Ikiwa wewe ndiye Masikini zaidi kati ya ndugu zako, epuka mikusanyiko ya Kifamilia

Ikiwa wewe ndiye Masikini zaidi kati ya ndugu zako, epuka mikusanyiko ya Kifamilia

Ukiona familia inabaguana ujue tatizo ni wazazi. Watu wanafanya jinsi walivyokuzwa. Kama mzazi anaabudu pesa lazima shida itokee kwenye familia. Mimi nimezaliwa familia ya kawaida ila ninawashukuru sana wazazi wangu kwa kuhimiza watoto tupendane. Baba yangu ilikuwa kama wimbo kila siku kutuambia pendaneni. Huku ukubwani akisikia mtoto flani ana shida atapigia watoto wake wote tuelekeze nguvu kusaidia yule mwenye shida. Mimi kwa baba sitegemei kurithi mali yoyote ila kaniachia urithi mkubwa sana wa malezi bora.

Huko uchagani ile December huwa ni mwezi maalum wa kwenda kudharauliana. Kama huna hela utapewa sana kazi za kupasua kuni, usafi na shughuli nyingi za kitumwa. Hata kwenye vinywaji utapewa zaidi mbege. Fred Saganda kaeleza vizuri kwenye huu wimbo.


• Hongera sana mkuu, kwa malezi yenu mazuri,

• Lakini kuhusu mikusanyiko ya kifamilia mara nyingi huwa ni ukoo mzima, Shangazi, mjomba, binam, babu, bibi na n.k, inaumiza sana unapo kuwa huna kitu kama ulivyo andika hapa chini
👇👇👇
Kama huna hela utapewa sana kazi za kupasua kuni, usafi na shughuli nyingi za kitumwa. Hata kwenye vinywaji utapewa zaidi mbege. Fred Saganda kaeleza vizuri kwenye huu wimbo.
 
No wonder mwanaume anawahi kufa! Maana hapa anasemwa mwanaume asiye na pesa, atasemwa na wanawake atasemwa na ndugu. Wanaume wenzangu tujikite kuukataa umasikini ikiwemo wanawake na ndugu maana wote Hao ukijinasibu nao hakika utakuwa masikini.
• masuala ya kifedha yanabeba wigo mpana sana, hasa katika mahusiano ya kifamilia.,

• Mtu kama hela hamna, mikosi, karaha mbali mbali, hizi huambana na mtu mwenye Ukata.
 
Umaskini ni mbaya sana, hasa pale ikiwa ndani ya ukoo wewe ndiye maskini zaidi kuliko wengine, epuka mikusanyiko ya familia hadi uwe na pesa.

• Ikiwa unajua wewe ndiye masikini zaidi kati ya ndugu zako au hufanyi vizuri kwenye masuala ya kifedha, ninapendekeza uepuke matukio ya familia au mikusanyiko hadi uwe na pesa. Kama kuna ulazima wa kuhudhuria, keti kwa huruma kwenye kona kama mgeni. Waruhusu watu wanaotoa chakula na zawadi wakuhudumie kama mmoja wa wageni, ili usije ukajiaibisha. Usikae karibu na mahali ambapo chakula na vinywaji vinatolewa , kaa sehemu ambayo utaonekana ni mtu tu wa kawaida.

Hii itakusaidia:-
Kuepuka Mizozo: Tofauti kubwa za kiuchumi zinaweza kusababisha mizozo na mvutano ndani ya familia. Kwa kuiepuka mikusanyiko, inaweza kupunguza nafasi ya kutokea mizozo inayohusiana na masuala ya pesa.

Kuhifadhi Heshima: Kuepuka mikusanyiko kunaweza kusaidia kuhifadhi heshima ya kila mwanafamilia. Baadhi wanaweza kujisikia vibaya kuhusu hali yao ya kiuchumi, kujitenga au kukaa mbali nao inaweza kusaidia kuzuia aibu au kujisikia kutengwa.

Kupunguza Mizaha na Kupotosha: Kwa kuepuka kuchanganyikana na familia, inaweza kuzuia mizaha au vitendo visivyofaa vinavyoweza kutokea kutokana na tofauti za kiuchumi.

Kutoa Nafasi ya Kibinafsi: Kujitenga inaweza kutoa nafasi kwa kila mwanafamilia kushughulikia masuala yao ya kiuchumi kwa faragha bila shinikizo la umma au kujitetea.

