Je, hayati John P. Magufuli alidanganywa na vyanzo vyake vya habari? Maana sasa ni kama kufedheheshana

Aliyefedhesha atafedheheshwa, alifuta nyayo za JK acha na yeye afutwe tu
 
Mimi ukinishauri ndio unaharibu kabisaa, sasa acha Mama afanyie kazi ushauri wa wataalamu.

Usikivu nao ni kipaji hauwezi kuota kundi la wataalamu then wewe ukawa ndio unawashauri wao na ukijua fika hawatokupinga.

Karume day njema.
 
Nyumbu hili
 
Hakuna kitu Magufuli amewahi kufanikiwa kwa kuwa alidhani ana akili sana na maono wakati yeye intellectually ni average student. Angalia uuzaji nuumba za Serikali, ununuzi kivuko cha Bagamoyo, meli ya Thailand na Biashara ya korosho. Yote ni madudu
 
Alikuwa mjuaji na hakushaurika!
Alijiona Alfa na Omega na ndio maana wajinga kama wewe mkaanza nyimbo za atake asitake tunamwongezea muda atawale milele! Mungu mwenyezi ni Fundi! amewaaibisha sana nyie wachumia tumbo!
 
Kipindi unachosemea ww Watanzania hawafiki milioni 15 wanaenda shule ni chini ya 4% sasa hv mpo milioni 60 wanaoenda au waliofikisha umri wa kwenda shule 98% wanaenda shule uoni kuna tofauti kubwa ?
Ww kiazi kweli, kipind hicho nchi ilikua bado hata haijaagusa uchimbaji wa madini...kilimo cha mkonge tuu watu wakasoma bure. Hao watu mil 60 wamedondoka kutoka sayar ya mars? Niishie hapo!
 
Nyerere alisema katiba yetu nimbaya,rais akija dikteta anaweza kujiamulia kufanya atakavyo hakuna wakumzuia!
Hii katiba inapaswa badilishwa maana nchi inaweza kupelekwa na mawazo yamtu mmoja vile ajisikiavyo yeye!!
Mifano ikowazi;
  • Nibunge gani lilipanga ununuzi wa midege haraka na kwa cash?? Jibu ni mwenda aliamua...
  • Nibunge gani liliamua kujenga daraja LA busisi?? Mwenda
  • bunge gani lilizuia madaraja na nyongeza za mishahara? Nimwenda tens alisema akitaka kutoka ndipo ataongeza...
  • Lihospitali la rufaa chato?
  • uwanja was ndege chato?
  • barabara za taa,umeme vijiji vyote,mipango chato kuwa mkoa karibuni?? ....
  • Reli yaumeme kuanza ujenzi pia tokea Mwanza ili isije badilishwa hata akiaga?
  • Maujenzi makubwa Dom? Kumzima supika?
-uteuzi kikanda zaidi mf. Waziri Nishati wakijjni kwake nk. wanajulikana
Kimsingi aliamua bila kujali mawazo ya wasaidizi wake,nao kwakuhofia kukosa vyote wakabaki kumwangalia huku wakitamani wapate nafasi warekebishe!!
Tutumie akili kidogo,hakuna MTU timamu atabeba mamipango ya mwenda yooote kama yalivyo!! Mama kasema miradi mkakati iendelee mingine atapima kwanza,heko heko kwake!! Taifa haliwezi kung'ang'ana kwanguvu kujenga Dom (ya rafikiye mtaniwe supwika),Mwanza (ya wakwe nawapush wenzie) na chato (kijj mwake).
 
Umewaza kama mimi big up sana mkuu
 
Inavyoonekana mama hakua anakubaliana na jiwe mambo mengi Ila sasa hakua na nguvu ya kuyapinga na pia jiwe alikua hashauriki.kaiharibu nchi sana yule marehemu.
 
Hatujabisha maana nyinyi mlikuwa wanufaika wakubwa kuliko tabaka la chini,, hasa walala hoi au wenye kipata cha chini,, haitaji kuwa na uwezo wa kufikiri kwamba huyu mtu alikuwaje,, vise versa alikuwa mtu siyo sahihi kwa taifa hili
 
Au maza kashalishwa kaseti na yule mzee mwenye tabasamu muda wote,

au maza nae alimchukia hayati kama walivyofanya mabeberu?

Au maza kafurahi paka ametoka?

Au maza anajua yaliyomkuta mzee?

Au maza, au au au
Kumbuka chama pendwa ni kile kile na watu wake ni wale wale
 
@mgaka12, laiti kama ungesoma post zilizotangulia, wala usingeuliza swali la kifala kama hili!
Rudi nyuma, soma post hasa #9 ya Chief Oswald Daudi Mwakibete, utaelewa tu kama usipofanya shingo yako kuwa ngumu.
 
Hii ndio maana ya 'kuzinguana'.
 
Au maza kashalishwa kaseti na yule mzee mwenye tabasamu muda wote,

au maza nae alimchukia hayati kama walivyofanya mabeberu?

Au maza kafurahi paka ametoka?

Au maza anajua yaliyomkuta mzee?

Au maza, au au au
AU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…