Inawezekana tuna watu wasio na uwezo katika nafasi wanazozitumikia?

Inawezekana tuna watu wasio na uwezo katika nafasi wanazozitumikia?

Kijanaa Mkuu wa Majeshi alipaswa kudictate Wakuu wa Mzena wamtoe akafie nyumbani,sasa Daktari angeanza vipi kuwaambia wakubwa wa Mzena.
Mtu anatibiwa alafu cdf aseme arudishwe nyumbani ili mumwangushie jumba bovu ripoti kama hiyo inatakiwa aitoe dr.
 
Mahojiano aliyofanya CDF Mstaafu Venance Mabeyo yamenifundisha kitu.

Nchi hii tuna shida kubwa sana ya watu kuwa kwenye nafasi za juu za maamuzi na uongozi ambao hawastahili kuwepo kwenye nafasi hizo kwa kukosa uwezo.

Hivi inakuwaje kwenye nchi tena yenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru watu kwenye nafasi za juu kabisa za maamuzi hawajui kuwa kwenye chain of Command baada ya Rais ni Makamu wa Rais?

Hivi inakuwaje Rais anafariki wa kwanza kutarifiwa ni Mkuu wa Majeshi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje na Mkuu wa Majeshi anaingia Kuanza kusema nimfaarifu Waziri Mkuu au Katibu Mkuu Kiongozi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje tuna viongozi kwenye nafasi za juu kabisa ambao hawajui hata Katiba ya Nchi inasemaje?

How comes wanaotuongoza hawaijui Katiba?

Kituko zaidi ni mtu aliyefika hadi kuwa Rais wa Nchi anaamuru Mkuu wa Majeshi aamuru atolewe hospitali na kupelekwa kijijini kwake?

Hivi alikuwaje Rais na hajui hata mipaka ya madaraka na uongozi?

Kusema kweli tuna tatizo kubwa kwenye hii nchi na hii ni kansa ambayo kusema kweli itatutafuna na kutumaliza kabisa.
Na tunao watu wanaodhani kujua kila kitu kama wewe msakatonge wa Chadema!

Afya ya mtu ni suala binafsi na inapofikia hatua ya umauti mfa mtarajiwa hubakia yeye nafsi yake pamoja na Mungu wake na sio katiba hizi siasa za kipumbavu za kibongo kupitia kwenye simu zinaongeza ujinga zaidi bila kutumia maarifa wala hekima.
 
Mahojiano aliyofanya CDF Mstaafu Venance Mabeyo yamenifundisha kitu.

Nchi hii tuna shida kubwa sana ya watu kuwa kwenye nafasi za juu za maamuzi na uongozi ambao hawastahili kuwepo kwenye nafasi hizo kwa kukosa uwezo.

Hivi inakuwaje kwenye nchi tena yenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru watu kwenye nafasi za juu kabisa za maamuzi hawajui kuwa kwenye chain of Command baada ya Rais ni Makamu wa Rais?

Hivi inakuwaje Rais anafariki wa kwanza kutarifiwa ni Mkuu wa Majeshi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje na Mkuu wa Majeshi anaingia Kuanza kusema nimfaarifu Waziri Mkuu au Katibu Mkuu Kiongozi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje tuna viongozi kwenye nafasi za juu kabisa ambao hawajui hata Katiba ya Nchi inasemaje?

How comes wanaotuongoza hawaijui Katiba?

Kituko zaidi ni mtu aliyefika hadi kuwa Rais wa Nchi anaamuru Mkuu wa Majeshi aamuru atolewe hospitali na kupelekwa kijijini kwake?

Hivi alikuwaje Rais na hajui hata mipaka ya madaraka na uongozi?

Kusema kweli tuna tatizo kubwa kwenye hii nchi na hii ni kansa ambayo kusema kweli itatutafuna na kutumaliza kabisa.
Yote hiyo ni ina describe namna Magufuli alivyokuwa ana operate nje ya mfumo rasmi.

Makamu wa Rais Samia alikuwa kama picha tu, au boya. Watu ambao Magufuli alikuwa anawashirikisha mambo nyeti ya nchi ni akina Bashiru Ally, Makonda, Dotto James etc.

Kwa hiyo hata akina Mabeyo, Diwani na IGP hawakuona sababu ya kumjulisha Samia
 
Hapana..!!

