Hizi ndege za ATCL zimemkosea nini Lissu? Mbona anaziwazia mabaya tu?

Tuchukulie Lisu kawa Raisi kwa hiyo atakuwa akilipwa pesa za walipa kodi kulipwa mshahara na marupurupu na pia atakuwa anajichotea pesa zingine za walipa kodi kujilipa fidia

Lisu uraisi hafai hana huruma na wala uchungu na pesa za walipa kodi na mali zao ikiwemo ndege zao walizonunua kwa kodi zao
 
Hapo kafanya mahesabu yake vibaya .
 
Ukweli usemwe: Tigo na serikali ina KESI ya kujibu.
Ni muda tu
 
Kwa nini Serikali isimlipe madai yake? Kinachoonekana ni kuwa Serikali inaanzisha yenyewe timbwili, ikishindwa kesi inagoma kulipa...Lissu anasema kama akishinda kesi yake, asipolipwa atakamata maboeing matatu yanayofanya safari za nje ya nchi.....Sidhani kama kuna ubaya wowote hapo. 🤔
 
Wewe ni mzalendo gani ? Ulishapelekwa hata kwa balozi wa nyumba 10 tu, ukiitetea nchi yako ? Nimekuonyesha alivyowatetea ninyi wauaji akapata madhara na bado mnamnyamazisha. Imekuuma siri za tigo kuanikwa. Ukiletewa ushahidi wa mwizi wa mali yako huwezi kunyamaza au kuwasemea wengine walioibiwa ili uonekane mzalendo. Unataka kwa issue hii tigo nani amsemee ?
 
Hii si mara ya kwanza kwa Lisu kupambana na ndege za ATCL kwani uvumi upo kwamba yeye ndiye aliyemshtua yule mkulima kuzikamata ndege zetu huko nje.
Thibitisha hili
 
Sina shida na tigo kushtakiwa,

Shida Inakuja ni kutumia mahakama za nje ilhali ni issue ya kimahakama inayoweza kuwa solved ndani ya nchi Kwa Sheria zetu.

Jambo lingine ni kutaka ndege zetu kukamatwa Ili apate fidia, sasa ndege zetu zinaingiaje hapo?

Kwa mwenye akili atajua, Kuna kundi Fulani linamtumia kuhujumu raslimali za nchi yetu.

Angeeleweka ikiwa angejumuisha Watanzania wote waliotekwa,kuumizwa na kuuwawa, akina Mawazo, sativa ,kibaonnk nk Si kuyaweka madai kibinafsi Kwakuwa anajua Sheria.

Sijui unaelewa?
 
Hujajibu maswali yote ya msingi niliyokuuliza. 1. Zilipokamatwa Canada na South Africa serikali ikalipa billions of money, ni yeye aliyeshtaki ? Kama sio yeye uliwasema ? Una ushahidi wa sauti yake au nukuu ya maneno akizitaja ndege kukamatwa ? Kama huna ushahidi nitakosea kukuona mhusika kwa jaribio la kumuua na unaogopa ushahidi wa kitechnolojia ya wazungu ? Waliosema wanachunguza jaribio la kutaka kumuua sasa ni miaka 7, bado wanachunguza ? Kama Mr Clifford asingeanzisha uchunguzi nani alikuwa na wazo au nia ya kuchunguza tangu 2017 ? Miaka 7 bila hata jalada la kesi kufunguliwa kwa aliyekuwa mbunge ni sawa ?
 
Inasemekana zile ndege ni za mchongo!
Lisemwalo lipo, hebu fikiria kati ya Boeing tatu zilizonunuliwa inafanya kazi moja tu. Jiulize mbili ziko ardhini muda wote kwa nini?
Zile Airbus nne ndio kabisa tatu hazifanyi kazi kabisa, moja tu ndio inafanya kazi ya punda.... Jiulize marubani sita waliosomea kurusha hizo Airbus tatu wako wapi? Sénégal? 😲
 
Umeona suala la Ndege ila sio la Lissu kupigwa risasi mbona watu amna ubinadamu kwani uongo serikali ikishidwa kumlipa madai yake wakamate ayo mandege siku nyingine tusipige risasi watu ambao tumeshindana kwa hoja
 

Si mlikataa kumlipa mafao yake na kumtibu.

Malipo yake sasa itabidi Dremliner moja lipigwe mna uko majuu.
 
Mkuu, tunahujumiwa na huu mfumo wa utawala unaovipa vyama vya kisiasa kuwa na mamlaka makubwa dhidi ya wananchi.
Wananchi wamewekwa kando, wanatumika tu kama dodoki la kuogea. Huu ugomvi wa masilahi binafsi ya vyama ndio chanzo cha kuanza kuuana wenyewe kwa wenyewe na kuhujumiana.
Wananchi tunatakiwa kusituka na kudai uhuru upya, kuweka misingi mipya ya utawala itakayoheshimika na yenye sheria zilizowazi za kuwawajibisha watawala wanaoingia kwenye siasa kwa masilahi yao binafsi au vyama vinavyo wadhamini.
Tuanzie kwenye Katiba mpya tena mwaka huu.
 
Ni mzalendo ila hakufanyiwa uzalendo tangu mpango wa tukio, muda wa tukio na baada ya tukio
 
Si mlikataa kumlipa mafao yake na kumtibu.

Malipo yake sasa itabidi Dremliner moja lipigwe mna uko majuu.
Hivi zile pesa watu walichanga kwa ajili ya matibabu ya Lisu zilitumika kwa matibabu au la? Anachodai ni kipi? Refund za pesa watu walichanga atibiwe ili awarudishie waliochanga pesa za matibabu au ni vipi?
 
Ndege zinakumbusha Magufuli, na kwa upande wake anaamini Magufuli ndio mtu aliyetaka kumuuwa hivyo analaani hadi ndege za Magufuli(mtu aliyetaka kumuuwa).
 
We angepigwa risasi mama yako au Baba yako ungekuja na hizi hoja? wacha wataifishe hata zote kabisa
Unazungumzia hisia, sio kitu cha msingi sana wakati mwengine. Mzazi hata kama anajua mwanae ni panya road ila akisikia mwanae kachomwa moto hadi kufa lazima ataumia tu kwa sababu ni mwanae ila sie wengine tutaona sawa sawa limeondoshwa tatizo. Sasa tusipende sana kusema "ungekuwa wewe au angekuwa mzazi wako au ndugu yako.....".
 
Hivi zile pesa watu walichanga kwa ajili ya matibabu ya Lisu zilitumika kwa matibabu au la? Anachodai ni kipi? Refund za pesa watu walichanga atibiwe ili awarudishie waliochanga pesa za matibabu au ni vipi?

Pamoja na vimichango vyenu yeye kama Mbunge alistahili alipiwe na serikali ..... Ni stahili yake. Kwa nini hutaki asilipwe...!!?
 
Tena ikiwezekana bibi safari akiruka nayo ikakamatwe huko alipokwenda ..

Siasa za Tanzania wananchi kwetu imekuwa movie tu... Ni burudani...
Ni burudani kweli ukichukulia serious utaumia kichwa tu, ndio maana utaona yakitangazwa maandamano mitandaoni watu wanaonesha kuwa piga ua lazima wafanye maandamano ila siku ya tukio hukuti mtu
 
Acha kuvuta bangi mchana, jitahidi kuwapa wanao wosio mzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…