Iran: Milipuko ilisikika mjini Tehran huku Israel ikithibitisha mashambulizi

Iran: Milipuko ilisikika mjini Tehran huku Israel ikithibitisha mashambulizi

Hatari sana
Ngoja panoge kwanza naona sisi tushachagua upande kwa hio Iran wakihitaji msaada wale wanaokula bure na kuenjoy mishahara minono bila kufanya kazi inabidi waende huko wakaongeze idadi ya wakata roho
 
Mhhhm!! Cnn na bbc huwa siwaamini, yani kuna wabongo bado tu wanafatiliaga hizi media 😂😂
 
IRAN IMESHAMBULIWA KWA UZITO

Toka asubuhi na mapema nimekuwa nikifuatilia kwa makini na utaratibu ili nije kuwapa taarifa za kina na zenye uthibisho. Masaa manne yaliyopita, Israeli imefanya mashambulizi makubwa ndani ya ardhi ya Iran, Siria na Iraq na wakati huo huo ikifanya mashambulizi ya anga ndani ya Lebanon na Gasa. Vituo vya kijeshi vya mamluki wa Iran ndani ya Siria na Iraq vimeshambuliwa. Na ndani ya Iran Israeli imeshambulia maeneo 20 katika mijimbo matatu.

Ndani ya Iran

Asubuhi na mapema ndani ya Tehran na majimbo mengine vilisikika vishindo vizito vya makombora. Serikali ya Iran ilikuwa kimya na haikuruhusu vyombo vyake vya habari virushe matukio ya mashambulizi pamoja na hilo ilifunga anga lake. Lakini taarifa za vyombo binafsi (wale wabishi) ndani ya Iran vimeripoti matukio ambayo yameilazimisha serikali ya Iran kukiri kwamba kuna uharibifu mkubwa umefanyika katika miji yake mitatu katika maeneo maalum ya kijeshi. Mamlaka ya Iran, imetangaza bayana kwamba nayo itayajibu mashambulizi ya Israeli.

Israeli baada ya shambulio la Iran la october 1 ambalo liligusa vituo vitatu vya kijeshi vya Israel na sehemu kadhaa za makazi ya raia, nayo ilipanga kujibu shambulio hilo na imejibu baada ya siku 25. Huku Iran ilitumia miezi miwili kujibu kwa kulipiza kisasi cha mauaji ya kiongozi wa Hamas, Ismail Haniyeh aliyeuawa 31 July pamoja na maofisa wengine wa Hezbollah na Iran waliouawa baada ya hapo. Hii inaonesha dhahiri kuwa intelijensia ya Israeli ni kubwa zaidi.

Mpango wa Israeli

Kabla ya shambulio la leo, balozi wa Israeli kwa UN, alitoa taarifa kwa UN iliyoikataza Israeli isijibu, alijibu kwa kusema Israeli lazima ijibu ili kuonesha dunia uwezo wake. Na waziri mkuu wa Israeli hapo nyuma alikuwa ametangulia kusema kuwa atajibu shambulio la Iran kwajili ya maslahi ya Israeli. UN na nchi kadha wa kadha zilionya kwamba aache ili kuepusha machafuko ya kikanda. Israeli ilikataa na Marekani wao wakaiunga mkono. Lakini Marekani haikuunga mkono mpango wa Netanyahu wa kuharibu vinu vya nyuklia na visima vya mafuta vya Iran kwa kile ambacho kwamba sumu ya nyuklia ingeleta sio tu uharibifu kwa raia wa Iran bali na kwa majirani zake na kwamba kama visima vya mafuta vingelipuliwa ingeleta shida ya upungufu wa mafuta duniani. Inasemekana Marekani ilivujisha mpango huu wa Israeli wa kushambulia sehemu hizo. Iran nayo ika respond kwamba kama Israeli inataka kuishambulia Iran basi nayo ijibu kwa kupiga vituo vya kijeshi kama walivyofanya wao. Wachambuzi wengine wanadai mpango huo kuvuja ulikuwa ni mpango wa kijasusi wa kuizubaisha Iran.

Hofu ya siku 24 ndani ya Iran

Ndani ya siku 24 kabla ya mashambulizi ya leo, wananchi wa Iran walikuwa wamejawa na hofu kuu. Hawakujua nini kitawakuta, wengi wao waliukimbia mji wa Tehran ili kujiepusha na mashambulizi ya Israeli. Serikali ya kislamu ya Iran, iliwatoa hofu wananchi wake kwamba wamejiandaa kuzuia mashambulizi ya Israeli.

Kujipanga kwa Iran dhidi ya mashambulizi ya Israeli

Urusi ambaye ni mshirika wa Iran, aliipa Iran betri za S 400 ili kuongeza nguvu kwa S 300 ambazo zipo Iran ambazo pia ni za Urusi. Hivyo betri za Iran na zile za Urusi zilifungwa katika mji wa Tehran na sehemu maalum za kijeshi na miundo mbinu muhimu.