Bila shaka, wewe ndiye hujui lakini hujui kuwa hujui!

Kikatiba, wakati wowote Rais anapokuwa hayupo au anaumwa au amekufa au kwa sababu zinazotajwa na katiba, basi Vice President automatic ndiye huchukua nafasi ya Rais. Na kwa hiyo anabeba nguvu na mamlaka (power & authority) ya position ya Rais...

CDF, IGP na DGIS ni washauri wa Rais ktk mambo ya ulinzi na usalama wa ndani ya nchi na mipaka yake. Hapo walikusanyana watatu wote kumshauri mgonjwa mahututi na baadaye maiti, au?

Je, hawakupaswa kutenda wajibu wao huo kwa VP ambaye ndiye anayetambuliwa na katiba kwa kuwa Rais alikuwa mahututi na baadaye kuwa amefariki dunia?

Ndiyo maana kwa sababu ya kifo, katiba inataka haraka sana VP apishwe na kuwa Rais ili kuvaa mamlaka ya u - Rais kwa ukamilifu wake..

Na kingine unachopaswa kukumbuka ni kuwa, nchi hii tangu mwaka 1961 imekuwa chini ya uongozi wa kiraia kwa mujibu wa katiba.

Hakuna mahali popote ndani ya katiba Jeshi limepewa mandate ya kuingilia na kuchukua mamlaka halali ya uongozi wa kiraia wa nchi uliowekwa kihalali kwa mujibu wa katiba.

In very rare cases mapinduzi ya kijeshi (Jeshi kupindua uongozi wa kiraia) ktk nchi yanaweza kutokea. Lakini , by then there was no thing like that..

Majukumu na mamlaka ya CDF yako very clearly stated kikatiba. Lord denning yuko sahihi. Kuna kitu kinafichwa hapa. Kwanini VP alitolewa kwenye chain of command ya mamlaka ya uongozi wa kiraia wa nchi?

Kwanini CDF, IGP na DGIS ndiyo walikuwa wamemzunguka Rais tangu kuumwa hadi kufa kwake huku wakitambua kuwa nchi hii iko chini ya mfumo na utaratibu wa uongozi wa kiraia na sio wa kijeshi?

Walikuwa wanapanga nini? Kwanini finally, dakika za mwisho ndo wanaona ingalau tuwashirikishe Karibu Mkuu kiongozi na Waziri Mkuu huku wakimwacha VP ambaye kikatiba ndiye aliyepaswa kujua jambo hili kila hatua?

Mimi naweza kusema, kwamba, kwa jambo hili, obviously kuna possibilities tatu;

Aidha

1. CDF alikuwa na maelekezo maalumu toka kwa hayati Rais Magufuli mwenyewe kuwa alipoona kuwa uwezekano wa kupona haupo. Ni wazi kuwa CDF aliambiwa maneno haya "....hawa watu wameshaniua. Sitapona. Tafadhali, bwana CDF nikifa hii nchi jeshi ndilo liongoze.."

Au;

2. CDF, IGP na DGIS wao wenyewe kwa mapatano wali - conspire kutaka kupindua uongozi wa kiraia wa nchi hii na kutumia kifo cha Rais Magufuli kusimika uongozi wa kijeshi na wao wenyewe walikuwa pale wakipanga nani atakuwa nani..

Na au;

3. Kulikuwa na kundi la viongozi wengine wa kiraia kwa kulishawishi Jeshi, walitaka kuleta mapinduzi kuzuia taratibu zilizowekwa na katiba kufuatwa ikiwemo VP kuapishwa na kuwa Rais..
Uchambuzi mzuri sana Mimi naziona possibilities zote tatu kuwa Vichwani mwa hao matop walikuwa wanamzunguka Rais kwenye Wakati wake wa mwisho, Inashangaza Sana Serikali ya Kiraia ambapo VP ni second in command anaachwa Kuwa informed mapema mpaka mzee anakufa akiwa Mikononi mwa makamanda, VP ilipaswa awa Part and parcel of the Plan
I smell something fishy
 
Yote hiyo ni ina describe namna Magufuli alivyokuwa ana operate nje ya mfumo rasmi.

Makamu wa Rais Samia alikuwa kama picha tu, au boya. Watu ambao Magufuli alikuwa anawashirikisha mambo nyeti ya nchi ni akina Bashiru Ally, Makonda, Dotto James etc.

