Hili suala la wanafunzi kubaki shule lina umuhimu mkubwa kwa maisha ya baadaye ya mtoto wako

Hili suala la wanafunzi kubaki shule lina umuhimu mkubwa kwa maisha ya baadaye ya mtoto wako

Kwani we ulisoma wapi?? Mwaka gani?? Au ulisomea Somalia nn???
Anachokwambia ni cha kweli kabisaa,haya mambo ya "madarasa ya mitihani" yameanza majuzi tu hapa baada ya sekondari kuanza kubeba watu woteee...nadhani baada ya sekondari kukabidhiwa hizi Halmashauri miaka ya 2008, na kuendelea ndio hayo mambo yalipoanza..

Watu wanasoma mwaka mzima bila mapumziko kwa lengo la kupata D mbili ili wasipate zero

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Anachokwambia ni cha kweli kabisaa,haya mambo ya "madarasa ya mitihani" yameanza majuzi tu hapa baada ya sekondari kuanza kubeba watu woteee...nadhani baada ya sekondari kukabidhiwa hizi Halmashauri miaka ya 2008, na kuendelea ndio hayo mambo yalipoanza..

Watu wanasoma mwaka mzima bila mapumziko kwa lengo la kupata D mbili ili wasipate zero

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Uko sahihi kabisa, kipindi iko kati wanafunzi 200 wanaochaguliwa labda 10 tu kwenda sekondari so mnakutana wote mna uwezo ila baada ya 2008, kuanzishwa shule za kata wanafunz wanaopelekwa sekondary wengne hawajui hata kusoma ssa unafkiri mwalimu atachukua hatua gani kma sio kumbakisha likizo asome (apo vidato vya mtihani vikaanzishwa). Lengo sio baya ila kma hamtaki wazaz baki na mwanao nyumbani, msiendeshwe na mihemko na matamko ya wanasiasa ambao leo yupo kesho atakuja mwingne na lake
 
Ipo haja serikali kwa maana ya Wizara ya Elimu na TAMISEMI pamoja na wadau wengine,kukaa na kuangalia kama muda uliotengwa kwa ajili ya masomo kwa mwaka mzima (siku 194/196) zinatosheleza au hazitoshi...

Haiwezekani kila inapofika likizo,anaibuka Waziri wa Elimu kukemea wanafunzi kubakizwa shuleni,na Waziri wa TAMISEMI anakuwa kimyaa kama hilo jambo halijui..

Haiwezekani pia walimu wengi na shule zao kila likizo wawaambie wanafunzi wao kubaki tena kwa lazima na michango juu na sisi tuhitimishe tu kuwa ni "njaa za walimu"..lazima kuna shida walimu wanaiona kwa wanafunzi waliokabidhiwa..

Lakini pia mtoto wa darasa la Nne unamwambia hafungi shule, abaki asome,kuna vinini vipya vilivyoongezeka huko la nne hadi kuwatesa watoto wadogo hao wasipumzike?

Ipo haja ya kujua kama tatizo ni muda wa ujifunzaji hautoshi au wajifunzaji bongo zao hazishiki vitu kwa haraka.

Lakini pia ni kwanini Waziri wa Elimu nae aje na maagizo ambayo anajua wazi kabisa walimu wa sasa hawamsikilizi wala hawatatekeleza maagizo yake? Maana siyo mara ya kwanza kuagiza na shule zinaendelea na kazi wakati wa likizo..pia agizo limejaa ukakasi mara shule za private zifanye hivi na za serikali zifanye vile
 
Tusiruhusu matamko ya siasa yaingilie elimu yetu, kuna waliokuja na Physic with Chemistry yaliunganishwa haya masomo wako wapi, kuna waliokuja na G.P.A wako wapi?? Sasa tupo likizo
 
