Je, kwa mshahara wa Shilingi 310,000 unaweza kuishi Dar es Salaam?

Je, kwa mshahara wa Shilingi 310,000 unaweza kuishi Dar es Salaam?

kwa taarifa yako bodaboda wanakipato kikubwa kupita watu wengi na ili waweze kupata kipato kikubwa wanatakiwa wafanye wafuatayo:-
  1. uaminifu kwa wateja
  2. usafi wao binafsi
  3. usafi wa bodaboda
  4. wajue uhitaji wa mteja.
hawa tunaweza kuwatumia kwa mikopo ya dharura kama gas imeisha au unahitaji mboga natoka asubuhi uliondoka mnara hausomi ikifika saa nne unampigia unamwambia samahani mdogo wangu naomba ninunulie nyama kilo moja na nyanya tutaonana jioni wapelekee nyumbani.
au gas ikiisha unamwagiza na yeye anatoa hela yake wakati wewe unachakarika au chakula chakuku kikiisha unaweza kumkopa achilia mbali kumwambia sementi imeisha site mafundi wamesimama naomba ninunulie mifuko miwili tutaonana! acha kabisa boda boda kwa kweli Mungu awalinde!
unajua hata bodaboda au bajaj huwa wanaingiza pesa kutokana na mahali walipo mkuu.
Bodaboda anaeingia hadi town na anafanya kazi sehemu ambapo watu ni middle income anaingiza pesa nzuri kuliko hawa wanaofanyia kazi sehemu ambazo watu wengi ni kipato cha chini maana kupata route za 5000 - 10000 ni ngumu

kingine mtu mwenye bodaboda yake anaweza akaingiza pesa nzuri tofauti na anaetakiwa kupeleka hesabu kwa boss.. Ndo maana nilisisitiza hapo mkuu
 
Kuna siku nilikua naongea na mtu haya mambo ya kipato, akawa ananipigia hesabu kiukweli ni za kufikirika, eti sukari kwa mwezi kilo 1 hivi kilo moja ya sukari inakataje mwezi jamani kwenye familia?

Ndio zile hesabu za shamba unaweka milioni moja unalima unapanda unavuna faida unapata mil 13 ukitoa garama nyingine inabaki mkononi na m12
Hahahah hesabu za online hizo mambo kwa ground ni mtiti
 
unajua hata bodaboda au bajaj huwa wanaingiza pesa kutokana na mahali walipo mkuu.
Bodaboda anaeingia hadi town na anafanya kazi sehemu ambapo watu ni middle income anaingiza pesa nzuri kuliko hawa wanaofanyia kazi sehemu ambazo watu wengi ni kipato cha chini maana kupata route za 5000 - 10000 ni ngumu

kingine mtu mwenye bodaboda yake anaweza akaingiza pesa nzuri tofauti na anaetakiwa kupeleka hesabu kwa boss.. Ndo maana nilisisitiza hapo mkuu
Ni kweli japo kwangu mimi watu wenye kipato cha chini ni biashara yangu na boda boda ndio watu wanaojibu maswali mengi ya kwangu kuhusu kipato kwa kuwa natumia usafiri wao kila siku. hivyo ninachokueleza kwa wao kupata hizo fedha inawezekana haijalishi yuko wapi ili mradi azingatie masharti na hasa wenye umri kati ya miaka 20-35
 
Tatizo msharaha ni fixed ,ukitilea mfano bodaboda ,muuza kandoro unakosea sana.Kuna bodaboda anaishi nyumba ya 150k muuza kandoro anakwambia kwa siku anaondoka na mpk 30k faida sometime inategemea na hali ya hewa (jua).
Kila kitu kinategemea location mkuu

sikatai kuna watu wanaingiza hela nzuri kwa kazi hizihizi za kawaida ila inategemea na lokesheni aliyopo .. Wa kariakoo si sawa na wa temeke au mbagala au makumbusho

kingine mkuu kama hao watu wangekuwa wanaingiza hiyo wastani wa laki 9 kwa mwezi, sidhani kama wangeendelea na hizo biashara maana kama kuna watu wanajua channel ya hela kwa kazi ambazo hazihitaji mtaji mkubwa bhasi ni wa hali ya chini
 
Ni kweli japo kwangu mimi watu wenye kipato cha chini ni biashara yangu na boda boda ndio watu wanaojibu maswali mengi ya kwangu kuhusu kipato kwa kuwa natumia usafiri wao kila siku. hivyo ninachokueleza kwa wao kupata hizo fedha inawezekana haijalishi yuko wapi ili mradi azingatie masharti na hasa wenye umri kati ya miaka 20-35
sawa mkuu naheshimu mawazo yako
 
310,000 mbona inatosha japo ni ngumu kufanya saving,kodi ya chumba na sebule medium quality 60000,umeme na maji 10000,chakula unasaga debe 2 za unga kila debe maximum 15000x2 ni 30000,maharage kilo 5x2000 ni 10000,mchele kilo 20x1200 ni 24000,mafuta Lita 5 ni 25000,mkaa nunua gunia moja 50000,gesi 25000 JUMLA NI 234000 hivyo ukiitoa kwenye 310000 itabaki 76000,suala la afya kata bima ya familia 54000 kwa mwaka,itabaki 22000 hii ya kubadilishia mboga kwa mwezi.Nauli kazini itabidi uwe mdau wa tz 11,suala la mavazi ni anasa,chai asubuhi ni anasa,king'amuzi ni anasa,bia ni anasa,kuhonga ni anasa, kutoa sadaka Mungu ndio anajua hali yako atakusamehe,YAANI KIFUPI UTAISHI KAMA SHETANI au nasema uongo ndugu zangu

Imebidi nicheke tu
 
Mimi kwa 310K naishi Dar bila zengwe.
 
70K Chakula Cha Mwezi Mzima.

20K Vocha.

40K kwa wazee.

50K nauli ya mizunguko ya mwezi.

Inayobaki ni ya kusave na pocket money.
Kuonga unaonga kiasi gani kwa mwezi?
Bia ngapi kwa wiki unakunywa au wewe msabato??
Mbona umesahau kuweka kwenye bajeti hayo
 
Kuonga unaonga kiasi gani?
Bia ngapi kwa wiki unakunywa au wewe msabato??
Mbona umesahau kuweka kwenye bajeti hayo
Ooh hapo kweli.

Mimi sinywi wala sivuti.

Aina ya wanawake ninaoruka nao kuhonga huja in terms of outing, kuumwa, pesa ya kula n.k nadra kulipishwa kodi. So pesa inayobaki inacover hapo.
 
Habari wadau!

Ebu nisaidieni hivi kweli 310,000/= inatosha mtu kufanya kazi na kuishi DAR au unatakiwa kuwa na miundombinu mingine?
Huwa najiuliza wale mama lishe huwa wanapata Tsh ngapi kwa mwezi.
Ghafla imeniijia sura ya yule mdada mpika vitumbua aliyekuwa na mtoto kapanga nyumba Ubungo, kuna mwamba mlinzi alikuwa analipwa 250k lakini aliufurahia sana ule mshahara ungemwezesha kuishi kwa raha kidogo mjini ana watoto wawili lakini wanaishi bwana.
 
Back
Top Bottom