Hivi kwanini Mabasi kutoka Dar kwenda Mpanda, Katavi yanazuiwa kuendelea na safari yakifika Sikonge, Tabora?

Unahamasisha rushwa?
 
Weeeh yani huko kulivo na misitu bora mlale hapo hapo Sikonge msije enda kutolewa marinda bus zima.
 
Sio kwa mapori ya hiyo njia ambayo inatokeza Mbeya pia. Hawa polisi wenu wakimbiza vijana wa bodaboda hawana uwezo huo watabakwa live.
Hiyo ya kwenda Mbeya ukitoka Sikonge ni pori mpaka Kitunda, ukitoka Kitunda ni pori tena mpaka Rungwa, ukitoka Rungwa mpaka ufike Kampikatoto unakutana na pori tu tena lenye wanyama wa kutosha utakatiza usiku pori hilo??
 
Acha kuongea engese kwenye hoja serious aisee...
Unasema hivyo kwa sababu hujawahi kusafiri kwenye hizo njia.

Ungekuwa ulishawahi kutekwa hata siku moja barabara hizo usingesema hiki.

Hebu jiulize uko katikati ya hifadhi ya ugala halafu unaambiwa uchague kufa au kuliwa kisa una 50k tu mifukoni mwako kipi utachagua?
 
Sahihi ukitoka Sikonge mpaka Mlele ni hifadhi ya misitu then Mlele to Mpanda pia ni hifadhi ya misitu pande zote mbili ya barabara hakuna Vijiji hapo kati lakin Serikali Kwa nini isiweke kambi kadhaa za jkt au jeshi, TFS,magereza au polisi shida nini na pale masaa matatu tu upo Mpanda

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Nyongeza hapo....
Kulikuwa na mabasi ya saa 10 jioni (mengi ni ordinary abiria 65)

Saa mbili usiku(luxury)

Utaratibu huu ulikoma baada ya ajali ya busi la Yalabi Salama, Dar kwenda Dodoma. Kwa amri ya Waziri Mkuu wa kipindi hicho.

Hii ni nchi ya matamko na sio uhalisia!
 
Pori lile sio poa, tumewahi zuiwa hapo enzi hamna lami, tunaitafuta Inyonga tupo na Land Cruiser LX ,tumetoka Sikonge kwenye majukumu X, tuliona Mjuba anatoka porini na chuma mgongoni kuingia kama anachungulia aone nani anakuja nahisi walikuwa wanalia mingo ndiga za abiria, tupo mwendo wa mateka, suka akatu alert tuwe tayari huku akiwa anapunguza mwendo, vioo vilishushwa na sisi upande wetu Wakurungwa wakazikoki kuzielekeza nje tayari kwa lolote kivyovyote. Yule mjuba akatokomea tena porini kama mshale na kukawa kimya na sisi tukaenda kusimama mbele maana kulikuwa na TaTa ya abiria tuliiacha nyuma kuisubiri. Ikapita tukaisindikiza tukaiacha tukasepa zetu bila kumstua dereva wala kuleta taharuki.
 
[emoji848][emoji848]
 
Tuvumilie kwa sababu gani wakati mtu angefika Mpanda saa 6 usiku na kesho anaenda kazini au kwenye biashara zake?
Kama huko ni porini sana, basi ungewekwa utaratibu wa mabasi kuondoka saa 6 usiku ili yafike Mpanda walau 12 jioni.
 
kwanza kufasiri na basi huo ni umasikini bora kuchelewa kufuka ukafika salama kuliko kuwai mkafika mapolilini mkakutana na warundu wakawageza nyete wanawake kwa zamu mbona jamabi awafai
 
Pumba
 
Siku hizi hata uwahi kabla ya saa tatu lazma ulale... Zamani ndio ilikua ukifika kabla ya saa tatu unaendelea
Hawa wanao lalamika wakitekwa au kupata hajari wakwanza kuilaume serikali heti mtu anasafiri na kitu kinacho jibuluza chini kama nyoke heti nae anataka kuwai mabasi mengi ya huko mpanda yana wabeba washamba wanaomlaumu dereva aipo endesha kwa kasi
 
kitendo cha kusafiri na basi tu ni umasikini tangu lini masikini akawa na haraka
 
hoja yako inamashiko
 
Kwa hiyo miaka 60 bado hatuwezi kusafiri usiku kweli? Yaani vibaka wanatupangia maisha kweli? Ina maana hatuwezi hata kutumia JW TZ watusaidie kudhibiti hawa vibaka??
ukitaka kuwai panda ndege
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…