Iran ni nchi ya maajabu sana

Iran ni nchi ya maajabu sana

Kumbe Israel wanapewa fedha za kujilinda na America?😎 Kweli wachovu
Mkuu si umeona jinsi Marekani imeahidi kuwasaidia tena mamilioni ya dola waisrael na pia kutuma meli na ndege za kivita, baada ya waziri mkuu Benjamin Netanyahu kuwaomba ili waweze kufanikisha vita vyao na Hamas.

Sasa kama Hamas tu kikundi kidogo kisichokuwa hata na askari elf 40, tena watumia silaha za kienyeji inawafanya waombe msaada mungine zaidi kutoka Marekani, je nchi hiyo inaweza kuwa na nguvu au ubavu wa kupambana na nchi yenye historia ya kupambana vita zaidi ya miaka elf 2 iliyopita na haijawahi kumsujudia Mmarekani au nchi yoyote ile?
 
Umetudanganya sana Kaka.
Wanaoipa msaada Israel ni USA.
Ule mzozo wa mwisho ambao Israel ililupua kambi ya wakimbizi Palestine USA senates waliweka kikao na kusema Israel inyimwe ufadhili wa silaha km ikilipua shule ya UN.
SISI TUNAJIELEWA BRO USITUFANYE WATOTO WADOGO,KILA MWAKA SENATE YA USA HUKAA NA KUPITISHA BAJETI YA UFADHILI WA PESA NA SILAHA KWA ISRAEL .
Israel sasa inalipua chochote kilichopo Gaza. Haijalishi iwe shule, kambi au Hospital ya UN au mtu binafsi. Wamarekani na maseneta wao wote ni wanafiki wakubwa. Na hii ndio sababu ya Israel kufanya chochote bila kufanywa kitu na Marekani wala nchi yoyote yenye nguvu au ushawishi.
 
Huna unalolijua we
Ile Vita Israel alivamia kambi ya ndege za Misri na akaenda kuvamia Syria.
Hakupigana na mataifa sita km mnavyodanganywa.
Nakutajia vita alizoshindwa Israel.
1) October war 1974,alipokonywa Sinai na Egypt chini ya Anwar Sadat hasira akahamishia Syria na mkataba wa camp david ulisaniwa kuiokoa Syria.
2)Israel-Lebanese war 2006,tena hapa hizbollah waliingia mipaka ya Israel na kuua Askari nane na kuteka nyara watatu.
Na ikumbukwe Hizbollah ni tishio kwa Israel mpaka sasa na hizbollah inafadhiliwa kisilaha na fedha na Iran.
ISRAEL AKIONA TAIFA TISHIO ANAIVAMIA NA NDEGE KM AFANYAVYO GAZA Ila mbona hafanyi hivyo kwa Iran?
Katika migogoro inayotokea baina ya Israel na Gaza Hizbollah hurusha makombora kwenda Israel takriban 10-15 lakini mbona Israel haipeleki ndege Lebanon?
Acheni kupelekeshwa kifikra.
Hao vijana wengi wao wanaongelea ushabiki tu, lakin uhalisia hawaujui.

Israel leo inatolewa kamasi hata na kikundi kidogo kisichokuwa na askari hata elf 40 (hamas) tena chenye silaha za kienyeji kama rocket na mizinga ya kurusha.

Sasa huo ubavu wa kupambana na Iran watautoa wapi?
 
Wanaweza kutoboa kwasababu yuko jirani na nchi ambazo hazifungamani upande wowote na zile zinazopingana na magharibi, kama Urusi, Uturuki, China, Azerbaijan, Armenia etc
Hili ndilo jibu la yote. Kwa hiyo ni kama hajawekewa vikwazo vile. Huduma zote anazipata vizuri tu kwa hizo nchi
 
Hili ndilo jibu la yote. Kwa hiyo ni kama hajawekewa vikwazo vile. Huduma zote anazipata vizuri tu kwa hizo nchi
Israel ni sawa na katoto kadogo kanakojaribu kuchokoza watu wakubwa (Iran) ili kakiguswa kakimbilie kwa baba yake (Marekani) na wajomba zake (Umoja wa nchi za Ulaya) waje kumsaidia kupambana.

