Jaji Warioba: Dkt. Bashiru ajibiwe kwa hoja, hajafanya kosa lolote acheni kumshambulia

Jaji Warioba: Dkt. Bashiru ajibiwe kwa hoja, hajafanya kosa lolote acheni kumshambulia

Hata mimi kosa la Bashiru sijaliona.

Watanzania sijui tuna pepo gani aisee, sifia sifia hii sijui itaisha lini.

Huku kusifia kila kitu, kule kupinga kila kitu. Mzani haubalance yani.

Wa huku akienda kule nae anaadopt tabia za kule vivyo hivyo sa kule akenda huku nae anasifia kila kitu.

Ni unafiki na ubinafsi tu.
 
Ukitafakari kwa kina aina ya viongozi tulio nao ndio tunapojua dhahiri taifa kama taifa kufikia maendeleo halisi ni ngumu sana .

Kama wengi wa viongozi wetu wanatoa maoni yao juu ya maoni ya mtuwingine kwa namna tunavyo ona tukubali tu kwamba sisi wananchi wa taifa hili ni miongoni mwa wenye kupata hasara.

Mtu ametoa maoni ya kawaida kabisa kwa akili za walio wengi na mitazamo ya walio wengi lakini wanatokea madaktari wa falsafa ambao ndio hujulikana kama wasomi wa hali ya juu wanakosoa maoni ya mtu na si kwa maslahi ya taifa bali kwa kikundi chao na kiongozi wao!

Sisi kama wananchi wa kawaida tunaangalia kwa umakini mtanange huu, lakini kama tungejaliwa kujua hakuna wakati mzuri sisi wananchi tunaopata kama wakati wa kupiga kura.

Bahati mbaya sana hatutumii wakati huo kwa maslahi mapana ya taifa letu na sisi kwa ujumla , badala yake ni kulia kulalamika na kulaumu miaka na miaka.
Umekosea mkuu hawakosoi maoni bali wanamuattack mtoa maoni.

Bora basi hata yajadiliwe maoni, cha ajabu anajadiliwa mtu.
Mara hana kadi
Sijui kadi hakurudisha , yote hayo yanatoka wapi.?? Ulikua wapi kuyasema kabla?? kwanini hukusema wakati anateuliwa.??
 
Mzee maisha yamempiga, anahaha tu kutafuta ajira kupitia wapiga debe wa katiba mpya.

Huyu alikaa na Nyerere kwa miongo kadhaa, hakumshauri kuhusu katiba, na aliiacha nchi imefilisika, kwa Sasa hivi hana la kutushauri, ni mtu wa hovyo tu, na pia alikula Hela katika kashfa ya meremeta.

Matapeli wa kisiasa waliobaki
Una uhakika kua maisha yamempika kuliko wewe yalivyokupiga?

Acha uroporopo, Acheni watu watoe maoni yao kwa uhuru, Kama ninyi mnavosifu na kuabudu
 
Ni kosa kutoa mawazo ya kinafiki kwa sababu mwenyekiti wake aliyetwaliwa alipenda sifa sana na hakuweza kumshauri haya anayosema hii inamaana angepata nafasi ya kuwa Rais kwa ticket ya ccm,angetaka sifa pia .Ni mfumo
 
Bado hamjitambui kabisa, bado wachanga sana kidemokrasia, demokrasia haina exceptions, eti itakupa haki yako kama hauna historia mbaya ya yaliyopita!.

Mnaonesha dhahiri kumbe hata huwa hamumuelewi Mbowe akisema hana visasi, nyie bado wachanga sana.

Kama mkianza kuleta habari hizo, hata huko ulipo nanyi kuna madudu mlifanya yanayostahili msisikilizwe, na tukianza kutazamana kwa jicho hilo, mwishowe hili taifa litakuwa la mabubu CCM wafanye wanavyotaka, usimfunge mdomo mwenzio ili nawe ukisema upate wa kukusikiliza.

..Nadhani uko kinadharia zaidi.

..You are dealing with human beings, not stones.

..kwamba watu wana kumbukumbu, wana hisia, na wana akili zinazofanya tafakuri.

..Wanamkumbuka Dr.Bashiru jinsi alivyokuwa fedhuli na mwenye kiburi cha madaraka wakati akiwa Katibu Mkuu wa Ccm.

..Leo amefikwa na nini kiasi cha kiasi cha kuanza kuwazodoa watawala, na kutetea wanyonge?

