Ikulu yakanusha Rais kusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba!

Ikulu yakanusha Rais kusaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba!

Safari hii Press release ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ina nafuu sana. Haina mipasho kama statements za nyuma.

Kuhusu rais ku-sign muswada. Ni kifungu gani cha sheria kinamtaka rais a-sign muswada hata kama anaamini muswada huo ni mbovu? Ukisoma statement ya Ikulu inaonekana kama - kisheria- Rais hawezi kukataa ku-sign muswada ukishapitishwa bungeni. Hii ni sahihi?

Asante kwa kuliona hilo mkuu!

Na mimi niulize, ikiwa ni kweli kuwa endapo mswada umeshatoka kihalali bungeni (kama wanavyodai) hivyo LAZIMA usainiwe kwanza alafu marekebisho yafuate baadae, je ni kwanini huwa hukumu halali zinazotolewa kihalali na Mahakama za watu kunyongwa huwa marais wetu hawalazimiki kuzisaini mara moja zifikapo Ikulu ili sheria ifate mkondo wake? Ni kijiswali tu cha kizushi!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Wewe unampongeza JK au unawapongeza JF kwa kumpa mtu Ban?
Habari ya Muswada kusainiwa na Mh Rais zilisambaa ktk mitandao yote. Na ndio maana Kurugenzi ya habari Ikulu iliona kuna umuhimu wa kutoa ufafanuzi juu ya jambo hilo.

Changia mada wacha Kimbelembele cha kujipendekaza kwa uongozi wa JF.
Mkuu mbona unaonekana umevurugwa hizo jazba za nini mbona mchangiaji kachangia vizuri,
wewe huna mamlaka ya kumfundisha mtu namna ya kuchangia kwani wewe nani hapa jf acha utoto wako.
 
Hivi inachukua siku ngapi kwa Documet kutoka Bungeni mpaka Ikulu?
Au Umetumwa kwa kutumia Bajaji?

Alafu kumbe ajausoma wala kuuona, ndio maana ilikuwa nimeambiwa, nimesikia, nimesimuliwa. Sasa aliusemea vipi na ilihali ajuhi hata ukoje?

.
Ikulu ya Tanzania ni majanga hasa baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani.
.
 
Hakuna mahali popote duniani ambapo mswada wa sheria uliopitishwa kihalali bungeni watu hupita mitaani na kutembea jangwani wakinshinikza asiusaini. Nikirudi kwa kauli yake kwamba wabunge warudi bungeni wafanye marekebisho hakuamaanisha kuwa mswada hatausaini. Sana sana alichosema ambacho nataka watu fulani ambao vichwa vyao ni vigumu kuelewa waelewe kuwa Mh Rais alizungumzia kanuni za Bunge kuhusu kamati ya Bunge ya sheria na katiba kutoenda Zanzibar. Baada ya maelezo yake akasema hakuna mahali popote, narudia hakuna mahali popote ambapo kanuni za kudumu za bunge zinasema kamati (yoyote) inabidi iende Zanzibar na kama wabunge wanaona iwe hivyo basi warudi Bungeni wafanye marekebisho ya kanuni. Sasa bahati mbaya kuna watu uelewa wao ni hafifu na wako humu kijiweni; walidhani Mh KASEMA MSWADA URUDI BUNGENI, UFINYU WA FIKRA NA UDHAIFU WA KUELEWA uliwafanya hawa DUNDUNDU wadhani kihivyo na kuanza kusherehekea ufinyu wao wa kuelewa. Ndani mwao kuna wengine wanaelewa alichosema Mh Rais lakini kwa kuwa wanaona wakiwaelimisha alichosema Mh watawachukia kwa kuwa vichwa vimejaa maji tu yaani ni watu wanaoelewa kutokuelewa. Mmoja wao ni Tundu, huyu anajua alichosema Mh Rais lakini amaeacha DUNDUNDU wachemke wenyewe wakidhani yupo pamoja nao. Fikiri kabla ya kutenda, na Waingereza wana msemo mzuri tu kwa kiswahili kisicho rasmi unasema, husiseme kabla hujafanya utafiti maana utaonekana boya na kituko.:frusty:

Ama kweli akili za kuazima haziwez kustili kichwa,wewe ndiwe unaye mwona kikwete ni mungu wako kana kwamba kila anachokisema lazima kiwe sahihi na kweli daima,kuna watu wana akili na uwelewa zaidi yako na kipimo cha uwelewa wa mtanzani sio shule,utajulikana kwa ushabiki wa vyama kama mtu unashabikia ccm unawezaje kuwa na akili timamu?
 
Raisi makini hawezi kulisemea jambo asilolisoma. Hata kama ofisi za Bunge zingekuwa Kanyigo-Bukoba lazima Mswada ungalikwisha fika Ikulu. Inawezekana mswada ulikwishafika ila Raisi hakupata nafasi ya kuusoma sababu alienda safari Marekani.
Jambo la msingi kulielewa ni kuwa hakuna anayesema ukweli kati ya Raisi mwenyewe na kurugenzi yao. Wote mali ya nyande-wamepungukiwa na utukufu. Kurugenzi inashindwa kusema amesaini na hatasaini-wanababaika .Hawana uhakika kama ukifika atausaini au hatausaini. Wanacheza na maneno. Lolote litakalo kuwa wapate pa kusimamia.
Hivi inachukua siku ngapi kwa Documet kutoka Bungeni mpaka Ikulu?
Au Umetumwa kwa kutumia Bajaji?