Bila udhamini wa Marekani na kuungwa mkono na Ulaya kiukweli Israel ingekuwa nchi nyepesi na ya hovyo sana kama walivyokuwa miaka ya nyuma kabla ya kushikwa mkono na wanaojifanya wababe wa Dunia.
 
Wakuu vipi, kwema.

Wakuu Iran ni mmoja kati ya nchi ambazo ziliwekewa vikwazo vikali na nchi za magharibi toka mnamo mwa miaka ya 70s huko hadi leo hii na siku zijazo.

Vikwazo hivyo ni vya kiuchumi, kijeshi nk, tena vimekuwa vikiongezwa siku hadi siku.

Tofauti na ilivyo kwa nchi nyingine kama vile Cuba, Venezuela nk zilizowekewa vikwazo pengine na marekan tu, au baadhi ya nchi za magharibi. vikwazo vya Iran vimewekwa na nchi za magharibi kama zote wakishirikiana na makampuni ya nchi hizo.

Lakini cha kushangaza Iran imeweza kuwa na uwezo hasa wa kijeshi sawa au pengine zaidi ya ule wa nchi ambazo hazijawahi kuwekewa vikwazo na nchi hizo.

Iran ni miongoni mwa nchi zenye eneo kubwa na watu wengi barani Asia, so pamoja na vikwazo vya kiuchumi walivyowekewa takriban miaka 50 na zaidi, lkn wameweza kuwa na mifumo mizuri ya kudhibiti hali ya umasikini nchini mwao, tofauti na nchi kama Venezuela ambazo vikwazo vya miaka miwili au mitatu vimesababisha mamilioni ya raia waishi maisha ya shida na ya umasikini kupita maelezo.

Pamoja na vikwazo vikali vya magharibi hasa kwa upande wa mambo ya ulinzi, lkn bado nchi hiyo imeweza kuonesha kuwa haipo chini au nyuma kijeshi hata siku moja. Wengi tuliona jinsi wa Iran walivyoziangamiza ndege zisizo na ruban zilizokuwa zinatumiwa na Marekan kupima upepo katika eneo lao, wengi tuliona jinsi Iran ilivyozilipua meli ambazo zilikuwa zinabeba wapelelezi mbali mbali wa magharibi karibu na eneo lake, wengi tuliona jinsi Iran ilivyoshambulia kambi kadhaa za Marekani kule Iraq na kusababisha maafa na uharibifu mkubwa katika kambi hizo baada ya Mmarekani kumuuwa mmoja wa maofisa wakubwa wa Iran kule Iraq, tena kabla ya kufanya mashambulizi hayo wa Iran walitoa taarifa mapema kuwa watalipiza kisasi kupitia kambi za wamarekan kule Iraq, so marekan ikajiandaa kuzuia shambulizi lkn mwisho wa siku shambulizi likashindikana kuzuilika na kuleta maafa kwa jeshi la nchi hiyo kubwa duniani.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyotoa msaada wa silaha kwa kundi la hezbullah ambalo liliichachafya Israel inayopata msaada mkubwa wa fedha kutoka Marekani kwa ajili ya ulinzi wao. Hiyo ilikuwa mwaka 2006 hadi jumuiya ya kimataifa ikaingilia kati na kuomba ipatekane suluhu ya kudumu baina ya Israeli na hezbullah.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyosimama na kumlinda Asad wa Syria katika vita vyake, hadi kupelekea mipango ya Marekani na nchi za magharibi kumng'oa imeshindikana.

Wengi tunashuhudia sasa jinsi silaha kidogo tu za ndege zisikuwa na rubani za Iran zinavyofanya uharibifu mkubwa, na kusababisha maafa makubwa na zaidi ya yale yaliokuwa yanafanywa na Russia kupitia silaha zake mwenyewe (Russia) huko Ukraine.
Mpaka Marekani na nchi zingine za magharibi zinapiga kelele, maana silaha zinazotumika sio zile za Russia ambazo zilikuwa zinampa jeuri raisi wa Ukraine kuona kwamba sasa vita vimekwisha.

