If it is government funds, why call it Samia scholarships?

Ivi nani alisema mwenge utolewe kwenye daraja la tanzanite ili waweke nembo ya tanzanite hii ndo Tanzania ya kundi la watu wanafki namba moja dunian
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Hilo ni jina tu mzee kwani Daraja la magufuli alitoa pesa yake? hospitali ya jakaya kikwete alitoa pesa mfukoni ? tumia akili Rais Samia Suluhu anaplan ya kuimarisha sekta ya elimu upande wa sayansi na technolojia
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Kwani uwanja wa mpira wa Taifa unaitwa jina gani kwani huyo mwenye jina ndio alitoa pesa zake kujenga uwanja

Ni utamaduni tu uliowekwa karibu dunia nzima na sioni ubaya wake

Maana jambo hilo limepewa nguvu kipindi cha utawala wake sio vibaya kuitwa kwa jina lake.
 
Amepotezaje mwelekeo wakati anatoa scholarship? Au mwenzetu hufahamu maana ya scholarship?
Swali la msingi sana maana wengine wapo bize kupinga a hawajui wanapinga nini Rais Samia Suluhu anaimarisha sayansi na teknolojia nchini kupitia hii scholarship wanafunzi watasoma kwa bidii zaidi
 
Exactly kila Rais huwa anaacha kitu alichokifanya kama alama kutumia jina lake magufuli ameacha alama kikwete, Nyerere kila Rais amefanya kitu kwa jina lake na Lengo na Samia Scholarship ni kuimarisha sekta elimu hasa upande wa sayansi na technolojia
 
Unahangaika bure,umewahi sikia kitu inaitwa Obamacare? Pesa zilikuwa za Obama? Muachage ujinga basi..

Sasa kwa taarifa yako sio tuu Kuna hiyo Samia Scholarship Bali Kuna Samia Housing Scheme pia.
Safi sana yani watu hawafikilii wanajiropokea tu kila Rais ameacha alama kuanzia Nyerere mpaka Magufuli so i'ts normal thing
 
Daraja la Kijazi ama Mfugale ni fedha za Umma why yanaitwa hivyo?

Airport je?
Hostel ya JPM je?
Mkicomment narudi
Don't miss the point mkuu. Ule ni mfuko wa pesa zinazotengwa na serikali kwa ajili ya ufadhili wa masomo. Kuita majengo, mitaa, madaraja etc. majina ya viongozi flani ni kumbukumbu kama ishara ya mchango aliotoa/waliotoa huyo/hao kiongozi/viongozi. Mifuko ya udhamini wa aina yoyote ile huwa haipewi majina ya viongozi. Mifano ni mingi lakini kwa uchache nitakutajia baadhi,
1. MO Foundation ( hauna vinasaba hata kidogo na pesa ya serikali.)
2. Benjamin Mkpa Foundation ( pia hauna vinasaba vya aina yoyote na pesa za serikali.)
3. Mo Ibrahim Foundation,
4. Nelson Mandela Foundation,
5. Mwl. Nyerere Foundation
Mifano ni mingi sana.....ila niseme tu kwa mara ya kwanza mimi ndiyo nasikia mfuko wa pesa za udhamini ( Scholarship) unapewa jina la kiongozi/mtu kwa sababu za political motives.
 
Swali la msingi sana maana wengine wapo bize kupinga a hawajui wanapinga nini Rais Samia Suluhu anaimarisha sayansi na teknolojia nchini kupitia hii scholarship wanafunzi watasoma kwa bidii zaidi
Haimarishi chochote bali kutengeneza matabaka tu yasiyo na ulazima na kutaka kuweka legacy kwa nguvu ambayo hata wananchi hawaitaki.pesa hizo siyo zake ni za watanzania na zinatakiwa zipelekwe HESLB.Na kama kuinua sayansi,waboreshe miundombinu ya shule zote za serikali kuanzia walimu wa kutosha,maabara ,mabweni nk.Yaani unachota pesa zetu unajiita scholarship yako wakati huo shule za kata hazina miundombinu ya maana
 
Exactly kila Rais huwa anaacha kitu alichokifanya kama alama kutumia jina lake magufuli ameacha alama kikwete, Nyerere kila Rais amefanya kitu kwa jina lake na Lengo na Samia Scholarship ni kuimarisha sekta elimu hasa upande wa sayansi na technolojia
Asante kwa kunielewa kiongozi.
 
Failed state
 
Haya unayoeleza ndo yananifanya nisione kama tuna waziri anayefaa. Wizara hii haijawahi pata waziri mzuri kwa kipindi kirefu. Huyu ni Profesa lakini pia yaonekana hana ubunifu wa kuinua elimu.

Haya uliyoyasema ni mazuri sana. Ongezea ukweli kwamba huwezi kuinua elimu vyuo vikuu wakati sekondari ziko hoi kiasi tunachokiona nchini. Hakuna maabara ikimaanisha hakuna practices za chemistry, biology na physics, na hakuna waalimu wa hesabu/hisabati. Yeye akiwa Waziri alistahili kuliona hilo, lakini naona shortsightedness haiondoki kwa kusoma PhD.
 
Rais Samia pesa anatoa wapi za kuwapa watu ufadhili? Au sijaelewa? If it is government funds, why call it Samia scholarships?
Mbona ata fedha ni nyara za serikali lakini zina sura za waliowahi kuwa marais??
Mbona hauulizi kwann ofisi za umma zina picha za Rais ???Swali la kitoto kabisa hili
 
Daraja la Kijazi ama Mfugale ni fedha za Umma why yanaitwa hivyo?

Airport je?
Hostel ya JPM je?
Mkicomment narudi
Mkuu hyo madaraja wanatumia watu wote...Ni tofaut na hzo scholarship???

Then jufunze kujibu swali sio kuuliza swal juu ya swali.
 
Vitu vinavyoendelea kubuniwa hapa nchini hasa elimu ya juu ni upuuzi mtupu. Hivi kwa sasa kuna umuhimu gani wa kufadhili hata kukopesha wanafunzi kwa ajili ya elimu ya chuo kikuu? Kwa wasomi wote waliojaa bado serikali ina peleka fedha huko ili ziharibike tu. Kwa nini hii bajeti ndogo iliyopo isielekezwe kwenye technical na vocation trainings ili watu wajiajiri wenyewe na kupewa mikopo kuwasaidia kujiajiri? Kwakweli bado tuna safari ndefu sana.
 
Nadhan ameuliza swali anataka kufahamu Zaid..
Kama unuekewa jaribu kumuelewsha
 
Nadhani ameuliza swali kuwa pesa zinatoka Selikalini au hapana.

Anataka kueleweshwa aelewe tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…