Uko sahihi kabisa, kipindi iko kati wanafunzi 200 wanaochaguliwa labda 10 tu kwenda sekondari so mnakutana wote mna uwezo ila baada ya 2008, kuanzishwa shule za kata wanafunz wanaopelekwa sekondary wengne hawajui hata kusoma ssa unafkiri mwalimu atachukua hatua gani kma sio kumbakisha likizo asome (apo vidato vya mtihani vikaanzishwa). Lengo sio baya ila kma hamtaki wazaz baki na mwanao nyumbani, msiendeshwe na mihemko na matamko ya wanasiasa ambao leo yupo kesho atakuja mwingne na lake
Hivi inakuaje kwa watu ambao wako siriasi wanampeleka mwanafunzi sekondari na hajui kusoma,achilia mbali kuandika?
Kusoma na kuandika ni vitu basic anavyotakiwa kuvipata akiwa primary,anavukaje huyo kwenda sekondari kwenda kufanya shule zisifungwe?
 
Hivi inakuaje kwa watu ambao wako siriasi wanampeleka mwanafunzi sekondari na hajui kusoma,achilia mbali kuandika?
Kusoma na kuandika ni vitu basic anavyotakiwa kuvipata akiwa primary,anavukaje huyo kwenda sekondari kwenda kufanya shule zisifungwe?

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Walimu wana mengi sana ya kuongea ila siasa inawaziba mdomo, matamko kila cku, kila mtu boss wake, kuna kitu kinaitwa MASOMO YA MKAKATI we acha tu ndo mana ni tabu kupata watto wanaosoma physics au chemistry
 
Walimu wana mengi sana ya kuongea ila siasa inawaziba mdomo, matamko kila cku, kila mtu boss wake, kuna kitu kinaitwa MASOMO YA MKAKATI we acha tu ndo mana ni tabu kupata watto wanaosoma physics au chemistry
Yes, ni kweli kabisa usemacho,shule nyingi zimechagua baadhi ya wanafunzi,na baadhi ya masomo ( Hayazidi masomo manne kwa shule nyingi) na kuyapa jina "masomo ya mkakati"..mwanafunzi anatakiwa kudeal na hayo tu ili mwisho apate D mbili waepuke zero, mwisho watakuwa wamekwepa matusi ya Afisa Elimu Kata, DEO,Mkurugenzi,Afisa Elimu mkoa,katibu Tarafa, DC nae akipata nafasi ,RC kwa uchache...

Wakipata zero matusi ya watu wote hao yanawahusu
 
Watoto waende likizo hakuna kazi isiyo na likizo tena kwa watoto wetu kupumzika ni muhimu sana. Mtoto akajifunze mambo mengine ya kimaisha mzazi mpeleke kijijini achunge,alime,apasue Kuni,salimie ndugu,ajifunze kilugha na milazao,acheze mitaani,akauze bidhaa sokoni nk.
Elimu yetu inakosa mpangilio mzuri wengine tulishauri mpangilio wa semister tatu mfumo uwe kamahivi;
3 Jan mpaka 31 machi - masoma(miezi 3).
1 April mpaka 30 April - likizo ya kwanza(mwezi 1).
1 may mpaka 31 July - masomo(miezi 3).
1 august mpaka 31 august - likizo ya pili(mwezi 1).
1 September mpaka 30 November - masomo(miezi 3).
1 December mpaka 2 January - likizo ya tatu(mwezi 1).
**Watoto watasoma jumla siku 180 (miezi 9 × 20 siku kwamwezi) ambazo zinatosha hazitofautiani na siku za masomo kwasasa!!
Darasa la saba wasome semister mbili tuu wafanye mtihani wa taifa Kisha Semister ya tatu (miezi mitatu) wanafunzi wa darasa la saba wafundishwe English na maths tuu kujiandaa kwenda sekondari, walimu wa sekondari wapelekwe primary wakati huo kusaidia ufundishaji maana sekondari kunakuwa hakuna mzigo mkubwa na walimu Huwa wengi sekondari nyingi kuzidi msingi!!
Serikali imekuwa nzito sana kufanya maamuzi katika elimu jambo linalozorotesha sana elimu yetu nakuongeza mdororo wa elimu kuwa na wahitimu wenye uwezo mdogo saaana hata katika kujieleza na kujisomea.
 