Hata zile himars za Marekani sasa hivi zinaonekana hazifanyi kazi mbele ya maangamizi ya ndege hizi za Iran.

Sasa tujiulize, kama nchi iliyowekewa vikwazo na mataifa makubwa duniani kwa zaidi ya miaka 50 bado ina uwezo iliyo nao leo, sasa je kama isingewekewa vikwazo kwa miaka yote hiyo 50 leo ni nchi gani ambayo ingeitisha pale Asia na hata duniani kwa ujumla.

Hizo nilizosema hapa ni zile silaha ilizotoa kuwawezesha hao niliwataja washinde mapambano yao, hapo hatujazungumzia silaha zake mwenyewe alizoweka kwa lengo la kujilinda ambazo kwa sheria za kijeshi duniani huwa zinafanywa siri kubwa ili adui asizione.

Mpaka sasa Marekani na nchi za magharibi zinashindwa kujua ni njia gani nyingine ya kumdhibiti huyu mtemi, maana wamarekani waliwahi kumtumia msaudi mwaka jana, hapo hapo Iran hakuchelewesha akaangamiza mitungi yake mikubwa ya kuwekea mafuta mpaka saudia na dunia ikapiga kelele.

Hili taifa ni la maajabu sana, japo lina maadui wengi lililotengenezewa na nchi za magharibi na halipati msaada wa kifedha kutoka kwa nchi yoyote lkn bado linajiamini kupita maelezo.

Mti wenye matunda ndio hurushiwa mawe, namaanisha ukiona nchi za magharibi na vibaraka wao wanapambana kwa hali na mali dhidi ya uchumi na ulinzi wa kijeshi wa nchi moja, basi jua kwamba wamagharibi hao wameshagundua kwamba nchi hiyo ni hatari maradufu kwa mustakabali wa uchumi wao pamoja na ulinzi wao.
Siri ya iran kufanikiwa ni kujitambua wao na mahitaji yao. Wengine hata mkifunguliwa milango mkaingia kila kona bila viza mtabakia kuwa vilaza tu. Mnapokea misaada hadi ya pedi mna akili kweli?
 
Ya ile ilikuwa ni ambush, yan shambulizi la kushtukiza. Lkn Iran yenyewe ilitoa taarifa mapema kuwa itashambulia kambi za Marekani Iraq na kweli ilishambulia na kusababisha uharibifu

Imagine mtu anatoa taarifa kabisa kuwa anataka kushambulia kambi yenye vifaa bora ya Marekan na mwisho wa siku anashambulia na kufanikiwa kufanya uharibifu mkubwa.
ulitaka Marekan wahamishe kambi?
 
Siri ya iran kufanikiwa ni kujitambua wao na mahitaji yao. Wengine hata mkifunguliwa milango mkaingia kila kona bila viza mtabakia kuwa vilaza tu. Mnapokea misaada hadi ya pedi mna akili kweli?
Jamaa wako vizuri mno kichwani. Miaka zaidi ya 2000 iliyopita waliowahi kuwa na Empire ambayo ilidumu kwa muda mrefu.

Sasa leo hii kanatokea kanchi kenye miaka Mia tatu tu toka kaanzishwe, eti kanakuja kuwatishia nyau na kujaribu kuwapangia jinsi ya kuishi watu wazima wenye akili zao.
 
ulitaka Marekan wahamishe kambi?
Nazungumzia ujasiri na uwezo waliokuwa nao Iran kwa Marekani. Ingekuwa nchi nyingine zingeigwaya Marekani.

Sana sana zingeishia kulalamika tu na kuliacha jambo lipite bila wao kuchukua hatua yoyote. Hii tunaona hata kwa Iraq yenyewe, ingawa hawahitaji tena jeshi la Marekani kuendelea kuwa katika ardhi yao lakini hawana uwezo wa kuwatoa au kuwalazimisha waondoke.
 
Nazungumzia ujasiri na uwezo waliokuwa nao Iran kwa Marekani. Ingekuwa nchi nyingine zingeigwaya Marekani.