Alafu kumbe ajausoma wala kuuona, ndio maana ilikuwa nimeambiwa, nimesikia, nimesimuliwa. Sasa aliusemea vipi na ilihali ajuhi hata ukoje?
 
Sekeseke kati ya JK na kamanda Lissu linaendelea...!
Rais kikwete kupitia taarifa ya ikulu atatia sahihi muswada mara utakapomfikia kwani kwa mujibu wa ikulu muswada huo umepitia hatua zote halali na muhimu za kisheria.iwapo kuna marekebisho yatafanyika baada ya kusainiwa mswada huo.
Tusubiri next move ya mh. Tundu lissu.

Source:TBC
 
Nakuwa wa kwanza kuungana na tarifa ya ikulu jk atie saini.
 
Kwa hiyo miswada inapelekwa
Bungeni ili kugongwa muhuri wa bunge pekee? Ndio maana wabunge waCCM
hawajadili miswada bali wanajadili Chadema na viongozi wake tuu kwa vile
kazi ya kugonga muhuri haina shida?

Mkuu hapa ndo hoja ilipojificha.
 
Asante kwa kuliona hilo mkuu!

Na mimi niulize, ikiwa ni kweli kuwa endapo mswada umeshatoka kihalali
bungeni (kama wanavyodai) hivyo LAZIMA usainiwe kwanza alafu marekebisho
yafuate baadae, je ni kwanini huwa hukumu halali zinazotolewa kihalali
na Mahakama za watu kunyongwa huwa marais wetu hawalazimiki kuzisaini
mara moja zifikapo Ikulu ili sheria ifate mkondo wake? Ni kijiswali tu
cha kizushi!

Mkuu upo sahihi kabisaa, watuambie ni kifungu gani inawalazimisha kusagin hata kama jambo lenyewe lipo bovu???
 
Watu acheni USHAMBA. Mswada kutiwa saini haimaanishi kuwa hauwezi kurekebishwa.

Kila sheria iliyopo kwenye vitabu vyetu inaweza kurekebishwa. Sheria pekee zisizoweza kurekebishwa ni zile zilizotoka kwa Mungu zilizopo kwenye vitabu vitakatifu.

mkuu hii nimeipenda sana only, usiue usizini etc
 
JK lazima awafanyie kitu mbaya mapimbi
anamfanyia mbaya nani?
Je ni kutaka kumuonyesha ubabe Tundu lissu?
Je ni ubabe kwa wapinzani?
Maamuzi ya ghadhabu au kusikia au kuambiwa au kutaarifiwa sio lazima yawe sahihi.
Ubaya wa katiba una athari kwa wananchi na ccm pia!
Wengi wana haki lakini wachache wanayo haki ya kusikilizwa!
 
Sekeseke kati ya JK na kamanda Lissu linaendelea...!
Rais kikwete kupitia taarifa ya ikulu atatia sahihi muswada mara utakapomfikia kwani kwa mujibu wa ikulu muswada huo umepitia hatua zote halali na muhimu za kisheria.iwapo kuna marekebisho yatafanyika baada ya kusainiwa mswada huo.
Tusubiri next move ya mh. Tundu lissu.

Source:TBC

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Leo, Jumatatu, Oktoba 7, 2013, zimetungwa habari, zikaingizwa kwenye Mitandao ya Kijamii na kusambazwa sana zikidai kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametia saini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambao ulipitishwa na Bunge katika Kikao chake cha mwezi uliopita.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu inapenda kufafanua kama ifuatavyo:

a) Kwanza, Ofisi ya Rais, Ikulu haijapokea Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Inawezekana Muswada huo umekwishakutumwa kutoka Bungeni lakini haujamfikia Mheshimiwa Rais. Hivyo, kama haujamfikia, Mhe. Rais hawezi akawa ameutia saini

b) Pili, Muswada huo ukimfikia Mheshimiwa Rais, inatarajiwa kuwa atautia saini kwa sababu Muswada huo umepitia katika mchakato sahihi na halali wa Kikatiba kwa maana ya kufikishwa Bungeni na Serikali, Kujadiliwa na hatimaye kupitishwa na Bunge.

c) Tatu, kama yapo marekebisho ambayo yanaonekana yanafaa kufanywa katika Sheria hiyo, basi yatafanywa na Bunge baada ya Mhe. Rais kuwa ametimiza matakwa ya Kikatiba ya kutia saini Muswada ambao umepitishwa na Bunge kwa kufuatia mchakato sahihi na halali wa Kikatiba.

d) Nne, na wala hii haitakuwa mara ya kwanza kwa Sheria kupitishwa na Bunge, ikatiwa saini na Mhe. Rais na baadaye kufanyiwa marekebisho na Bunge baada ya kuonekana umuhimu wa kufanya marekebisho hayo. Mwishoni mwa mwaka 2012, Sheria ya Marekebisho ya Katiba ilipitia njia hiyo.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

7 Oktoba, 2013
 
Asante kwa kuliona hilo mkuu!