We mjinga ulio faulu ume lega ugunduzi gani? Sana sana Umeajiriwa hapo ulipo ndio mwisho wa akili zako, Hao watotonwako zaidi ya akili ya kupata A wana kingine special?
Nilijua utaelekea huko,pole sana ngoja nikupuuze tu. Katika swala la Elimu mara zote nasimama kidete yaani nasimama upande wa wananchi na upande ulio sahihi. Mlileta hoja eto boarding za watoto zifungwe nilisimama mpaka mwisho...ACHENI KUKURUPUKA KATIKA KUFANYA MAAMUZI.
 
Watoto waende likizo hakuna kazi isiyo na likizo tena kwa watoto wetu kupumzika ni muhimu sana. Mtoto akajifunze mambo mengine ya kimaisha mzazi mpeleke kijijini achunge,alime,apasue Kuni,salimie ndugu,ajifunze kilugha na milazao,acheze mitaani,akauze bidhaa sokoni nk.
Elimu yetu inakosa mpangilio mzuri wengine tulishauri mpangilio wa semister tatu mfumo uwe kamahivi;
3 Jan mpaka 31 machi - masoma(miezi 3).
1 April mpaka 30 April - likizo ya kwanza(mwezi 1).
1 may mpaka 31 July - masomo(miezi 3).
1 august mpaka 31 august - likizo ya pili(mwezi 1).
1 September mpaka 30 November - masomo(miezi 3).
1 December mpaka 2 January - likizo ya tatu(mwezi 1).
**Watoto watasoma jumla siku 180 (miezi 9 × 20 siku kwamwezi) ambazo zinatosha hazitofautiani na siku za masomo kwasasa!!
Darasa la saba wasome semister mbili tuu wafanye mtihani wa taifa Kisha Semister ya tatu (miezi mitatu) wanafunzi wa darasa la saba wafundishwe English na maths tuu kujiandaa kwenda sekondari, walimu wa sekondari wapelekwe primary wakati huo kusaidia ufundishaji maana sekondari kunakuwa hakuna mzigo mkubwa na walimu Huwa wengi sekondari nyingi kuzidi msingi!!
Serikali imekuwa nzito sana kufanya maamuzi katika elimu jambo linalozorotesha sana elimu yetu nakuongeza mdororo wa elimu kuwa na wahitimu wenye uwezo mdogo saaana hata katika kujieleza na kujisomea.
Yote hayo tumekaririshwa ...kwani wakisoma zaidi ya siku 180 kuna shida gani kama malengo ni kuwajenga vijana wafaulu vizuri ili waje walijenge Taifa letu.
 
Kuna wazazi wakisha wabwaga watoto shule, hamutaki kuwaona tena!! Imekuwa kama muna alergy, hakuna bond kabisa! Mmeshindwa kulea basi ngoja mlelewe
Haya ni mawazo yasiyo sawa...hivi unafikiri watoto wanaobakishwa au kuendelea na masomo ni wale wa shule za kulala yaani bweni tu? Tatizo wengi mnaliongelea ili swala wakati mpo nje ya hii sekta.
 
Wazazi mwanao kama yupo form four, aendelee kusoma na kujisomea, haya matamko ya wanasiasa ni matamko ya kisiasa.

Wewe mwanao yupo shule ya kata, na unajua kuwa ili aweze kupata nafasi ya kwenda hata VETA au kuongeza ujuzi wowote basi cheti cha Form four lazima.

So akili kichwani, yaani mzazi unakaa na kusubiri future ya mwanao ambaye yupo shule ya kata iliandaliwe na waziri!

Mwanao akipata zero hata upolisi hawamchukui na huko mtaani ndio kizazi cha singeli hiki, pathetic.