Sana sana zingeishia kulalamika tu na kuliacha jambo lipite bila wao kuchukua hatua yoyote. Hii tunaona hata kwa Iraq yenyewe, ingawa hawahitaji tena jeshi la Marekani kuendelea kuwa katika ardhi yao lakini hawana uwezo wa kuwatoa au kuwalazimisha waondoke.
Ila sidhanii kama Americant ataendelea kukaa iraq
Acha tuone ila Americant anaondoka Iraq ni suala la muda tuuu
 
Ila sidhanii kama Americant ataendelea kukaa iraq
Acha tuone ila Americant anaondoka Iraq ni suala la muda tuuu
Marekani kuondoka Iraq sio rahisi mkuu, ukizingatia pale kuna masilahi yao muhimu wanayapata kwa bure kupitia kile anachodai kupambana na magaidi.

Labda kama Iraq itataka kushirikiana kwa njia ya siri na Iran kupitia yale makundi ya wapiganaji yanayodhaminiwa na Iran. Yani Iraq iwe inatoa mchongo wa njia, silaha za kimya kimya (sio mpaka wasubiri zivuke kutoka Iran) washiriki kuwapa wapiganaji hao siri ya kile kinachoendelea katika kambi hizo.

Hapo kwa namna fulan wataweza kuwafanya Marekani wakimbie kama Afghanstan maana itakuwa ni mashambulizi ya usiku na mchana bila kupumzika.
 
Waende wakajaribu, wasiishie kuongea maneno ya kwenye kanga, unajua historia ya vita ya mwaka 1967 Isreal alivyowakalisha waarabu wakati huo Ariel Sharon akiwa general aliyeongoza vita.......fuatilia historia, Isreal wakishindwa vita ni kwa kuwa Mungu kawapa adhabu na si vinginevyo.​
Do akili hizi za walokole bana

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Wakuu vipi, kwema.

Wakuu Iran ni mmoja kati ya nchi ambazo ziliwekewa vikwazo vikali na nchi za magharibi toka mnamo mwa miaka ya 70s huko hadi leo hii na siku zijazo.

Vikwazo hivyo ni vya kiuchumi, kijeshi nk, tena vimekuwa vikiongezwa siku hadi siku.

Tofauti na ilivyo kwa nchi nyingine kama vile Cuba, Venezuela nk zilizowekewa vikwazo pengine na marekan tu, au baadhi ya nchi za magharibi. vikwazo vya Iran vimewekwa na nchi za magharibi kama zote wakishirikiana na makampuni ya nchi hizo.

Lakini cha kushangaza Iran imeweza kuwa na uwezo hasa wa kijeshi sawa au pengine zaidi ya ule wa nchi ambazo hazijawahi kuwekewa vikwazo na nchi hizo.

Iran ni miongoni mwa nchi zenye eneo kubwa na watu wengi barani Asia, so pamoja na vikwazo vya kiuchumi walivyowekewa takriban miaka 50 na zaidi, lkn wameweza kuwa na mifumo mizuri ya kudhibiti hali ya umasikini nchini mwao, tofauti na nchi kama Venezuela ambazo vikwazo vya miaka miwili au mitatu vimesababisha mamilioni ya raia waishi maisha ya shida na ya umasikini kupita maelezo.

Pamoja na vikwazo vikali vya magharibi hasa kwa upande wa mambo ya ulinzi, lkn bado nchi hiyo imeweza kuonesha kuwa haipo chini au nyuma kijeshi hata siku moja. Wengi tuliona jinsi wa Iran walivyoziangamiza ndege zisizo na ruban zilizokuwa zinatumiwa na Marekan kupima upepo katika eneo lao, wengi tuliona jinsi Iran ilivyozilipua meli ambazo zilikuwa zinabeba wapelelezi mbali mbali wa magharibi karibu na eneo lake, wengi tuliona jinsi Iran ilivyoshambulia kambi kadhaa za Marekani kule Iraq na kusababisha maafa na uharibifu mkubwa katika kambi hizo baada ya Mmarekani kumuuwa mmoja wa maofisa wakubwa wa Iran kule Iraq, tena kabla ya kufanya mashambulizi hayo wa Iran walitoa taarifa mapema kuwa watalipiza kisasi kupitia kambi za wamarekan kule Iraq, so marekan ikajiandaa kuzuia shambulizi lkn mwisho wa siku shambulizi likashindikana kuzuilika na kuleta maafa kwa jeshi la nchi hiyo kubwa duniani.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyotoa msaada wa silaha kwa kundi la hezbullah ambalo liliichachafya Israel inayopata msaada mkubwa wa fedha kutoka Marekani kwa ajili ya ulinzi wao. Hiyo ilikuwa mwaka 2006 hadi jumuiya ya kimataifa ikaingilia kati na kuomba ipatekane suluhu ya kudumu baina ya Israeli na hezbullah.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyosimama na kumlinda Asad wa Syria katika vita vyake, hadi kupelekea mipango ya Marekani na nchi za magharibi kumng'oa imeshindikana.