Kuepuka Uonevu: Tofauti za kiuchumi zinaweza kusababisha hisia za uonevu au wivu. Kuepuka mikusanyiko kunaweza kupunguza nafasi ya hali hizo kutokea na kuhifadhi amani ndani ya familia.
Asilimia kubwa umeongelea ukweli, ila pia inategemea. Maana hata biblia imeandika “amtegemeaye mwanadamu amelaaniwa”.

Mtu anakudharau kulingana na wewe mwenyewe unavyojiweka. Mie huwa nashangaa nikiwa kwenye mikusanyiko ya ki ukoo au hata ya kikazi ama mtaani, unakuta wanatumwa tumwa watu wengine kabisa ambao nikiwaangalia wamenizidi umri na hawakupaswa kutumwa wao kujilinganisha na umri wangu, na nikijiangalia mimi sijioni kama nina hizo pesa za kuwafanya waogope kunituma.

Sema huwa nina ishi kwa standard zangu yaani huwezi kunikuta kila sehemu na pia huwezi kunitabiri kwa lolote.

Na nikipanga kutokea hiyo sehemu huwa na treat watu kwa utu wao na sio vitu walivyonavyo, hiyo kitu imenijengea sana confidence na heshima.

Ukiwa mnyenyekevu na mwenye kujitegemea hakuna atayekudharau, apply leo utaona faida zake.
 
nakumbuka siku nilihuduria kikao cha msiba kanda ya kaskazini mimi kama mkwe wife kanitambulisha kwa mjomba wake kila dakika mjomba ananiuliza umekuja na gari gani
ikabidi tu nimpotezee wao wanadhani kila anayemwoa binti yao ni tajiri


nakumbuka siku nilihuduria kikao cha msiba kanda ya kaskazini mimi kama mkwe wife kanitambulisha kwa mjomba wake kila dakika mjomba ananiuliza umekuja na gari gani

😬😬😬, Utakua ulitamani ugeuze home siku hiyo hiyo,
 
Nachukia watu washamba na malimbukeni wanaotweza utu wa mtu kisa pesa
Ni jambo la kipuuzi sana na hufanywa na watu wasio na akili wala exposure na wengi wana insecurities zao nyingi sasa huwa wanaona kuficha hizo insecurities zao ni kutweza utu wa mtu
Na wengi ni hawa kajambanani unakuta ana vichenji vya kubadilisha mboga nae ana treat watu kama Jalala na kujiona multibillionaire , ni ukosefu wa akili
Utafanyaje mkuu, kama chain ya hela huna lazima utreatiwe, na mwenye nazo hata kama anazo kiasi,
 
Kabsa kwetu mkwilima ana hela kuliko shemeji zake. Akitia timu ukweni mama na mzee humkaribisha Kama raisi. One day uncle ambaye ni shemeji yake walitofautiana kisa anaambiwa you are above 40 na bado uko home. Kauli hyo ilileta Timb wili mpaka kufikia hata ya kutaka kuzipiga. But at the end of the day shemeji mtu Ali win the loyar rumble course uncle alitukanwa mbaya na bibi akiambiwa Hana adabu kwa mkwilima.
Tutafute pesa kujenga heshima mjini
 
Asilimia kubwa umeongelea ukweli, ila pia inategemea. Maana hata biblia imeandika “amtegemeaye mwanadamu amelaaniwa”.

Mtu anakudharau kulingana na wewe mwenyewe unavyojiweka. Mie huwa nashangaa nikiwa kwenye mikusanyiko ya ki ukoo au hata ya kikazi ama mtaani, unakuta wanatumwa tumwa watu wengine kabisa ambao nikiwaangalia wamenizidi umri na hawakupaswa kutumwa wao kujilinganisha na umri wangu, na nikijiangalia mimi sijioni kama nina hizo pesa za kuwafanya waogope kunituma.

Sema huwa nina ishi kwa standard zangu yaani huwezi kunikuta kila sehemu na pia huwezi kunitabiri kwa lolote.

Na nikipanga kutokea hiyo sehemu huwa na treat watu kwa utu wao na sio vitu walivyonavyo, hiyo kitu imenijengea sana confidence na heshima.

Ukiwa mnyenyekevu na mwenye kujitegemea hakuna atayekudharau, apply leo utaona faida zake.
🤔, Mkuu kwa maelezo haya, lazima utakuwa na vitu kama usafiri wako, na biashara fulani inayojulikana, tofauti na hapo, heshima lazima ishushwe tu.
 
