaseja huko ndio mji ulipoanzia, ni ngome ya kiislamu Watu wa huko ni masikini mno pia Kuna waganga wengi sana na mambo ya kichawi ni mengi mno, kukuta vyungu vimepasuliwa njia panda ni jambo la kawaida HAKUNA MTUMISHI YOYOTE WA SERIKALI ANAEKAA KIGOMA UJIJI, huko Hadi watoto wanajua uchawi ni nini kwenda kwa mganga ni jambo la kawaida.....huku Kigoma Ujiji harusi ni Kila siku huwezi pitisha siku hakuna harusi maisha magumu nyumba za udongo Lakini ni waswahili balaa, huko Ujiji maduka yanayokodisha mziki yanafika 40.

PALE KIGOMA MJINI.....ni center ndogo ya Kibiashara Lakini hakuna mzunguko wowote wa Hela Hapo wenyeji ni wengi na wengi wanauza kwa madawa usitegemee wa kuja ukafungua duka huku utapigwa zengwe mpaka uone moto.

Huu ni mji wa kinafiki, watu wanaishi kinafiki kinafiki saana, mvua zikinyesha unaomba Mungu radi zinapiga vibaya mno tena Kwa sauti kubwa sana.
Mwaka Gani mkuu,maana Waha wanasema Kigoma kuchelee
 
Jambo la Mwisho saaana huku mashamba Bado ni mengi mno, kama Maeneo ya uvinza -nguruka unaweza uziwa ekari moja kwa 50,000/= nikifanikiwa kwenda kibondo huko mashambani sikuona tractor Bali nguvu kazi ni watu nilivyouliza wenyeji wakanambia wanaolima wengi ni wakimbizi kutoka Burundi wanalimishwa hekari moja Kwa SHILINGI 30,000/_40,000/= warundi ni watu wenye roho mbaya sana na makatili story niliyoipata huko ni kwamba hawapendi dhuruma ukimlimisha Shamba alafu umcheleweshee malipo yake basi jiandae kukutana na kitu kizito sana Huwa hawapendi masikhara kwenye haki Yao, story iliyopo huku ni kwamba Zamani kulikua Kuna watekaji wengi walitokea Burundi, serikali ilijitahidi sana kupambana nao hao maharamia kwa Sasa hizo story za utekaji ni kama hazipo...

Kutoka kigoma kwenda dar, ni safari ya masaa 24 non stop Lakini ukitoka daresalam kuja kigoma lazima mtalala pale kaliua -tabora kwa sababu ya usalama, pale mbele kidogo ya kaliua Kuna mbuga na misitu Pamoja na vichaka kwahiyo watu wenye Nia ovu ni rahisi kutimiza adhima yao.

Wafanyabiashara wengi wakubwa huku lazima awe anapeleka mzigo congo na kwenda congo njia nyepesi lazima uvuke maji so kama sio katili au mtu wa fitina basi omba Mungu tu maana mnavuka kwenye mitumbwi na usalama wa huko sio guarantee sana.

Kigoma fursa zipo Lakini usiwe na jicho tu la Kuona fursa lazima Uwe na jicho la kujikinga na mazindiko ya kutosha, huko mtu kuongea swala la ndagu ni kugusa tu wala sio jambo la ajabu.


Anyway karibuni sana kigoma
Bunduki nasikiaga Laki 2 tu unapata 47 ni kweli?
 
Back
Top Bottom