christeve88
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 2,841
- 4,531
Likizo ni muhimu mkuu hawa watoto wanayakujifunza mengi huko nyumbani ikiwemo utu.Sijakataa likizo wasiende bali vidato vya mitihani wabaki.
Wakati unasoma wewe ulienda likizo kwa vidato vya mitihani?? Kma ni ndio basi tunaanza kujenga taifa la vilaza
Hilo jina utakuwa mtu wa Kusini au pwani au Tanga ambako elimu siyo kipaumbele ndiyo maana hiyo mikoa inashika mkia kwenye mitihaniWatoto waende nyumbani kupumzika na kuwasaidia kazi wazazi wao. Muda wa kupumzika uheshimiwe.
Kijijini atakwenda shambani, mjini atazurura mitaani na mimba zitaongezekaNdio maana ikaitwa likizo, mtoto arudi nyumbani kupumzisha akili, kusaidia wazazi, kujisomea akiwa nyumbani, wazazi wafahamu tabia za mtoto.
Elimu ya darasani sio kila kitu katika makuzi!!
Ulifaulu level gani? Wakati wako siyo sawa na wakati tuliopokama Mimi nilisoma saint kayumba na nikafaulu vizuri na Kila likizo nilikua naludi nyumbani sihitaji mtoto wangu abaki shule likizo. Hawa watoto wanaoshinda boarding tutajenga nao bond lini sisi wazazi. tumeweka ufaulu mbele sana. Kuna maisha baada ya A za darasani.
Wazazi wanahangaika mjini kutafutia watoto wao tuition hahahahaMapumziko pia ni muhimu
Wameenda tunawasubiri July break ya kwanza ni kuwapima mimba hapo Kila mmoja atabeba mzigo wakeMkuu sisi enzi zetu ikifika lilizo tulikuwa tunaruhusiwa kwenda nyumbani lakini tulifaulu masomo vizuri. Walimu hakikisheni mnakwenda na syllubus vizuri na kwa wakati! Lakini kwa habari ya Afya watoto waruhusiwe kupumuzika.
Kwa mjini watoto kuachwa bila uangalizi wa mzazi au mwl ni hatari.Alie kuambia akibaki shile ndio atapata A ni nani? Mtoto.kama hana akili hana tu na ka anazo anazo tu,
Wewe unamlea mwanao na kusimamia maadili ya mwanao Kama mhindi??Sikiliza Wahindi sio wajinha kuto hata hata ruhusu watoto kukaa Bording, anaye waambia watoto wabatakiwa kusoma muda wote ni nani? Hakuna mambo mengine ya kujifunza nje ya vitabu?
Mkuu sikiliza enzi tulizo soma sio za sasa kwa sasa watoto wanatakiwa kuelwa mambo, kuuliza na kudadisi sio kusolve past paper, hizi nyakati sio hata za miaka ya 90 mkuu.
Tumesoma sisi tukikaririshwa past paper
Kama mzazi unashindwa kumsimamia mtoto kipindi kifupi cha mwezi mmoja tu unafaa kuitwa mzazi kweli? Ulizaa ili nani abebe majukumu yako kama likizo ya mwezi mmoja tu inakushinda kukaana mtoto.Kijijini atakwenda shambani, mjini atazurura mitaani na mimba zitaongezeka
Mazingira yanatofautiana. Watoto kubakizwa shule ni makubaliano ya mzazi na mwl na hata watoto wenyewe na mwl. Mazingira ya mijini siyo sawa na ya vijijini. Watoto wengine ni wasahailifu sana, akikaa wiki moja hajaahika daftari, akija kufungua mwl unaanza nae upya hakuna anachokikumbuka.Likizo ni muhimu mkuu hawa watoto wanayakujifunza mengi huko nyumbani ikiwemo utu.
Embu fikiria wakati mtoto yupo shule alifiwa na ndugu huko mkoani let say baba mdogo, bibi, shangazi nk. na hakupata wasaa wakuhururia, kipindi cha likizo ndio hukitumia kwenda kuona hata mahali walipolala wapendwa wao. Tusiharibu tamaduni zetu jamani tukitumia ratiba na usimamizi mzuri watoto watafaulu tu. Pia tukae tukijua kuwa elimu ni pyramid in shape sasa hofu ya nini?
Kumbe hujui malezi ya watoto wengi wa Sasa? Nenda hapo unga Ltd watoto wengi zaidi ya 90% wanalelewa na single parent na wengine ni bibi au Babu zao hakuna Cha wazaziKama mzazi unashindwa kumsimamia mtoto kipindi kifupi cha mwezi mmoja tu unafaa kuitwa mzazi kweli? Ulizaa ili nani abebe majukumu yako kama likizo ya mwezi mmoja tu inakushinda kukaana mtoto.