Umaskini ni mbaya sana, hasa pale ikiwa ndani ya ukoo wewe ndiye maskini zaidi kuliko wengine, epuka mikusanyiko ya familia hadi uwe na pesa.

• Ikiwa unajua wewe ndiye masikini zaidi kati ya ndugu zako au hufanyi vizuri kwenye masuala ya kifedha, ninapendekeza uepuke matukio ya familia au mikusanyiko hadi uwe na pesa. Kama kuna ulazima wa kuhudhuria, keti kwa huruma kwenye kona kama mgeni. Waruhusu watu wanaotoa chakula na zawadi wakuhudumie kama mmoja wa wageni, ili usije ukajiaibisha. Usikae karibu na mahali ambapo chakula na vinywaji vinatolewa , kaa sehemu ambayo utaonekana ni mtu tu wa kawaida.

Hii itakusaidia:-
Kuepuka Mizozo: Tofauti kubwa za kiuchumi zinaweza kusababisha mizozo na mvutano ndani ya familia. Kwa kuiepuka mikusanyiko, inaweza kupunguza nafasi ya kutokea mizozo inayohusiana na masuala ya pesa.

Kuhifadhi Heshima: Kuepuka mikusanyiko kunaweza kusaidia kuhifadhi heshima ya kila mwanafamilia. Baadhi wanaweza kujisikia vibaya kuhusu hali yao ya kiuchumi, kujitenga au kukaa mbali nao inaweza kusaidia kuzuia aibu au kujisikia kutengwa.

Kupunguza Mizaha na Kupotosha: Kwa kuepuka kuchanganyikana na familia, inaweza kuzuia mizaha au vitendo visivyofaa vinavyoweza kutokea kutokana na tofauti za kiuchumi.

Kutoa Nafasi ya Kibinafsi: Kujitenga inaweza kutoa nafasi kwa kila mwanafamilia kushughulikia masuala yao ya kiuchumi kwa faragha bila shinikizo la umma au kujitetea.

Kuepuka Uonevu: Tofauti za kiuchumi zinaweza kusababisha hisia za uonevu au wivu. Kuepuka mikusanyiko kunaweza kupunguza nafasi ya hali hizo kutokea na kuhifadhi amani ndani ya familia.
Naam hudharauliki wewe tu hata watoto wako hawapewi kipaumbele kivile,
Ni huzuni sana

Sent from my TECNO BE6 using JamiiForums mobile app
 
Yaan hata taarifa za matukio hupewi Kuna siku nikahoji mbona hajaambiwa kuhusu hili tukio wazee wakasema achana atakuja kutuletea fujo maana huwa mtata katika kutaka kunyoosha Jambo wakati pesa hana.
 
Mkuu majani siwezi acha aisee, kwa upande wa hela nilishapishana nazo. Kuna stage ukifika inabidi ukubali matokeo vinginevyo unaweza kuishia jela au kujiletea msongo wa mawazo.
• 😟😟, Kwamba time ya utafutaji, imeisha??,
• maana yake unakula Majani kwa ajili ya kupooza machungu na hasira za maisha?
 
Kabsa kwetu mkwilima ana hela kuliko shemeji zake. Akitia timu ukweni mama na mzee humkaribisha Kama raisi. One day uncle ambaye ni shemeji yake walitofautiana kisa anaambiwa you are above 40 na bado uko home. Kauli hyo ilileta Timb wili mpaka kufikia hata ya kutaka kuzipiga. But at the end of the day shemeji mtu Ali win the loyar rumble course uncle alitukanwa mbaya na bibi akiambiwa Hana adabu kwa mkwilima.
Tutafute pesa kujenga heshima mjini

One day uncle ambaye ni shemeji yake walitofautiana kisa anaambiwa you are above 40 na bado uko home
• 😬😬 Jamaa, anafeli sana 40 years lakini bado yupo home tu,
• Huyo asubili kufa tu sasa, maana time imeisha,
 
Yaan hata taarifa za matukio hupewi Kuna siku nikahoji mbona hajaambiwa kuhusu hili tukio wazee wakasema achana atakuja kutuletea fujo maana huwa mtata katika kutaka kunyoosha Jambo wakati pesa hana.
wakasema achana atakuja kutuletea fujo maana huwa mtata katika kutaka kunyoosha Jambo wakati pesa hana.
😀😀, Hapo wanajua hata akija hawezi changia pesa inayo eleweka,
 
Back
Top Bottom