..Je, tumuamini tu bila ya kumdadisi? Je, atetewe tu bila kwanza kukiri makosa yake, na kuwaomba radhi waliodhulumiwa wakati akiwa sehemu ya genge la watawala?

..Kuielewa hoja yangu labda nitoe mfano huu mdogo. Hivi mtu ambaye anajulikana kwa kumkashifu Mtume Muhammad, je ana uhalali siku yoyote ile atakayoamua aingie Msikitini?

..Je, waumini hawana haki ya kumhoji kama ame Silimu? Je, hatakiwi kuulizwa kama ametawadha kabla hajaingia Msikitini? Je, aachwe tu aingie Msikitini na viatu?

..Narudia tena, Dr.Bashiru atubu, aombe radhi, ajitenge na ufedhuli na unyanyasaji wa awamu ya 5. Baada ya hapo atakuwa na uhalali wa kutetea uhuru wa maoni.
 
..Nadhani uko kinadharia mtu.

..You are dealing with human beings, not stones.

..kwamba watu wana kumbukumbu, wana hisia, na wana akili zinazofanya tafakuri.

..Wanamkumbuka Dr.Bashiru jinsi alivyokuwa fedhuli na mwenye kiburi cha madaraka wakati akiwa Katibu Mkuu wa Ccm.

..Leo amefikwa na nini kiasi cha kiasi cha kuanza kuwazodoa watawala, na kutetea wanyonge?

..Je, tumuamini tu bila ya kumdadisi? Je, atetewe tu bila kwanza kukiri makosa yake, na kuwaomba radhi waliodhulumiwa wakati akiwa sehemu ya genge la watawala?

..Kuielewa hoja yangu labda nitoe mfano huu mdogo. Hivi mtu ambaye anajulikana kwa kumkashifu Mtume Muhammad, je ana uhalali siku yoyote ile atakayoamua aingie Msikitini?

..Je, waumini hawana haki ya kumhoji kama ame Silimu? Je, hatakiwi kuulizwa kama ametawadha kabla hajaingia Msikitini? Je, aachwe tu aingie Msikitini na viatu?

..Narudia tena, Dr.Bashiru atubu, aombe radhi, ajitenge na ufedhuli na unyanyasaji wa awamu ya 5. Baada ya hapo atakuwa na uhalali wa kutetea uhuru wa maoni.
Kwa kuwa alikuwa fedhuli akiongea ukweli unageuka kuwa uongo!?
Mbona kabla ya kuwa ccm hamsemi kuwa alikuwa sio fedhuli mnayoangalia ni hayo ya miaka miwili ambayo hayakuwa furahisha.
Machawa jibuni hoja zake
 
Hebu tupe mfano wa mtu mmoja toka CCM, au wale wengine mashabiki wa walamba asali aliyejibu hoja za Dr. Bashiru ukiondoa hizo kelele za kina Lusinde na wenzake.

Halafu unawaingiza wakina Lissu na wengine sijui wanahusiana nini kwenye kujibu hoja za Dr. Bashiru, mimi naona ndio unataka apuuzwe kisa historia yake.

Mtambue whatever Dr. Bashiru alifanya kabla, hakumuondolei haki yake ya kuzungumza na hoja zake kujibiwa.

Hiki mnacholazimisha kuleta ndicho kinawakuta nanyi halafu mnalalamika, ndio maana mikutano ya siasa mmezuiwa japo ni haki yenu, mnaendelea kuwakomaza CCM wazidi kuvunja sheria bila kujua, amkeni; msiwe wabinafsi, haki haichagui rangi, historia, wala chochote..

Ukimnyima haki mwenzio mjue nanyi mtamyimwa, mjifunze kuihubiri demokrasia na kuitenda, sio mnaishia kuihubiri pekee, hii demokrasia yenu unayoileta ina exceptions, hamtaki fulani asikilizwe kisa historia yake, hii kitu haipo hapa duniani.
Bashiru kajibiwa, Kajibiwa na Kigwangala kuhusu masuala ya serikali kuongeza bajeti ya kilimo, ruzuku ya mbolea, kufungua masoko n.k
Kama hujaridhika na majibu Hilo ni lingine, Ila Kajibiwa
 
..nakubali Bashiru atetewe.

