Hii sheria ya ardhi kuhusu wageni kumiliki ardhi isipokuwa makini mtakuja kulaumiana mbeleni

Hii sheria ya ardhi kuhusu wageni kumiliki ardhi isipokuwa makini mtakuja kulaumiana mbeleni

Yaan mawazo yako hayana tofauti na watu wa kijijini au watu duni wasio elewa maana ya maendeleo

kwanza matumiz ya kuni na mkaa yanapaswa kupigwa marufuku, nishati ya kupikia iwe gesi na umeme

pili
hao wamasai na wasukuma wanaharibu sana mazingira kwa ufugaji usio na tija wa kuhama hama, wanapaswa kufuga ng'ombe wachache wa kisasa wenye tija

tatu
baadhi ya maeneo ya kimkakati yatatengwa kwaajiri ya uoto wa asili, hifadhi ya wanyama na mimea ya asili au kwaajiri ya utalii
Eti maeneo ya kimkakati🤣 Unaongea lugha ya kitapeli na isyoendana na uhalisia inayoongelewa na wanasiasa. Uhalisia ni kuwa watanzania wengi bado wanapikia kuni na mkaa. Upige marufuku kuni na mkaa una umeme na gesi ya kupeleka huko Itilima vijijini? Una hela za kununua nyama na maziwa ya ng'ombe waliofugwa kisasa na kwa "TIJA🤣?" Unaongea vitu vya ndotoni.

Usione hiyo misitu imekaa bure, watu wengi sana wanaitegemea kuendesha maisha yao. Ndiyo nyie mkiona viwanja vya wazi mnakuwa mnadhani kuwa vimekaa bure.
 
Mkuranga yote itakuwa mali ya wachina
 
Hongera waziri wa ardhi Jerry Silaa nili kunukuu kuhusu swala la wageni mnafanya maboresho kuhusu wageni kumiliki ardhi.

Tatizo linaweza kutokea mbeleni kwenye sheria hii sababu wananchi wengi wako kwenye wimbi la umaskini ususani vijijini ambapo ndio maeneo yenye rasilimali kama madini,kilimo na biashara.

Wananchi hawa watajikuta wakiingia na tamaa za wageni kwa dau watakazopewa kuuza ardhi zao na mwisho wa siku ardhi ya tanzania itakuwa ardhi mataifa mengine yenye maeneo yao.

Kuna nchi zinazo zitolea macho tanzania ilivyo barikiwa na kila kitu

Naiona tanzania ikijitakia inachokitaka
Si Bora mtu apewe chake auze Kuliko uambiwe Ni chako lakini pia hupewi
 
Back
Top Bottom