Wengi tunashuhudia sasa jinsi silaha kidogo tu za ndege zisikuwa na rubani za Iran zinavyofanya uharibifu mkubwa, na kusababisha maafa makubwa na zaidi ya yale yaliokuwa yanafanywa na Russia kupitia silaha zake mwenyewe (Russia) huko Ukraine.
Mpaka Marekani na nchi zingine za magharibi zinapiga kelele, maana silaha zinazotumika sio zile za Russia ambazo zilikuwa zinampa jeuri raisi wa Ukraine kuona kwamba sasa vita vimekwisha.

Hata zile himars za Marekani sasa hivi zinaonekana hazifanyi kazi mbele ya maangamizi ya ndege hizi za Iran.

Sasa tujiulize, kama nchi iliyowekewa vikwazo na mataifa makubwa duniani kwa zaidi ya miaka 50 bado ina uwezo iliyo nao leo, sasa je kama isingewekewa vikwazo kwa miaka yote hiyo 50 leo ni nchi gani ambayo ingeitisha pale Asia na hata duniani kwa ujumla.

Hizo nilizosema hapa ni zile silaha ilizotoa kuwawezesha hao niliwataja washinde mapambano yao, hapo hatujazungumzia silaha zake mwenyewe alizoweka kwa lengo la kujilinda ambazo kwa sheria za kijeshi duniani huwa zinafanywa siri kubwa ili adui asizione.

Mpaka sasa Marekani na nchi za magharibi zinashindwa kujua ni njia gani nyingine ya kumdhibiti huyu mtemi, maana wamarekani waliwahi kumtumia msaudi mwaka jana, hapo hapo Iran hakuchelewesha akaangamiza mitungi yake mikubwa ya kuwekea mafuta mpaka saudia na dunia ikapiga kelele.

Hili taifa ni la maajabu sana, japo lina maadui wengi lililotengenezewa na nchi za magharibi na halipati msaada wa kifedha kutoka kwa nchi yoyote lkn bado linajiamini kupita maelezo.

Mti wenye matunda ndio hurushiwa mawe, namaanisha ukiona nchi za magharibi na vibaraka wao wanapambana kwa hali na mali dhidi ya uchumi na ulinzi wa kijeshi wa nchi moja, basi jua kwamba wamagharibi hao wameshagundua kwamba nchi hiyo ni hatari maradufu kwa mustakabali wa uchumi wao pamoja na ulinzi wao.

Siku nyingine uwe unaongea kwa takwimu sio insha nyingi
msaada ambao israel inapokea n 2B sasa unasemaje mabilion ya fedha kutoka US
si hivo tu US inawapa palestina,Rwanda,n nchi mbali mbali misaada tofauti ni kuwa wanafanyia nn!