..lakini itapendeza kama Bashiru atawaomba radhi wale waliodhalilishwa na kuteswa wakati akiwa Katibu Mkuu wa Ccm.
Ninani aliyezalilishwa wakati wa Bashiru?Bashe na Nape ndio walikuwa wakosoaji sana kipindi cha Magufuli, pamoja na ukosoaji Bashe alipewa unaibu Waziri wa kilimo tena Magufuli alimwambia hadharani kuwa kuwa yote uliyokuwa unayakosoa nenda kayafanye,Makamba na Nape Kinana na Ngereja walinaswa wakimtukana Magufuli, lakini aliwapotezea utukusikia kelele za kuwavua ubunge au wanachama.Bashiru kutoa maoni tu kuwa watawala inabidi kutimiza wajibu wao na Sio hisani kwasababu ni waajiliwa wetu nayo imekuwa nongwa,harafu wanasema Samia karudisha democrasia kwenye chama,watu wanatoa maoni yao bila wasiwasi,hiki ni kichekesho kingine.
 
Hapa ndipo unapotofautisha maoni ya msomi, na mashabiki wanaotafuta madaraka na vyeo kwa kumshambulia Bashiru kwa ajili ya matumbo yao.

Utashangaa mpaka kina Msukuma na Lusinde leo wanaonekana wa maana kisa wanamshambulia Bashiru, tuna taifa la mihemko sana, ambalo kila siku linazidi kupoteza muelekeo.
Na linapoteza Kweli !! Tumuombe Mungu sana. !!
 
Dr.Bashiru katika video hii fupi binafsi sijaona wala kusikia akiongea baya lolote, hasa kwa watu aliokuwa anaongea nao, hii kauli ya Bashiru tafsri yake ni kwamba lazima tuwawajibishe Watawala, wao kututumikia sio fadhila bali ni wajibu wao.
Msikilize Dr. Bashiru halafu uamue kama tumsimange au tufuate ushauri wake.
View attachment 2423256
Watu wanakaripia unafiki wake maana yeye alimtukuza magufuli kuzidi Mungu, aliwa master mind wa ukatili dhidi ya binadamu alioufanya magufuli, halafu leo anageuka kukemea maovu aliyoyaasisis wakati wa magufuli ambaye naye alimpambia kama haa wanavyompambia samia
LAKINI ANAYOSEMA YAKO SAHIHI!
 
Kwa mantiki yako hii maana yake hakuna mtu anayepaswa kutoa ushauri wowote juu ya uongozi katika Nchi hii.
Sababu tukisimamia misingi unayoamini hakuna msafi hata mmoja.
Hivyo tuache kulalamika kwa lolote,kuanzia mfumuko wa maisha,ufisadi n.k maana hakuna msafi

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
Kule mahala vile vichwa vyenye uwezo wa kupangua hoja havipo tena kuanzia mwaka 2010 mwanzoni
 
Hata mimi kosa la Bashiru sijaliona.

Watanzania sijui tuna pepo gani aisee, sifia sifia hii sijui itaisha lini.

Huku kusifia kila kitu, kule kupinga kila kitu. Mzani haubalance yani.

Wa huku akienda kule nae anaadopt tabia za kule vivyo hivyo sa kule akenda huku nae anasifia kila kitu.

Ni unafiki na ubinafsi tu.
95 % jamaa ni Selfish !!
 
Kwa kuwa alikuwa fedhuli akiongea ukweli unageuka kuwa uongo!?
Mbona kabla ya kuwa ccm hamsemi kuwa alikuwa sio fedhuli mnayoangalia ni hayo ya miaka miwili ambayo hayakuwa furahisha.
Machawa jibuni hoja zake

..tatizo la Dr.Bashiru ni uongo, ufedhuli, na ukatili, aliokuwa akiuunga mkono wakati akiwa Katibu Mkuu wa Ccm.

..kuna watu walifungwa, wametiwa ulemavu, wamepotezwa, kwa kuwa walikuwa wakosoaji wa Ccm na serikali yake wakati Bashiru akiwa Katibu Mkuu wa chama.

..sikuwahi kumsikia Dr.Bashiru akiwasemea au kuwatetea hao. Sanasana nilimsikia akiwabeza na kutetea watawala wakati wote.

..Dr.Bashiru alipaswa kutubu kwamba alikosea. Kwamba aliunga mkono utawala dhalimu wa awamu ya 5. Akifanya hivyo itakuwa rahisi zaidi kutetewa na wapenda haki, demokrasia, na uhuru wa mawazo.
 
Back
Top Bottom