Huyu kijana Amedhalilika sana

Ningekuwa Mimi ndo ungekuwa mwisho wa mchakato wa harusi ningepotea mazima n kuendelea na mishe zangu na ungekuwa msala kwa MC.Kutokujiamini na kuwa na misimamo kama mwanaume imewagharimu wanaume wengi sana kwenye mahusiano na hata ndoa.Usimshobokee demu hadi aone huna pa kwenda , tambua mwanaume unaweza poteza na ukapata kilicho bora kuliko ulichopoteza.Men stand up!!!!
 
Kwanini asiseme "Debora tunawapa nyumba"?
Hiyo ni zawadi ya wazazi kwa binti yao.
Huyo jamaa anahusikaje?
Debora atazitumia kwa manufaa yake binafsi, ikiwemo kuuza ama kupangisha.

Na hiyo ilikuwa send-off.
Zawadi za wanandoa hutolewa siku ya harusi.
 
Umeleta mfano usio endani na uhalisia,rudi tafakari njoo na mfano halisi!! Chombo cha plastic na ghorofa Mbweni, wapi na wapi!!??
 
Umeleta mfano usio endani na uhalisia,rudi tafakari njoo na mfano halisi!! Chombo cha plastic na ghorofa Mbweni, wapi na wapi!!??
Zote ni zawadi, lakini nyumba zimekuwa jambo kubwa kwa sababu hauna.
Ungekuwa na nyumba zako, nyingi na kubwa kuliko anazopewa mkeo, ungeona ni jambo la kawaida mno.
Hiyo insecurity yote inasababishwa na umasikini tu.
 
Naam, wao wamemtaja mtoto wao tu.
MC ndiyo ameamua kumhusisha mwamba, lakini bi mkubwa alikuwa anamrejelea Debora tu.
Je mc anayo mamlaka kisheria kumuhusisha mume na mali alizopewa mke kutoka kwa wazazi wake!!??
 
Zote ni zawadi, lakini nyumba zimekuwa jambo kubwa kwa sababu hauna.
Ungekuwa na nyumba zako, nyingi na kubwa kuliko anazopewa mkeo, ungeona ni jambo la kawaida mno.
Hiyo insecurity yote inasababishwa na umasikini tu.
Kwa sababu ni nyumba ndiyo maana katajwa Deborah peke yake,lakini yangekua hayo Maplestead ya vyombo wangepewa wote kama wana ndoa, kwa hiyo hiyo insecurity na umasikini uko kwa familia ya Deborah shubamiti!!
 
Hiyo ni zawadi ya wazazi kwa binti yao.
Huyo jamaa anahusikaje?
Debora atazitumia kwa manufaa yake binafsi, ikiwemo kuuza ama kupangisha.

Na hiyo ilikuwa send-off.
Zawadi za wanandoa hutolewa siku ya harusi.
Kwangu mwiko pgo hizo
 
Kwa sababu ni nyumba ndiyo maana katajwa Deborah peke yake,lakini yangekua hayo Maplestead ya vyombo wangepewa wote kama wana ndoa, kwa hiyo hiyo insecurity na umasikini uko kwa familia ya Deborah shubamiti!!
Kuna harusi na send-off. Kinachotolewa siku ya harusi ni cha wanandoa, cha kwenye send-off ni cha mhusika.
Ndiyo maana unamwona mwamba kanyanyuliwa kutoka kwenye mabenchi ya watu baki. Haikuwa shughuli yake, sasa zawadi zitamhusuje?
 
Wasukuma walivyo washamba washamba hiyo ndoa km naiona inavyochechemea..!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…