Inawezekana tuna watu wasio na uwezo katika nafasi wanazozitumikia?

Inawezekana tuna watu wasio na uwezo katika nafasi wanazozitumikia?

Philip Mpango alipotea vile vile mwezi December kwenda kwenye matibabu South Korea.

Watu wakapaza sauti kuuliza , hawakupewa majibu ya kueleweka.

Karudi kimya kimya kaibukia kanisani Dodoma

Mambo yale yale hayajabadilika mpaka litokee tukio lingine.
Utawala ambao unaona kuwa hakuna consequences zozote mbaya kutokana na matendo yake ya kutoheshimu watawaliwa, hauwezi kujirudi na kujisahihisha.

Ujisahihishe kwa nini wakati hata usipojisahihisha hautatokewa na lolote baya?

Ndiyo maana unaona PM Majaliwa kadanganya watu waziwazi kuwa rais yuko Ikulu anachapa kazi, tena mbele ya waumini msikitini, lakini mpaka leo hajaomba radhi.

Tena tunakuja kusikia habari kuwa alikuwa anapewa habari zote za maendeleo ya afya ya Rais kuwa mbaya, alijua Rais anaumwa hoi yuko hospitalini.

Akadanganya tu watu.

Lakini hajajisikia hata kuomba radhi watu mpaka leo.

Watanzania wanachukuliwa poa tu kupita maelezo.
 
Na kama mliona wanawake hawaezi kuhimili taarifa za misiba kwa nini mmeruhusu kikatiba mwanamke awe Makamu wa Rais anayeweza kuja kuwa Rais kwa msiba?

Si mngesema kwenye katiba Makamubwa Rais hatakiwi kuwa mwanamke, kwa sababu wanawake hawawezi kuhimili habati za msiba.
Hivi yeye mwenyewe kwa akili zake aliona ni sahihi kuondoka na kumwacha mgonjwa akiwa hoi? Watasema alipangiwa safari, je hakukumbuka kuwa za kuambiwa achanganye na zake kweli?
 
Kwa Kweli walimdharau mno mama, Nimefurahi alivyowatia adabu. Mpaka sasa wanaishi na machungu sana.
 
Na yeye mwenyewe aliona ni sahihi kuondoka na kumwacha mgonjwa yu mahututi?
Mkuu,

Ungefuatilia mantiki ya mazungumzo haya, ungeona hapa kuwa swali lako limejengwa katika misingi iliyo misinformed na ni swali la "blaming the victim".

Kitu kikubwa kinachoonekana katika sakata la kifo cha Magufuli, na hata kabla ya kifo , kwenye ugonjwa, na hata kabla ya ugonjwa, kwenye serikali, ni kuwa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Ofisi nzima ya Makamu wa Rais walitengwa kwenye mambo mengi sana.

January Makamba kwenye hotuba yake ya kumkaribisha Samia ughaibuni, nafikiri Italy, hivi majuzi amekuja kuthibitisha hizi habari kutoka kuwa tetesi na kuwa habari rasmi.

Na ukimsikiliza Mabeyo, jinsi taarifa zikivyokuwa zinatolewa, taarifa alikuwa anaopea Waziri Mkuu Majaliwa, si Makamu wa Rais Samia.

Na zaidi, Mabeyo anasema kulikuwa na mpango wa kupindisha katiba ili Samia asiwe Rais kama katiba inavyotaka. Kwa bahati waliweza kusimamia katiba Samia akaapishwa kuwa Rais.

Maana yake kulikuwa na mpango wa watu wakubwa sana serikalini (Mkuu wa Usalama ametajwa) na wa makusudi kabisa, kutaka kumuweka rais mtu kinyume na katiba, Samia arukwe.

Sasa, hapo utaona kuwa Samia alitengwa, hata habari za ugonjwa hakupewa, kapewa habari baadaye baada ya Magufuli kufariki.

Mtu kama huyo unamlaumu vipi kwamba kamuacha mgonjwa wakati pengine na yeye alikuwa anaambiwa rais yuko Ikulu anachapa kazi tu, hakujua mgonjwa? Pengine hata hiyo safari ya Tanga kapangiwa ili watu wakitaka kupindua katiba iwe rahisi.

Wewe unafikiri Samia angejua Magufuli anaumwa mahututi, na yeye Samia ndiye mrithi wa Magufuli, na kuna uwezekano wa mchezo mchafu kuchezwa kupindua katiba, angekubali kwenda Tanga na kuacha kuwa karibu na rais kujua hali inaendaje?

Samia kama hakujua Rais Magufuli anaumwa, ana hali mbaya, angemuacha vipi mgonjwa kama hakujua Magufuli ni mgonjwa hivyo?

Huoni kuwa kumlaumu mtu aliyenyimwa habari kwamba kuna mgonjwa kwa kosa la kumuacha mgonjwa ni kumuonea mtu ambaye na yeye ni muhanga tu wa power politics?
 
