IGP Sirro: Hatuna barua ya kumkamata Askofu Gwajima, utaratibu ufuatwe

IGP Sirro: Hatuna barua ya kumkamata Askofu Gwajima, utaratibu ufuatwe

IGP Sirro amesema kuwa jeshi la polisi linaendeshwa kwa maandishi na kuna taratibu hivyo wanasubiri barua kutoka kwa waziri ili waangalie wanatekeleza vipi agizo lake.

Pia ameongeza kuwa hayo maelekezo ameyaona kwenye mitandao ya kijamii hivyo anasubiri barua rasmi ili waangalie jinsi ya kuyatekeleza hayo maelekezo ya Waziri wa afya kwani serikali inakwenda kwa maandishi.

Sirro pia amesema wataangalia kama kweli kuna jinai au lah ambayo ina haja ya kufungua mashitaka...

Na ameendelea kusema pia kama hatokuta jinai watashauri jinsi ya kumaliza hilo swala katika njia nzuri.

Source: Clouds FM

Pia soma:
- #COVID19 - Waziri Gwajima aagiza Askofu Gwajima kukamatwa ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na viongozi kuhusu chanjo ya UVIKO-19
Nijuavyo mimi mbunge kama mbunge ana sheria zake kukamatwa sasa wakimkamata hovyo hovyo anaqeza waumbua kama anaijua sheria kingine hata wakisema wampandishw kizimbani bado atawashinda kwa mfano akiwauliza hayo maneno aliyazungumzua wapi ma awrikali imjibu kanisani je?serikali si imesema haina dini? imekuwaje tena inatambua hilo
 
Gwajima awe makini na Hizi kauli,nadhani angefuata busara Kama ya Polepole ya kusema mara moja tu na kue ndelea na ishu nyingine
 
Tena huyo Waziri angeshauriwa akaachana na mambo binafsi ya huyo Bwana Askofu.

Hizo ndizo anga zake atampoteza.
 
Kumbe wanao wakamataga wanapewaga barua eee! Au ndio Ile maelekezo kutoka juu
 
Kwa kadiri ya Siro chanjo ni feki
Chanjo zina madhara
Pia Kuna viongozi wamekula hela za Mabeberu possibly Rais ndo kala.
 
Yapi hayo? Ya mkuu wa wilaya kumuamrisha mkuu wa majeshi au?

Huu upuuzi kawahadithie wazee wenzako kwenye kahawa[emoji23][emoji23][emoji23]
Huu mjadala nimeupenda....

Ni kweli hicho kitu hakiwezekani CDF atii amri kutoka kwa NIKKI WA PILI[emoji23][emoji23]

Lakini nimeshawahi kuona kwenye mkuu wa wilaya akipigiwa salute na mwanajeshi (Hawa wenye vyeo vyeo) nadhani ilikuwa kisarawe Kama sikosei
Hii ipoje?

Au Mara nyingi tumeshaona mawaziri wakitembea na wanajeshi kwenye misafara yao, je hawawezi kupokea amri kutoka kwa waziri?

Lakini Mara kibao tumeona wakuu wa mikoa/wilaya wakitoa amri kwa polisi Tena haswa kwenye mikutano ya hadhara....hii ipoje?

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
IGP Sirro amesema kuwa jeshi la polisi linaendeshwa kwa maandishi na kuna taratibu hivyo wanasubiri barua kutoka kwa waziri ili waangalie wanatekeleza vipi agizo lake.

Pia ameongeza kuwa hayo maelekezo ameyaona kwenye mitandao ya kijamii hivyo anasubiri barua rasmi ili waangalie jinsi ya kuyatekeleza hayo maelekezo ya Waziri wa afya kwani serikali inakwenda kwa maandishi.

Sirro pia amesema wataangalia kama kweli kuna jinai au lah ambayo ina haja ya kufungua mashitaka...

Na ameendelea kusema pia kama hatokuta jinai watashauri jinsi ya kumaliza hilo swala katika njia nzuri.

Source: Clouds FM

Pia soma:
- #COVID19 - Waziri Gwajima aagiza Askofu Gwajima kukamatwa ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na viongozi kuhusu chanjo ya UVIKO-19
Yaani askofu Gwajima anatoa matamshi ya kumtuhumu Rais aliyeko madarakani kuwa amepokea rushwa kuruhusu chanjo kuingiziwa nchi halafu IGP haoni kuwa kuna jinai hapo. Hii ni dhahiri kuwa zero anatumika na Sukuma Gang kumhujumu Rais Samia.
 
Toka lini waziri akawa amiri jeshi? Yaani waziri atoe amri kwa jeshi? Tukiendekeza hilo kuna siku we waziri Mulamula ataamrisha jwtz ivamie Malawi!
Ndio maana nimewahi kusema humu katba ibadilishwe jeshi letu lisiongozwe na wanasiasa iwe na mwakilishi anaetoka jeshini Hawana haja ya waziri kwani jeshini hamna wasomi?
 
court-rule-7-2-3-arrest-warrants.jpg
 
Back
Top Bottom