Lakini hujaeleza kua Iran pia baada ya sanction ilitegemea bidhaa za magendo,na nchi za Asia

Lakini pia kuna nchi kama North korea ambayo vikwazo vimedunda pia
Ni akili tu za watawala
 
Dunia hii na karne hii ya 21 bado unashikiwa akili na kudanganywa utafikiri bado upo katika karne ya 10 huko.
Wengi mnamezeshwa uongo na nyinyi bila kujitambua au kutafakari mnameza tu.
Ukweli ni kwamba Israel inafadhiliwa kijeshi na kifedha na serikali ya Marekani ikishirikiana na nchi zingine za magharibi. Obvious ni kweli kuna matajiri wa Israel na hata wasiokuwa Israel wanaifadhili Israel lkn, lkn serikali za nchi hizo nilizotaja hapo juu ndio wafadhili wakubwa wa Israel ndio maana utasikia serikali ya Marekani inaipa au imeipa Israel bilioni fulan kwa ajili ya kuimarisha shughuli zake za ulinzi na kiuchumi, vigumu kusikia taarifa ya habari ikisema matajiri kadhaa wa Marekani wameipa Israel bilion fulan kwa ajili ya shughuli fulan nk.

Sasa jiulize taifa teule kwanini litegemee misaada ya kifedha na kijeshi kutoka nje?
Kwanini ling'ang'anie kusema Iran iendelee kuwekewa vikwazo? Yenyewe si ina nguvu inaogopa nini sasa hadi ing'ang'anie mwenzake aendelee kuwekewa vikwazo?

Israel ni sawa sawa na bondia 'A' ambae anataka kupigana na bondia 'B' ambae ni Iran, afu Israel bondia
A anasema kwamba kabla ya pambano bondia 'B' afungwe kwanza mikono (awekewe vikwazo) afu ndo aingie mapambanoni.

Pamoja na kuachiwa atengeneze silaha, na msaada wa kijeshi juu kwa zaidi ya miaka 50 lkn bado anahofia Iran ikiwa huru inaweza kutengeneza silaha ambazo zitaleta maangamizi makubwa katika ardhi yake.

Israel pia ni kama CCM, yenyewe iko huru kufanya mikutano na kampeni mbali mbali ikisaidiwa na serikali (USA, UK, France nk) huku ikizuia wapinzani (Iran) wasifanye mikutano wala kampeni (vikwazo) afu kwenye uchaguzi wanategemea kusema eti wameshinda uchaguzi huo kwa njia ya haki kweli?

Kwanini wasiwaachie (waondoe vikwazo) na wapinzani (Iran) kufanya mikutano na kampeni zao kama ilivyo kwa CCM (Israel)
Afu sasa ndio waende kwenye mpambano wa uchaguzi (vita) kuona nani ni mshindi wa kweli?

Jinsi CCM inavyoogopa upinzani na kuuzuia usifanye mikutano yake, ndo jinsi Israel, Marekani, Saudia na nchi za magharibi zinavyoihofia Iran isiwe huru kutengeneza silaha zake na kuboresha uchumi wake.

Mkuu mtu akikusikiliza anaweza akasema unaakili kumbe akili zako zinasoma kurudi nyuma[emoji23][emoji23][emoji23]Kweli kuna machizi wenye IQ

Hujaeleza ilikuaje US ikawa inapeleka hizo ela Israel?? na hujui hadi leo kwann?? (so usibwabwaje usichokijua)
Kati ya waarabu na waisrael wapi wapo wengi ulaya na US ?? kwann sasa hzo hela haziendi nchi za kiarabu


Eti kama taifa teule kwann wanashinikiza vikwazo!!?? bado hujui
Adui mwombee njaaa (nadhani hii nayo huijui)

Ushindi upo katka kumdhoofisha adui na si kumuacha akue. Hakikisha unammaliza adui kabisa kabisa (kasome 48rules of power)

Israel inatumia slogan hii

“if the enemy want to kill you, wake up and kill him first”

ukielewa hapa hutaandika uo ujinga ulioandika siku nyingine
 
Jamaa wako vizuri mno kichwani. Miaka zaidi ya 2000 iliyopita waliowahi kuwa na Empire ambayo ilidumu kwa muda mrefu.

Sasa leo hii kanatokea kanchi kenye miaka Mia tatu tu toka kaanzishwe, eti kanakuja kuwatishia nyau na kujaribu kuwapangia jinsi ya kuishi watu wazima wenye akili zao.
Kwa Middle East Iran ni nchi ya pili kwa kuwa na Wayahudi wengi baada ya Israeli, hivyo usihangae maarifa yao.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Siku nyingine uwe unaongea kwa takwimu sio insha nyingi
msaada ambao israel inapokea n 2B sasa unasemaje mabilion ya fedha kutoka US
Nilijua tu kuwa atatokea myahudi wa kisukuma aje kuwatetea wayahudi wa kizungu bila kuwa na fact ya kile anachotetea.