Na mimi niulize, ikiwa ni kweli kuwa endapo mswada umeshatoka kihalali
bungeni (kama wanavyodai) hivyo LAZIMA usainiwe kwanza alafu marekebisho
yafuate baadae, je ni kwanini huwa hukumu halali zinazotolewa kihalali
na Mahakama za watu kunyongwa huwa marais wetu hawalazimiki kuzisaini
mara moja zifikapo Ikulu ili sheria ifate mkondo wake? Ni kijiswali tu
cha kizushi!

kwenye adhabu ya kifo au yoyote inayotolewa na mahakama yaweza kulingana na muswada. hukumu ikitolewa mahakamani, rais hana mamlaka isipokuwa anaweza kuchelewesha tu adhabu yake. vivyo hivyo kwa bunge. sheria ikitungwa na bunge, rais hawezi kuikataa isipokuwa atatoa ushauri pale ambapo anaona pana dosari
 
JK atausaini Muswada kuyaliridhisha ma CCM na kuonesha kuwa yungo Ngangari na Tamko la Wapinzabi... then ataurudisha bungeni for ammendments kwa kuwa Moyoni anajua kabisa huo Muswada hauna Maslahi kwa umma bali Maslahi ya ma CCM hence kukubaliana na hoja za wapinzani.
Hii inaitwa kuuma na kupulizia..ma CCM yataridhika kabisaaa kama ma toto vile...Mark my words na ningependa niwekwe kwenye kumbu kumbu.
 
Raisi makini
hawezi kulisemea jambo asilolisoma. Hata kama ofisi za Bunge zingekuwa
Kanyigo-Bukoba lazima Mswada ungalikwisha fika Ikulu. Inawezekana mswada
ulikwishafika ila Raisi hakupata nafasi ya kuusoma sababu alienda
safari Marekani.
Jambo la msingi kulielewa ni kuwa hakuna anayesema ukweli kati ya Raisi
mwenyewe na kurugenzi yao. Wote mali ya nyande-wamepungukiwa na utukufu.
Kurugenzi inashindwa kusema amesaini na hatasaini-wanababaika .Hawana
uhakika kama ukifika atausaini au hatausaini. Wanacheza na maneno.
Lolote litakalo kuwa wapate pa kusimamia.

Mkuu, hilo la kussaini, shaka ondoa. mheshimiwa Rais lazima asaini na mambo mengine yataendelea ukiwa umesainiwa. kuhusu muswada kufika Ikulu, hapa ndipo makanjanja wengi wasipoelewa. kusema kuwa muswada haujafika Ikulu haina maana kuwa Mh RAis hana nakala ya muswada huo. ila taratibu za kisheria ndo hazijafanyika kwa maana ofisi ya Bunge kuwasilisha ile nakala ambayo inatakiwa kusainiwa
 
JK kuna haja gani ya kusaini kitu ambacho unajua kuwa ni takataka?hizo ni mbwembwe zisizo na tija kwa nchi yetu!!!huko ni kupoteza resources tuuu.UNASAINI KISHA UNAURUDISHA BUNGENI,KISHA UJE KWAKO TENA USAINI haina maana mkuu
 
Eti "mswaada umepita hatua zote muhimu bungeni na sasa hatua iliyobaki ni kusign"

Kama kile kitendo walichokifanya wabunge wa ccm kumtusi mbowe na kuwajadili wabunge wa upinzani ndiyo hatua "muhimu" na "taratibu" bs mie naunga mkono mswada usigniwe hata usiku huu.

I cal it uzandiki na unafiki wa wabunge wa ccm, ule mswaada haukujadiliwa kabisa na hilo wanalijua na hata idadi ya wabunge haikutimia ili kupitisha mswaada huo, kama kweli Rais anania ya kutengeneza katiba ya watanzani bs ajiridhishe tu kwa kuangalia hansard za bunge za siku mswaada unapitishwe kibabe na wazandiki wa ccm, walaaahi mtukufu rais ukiona hizo hansard hutasigh tena bali utaomba na ww hata uwepo bungeni ili uone watu wako wakoje, (japo kanuni haziruhusu)

Kifupi alietoa maelekezo kwa job ndiyo alieharibu mchakato wote, maana job alikuwa na jazima toka kipindi cha bunge kinaanza na maneno aliyokuwa akiyatumia mfano"zege halilali"nataka leo tumalizane kabisa humu humu" sasa refa akiwa na maneno kama hayo hapo kutakuwa na fair play? Haya nayosema hayana ushabiki wowote ni ukweli mtupu, Jitahidi tu utuachie Taifa lililo moja na sio lililogawanyika sababu ya chama chako.
 
Back
Top Bottom