Nimeandika maana nipo uswahilini De es Salaam, nimeona watoto wa kike na kiume wakikaa mtaani wanaishia kupoteza mwelekeo huku mtaani, hakuna mzazi makini wakumpa malezi bora mwanae.
Mananga kama wewe hutakiwa kujishughulisha na mambo ya familia zao tu. Huna uelewa wowote kuhusu education psychology wewe.
 
Watoto waende nyumbani kupumzika na kuwasaidia kazi wazazi wao. Muda wa kupumzika uheshimiwe.
Watoto ambao wazazi wao wameridhia kuendelea kusoma wanayo haki kuendelea na masomo freedom of choice.Hakuna sera wa kalenda ya Elimu hapa Tanzania inayosema ni lazma watoto wote na shule zote zifunge muda wa likizo.
 
ndio kizazi cha singeli hiki, pathetic.
Kati ya singeli na upolisi kipi bora?
Kati ya singeli na ualimu kipi bora?
Kati ya singeli na unesi kipi bora??
Kati ya singeli na usekretari kipi bora?
Kati ya singeli na uaskari magereza kipi bora?

Kwa taarifa yako waimba singeli wametoboa kimaisha kuliko makundi mengi ya wafanya kazi nchi hii
 
Education psychology mnaisoma vyuoni ili kufauru na kupata vyeti. Uhakika nikua mnacopy na kupaste mambo ya wazungu huku mkishindwa kujua mazingira,makuzi,mahitaji na malengo ni tofauti. Nadhani kuna haja ata ya kuiangalia tena Elimu ya vyuo vyote yaani vya kati na juu.
Mananga kama wewe hutakiwa kujishughulisha na mambo ya familia zao tu. Huna uelewa wowote kuhusu education psychology wewe.
 
Education psychology mnaisoma vyuoni ili kufauru na kupata vyeti. Uhakika nikua mnacopy na kupaste mambo ya wazungu huku mkishindwa kujua mazingira,makuzi,mahitaji na malengo ni tofauti. Nadhani kuna haja ata ya kuiangalia tena Elimu ya vyuo vyote yaani vya kati na juu.
Kufauru = kufaulu, tufundishane kwanza. Approach ya binadamu wote kwenye kujifunza inafanana. Waliosema kuwe na likizo walifanya tafiti nyingi na wakagundua kuwa ili mwanafunzi aweze kuulewa vizuri anachosoma, basi anahitaji mapumziko. Mwili unapofanya kazi kwa muda mrefu huchoka. Ubongo ni sehemu ya mwili hivyo nao unahitaji mapumziko ili uwe tayari kusoma mambo mapya!
 
Kufauru = kufaulu, tufundishane kwanza. Approach ya binadamu wote kwenye kujifunza inafanana. Waliosema kuwe na likizo walifanya tafiti nyingi na wakagundua kuwa ili mwanafunzi aweze kuulewa vizuri anachosoma, basi anahitaji mapumziko. Mwili unapofanya kazi kwa muda mrefu huchoka. Ubongo ni sehemu ya mwili hivyo nao unahitaji mapumziko ili uwe tayari kusoma mambo mapya!
Nashukuru kwa kunikosoa hapo juu.
Kwahiyo mkuu unataka kusema wanafunzi hao awapumziki?
Kuna mapumziko ya kila siku, kila juma,mwezi wa nne na baada ya mitihani.Mfano waliomaliza kidato cha nne mwaka jana mwezi wa Novemba mpaka leo wapo nyumbani takribani miezi nane.
Shule na wazazi waliokubali watoto wao kuendelea na masomo wako sawa in haki yao. Utafiti unaosema ninao uhakika wala ujui. Vijana waendelee na masomo tu ili waweze kufauru na kuendelea na masomo ya juu...
Wizara iachane kuangaika na vitu vidogo wakati kuna mambo makubwa kwenye in changamoto.
Nyumba za walimu,umeme,vyoo,usafiri,chakula,vitabu nk
 
Back
Top Bottom