Umesema siku nyingin niwe naongea kwa takwimu, lakini wewe mwenyewe ulieni quote unashindwa kuweka takwimu ya ulichoandika. Yani wayahudi wa Chato mnachekesha sana mnapoingia kichwa kichwa na mihemko yenu kuwatetea wayahudi wa kizungu ambao nina hakika hawawafahamu 😂😂😂

Angalia picha hapo chini ili ujifunze hii fact iliyo katika takwimu kama inafanana na kile ulichotoa kichwani kwako mwenyewe bila ya kutafiti.

si hivo tu US inawapa palestina,Rwanda,n nchi mbali mbali misaada tofauti ni kuwa wanafanyia nn!
Misaada wanayopewa Palestina ni ya kinafiki, hauwezi kufananisha na ile ya kiyahudi kwa sababu kadhaa ambazo wewe myahudi wa kisukuma hauzijui.

A. Misaada wanayopewa wapalestina ni ya masharti maalumu yani hawaruhusiwi kuitumia kununua silaha yoyote ambayo wanaweza kuitumia kujilinda. Ila wanayopewa Israel ni ruhusa kununua silaha au kuitumia kutengeneza silaha zao wenyewe, kuboresha jeshi lao nk.

B. Misaada wanayopewa wapalestina ni kwa ajili ya kununua madawa, chakula na huduma zingine za kawaida. Ila wanayopewa Israel ni ruhusa kuitumia kuimarisha jeshi lake, kuboresha silaha zake kwa ajili ya kupambana na majirani zake na zingine wanazitumia hadi kuwajengea watu wao katika ile ardhi ambayo sio ya kwao na sheria za kimataifa, ikiwepo hiyo Marekani yenyewe haziwaruhusu kujenga.
Lakini hujaeleza kua Iran pia baada ya sanction ilitegemea bidhaa za magendo,na nchi za Asia
Yes kutumia magendo ndo ujanja, ubabe na uwezo wenyewe. Nchi nyingi ziligwaya, zilianguka kiuchumi, kijeshi na kiuongozi baada ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa mataifa.

Leo hii Israel achilia mbali kuwekewa vikwazo, hata wakinyima misaada na Marekani kwa muda wa miaka mitano tu. Itakuwa nyang'a nyang'a kama Cuba ambayo leo hii limebaki jina tu ila uchumi wa nchi na jeshi ni hovyo kabisa.
Lakini pia kuna nchi kama North korea ambayo vikwazo vimedunda pia
Ni akili tu za watawala
Vikwazo vya North Korea ni tofauti na vile vya Iran. Inatumika nguvu kubwa zaidi ya vikwazo kwa Iran kwa sababu mbili kubwa.

1. Geography yake ya kuwa karibu na nchi ya Israel, ambayo inaifanya Marekani, USA, UK na umoja wa Ulaya wahofie kwamba Iran isipowekewa vikwazo vya silaha, na uchumi basi kuna uwezekano mkubwa wa siku moja nchi hiyo ikafanya kitu ambacho watu wengi hawatokitegemea kutokea huko Israel na mashariki ya kati kwa ujumla.

2. Historia yake, kama nchi yenye historia ya kuwa na nguvu pamoja na jeshi bora kwa zaidi ya miaka 2000 iliyopita, hata kama hauipendi Iran na hauna ujuzi wa historia, lakini nakushauri uingie google usome kuhusu persia empires, au uende kwa biblia ukaisome historia ya uajemi.

Ni tofauti na vinchi kama US ambavyo vimeanzishwa miaka mia tatu tu iliyopita na waingereza.
 

Attachments

  • Screenshot_20240112-122650.jpg
    Screenshot_20240112-122650.jpg
    105.1 KB · Views: 2
  • Screenshot_20240112-121127.jpg
    Screenshot_20240112-121127.jpg
    74.3 KB · Views: 2
Back
Top Bottom