IGP Sirro: Hatuna barua ya kumkamata Askofu Gwajima, utaratibu ufuatwe

Hapo ndipo utakapojua kuwa Wasukuma ni watu wa ajabu sana. Huyu mama na Gwaji boy, ni Mtu na shemegie, tazama jinsi wanavyopapurana. Kumbuka wakati ule alikuwa Gwaji na mkuu wa mkoa DSM, wote wasukuma, tena toka kolomije .
 
IGP Sirro ata ukimuangalia unaona umri umeenda may be tunahitaji mwingine.

It is very irresponsible of him kutaka kupingana na waziri hadharani.

Yeye IGP Sirro kipindi kile anapambana na mauaji ya Kibiti na Rufiji angetokea mtu nakuanza kusema hayo mauaji ni polisi wenyewe wanafanya, sijui hakuna mauaji ni sinema ya kutengenezwa na polisi starling ni IGP mwenyewe. Yeye kwa nafasi angekuwa na reaction gani na hao watu kipindi kile.

Huyu mtu apelekwe KCMC siku nzima, wakitoka hapo wampeleke Mount Meru hospitali, Bugando na Hospitali zingine zenye wagonjwa wanaopumulia oxygen aone changamoto za wizara za kuangaika na hawa patients wa COVID waliopo kwenye intensive care kwenye kuokoa maisha yao.

Halafu mtu kama Dr Gwajima anachangamoto za kutakiwa kutokusema ukweli wote kulinda mapato ya utalii na ajira.

The only way Dr Gwajima anaweza pambana ni kuona watu wanapewa chanjo; halafu anatokea mtu huko anawatungia uongo waziri na raisi; kuongopa juu ya chanjo zenyewe na ku downplay ugonjwa wote.

Sirro anaanza kuzeeka, Azoray Gwanda kukosoa operation yao wamempoteza (kwa mujibu wa CDM) sembuse ugumu huyo askofu anaowapa wenzake katika kazi yao kila siku.

Very ignorant of IGP kumjibu waziri hadharani, aende Bugando kwa siku aone na ugumu wa kazi ya wenzake.
 
Huyu mama gwajima wakupuuzwa kabisaaa,ukimuangalia ktk ile video baada ya kuchwanjwa anavyokimbia kimbia utajua kuna nati inechomoka.
Rudi ktk zile video za kupiga nyungu na wakikimbia na mumewe aisee Huyu kuna sehemu ipo tatzo
Tumepigwa mkuu 😅😅😅
 
Hivi gwaji boy akikamatwa safari hii atapanda pushchair kama Enzi za maharage ya kardinal pengo ?
 
Toka lini waziri akawa amiri jeshi? Hilo likiruhusiwa kuna siku waziri atatoa order kwa jwtz ivamie nchi nyingine. Mawaziri wajifunze namna ya kufanya kazi.
Mara ngapi ma DC/RC wamewaweka watu rumande masaa 24 ..?
 

..mimi kwa maoni yangu Polisi wamezembea kumkamata Askofu.

..unajiuliza kama maofisa upelelezi wa wilaya, na mkoa, wanafanya kazi zao sawasawa.

..kamati za ulinzi za wilaya na mkoa zinafanya kazi ikiwa mtu anaachwa anapotosha kwa muda mrefu kiasi hiki?

..Polisi walitakiwa wamkamate Askofu Gwajima muda mrefu uliopita, na maelezo na malalamiko ya Waziri ni kielelezo kwamba kuna uzembe ktk vyombo vyetu vya usalama.
 
Mama analikoroga vibaya mno
 
Huu mjadala nimeupenda....

Ni kweli hicho kitu hakiwezekani CDF atii amri kutoka kwa NIKKI WA PILI...
Rc na DC ndie wenyekiti wa kamati za ulinzi na usalama kwenye wilaya na mikoa yao kupokea maagizo ni sawa Ila sio kwa mawazili ,nahisi kauli ya wazir ina kaubabe flani hvi ,kwa tafsir nyingne hayo alosema siro ni onyo kwa waziri waheshimu vyombo vyombo vya ulinzi na usalama
 
Haahaa hakuna chochote hapo...
 
Huyu mama gwajima wakupuuzwa kabisaaa,ukimuangalia ktk ile video baada ya kuchwanjwa anavyokimbia kimbia utajua kuna nati inechomoka.
Rudi ktk zile video za kupiga nyungu na wakikimbia na mumewe aisee Huyu kuna sehemu ipo tatzo
Ile kukimbia na Mumewe,alikua anamchoresha sana Mumewe,na inaonekana hata Mume alikua hataki sema Dorothy anaonekana ana sauti kwa Mumewe!!
 
IGP Sirro amesema kuwa jeshi la polisi linaendeshwa kwa maandishi na kuna taratibu hivyo wanasubiri barua kutoka kwa waziri ili waangalie wanatekeleza vipi agizo lake
Waziri anachukua madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu!!
 
Kumbe nchi yetu kuwakamata 'waheshimiwa' ni mpaka barua? Kumbe kuna WAO (wala nchi) na SISI (walalahoi)?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…