Je, Israel ana combat superiority dhidi ya Iran?

Israel alishapambana na Hezbollah ambao huwa wanavaa gwanda lakini walipigwa, walichofanya ni kushambulia makazi ya watu na kuua raia.

Russia kawamaliza ISIS pale Syria na walikua wanavaa nguo za kiraia.
 
Tuone hio picha ya s 300 iliyopigwa.
Hata ya satellite.

Tuone hata picha ya mlipuko kipindi inapigwa?
Hakuna air defense system inayoweza kuzuia mashambulizi kwa asilimia 100, unapaswa kufahamu.
Ndio maana EU,US na Israel walijipanga kuzuia mashambulizi ya Iran lakini ikashindikana matokeo yake wakapiga kambi za kijeshi na kusababisha hasara.


Achilia nchi kama Jordan iliyojaribu kuzuia baadhi ya mashambulizi yakipita kwenye anga lake.

Kingine haiwezekani kwa Israel kushambulia akiwa ndani ya Iran, hapa tayari naona kuna ulakini kwenye habari yako, jaribu futilia vyema.

Halafu unaposema S 300 imeshambuliwa bado hujadadavua vyema, s 300 battery inajumuisha search radar, engagement radar, command and control vehicle na launcher, hizo zote ni vehicles na zinaweza kukaa umbali hadi wa km 35.

sasa Israel ilipiga vehicle ipi? launcher, search radar, engagement radar au command and control?
 
unaposema haiwezekani israel kushambulia ndani ya iran ndo inaonesha uwezo wako wa kufikiri ni mdogo, ndo wameweza sasa
 

Satellite photos suggest Iran air defense radar struck in Isfahan during apparent Israeli attack​

 

Precision and power: Israel used 'Rampage' missile to target Iran - Times of India
 
unaposema haiwezekani israel kushambulia ndani ya iran ndo inaonesha uwezo wako wa kufikiri ni mdogo, ndo wameweza sasa
Leta picha wameshambulia wapi?
Gharama ya damage waliofanya ni kiasi gani?

Nachosema ni kwamba Israel haina uwezo wa kupambana na Iran kivita, hata kama watashambulia wanaangalia nyakati na kufanya calculation ya nini kitatokea, hivyo wanajua wazi hivi sasa Iran amechukia na anamaanisha hivyo shambulizi loloteambalo lingegharimu maisha ya watu lazima wangewajibika.

Hivyo ni shambulizi la uoga.

Miaka yote wamekua wakiua watu wa Iran, this time around Iran kamtolea uvivu, Israel imerudi nyuma, sio ile Israel ambayo tumeizoea.
 
angalia link nilizotuma utaona picha, then kama ana uwezo huo au hana iran ndo anajua we waulize iran ndo watakaokupa jibu hilo mzee, iran ndo aliyefanya shambulizi la uoga mana alijiandaa wiki mbili wakati mwenzake kachukua siku mbili tu na hajatoa taarifa yeyote, iran alitoa taarifa kabisa sasa maroketi yamerushwa israel na watu wako club wanakula bata si zarau asee? alichofanya israel ilikua tu ni kutoa onyo kwamba wewe naweza kukufanya chochote naweza kukupiga hapa hapa ndani kwako so jiangalie
 
kamtolea uvivu je amempiga wapi? yeye iran kapigwa tena mara mbili, sasa iran yeye makombora yake karusha yote yameishia jordan na iraq tena sio kwa kutunguliwa bali yameishiwa nguvu yakaanguka yenyewe
 
kamtolea uvivu je amempiga wapi? yeye iran kapigwa tena mara mbili, sasa iran yeye makombora yake karusha yote yameishia jordan na iraq tena sio kwa kutunguliwa bali yameishiwa nguvu yakaanguka yenyewe
Hivi hujasikia mashambulizi waliyofanya yamepelekea hasara ya dol bilioni 1.35 pengine zaidi.
Kwamba wamepiga s 300, kama wamerusha kombora 1 imewezekana vipi kupiga mfumo wote wa s 300? ok fanya wameshambulia moja ya gari linalokamilisha battery ya s 300 labda launcher, sasa launcher ina cost kiasi gani?
 
Onyo za wapi wewe?
Hana huo uwezo, kama migambo ambao wanapewa chakula, silaha na mavazi na Iran wanamkimbiza mwezi wa sita huu atapambana na Iran?

Huwa anaitamani sana Iran kupiga nuclear facilities si angepiga ukaona movie, Israel hana lolote, Israel hata uwezo wa kupambana na Pakistan hana.

