baba-mwajuma
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 4,178
- 7,591
Kodi zipo na hapo hata hazijawekwa zote kwenye list sijaona manispaa Leseni, maana kuna Jiji service levy na Manispaa leseni.Mh Rais ni kweli umeamua kuuwa uchumi na biashara kabisa? Hivi kweli umeruhusu kadi za namna hii?
Hii nimeikopi kwa mwana jf wakukurupuka1
Nanukuuu
“Leo Kuna mgomo kwa wafanya biashara soko kuu kkoo kutokana na kila wiki uzinduzi wa kodi mpya
Baadhi ya kodi unazotakiwa kulipa
1: TRA.
2: FIRE.
3: JIJI.
4: USAFI.
5: Kodi ya store.
6: Makato 10% kweny commission (watu wa mihamala)
7: Kodi yakupeleka lori kkoo kubeba au kushusha mizigo”
Mwisho wa kunukuu
Hivi kweli mtu awe na store ya kuhfadhi mzigo wake halafu anatakiwa kulipa kodi? Na akitoa huo mzigo kwenda dukani akiupakia atatakiwa kulipa kodi na akifika dukani kwake atatakiwa kulipa kodi ya kushusha mzigo halafu akianza kuuza atatakiwa kulipa kodi tena hivi hii ni kweli au TRA wanasingiziwa?
Hivi kodi zipo kwa mtu mmoja au wafanyabiashara wanachangia kwa pamoja? Hivi kweli kuna mfanya biashara ataweza kudumu bila kutoa rushwa? Kuna mfanyabiashara atadumu bila kufanya magendo? Mbona kodi ni nyingi sana kwa mtu mmoja? Hii ni zaidi ya double taxation!
Hivi hizi kodi kweli zipo zote au TRA na serikali wanasingiziwa?
Kwanini Rais usimamii maneno yako?’hizi kodi zote hasa hiyo ya store na kushusha mzigo sio uporaji na unyang’anyi kabisa? Msaada wako uko wapi? Kwanini unayaacha haya au sio kweli?
Issue hapa mkuu Zigo lote anaangushiwa Mfanyabiashara mwenye Frame, nitakupa mfano hapo kwenye Takataka Duka linalipa hadi 40,000 kwa mwezi, Hilo Duka unakuta Wiki Nzima hata Dust bin haijai. Muda huo huo mbele yako kuna Machinga anauza Matunda anajaza Pipa la uchafu, Pengine anapata Faida kuliko wewe na halipi hata sh 10.
Habari hio hio kwenye Zimamoto na kwengineko.
Bado Tra hawajakuja hapo na Polisi wanaojipa Vyeo vya Tra, wanatengeneza mazingira yoyote yale Wapige Hela.