Imenishangaza Katibu Mwenezi Chama Kikubwa Ndugu Paul Makonda hana Agenda; Anajitwangia tu

Sio kazi yake hiyo yaan katibu mwenezi aje kutatua changamoto ya umeme waziri yuko wapi? Naibu wzir yuko wapi?

Kwahiyo kazi yake ni kupatanisha ndoa za watu, au chama hakiisimamii serekali kwenye masuala ya umeme?
 
Nani kasema anatumia pesa za umma? Chama chetu kina kila aina ya rasilimali za kukifanya kiwa na pesa za kutosha kuendesha na kufanya shughuli zake za chama.
Rasilimali gani chama kimejaa mafisadi?
 
Nilimwelewa Mwanasheria wa Serikali kwamba ziara ya Mwenezi imemfumbua ufahamu kwamba wananchi wana changamoto nyingi sana ambazo hazijapatiwa ufumbuzi.

AG alienda mbali na kusema ataunda kikosi kazi ili kutatua changamoto hizo ambazo nyingi ni za kisheria, haki, wajibu na uwajibikaji.

Binafsi, ziara za Makonda zimenifundisha kitu, kwamba wananchi hawana tatizo lingine kubwa zaidi ya kukosa sehemu ya kupeleka kero zao.

Wenyeviti wa Vitongoji, Watendaji wa Mitaa/Vijiji, Kata na Katibu Tarafa wanahitaji waongeze nguvu katika kushughulika na kero za wananchi.
 
Hakuna chama chenye ubavu wala uwezo wala nguvu ya kuitikisa CCM katika sanduku la kura.

Kwa sababu sanduku la kura hapa Tanzania ni sehemu ya maonyesho ya ujinga wa mtu Mweusi kwenye box la kura.
 
Makonda hawezi kuwa na ajenda zake, anatekeleza ajenda za CCM. Naona wewe umeandika ajenda zako unataka ziwe za makonda
Yeye anaenezq mambo ya CCM, wewe unataka aeneze hayo yako haiwezekani.
 
Hiyo yoote ni system failure ya CCM.


AG anajua kila kitu anazuga tu
 
Makonda hawezi kuwa na ajenda zake, anatekeleza ajenda za CCM. Naona wewe umeandika ajenda zako unataka ziwe za makonda
Yeye anaenezq mambo ya CCM, wewe unataka aeneze hayo yako haiwezekani.
Hizo za ccm zenyewe ziko wapi?
 

Yule ili awe relevant lazima afanye vile. Bila hivyo anasahaulika.
 
Kwahiyo kazi yake ni kupatanisha ndoa za watu, au chama hakiisimamii serekali kwenye masuala ya umeme?
Ni moja ya kazi zake coz chama kipo kutumikia raia leta hoja nyngn hy dhaifu kama misimamo ya chadema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…