Kwa hiyo hata akina Mabeyo, Diwani na IGP hawakuona sababu ya kumjulisha Samia
Huu ndiyo ukweli
 
Lakini mi navoona Vp kwa bongo ni cheo ila kipo kipo tu hakina nguvu, hata kipindi cha magu kwenye kutumbua kama sio Magu basi ni majaliwa basi hatujawahi kumsikia hangaya akimtumbua hata mjumbe wa nyumba 10.
 
Hivi inakuwaje kwenye nchi tena yenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru watu kwenye nafasi za juu kabisa za maamuzi hawajui kuwa kwenye chain of Command baada ya Rais ni Makamu wa Rais?

Hivi inakuwaje Rais anafariki wa kwanza kutarifiwa ni Mkuu wa Majeshi na sio Makamu wa Rais?
Hii ni laana na ndio maana hatuwezi kutoka hapa tulipo kwa viongozi wa aina hii!
 
Story za vijiweni sio ndio zilisema Magufuli kafariki siku tano Kabla ya serekali kutangaza, unaachaje kuamini taarifa za vijiweni zenye ukweli wa hivyo?
Wewe kama unaamini story za vijiwen basi kuna shida maana hao hao wa vijiwen walisha sema mzee amekufa na akawaumbua kwa kuibukia ikulu, haya maneno ya vijiweni yanaweza kukua hata wewe ungali hai
 
Wewe kama unaamini story za vijiwen basi kuna shida maana hao hao wa vijiwen walisha sema mzee amekufa na akawaumbua kwa kuibukia ikulu, haya maneno ya vijiweni yanaweza kukua hata wewe ungali hai
Hata waziri mkuu alisema rais ni mzima na anachapa kazi, kuna tofauti gani na hizo story za vijiweni? Ww ndio uendelee kuamini hizo taarifa za serekali ambazo nyingi ni za kupika.
 
Usipate mkanganyiko mkuu. Aliyekua na mamlaka ya mwisho kwakipindi hicho labda hakutaka msaidizi wake ashirikishwe kwa ukaribu
 
Nilikuwa nakujibu suala la kwamba Magufuli alikuwa na haki ya kutaka kufia kwake.

Hilo halina mjadala.

Kuhusu kumwambia CDF, katika mawazo yake aliona kawaambia madaktari hawajakubali sasa amwambie CDF aamrishe kijeshi.

Magufuli alikuwa mtu wa amri. Inawezekana alikosea kumwambia CDF, lakini ikiwa aliwaambia madaktari wakamkatalia huku wakijua huyu anafariki, ama walijua hiyo safari hataimaliza ndiyo maana wakamkatalia.

Au pengine alikuwa na Covid wakaona kumpeleka nyumbani itakuwa vigumu kuepusha maambukizi kwa ndugu.

Vinginevyo, wamemkatalia haki yake ya kufia nyumbani na dignity.
Logic ni moja tu kwamba Rais anakuwemo ndani ya itifaki ambayo inaangalia na kuzingatia kila kitu kiende kwa usalama na amani na ulinzi wa hali ya juu !
Hivyo basi akiwa mzima au akiwa mgonjwa Hiyo itifaki inaendelea kuwa applied, na kwamba sio kila kitu atakachotaka kufanya atakubaliwa kwa sababu kitu kinachoangaliwa zaidi ni Usalama wake kwanza !!

Mkuu wa Nchi ana umuhimu katika usalama wa Nchi kuliko tunavyoweza kufikiria,
Ndio maana ulinzi wao huwa ni wa hali ya juu sana katika Nchi yeyote humu Duniani !
Na yapo maneno mengine huwa hayaelezwi hadharani ndio maana utaona watu wanajiuliza maswali mengi kwamba mbona kasema hivi na kwanini haikuwa hivi !
Sio kila kitu huwa kinawekwa hadharani !
Vingine ni Confidential !!
 
Lakini mi navoona Vp kwa bongo ni cheo ila kipo kipo tu hakina nguvu, hata kipindi cha magu kwenye kutumbua kama sio Magu basi ni majaliwa basi hatujawahi kumsikia hangaya akimtumbua hata mjumbe wa nyumba 10.
Kutumbua ndiyo nini? Ni ujinga tu alioanzisha Magufuli kisha wananchi wajinga wakawa wanaitikia kama chorus.