Mashambulizi ya Israeli

Israeli kuanzia saa 10 usiku, ilituma ndege zake za F35 pamoja na makombora kadha wa kadha kwenda Iran. Mifumo ya anga ya Iran ikiwemo S 400 ilishindwa kuziona ndege hizo ambazo zilishambulia sehemu muhimu na kutoka. Pia makombora nayo yakalenga kwenye malengo yaliyopangwa na kuleteleza uharibifu katika maeneo makuu matatu ya kijeshi na sehemu zingine 20 ambazo nazo zoliguswa na makombora na mabomu ya ndege.

Hapa kuna sasisho (update) za hivi punde kutoka Aljazeera:

Jeshi la Israel limefanya mashambulizi dhidi ya Iran na kushambulia maeneo 20 kwa saa kadhaa kujibu shambulio la kombora la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran tarehe 1 Oktoba.

Msemaji wa jeshi la Israel alisema shambulio hilo ambalo sasa limekamilika, ambalo alilitaja kama operesheni ya "Days of Reckoning of" yaani Siku za hesabu", lilishambulia "zana za kutengeneza makombora" ya Iran, pamoja na mifumo ya makombora ya kutoka ardhini hadi angani na uwezo mwingine wa ulinzi wa anga.

Jeshi la Iran limethibitisha kuwa mashambulizi hayo ya Israel yalilenga vituo vya kijeshi katika majimbo ya Ilam, Khuzestan na Tehran, na kusema yalisababisha "uharibifu mdogo".

Israel imeionya Iran dhidi ya kulipiza kisasi, ikisema "italazimika kujibu" tena, na kuongeza kuwa ina "malengo ya ziada" ambayo inaweza kushambulia ikiwa hilo litatokea.

Msemaji wa Baraza la Usalama la Taifa la Marekani alisema Washington inafahamu kuhusu mashambulizi ya mshirika wake, lakini haikushiriki, akielezea operesheni hiyo kama "zoezi la kujilinda".

Baada ya mashambulizi ya Israeli

Msemaji wa jeshi la Israel Daniel Hagari amethibitisha kuwa mashambulio ya kulipiza kisasi ya Israel dhidi ya Iran yamekamilika.

"Tulifanya mashambulizi yaliyolengwa na sahihi dhidi ya malengo ya kijeshi nchini Iran - na kuzuia vitisho vya mara moja kwa Taifa la Israeli," alisema.
hagari aliionya serikali ya Iran kwamba Israel iko tayari kulenga shabaha zaidi nchini humo ikihitajika.

"Tutajua jinsi ya kuchagua shabaha za ziada ... na kuzipiga ikihitajika. Huu ni ujumbe ulio wazi, yeyote atakayeitishia Israel atalipa gharama kubwa,” alisema.

Karibu kwa maoni

Na Jeff Massawe
0757722557
 
2024-10-01t212137z-1176242950-rc2rbaank5sr-rtrmadp-3-israel-palestinians-lebanon-iran.jpg

Hii picha ni mashabulizi ya Iran Oct 1 nchini Israel, wananchi wamejificha kwenye mahandaki wanaona kama mwisho wa dunia umefika...

Ustadh umeona video lakini? Mumepigwa bila uwezo wa kuzuia hata kombora moja, yaani huwa mko hovyo sana, sasa huyo Iran ndiye alikua tegemezi wenu duniani na imedhirishwa anapigika tu ikihitajika apigwe.
 
Kabisa sisi tumejiweka waziwazi tunashirikiana na Iran 🇮🇷
Naam kwa hio wakihitaji backup tushasaini MoU ya kimkakati watahitaji tu wa kwenda kuongezea idadi ya vifo kwa hio jamaa zangu kule waanze mazoezi ya kulenga shabaha na kukwepa mabomu mazito mazito soon wataambiwa waende wakaongezee nguvu
 
israel anajitahidi kutumia busara kwa mpumbavu.
 
Sasa hapo ni Israel au ni USA chini ya Israel? Mpaka Blinken aende kutoa kibali na katoka huko jana
kwan Iran hata yeye si anafanya chini ya Urusi? yeye kama yeye ana jeuri hata ya kurusha jiwe kwa manati?
 
Kama nikweli amelipiza, unafikiri israel bila marekani na nato ataweza!

Juzi ama jana wanajeshi 70 wameuawa na hezbullah, kwa iran ataweza! Mnachekesha sana

Wewe unafikiria ni kazi rahisi kuingia kwenye gheto za hao magaidi wa hiyo dini, hapo hata Israel wamejaribu sana.
 
Back
Top Bottom