Inawezekana vipi mtu kuweka roho yake kwenye mti?

Inawezekana vipi mtu kuweka roho yake kwenye mti?

Haya ni mazindiko ya kiafrika, roho haikai kwenye mti ila anafanya zindiko anaungana na ule mti ukitaka kumuua ni mpaka ule mti ufe kwanza. Hizi zilitumika kama kinga enzi zile watu wanatekwa maporini safari za miguu hamna magari. Zipo nyingi ambazo nimewahi kuziona in action ni kama;
1. Dawa ya mbio- hii kulikuwa na jambazi sugu wanamtafuta kila wakija akitoka mbio hata mbwa hawafati hiyo speed ya jamaa.

2. Kukosekana kwenye hatari- hii mtu akija akudhuru anakuwa hakuoni, walihangaika na huyo mtu mpaka wakaamua kuua mwanae kwa hasira baada ya kumkosa muhusika kila wakati.

3. Dawa ya kurusha ngumi- hii ukimpiga mtu ngumi anazikwa, inafanya kazi pale tu unapokuwa unaonewa lakini ukianzisha ukorofi utapigwa kama ngoma.

4. Dawa ya kurusha jiwe au fimbo - hii kama mtu kakukimbia na huwezi mpata basi ukichukua kitu chochote ukarushia uelekeo wake humkosi, hata awe mbali wa viwanja 3 vya mpira.

Na zingine kibao kwa nyie watoto wa miaka ya 90 na 2000 hamuwezi elewa.
Kweli ulimwengu ni mpana kuliko tunavyoufahamu.
 
Hakuna ajabu yoyote ila ni elimu, hio haina tofauti na uhai uliofichwa kwenye sindano na vidonge kwani usipochomwa au kumeza unakufa na ukitumia unapona.
Hivyo kuna tofauti gani na aliyelinda uhai wake kutumia mti?

Nikupe mfano mwingine,
Huyo mzee hata ingetokea ajali asingekufa kirahisi, Je ipi teknolojia bora kati ya hiyo ya kujikikinga na miti au vitu na teknolojia ya Airbag ambayo inapunguza risk wakati wa ajali?
Hawa hawapati ajali ni nidra sana kabla hajaanza safari machale yanamcheza unashangaa tu mtu gafla anahairisha safari
 
Hii niliona kwa bibi mmoja x alikua anaoza pale ndani tunamuona.
Alikufa badae sana.
Kila kiumbe hai lazima tu kitaonja mauti, sasa mbwembwe zote hizo za nini kama si kuchelewesha tu kesi Mahakamani ilihali hukumu lazima ihusike?
 
katika maisha yangu sitaki kabisa mambo ya imani, licha ya kuwa nina elimu kubwa kutoka kwa wazee na pia nimeshuhudia mambo manne makubwa ambayo science ninayoiamini bado haijanipa jibu.....wasikilizeni waliowapigia simu....
Tupe mawili mkuu NACKO tujifunze kitu
 
Nilishashuhudia huu utopolo. Mtu katafunwa na kansa ya jicho, jicho lote limeng'oka limebaki shimo tu ukiangalia hata ubongo unaweza kuuona halafu shimo liko infected limeoza lakini jamaa hafi. Mpaka madaktari wanashangaa kwa sababu hali aliyokuwa nayo ni ile wanaita medical impossibility!

Mpaka akaja mdogo wake akawatonya kuwa watoboe paa hapo alipolala ili apigwe na mwanga wa jua hasa jua la saa 6 mchana. Kweli wakafanya hivyo na japo alikuwa kwenye coma jamaa alijitikisa; na hata siku moja hakumaliza akafariki. Bila kufanya hivyo sijui ingekuwaje.

Mwafrika bado ana hizi hekaheka. Imagine mtu unajifanyia madawa ili usife hata uugue vipi. Na Mungu naye kwa vile si Athumani ndiyo unatandikwa na kansa. Unaishia kujitesa si wewe tu bali na wapendwa wako. Mambo mengine hayafai![emoji706]
Yale yale ya Michael Jackson ya kujitafutia madaktari zaidi ya 15 kwa majivuno tele kuwa anataka kuishi miaka 150, hatimaye aliyemuumba akampumzisha akiwa na miaka 50 tu.

Uhai mrefu ni kwa rehema na neema za Mungu tu mbali na hapo ni sawa na kujilisha upepo tu.
 
