ITV siyo sahihi kutoa sauti ya Hotuba ya Tundu Lissu katika Mkutano wa ACT-Wazalendo

ITV siyo sahihi kutoa sauti ya Hotuba ya Tundu Lissu katika Mkutano wa ACT-Wazalendo

Ata sioni sababu ya kumfungia sauti mtu ambae kila anapopewa nafasi anajikaanga kwa mafuta yake mwenyewe.

Shida yake ni Magufuli sio kuwatumikia watanzania, wakati Magu mwenyewe ndio kwanza anatafuna mahindi kwenye TV mpaka kuongea anashindwa.
 
Ata sioni sababu ya kumfungia sauti mtu ambae kila anapopewa nafasi anajikaanga kwa mafuta yake mwenyewe.

Shida yake ni Magufuli sio kuwatumikia watanzania, wakati Magu mwenyewe ndio kwanza anatafuna mahindi kwenye TV mpaka kuongea anashindwa.
Lini alijikaanga?
 
Lini alijikaanga?
Ana obsession na vitu ambavyo havipo yupo so defensive nani kamwambia atopewa form ya uraisi.

Kingine juzi tu hapa tume imetangaza hakuna kufunga ofisi kila mgombea wa ubunge na udiwani apewe form kwenye uchaguzi, yeye bado analalamika tu aamini maagizo yanayotolewa NEC.

Ni kumuacha tu mtu kama huyo kupayuka with time watu wamuone inawezekana hayuko sawa maana anaongea vitu ambavyo havipo, nchi sijui aina marafiki dunia nzima ipo peke yake kisa Magufuli apendwi nje.
 
Nimeshasema mara nyingi kwamba Wadanganyika tungali ktk dark ages . Yaan nimeshindwa nitazame TV gani objective??
 
ITV wametia aibu kubwa

Eti Superbrand, Superbrand my foot
Wanaogopa kurusha maudhui halisi wanamzimia mzungumzaji sauti

Wamenibore kinyama hawa watu!
Kwahiyo mnazidiwa akili hata na Kina Joti? Kwani clip zao mitandaoni zinarushwa na ITV?

Nilitegemea kwenye thread hii utuwekee video clip yenye sauti tumsikie Lisu alikuwa anasema Nini na Hawa mbwa wa Marehemu Mengi hawataki tusikie Nini.

Badilikeni huu siyo muda wa kulialia, CCM wameinunuwa channel ten mapema tu wanajuwa media ni Nini.
 
Kuonyeshwa live ni mpaka ulipie ,je wamelipia?,wakakataliwa?
Tumia akili bhasii kwani ACT wakati wanarushwa Live hawakulipwa??? Tatizo sio kulipia tatizo ni Ccm haitaki upinzani usikikee kabisaaa... Dikteta yoyote kamwe hawezi achia vyombo vya habari viwe huruuu ndo haya sasa. ITV hata kwenye habari zao habari za Chadema kuziona kwa tochi sana tena hapo ukute chadema wapo mahakamani au wanashitakiwa kwa Jambo fulani ila sio Mambo Positive ya chadema...Superbrand mafi mafii tu
 
Ukiona Taifa hadi vyombo vya habari vina kitete ... basi hilo taifa kinakwenda shimo la tewa!! Ni wajibu wetu kuliokoa.
Tatizo wakati wajumbe wa CCM wanawanyowa kwa kura sufuri watia Nia hamkuwa makini kuyafuatilia majina ya watia Nia na fani zao, Pasco Mayalla kura moja.
 
Nimeshasema mara nyingi kwamba Wadanganyika tungali ktk dark ages . Yaan nimeshindwa nitazame TV gani objective??
Ni DStv tu. Hata makocha wanaokuja kufundisha Simba na Yanga moja ya sharti la mkataba ni kuwekewa DStv na WiFi.
 
Ana obsession na vitu ambavyo havipo yupo so defensive nani kamwambia atopewa form ya uraisi.

Kingine juzi tu hapa tume imetangaza hakuna kufunga ofisi kila mgombea wa ubunge na udiwani apewe form kwenye uchaguzi, yeye bado analalamika tu aamini maagizo yanayotolewa NEC.

Ni kumuacha tu mtu kama huyo kupayuka with time watu wamuone inawezekana hayuko sawa maana anaongea vitu ambavyo havipo, nchi sijui aina marafiki dunia nzima ipo peke yake kisa Magufuli apendwi nje.
Magufuli anapowaita watu weupe mabeberu unamchukuliaje?
 
Lisu ni mmoja wa Watu risk kwa TV ,ITV walishaponzwa na Chadema kuna siku mchungaji Msigwa walimrusha live akaanza kumporomoshea matusi Naibu Spika Tulia Ackson kitu ambacho Ni kinyume na maadili ya utangazaji wakalipishwa faini mamilioni na TCRA

Lisu hajiheshimu akianza kuropoka aweza ponza chombo Cha habari kikafungiwa ndio maana hata magazeti wanakwepa kaandika anayosema sababu yako kinyume na maadili ya uandishi wa habari .Ukiyaandika Ni at your own risk na hajali hata ufungiwe sawa na mikesi haji mahakamani anakutekezea likesi lako

Yuko so careless when it comes to public speaking .Akili yote huwa anaiacha nyumbani kwake kurusha live Ni kujitakia shida hujui Ni wapi atachomoka na dude lililo kinyume na maadili ya uandishi na kulirusha hewani
Lisu anavyolopoka ni Kama Magufuli tu.
 
Achana na hivyo vyombo vya habari vya Tanzania ndugu. Wanadhani Magu anashinda uchaguZi wa mwaka huu. Wasichojua ni kwamba Tanzania inaenda kushangaza ulimwengu mwaka huu. Fundi Antipas Lissu anaenda kuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka huu na wote waliomdhiaki wataenda kumwomba msamaha
Ni ndoto ya badae Sana mkuu, sure! Haiwezi kuwa hata ungealika na walioahidiwa chochote baada ya hapo! Haiwezekani, hiyo Nguvu na ushawishi wa kumwondoa Magu Kwa bongo hii Kwa sasa, hayupo mkuu.
 
Magufuli anapowaita watu weupe mabeberu unamchukuliaje?
Beberu ni mnyonyaji, hana rangi! Yeyote Yule anayefanya kazi za kinyonyoji ni Beberu, hata wewe kama unafanya kazi za kinyonyoji, ni beberu tu
 
Achana na hivyo vyombo vya habari vya Tanzania ndugu. Wanadhani Magu anashinda uchaguZi wa mwaka huu. Wasichojua ni kwamba Tanzania inaenda kushangaza ulimwengu mwaka huu. Fundi Antipas Lissu anaenda kuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka huu na wote waliomdhiaki wataenda kumwomba msamaha
Amka bro kumekucha usiote mchana wotee huu
 
I T V T B C

HAO WOTE WANAMUOGOPA

M W E N Y E N Y U M B A....!!!!!!
 
Back
Top Bottom