Unadhani wakibaki Likizi mojaa bila kwenda Nyumbani kuna kitu gani kikubw watapungukiwaa??? Kubaki shule ni kupata muda mzuri wa kujiandaa na mitihani na hata waalimu huwa hawafundishi mostly ni nyie kujisomeaaa huku mmerelax... Sasa huo ujinga sijui kamiss ndugu mara apumzishe akiliii ni ovyoo sanaa.Likizo ni muhimu mkuu hawa watoto wanayakujifunza mengi huko nyumbani ikiwemo utu.
Embu fikiria wakati mtoto yupo shule alifiwa na ndugu huko mkoani let say baba mdogo, bibi, shangazi nk. na hakupata wasaa wakuhururia, kipindi cha likizo ndio hukitumia kwenda kuona hata mahali walipolala wapendwa wao. Tusiharibu tamaduni zetu jamani tukitumia ratiba na usimamizi mzuri watoto watafaulu tu. Pia tukae tukijua kuwa elimu ni pyramid in shape sasa hofu ya nini?
TATE unaupiga mwingi hadi naogopa.Kuna Watanzania wanapenda sana kulalamika. Wakati walimu wanapambana kuhakikisha watoto wao wanafaulu kwa kuwabakisha wakati wa likizo ili wajisomee! Wao wanalalamika warudi nyumbani.
Halafu wakirudi nyumbani kwenyewe, hawasimamii nidhamu na mienendo yao ya kila siku, likiwemo zoezi la kujisomea, na baada ya likizo, watoto hao hurejea shuleni huku kichwani wakiwa ni empty heads na wakifeli mitihani yao ya mwisho, utawakuta hao wazazi wanaanza tena kuwalalamikia walimu walewale tena, eti kwa kufelisha watoto wao!
Hovyo kabisa. Binafsi naunga mkono shule mbalimbali nchini kubakiza madarasa ya mitihani, ili kujisomea na kujiandaa kwa mitihani yao.
Mbona papuchi haipumzikagi?Watoto wapumzike
Kwa hiyo single parent yeye hana uwezo wa kulea mtoto wake, yeye abaki tu shuleni kisa mama/baba yake hawezi kukaa nae mwezi mmoja wa likizo.Kumbe hujui malezi ya watoto wengi wa Sasa? Nenda hapo unga Ltd watoto wengi zaidi ya 90% wanalelewa na single parent na wengine ni bibi au Babu zao hakuna Cha wazazi
Acheni kutetea ujinga na upimbi ,inawezekanaje mtoto wa miaka kumi na moja anapigishwa kwata ya kusoma kuanzia saa kumi na mbili asubui hadi saa tatu usikua kwa siku saba na bado unataka watoto husika wasipewe likizo ?Wazazi mwanao kama yupo form four, aendelee kusoma na kujisomea, haya matamko ya wanasiasa ni matamko ya kisiasa.
Wewe mwanao yupo shule ya kata, na unajua kuwa ili aweze kupata nafasi ya kwenda hata VETA au kuongeza ujuzi wowote basi cheti cha Form four lazima.
So akili kichwani, yaani mzazi unakaa na kusubiri future ya mwanao ambaye yupo shule ya kata iliandaliwe na waziri!
Mwanao akipata zero hata upolisi hawamchukui na huko mtaani ndio kizazi cha singeli hiki, pathetic.
Nimeandika maana nipo uswahilini De es Salaam, nimeona watoto wa kike na kiume wakikaa mtaani wanaishia kupoteza mwelekeo huku mtaani, hakuna mzazi makini wakumpa malezi bora mwanae.
Anakaa nae saangapi wakati yupo samunge anauza mchicha apate mahitaji ya mtoto au mjukuu? Sasa yeye akiwa samunge, mtoto yupo vibanda vya movie. Je vibanda vya movie na shuleni wapi Bora?Kwa hiyo single parent yeye hana uwezo wa kulea mtoto wake, yeye abaki tu shuleni kisa mama/baba yake hawezi kukaa nae mwezi mmoja wa likizo.
Acheni excuses za ajabu wakuu, walioweka vipindi vya mapumziko walijua ubongo unahitaji nini ili ukue. Unataka mtoto ajifunze Ax² + Bx + C = 0 mwaka mzima asifundishwe mambo mengine ya kimaisha? Usipoishi na mwanao utamfundishaje tabia njema, utatengeneza lini bond kati yenu?