Kwa mfano alimtumbua Wilson Kabwe akiwa anazindua daraja la Nyerere pale Kigamboni. Kisha Wilson Kabwe akafariki baada ya siku chache. Je wewe Raia mpya ulipata nini kwa kitendo hicho
 
Logic ni moja tu kwamba Rais anakuwemo ndani ya itifaki ambayo inaangalia na kuzingatia kila kitu kiende kwa usalama na amani na ulinzi wa hali ya juu !
Hivyo basi akiwa mzima au akiwa mgonjwa Hiyo itifaki inaendelea kuwa applied, na kwamba sio kila kitu atakachotaka kufanya atakubaliwa kwa sababu kitu kinachoangaliwa zaidi ni Usalama wake kwanza !!

Mkuu wa Nchi ana umuhimu katika usalama wa Nchi kuliko tunavyoweza kufikiria,
Ndio maana ulinzi wao huwa ni wa hali ya juu sana katika Nchi yeyote humu Duniani !
Na yapo maneno mengine huwa hayaelezwi hadharani ndio maana utaona watu wanajiuliza maswali mengi kwamba mbona kasema hivi na kwanini haikuwa hivi !
Sio kila kitu huwa kinawekwa hadharani !
Vingine ni Confidential !!
Sasa mtu anakufa, madaktari washaona huyu hatoboi anakufa, unamfanyia itifaki ya usalama wa hali ya juu asiende kufa nyumbani kwake, akibaki hospitali ndiyo utazuia asife?

Itifaki haifanywi kwa sababu ya itifaki tu, inafanywa kwa rationale.

Ukiondoa hizo sababu possible nilizozitaja, rationale ya kumzuia rais anayetaka kwenda kufia nyumbani kwake asiende kufia nyumbani kwake ni ipi?
 
Mahojiano aliyofanya CDF Mstaafu Venance Mabeyo yamenifundisha kitu.

Nchi hii tuna shida kubwa sana ya watu kuwa kwenye nafasi za juu za maamuzi na uongozi ambao hawastahili kuwepo kwenye nafasi hizo kwa kukosa uwezo.

Hivi inakuwaje kwenye nchi tena yenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru watu kwenye nafasi za juu kabisa za maamuzi hawajui kuwa kwenye chain of Command baada ya Rais ni Makamu wa Rais?

Hivi inakuwaje Rais anafariki wa kwanza kutarifiwa ni Mkuu wa Majeshi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje na Mkuu wa Majeshi anaingia Kuanza kusema nimfaarifu Waziri Mkuu au Katibu Mkuu Kiongozi na sio Makamu wa Rais?

Inakuwaje tuna viongozi kwenye nafasi za juu kabisa ambao hawajui hata Katiba ya Nchi inasemaje?

How comes wanaotuongoza hawaijui Katiba?

Kituko zaidi ni mtu aliyefika hadi kuwa Rais wa Nchi anaamuru Mkuu wa Majeshi aamuru atolewe hospitali na kupelekwa kijijini kwake?

Hivi alikuwaje Rais na hajui hata mipaka ya madaraka na uongozi?

Kusema kweli tuna tatizo kubwa kwenye hii nchi na hii ni kansa ambayo kusema kweli itatutafuna na kutumaliza kabisa.
Tulia. 2025 kabla ya uchaguzi ndo utausikia ukweli wenyewe; Mabeyo anawaandaa tu Kisaikolojia. Mtakayoyasikia mtalazimika kumpumzisha mtu. Tulia
 
Kwa mujibu wa CDF Mabeyo Makamu wa Rais alirukwa kabisa kwenye updates za kutoka hospitalini, habari alikuwa anapewa Waziri Mkuu Majaliwa. Licha ya kwamba Makamu wa Rais ndiye mrithi wa Rais, ikiwa Rais atafariki, kikatiba.
Mkuu Kiranga Mabeyo hajazungumza kuhusu swala la Waziri mkuu kuwa anapewa updates ya Hali ya afya ya Magufuli, Ila ameelezea baada ya Magufuli Kufariki ni Majaliwa na Bashiru Alli ndio walikuwa wakwanza kabisa kutaalifiwa kwamba Magufuli katutoka kabla ya Rais Samia.
 
Back
Top Bottom