Mmekesha humu mkjisifu Iran irushe hata jiwe, sasa wamepiga kambi za kijeshi na kufanya damage, halafu wakatulia wakasema Israel ikijibu itawashambulia vibaya, Israel kwa nini asipige nuclear facilities, apige kambi za kijeshi za Iran?

Matokeo yake wameanza kumlaumu Biden na serikali ya US kujitoa kwenye vita.

US wanaifahamu vita, wanafahamu fika Israel haiwezi kupambana na Iran.
 
Wewe hizo data umezipata wapi mbona hujaweka kumbukumbu rejea au ni maoni yako.
 
Wewe hizo data umezipata wapi mbona hujaweka kumbukumbu rejea au ni maoni yako.
Nenda Aljazeera na hata BBC zipo article zinazozungumzia vita za mashariki ya kati.
Unalo bundle nenda.
 
Hufahamu kuwa kuna media bias pia, mfano aljazera wako symphasized na palestine unaweza kuwa misinformed kama huna independent mind. Misconception inatokea mara nyingi ukiwa unataka taarifa za upande mmoja.
 
Hufahamu kuwa kuna media bias pia, mfano aljazera wako symphasized na palestine unaweza kuwa misinformed kama huna independent mind. Misconception inatokea mara nyingi ukiwa unataka taarifa za upande mmoja.
Suala la Palestina na la vita zingine nilizozungumza hapo havihusiani.
Article nilizosoma hazipishani hata upunje kwa vyombo vikubwa vya habari duniani.
Hata tukija suala la Palestina Aljazeera hakuna fabricated news anazorusha isipokua tu anazipa kipaumbele habari za Palestina kwasababu vyombo vingine vimeipuuza Palestina kwa miongo mingi.
 
Huwezi kupata taarifa rasmi kama huna independent mind kwa sababu kwenye media kuna biases nyingi sana. Maana yangu ni kwamba ukiwa umechukua upande ukikutana na taarifa tofauti ni zile unazotaka wewe utaona uzushi. Kwa mfano mgogoro wa mashariki ya Kati ni sehemu yenye propaganda nyingi sana hivyo inaweza kuwa vigumu kupata hitimisho juu ya flani. Juzi umeona CNN walivyo disclose maovu ya us marine kwenye uwanja wa ndege kabul. Mambo ni mengi ukiwa neutral ndipo unaweza kujifunza mengi
 
kwan hapa point ilikua ni gharama au kuzuia mashambulizi? unachotakiwa ujue kwa israel yeye kutumia gharama kwake sio shida linapokuja suala la usalama wake yeye atatumia gharama yeyote yeye kwake pesa sio shida, ila angalia, israel labda useme katumia gharama so kapata hasara ya pesa..ila iran magenerali wameliwa vichwa wamepotezwa so hapo nani kapata faida nani kapata hasara? pesa zinatafutwa, je hao waliokufa utawareplace na nini?

kama iran alikua analipiza kisasi basi na yeye ilitakiwa afanye mashambulizi ambayo yangeua watu nchini israel
 
sasa iran walisema israel ikijibu itawashambulia vibaya, haya israel kajibu baada ya siku mbili tena mbona iran hajafanya lolote? mana kipigo tu alichopewa alibaki mdomo wazi hajaamini hata kidogo kama anaweza kupigiwa nchini mwake.
 
sasa iran walisema israel ikijibu itawashambulia vibaya, haya israel kajibu baada ya siku mbili tena mbona iran hajafanya lolote? mana kipigo tu alichopewa alibaki mdomo wazi hajaamini hata kidogo kama anaweza kupigiwa nchini mwake.
Military actions are not for granted unless you want to go to hell. Usipende kujadili vitu kwa hisia kama kweli ulienda shule kujifunza namna ya kutumbua mambo. Hakuna anayeweza kuingia vitani kama ng'ombe kwa dunia ya leo ndio maana Marekani alionya Israel akijibu mapigo basi ayanywe mwenyewe. Iran pia sio wajinga ndio maana walishambulia bila tangazo la vita maana wanajua vita ilivyo chungu
 
Nipo neutral na ndio maana najifunza na nimejifunza mengi.
Na huwa siegemei upande mmoja,ndiomaana nikiwa natizama habari za kimataifa hugeukia vyombo takriban vyote vya habari kupata confirmation kama habari ni uhakika ama ni fabricated.
Nitaanza Aljazeera nitakuja CGTN nitakuja Africa news kesha nitamalizia na France24/BBC.
Huwa siegemei upande mmoja.
Na ndio maana ninapata ubavu wa kusimama na kupinga ama kuiunga mkono habari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…