Zipo sababu za msingi kabisa ambazo hakukuwa na ulazima zisemwe hadharani za kwanini mh. Makam wa Rais ambaye ndiye Mh. Rais wa sasa alitafutiwa namna yake ya pekee kujulishwa habari hizi
Sababu zipi boss, kama hamuwezi kuzisema acheni tuseme tunavyoona sisi. Hata hivyo ni kipi kulikuwa hakifahamiki Hadi huyo makamu wa rais afichwe? Hicho kifo si Hadi huku Mirandaoni watu walikuwa wanambiana? Kenya hapo si Kuna kituo Cha habari kilisema kabisa jamaa hayupo?
 
CDF ni zaidi ya Makamu wa Rais katika mfumo gani mkuu?

Unafahamu kanuni ya "Civilian control of the military"?

Katika succession plan ya kurithi urais wa nchi ikiwa rais kafariki , Makamu wa Rais yupo namba ngapi na CDF yupo namba ngapi?
Huyo niliyemjibu nimemjibu hivyo Ili ajae ninapotaka.
 
Hizo kauli hazijaanzia kwa Makamba.

Zilikuwapo tangu Magufuli yupo hai kulikuwa na habari kwamba Samia anatengwa na anaburuzwa kwenye maamuzi mengi.

Tulizijua.

Makamba anathibitisha tu.

Na Makamba si mjinga kuropoka mbele ya Samia.

Na Samia hana shida ya kutunga uongo dhidi ya Magufuli.

Au mnataka tufukue mijadala ilivyoenda? Uzuri mijadala yote ipo JF hapahapa.
🤝🙏
 
Utawala ambao unaona kuwa hakuna consequences zozote mbaya kutokana na matendo yake ya kutoheshimu watawaliwa, hauwezi kujirudi na kujisahihisha.

Ujisahihishe kwa nini wakati hata usipojisahihisha hautatokewa na lolote baya?

Ndiyo maana unaona PM Majaliwa kadanganya watu waziwazi kuwa rais yuko Ikulu anachapa kazi, tena mbele ya waumini msikitini, lakini mpaka leo hajaomba radhi.

Tena tunakujabkusikia habari kuwa alikuwa anapewa habari zote za maendeleo ua afaya ya Rais kuwa mbaya, alijua Rais anaumwa hoi yuko hospitalini.

Akadanganya tu watu.

Lakini hajajisikia hata kuomba radhi watu mpaka leo.

Watanzania wanachukuliwa poa tu kupita maelezo.
Very right!

Makamu anapotea juma zima hakuna taarifa rasmi katika vyombo rasmi vya serikali .

Halafu anaibuka ghafla kanisani Jumapili anasema alikua katika majukumu aliyotumwa na alikua akiona mitandaoni wanavyomzushia amefariki akabaki anasikitika.
 
Hivi yeye mwenyewe kwa akili zake aliona ni sahihi kuondoka na kumwacha mgonjwa akiwa hoi? Watasema alipangiwa safari, je hakukumbuka kuwa za kuambiwa achanganye na zake kweli?
Mimi nimekupa linguistic facts ambazo hukutaka kuzibaddress.

Kwa sababu kuna tafsiri moja ingekutoa kwenye ligi ya "nani zaidi" unayoitaka.
 
Kijanaa Mkuu wa Majeshi alipaswa kudictate Wakuu wa Mzena wamtoe akafie nyumbani,sasa Daktari angeanza vipi kuwaambia wakubwa wa Mzena.
Mkuu wa Majeshi naye yuko hospitali anatakiwa asikilize madaktari.

Kwa sababu rais anaweza kuwa ana Covid anataka kwenda nyumbani, halafu nyumbani hakuna utaratibu mzuri wa kuzuia Covid isienee zaidi kwa ndugu zake.

Akifika huko badala ya kupata msiba wa Magufuli tunapata msiba wa Magufuli, mama yake na wajomba zake wote.

Au rais anaweza kuwa anataka kwenda nyumbani, lakini daktari anaona kabisa kuwa huyu Rais akinyanyuka tu hapa kitandani tuna msiba wa kitaifa.

Hapo ndiyo unakuta manyota yote ya kiserikali na kijeshi hayawezi kuamrisha maamuzi ya kitabibu.

Rais huwa anataka kufanya mambo mengi kwa utashi wake (kutembea kwa uhuru, kuchanganyika na watu etc), lakini mengine anakatazwa kutokana na itifaki.
 
Sababu zipi boss, kama hamuwezi kuzisema acheni tuseme tunavyoona sisi. Hata hivyo ni kipi kulikuwa hakifahamiki Hadi huyo makamu wa rais afichwe? Hicho kifo si Hadi huku Mirandaoni watu walikuwa wanambiana? Kenya hapo si Kuna kituo Cha habari kilisema kabisa jamaa hayupo?
Unayo yaona yepi ? kwan na wewe ulikuwepo pale mzena kumuuguza marehemu magufuli? Maana usije ukawa unatupigia kelele hapa wakati na wewe unastory za vijiweni, maana aliye kuwa makamu wa rais ambaye ndiye rais wa sasa wala haja lalamika, mnao lalamika nyie huku wafia keyboard.
 
Back
Top Bottom