Masharti yake ni madogomadogo kwa kipindi cha wiki moja tangu kuzindikwa.
Kila koo ina mizimu ya kukuongoza na masharti yake

Kwenye familia yetu sijajua maana huenda kuna mtu anaenda kisirisiri, ila kwenye ukoo wetu, wapo wengi sana, Sisi Wafipa, utatuambia nini kwenye haya masuala?
Sema koo zetu zimesambaa wengine wako Kaliua Tabora, kuna walioko Milala, Sumbawanga mjini, Tanganyika huko, Kigamboni na Mpimbwe.
Japo nina wajomba zangu wako kijijini Chipu....unapajua?, uliza kwa watu.
Mie hata sasa nikitaka kuwa mchawi inawezekana, uchawi wetu uko malangoni.
Hapa kwa Wafipa nazungumzia upande wa mama
Baba ni kule Tanga...
Heshima yako mkuu kama chipu ni kwa wajomba zako
 
Ukiambiwa hadharani wewe ni mbaya unabatilisha hadarani kwa kuonyesha uzuri wako siyo unajificha na kunong'oneza watu kwa usiri mkubwa kuhusu uzuri wako.
Hao unaowahusudu walikwambia kwanini walijenga daraja la mto Rumi Mara ulioua Watu wengi sana kabla ya kujengwa daraja na hawakutaka kuhusisha Mwafrika yeyote?

Kwanini hawakufundishi hadharani hata teknolojia tu ya kutengeneza teeth sticks mbali na simu, magari, vinu na mabomu ya nyukilia?
 
Hiyo ni kwa mujibu wa nani?

Kwa haraka haraka kupitia majibu yako, one would say the “Master has successfully conquered your mindset and thoroughly washed your brain.

Logic ya watu kufanya haya mambo Siri iko wazi, huwezi kuzungukwa na maadui wanaowinda ulichonacho na wewe ukaanza kukinadi hadharani, labda husiwe na akili.

Lakini pia naelewa kwanini wengi wenye utaalamu huu wa science ya Afrika wamegeukia kuutumia katika kuumizana, imagine mtu Kama wewe unavyorefusha huo mdomo kwa ubishi halafu Mimi niwe na utaalamu wa kukugeuza mdomo uwe makalioni na makalio yawe usoni, unadhani nitakuacha?

The worst enemy in this life, is your own kind.
Hawajui weupe vizuri huyo, Watu wana tiba za asili za kisukari, kansa, UKIMWI n.k lakini huogopa kujitanabaisha sababu wema wao ndiyo utaharibu dili za wenyewe wafanyao biashara kupitia miili ya Watu kuumwa (magonjwa) kwa kuwauzia dawa n k kama ilivyo Malaria haipo kwao ila Africa ni dili kwa uuzwaji wa neti na dawa.
 
Hii tafsiri inaishia anga la Afrika tu si ndio?

Maana kule kwa wenzetu Mila zao zinaitwa Dini, marehemu wao (mizimu kwetu) wanaitwa watakatifu.

Na huu ujuzi wa kwamba mila na tamaduni hizi ni kuingia mikataba na shetani umeupatia wapi?
Soma Biblia uielewe ndugu.Imani ya umizimu,ibada ya wafu n.k.ni desturi za kipagani za kirumi [rumi ya kipagani]zilizoingizwa kwy dini [ukristo]kipindi cha utawala wa mwanzo wa upapa sambamba na mengine kadhaa na kufanywa kuwa sehemu ya ibada .
 
Hao unaowahusudu walikwambia kwanini walijenga daraja la mto Rumi Mara uliloua Watu wengi sana kabla ya kujengwa daraja na hawakutaka kuhusisha Mwafrika yeyote?

Kwanini hawakufundishi hadharani hata teknolojia tu ya kutengeneza teeth sticks mbali na simu, magari, vinu na mabomu ya nyukilia?
Unaowajua ninao wahusudu? Assumptions.
 
Wakati nasoma chuo kulikuwa na mkaka kwao sumbawanga aliwahi kunisimulia story inafanana na hii alisema huyo mtu had aliwaambia mwenyew wafukue mlangoni wakakuta nguozake zimezikwa walivozitoa ndio akafa
Mmhhh. Kweli tuliyoyaona ni asilimia ndogo sana....hatujaona mengi sana
 
Back
Top Bottom